Facts: 16 most powerful militaries in Africa

Facts: 16 most powerful militaries in Africa

Ukana Shilungo,
Nasikitika kwa kutokuielewa mantiki ya thread hii,

Kwanza niwapi Yericko alipolitusi jeshi? kukopi link inayohusu nchi yetu ni tusi au kuelimisha.

Pili mifano yako kuwa Kenya inashindwa na al shabab tu siyo irrelevant utafiti huu ni wa uwezo wa nchi na nchi sio wa kupambana na vikundi vya kigaidi, unachanganya kazi ya jeshi la polisi na kazi ya jwtz.

Jeshi letu kukishinda kikundi cha M23 kuna factors nyingi mojawapo hatukuwa peke yetu pili hatukuenda na vifaa tulikuwa chini ya uangalizi wa un hata mishahara haikutoka kwetu.

Kwa hiyo kusema kuwa Nigeria wanashindwa na Boko haram basi hawana jeshi imara ni kujidanganya, mbona sisi tunahangaishwa na panya road wenye mapanga tu ina maana jeshi letu halina uwezo kiasi hicho.
 
Hii list imepangwa kibiashara tu mpanga listi anataka tukanunue silaha kwao
 
tanzania imeshinda waasi gani? na kwambia usiombe tanzania watokeee waasi tutajuta hakuna jeshi humu siasa kila kona imejaa tutakufa mpaka basi

kitendo cha kukosekana waasi tz ni ishara tosha kuwa tuna jeshi makini! Nakuhakikishia hakuna kenge yeyote atakaeleta kitovu chake tz na akabaki mzima!!

Hapa pigeni domo tu mfurahishe genge ila jwtz ni moto wa kuotea mbali. Km umewahi kutembelea nchi za afrika nenda ukawaulize wanalifahamu vp jeshi la tz! Watakuambia.

Kweli nimeamini nabii hakubaliki nyumbani kwao.
 
Hii list imepangwa kibiashara tu mpanga listi anataka tukanunue silaha kwao
Umeona eeeeeh! Nadhani Tanzania tumewekwa wa mwisho kutokana na kutonunua silaha kwenye mataifa ya Uingereza, Ufaransa na Ujerumani
 
Watu wanatumia nguvu nyingi sana kumpiga mleta mada, lakini wanasahau utafiti unapigwa kwa utafiti na kuangalia vingezo vilivyotumika katika utafiti husika.
kimsingi tunapaswa kujitasimini kwa kina sana
 
Ripoti ya hovyo sana hii, hakuna tofauti na ile iliyoonyesha eti Tanzania ni ya pili kwa umaskini duniani. Akili za kuambiwa tuchanganye na zetu,
 
Sikuballiani na hii ripoti uchwara.Yaani DRC tumewasaidia kuanzia kufundisha askari wao hadi kuwafurusha M23.Kenya jeshi lake ni hovyo kabisa tazama tangu wamekwenda Somalia wamefanya nini,Uganda jeshi lao tumewafunza,Sudan nchi imegawanyika baada ya vita vya muda mrefu sana.Somalia wana jeshi zuri kuliko Tanzania huu ni uongo wa mchana kweupe.

Mkuu Ni Busara Sana Kulipa Jeshi Letu Heshima Yake! Lakini Ogopa Sana Nchi Ambayo Majeshi Yake Yako Kwenye Operation Za Kiusalama Muda Wote. Waliotoa Repoport Wana Sababu Zao Tusiwabeze. Hizi Changamoto Kwa Wakuu Wa Majeshi Ya Kwetu. Ila Si Siamini Kama Nchi Yetu Jeshi Lake Ni La Kisiasa Kuliko Hata Uganda.
 
Kwenye hili nimejikuta nacheka....

Seriously,

DRC inayoshindwa kulinda mipaka yake, imegeuzwa shamba la bibi na Rwanda eti iko juu yetu, tulioenda kuwatoa M23 and mind you, hawa jamaa wangepewa mwezi mmoja wangekuwa Kinshasa.

This is a joke
 
kitendo cha kukosekana waasi tz ni ishara tosha kuwa tuna jeshi makini! Nakuhakikishia hakuna kenge yeyote atakaeleta kitovu chake tz na akabaki mzima!!

Hapa pigeni domo tu mfurahishe genge ila jwtz ni moto wa kuotea mbali. Km umewahi kutembelea nchi za afrika nenda ukawaulize wanalifahamu vp jeshi la tz! Watakuambia.

Kweli nimeamini nabii hakubaliki nyumbani kwao.
Nakubaliana na wewe Mkuu. Tanzania tunasambaratisha maadui kabla hawajaweka ngome. Somo tosha tumelipata kule Mtwara ambako vijana walijikusanya wakawa wanapata mafunzo ya kigaidi. Tuliwateketeza wote japo hatujawaua
 
Nivigumu siasa kuongoa mambo ya kitaalamu, hili hata wahenga walilinena, wakati wenzetu wakijenga mataifa yao kijeshi na kiulinzi yakawa imara na ya kisiasa zaidi, sisi tunaendelea kuonyeshana namna mwanajeshi anavyopasua tofari kwa kichwa, yani utafiki ni jeshi la enzi za akina Mkwawa.
Wakati wa miaka ya sitini mpaka miaka ya tisini, Tamzania ilikuwa ya kwanza barani Afrika kwakuwa na idara ya ujasusi imara ikifuatiwa na Zimbabwe, lakini leo Zimbabwe ni ya kwanza ikifuatiwa na Misri na Tanzania ni ya Tatu.


Sifa hizi zilieneoa duniani kote na tafiti nyingi za mashirika ya kijasusi zikafanywa nakusema Tanzania ni nchi ya kwanza Barani Afrika kwakuwa na Jeshi imara la miguu,

Chanzo: Countries Ranked by Military Strength (2014)

Wale wa lumumba kama kawaida na uvivu wao wakusoma watakuja humu na vijembe oh! ilienda ikarudi.Siasa ikishaingizwa kwenye fani yoyote kila kitu kinajiangukia/kuporomoka kama mabua ya mahindi.

Kuna haja sana! Makamanda wa vikosi husika kuwa wadadisi wa mambo na kuchukua hatua mara moja!Naamini tusinge fikia kiwango hicho kama kweli maofisa husika na wale wanasiasa wanaopewa majukumu husika kutimiza majikumu yao sawa.

Tatizo la msingi limeanzia toka enzi ya Rtd General Mboma,pale JWTZ ilipogeuka kuwa mfanyabiashara ,badala ya kuwa Mlinzi wa Umma wa watanzania-chini ya Usimamizi na uangalizi wa Ikulu-Raisi mstaafu Ben Mkapa

NB.Bila kuwa shughulikia wahusika wote na Scandali hii-JWTZ itaendlea kuporomoka zaidi ya hapo ilipo.
Na kingine lakutupiwa jicho ni uteuzi wa Waziri wa Wizara husika na dhani sasa utamaduni huu wa kujiteulia watu wasio na uzoefu au hata mwanga wa nini Jeshi linahitaji au mwelekeo gani inatakuwa kuwa nao unafaa ubadilike.




[h=3]Chadema Blog: Zitto: Kashfa za Meremeta zisijirudie JWTZ[/h][h=2]Sunday, May 5, 2013[/h] [h=3]Zitto: Kashfa za Meremeta zisijirudie JWTZ[/h]

MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (CHADEMA), amekemea vikali baadhi ya kashfa za Meremeta na Suma JKT ambazo zimekuwa zikilikumba Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na kuchafua sifa ya jeshi hilo.
Zitto alitoa kauli hiyo jana bungeni mjini hapa alipokuwa akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa mwaka wa fedha 2013/2914 iliyowasilishwa na Waziri Shamshi Vuai Nahodha.
Pia alilitaka jeshi hilo kuwajali askari wake kwa kuwalipa vizuri mshahara na mafao yao ili wawatumikie wananchi wao kwa ufanisi, waondokane na tamaa ya kuweza kurubuniwa na waasi ambao wanaweza kujitokeza kutoka nchi jirani.
“Kashfa hizo zinazoiandama JWTZ hazina budi kutatuliwa ili kuepuka yanayotokea katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) ambapo baadhi ya wanajeshi wameasi,” alisema.

Apr 15, 2008 - Kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) iliyoitwa Buhemba ilivunjwa. Askari walihamishwa kwa mikokoteni ya kukokotwa na ng'ombe ili kupisha ...
 
Ukana Shilungo,
Nasikitika kwa kutokuielewa mantiki ya thread hii,

Kwanza niwapi Yericko alipolitusi jeahi? kukopi link inayohusu nchi yetu ni tusi au kuelimisha.

Pili mifano yako kuwa Kenya inashindwa na al shabab tu siyo irrelevant utafiti huu ni wa uwezo wa nchi na nchi sio wa kupambana na vikundi vya kigaidi, unachanganya kazi ya jeshi la polisi na kazi ya jwtz.

Jeshi letu kukishinda kikundi cha M23 kuna factors nyingi mojawapo hatukuwa peke yetu pili hatukuenda na vifaa tulikuwa chini ya uangalizi wa un.

Kwa hiyo kusema kwa kuwa Nigeria wanashindwa na Boko haram basi hawana jeshi imara ni kujidanganya, mbona sisi tunahangaishwa na panya road wenye mapanga tu ina maana jeshi letu halina uwezo kiasi hicho.


ndg yng km mambo huyajui ni heri ukae kimya, kuhusu kuwapiga m23 ktk misitu ya kongo ni makomando wa jwtz ndio waliowang'oa wale waasi.

Jiografia ya nchi ya kongo yenye milima na misitu mikubwa iliyashinda majeshi mengi ikiwemo afrika kusini. Ni juhudi ya makomandoo jwtz kutega mabomu ktk njia za waasi baada ya kuwasoma mbinu zao na jwtz waliwakurupusha m23 ktk moja ya maficho yao na kisha kujikuta wanaingia kwenye mtego wa jwtz na ndipo mabomu yalipoanza kulipuliwa na waasi kupoteza dira.

Haikuwa kazi nyepesi na majeshi yote ya ukombozi waliwapigia saluti jwtz kwa kazi nzuri ya kishujaa! Leo ww kiumbe mdogo unabeza.

Jwtz wanafanya kazi kwa amri ya amiri jeshi mkuu, kuhusu panya road jwtz hawakupokea amri yeyote inayowataka wakapambane na hao uimburu na wala jeshi la polisi hawakukiri kushindwa so jwtz hawakurupuki ktk kufanya kazi.

Ktk mambo ya msingi tuache ushabiki maandazi.
 
EnyiwanaTanganyika hii ripoti inaukweli hebu tujiulize ubora wa intelijensia yetu upo wapi, uimara wa jeshi unaanzia kwenye intelijensia.

Ukiwa na zero intelijensia jeshi halina cha maana.

Mpaka leo hatujuwi nani kapokea fedha za Escrow hapo Stanbic

Mpaka leo hatujuwi nani alilipuwa wahanga wa soweto Arusha

Mpka leo haijulikani nani aliuwa padri kule zanziba na kujeruhi wengine

Mpaka leo hatujuwi wezi waliohifadhi fedha Uswisi

Mpaka leo hatufaham nani na nani kwa ujumla wao walipakiza twiga na swala wakiwa hai ndani ya ndege ya jeshi kilimanjaro

Mpaka leo hatujuwi nani alipakia meno ya Tambo ndani ya meli ya katibu mkuu wa ccm

Mpaka leo hatujuwi wauza dawa za kulevya wale mabosi

Mpaka leo hatujaambiwa Gavana wa zamani alikufa yaani Balali na ilikuwaje

Mpka leo mambo ya Deep green, meremeta, kagoda, Epa namengineyo bado kitendawili

Mpaka leo IPTL, Dowans, Pap nk wanatuibia tu, na nimakampuni feki

Mpaka leo faru wamekwisha anayemaliza hatumjuwi

Sasa hilo jeshi litapataje kuwa lakisasa na bora kama intelijensia yao ipo chini kiasi hicho??????????????????????????????
 
MKUU YERIKO Nakukubali mno,kwa hili nipo kinyume.

  1. Kenya wanasumbuliwa na al shabaab,wakenya wanauwawa na vijikundi vya kigaidi vidogo dogo.wangekuwa na intelgensia imara na jeshi imara,wasingesumbuliwa.kenya hajawahi kufanya mission yoyote ya kijeshi kama vile ukombozi wa kusini mwa Afrika nyakati zile,wana well equiped army,wanakosa displined army,wanakosa experienced army.
  2. Kongo hawana jipya,kabla aliingiliwa ikulu karibu auawawe miaka miwaili iliyopita,anasumbuliwa na vikundi vya waasi,M23 TZ chini ya mwavuli wa UNO waliwapa kipigo cha paka mwizi,na biashara yao ikaisha.Kongo angekuwa na inelgensia imara na jeshi imara angekuwamaliza vikundi vya waasi mwenyewe.Jizi tu Mheshimiwa Rais Kikwete alifunga mafunzo ya maafisa wa Jeshi,wengi walikuwa toka Kongo.
  3. Uganda zaidi ya miongo miwili anasumbuliwa na Joseph Kony,kijikundi tu kidogo ambacho kikitokea tanzania wanagongwa toka kwenye pori walilojificha na kesho tunahesabu Mizoga tu.angekuwa na jeshi imara asingesumbuliwa namna hiyo.
NB.Opesesheni ya Kumuondoa Mohamedi Bakari Commoro ilisemekana ni impossible Tz iliomba logistic tu,ikapata ikaenda na yule bwana aliondoka alfajiri na majeshi yetu yakamvalisha dila na mtandio,wakamwambia aende kwa amani.

Ukombozi wa nchi za kusini Mchango wa Tanzania,Sudani na nyingine nyingi.Nasikitika Yeriko kuwa mimi ni shabiki mkubwa na mwanachama wa CHADEMA,inapokuja issue ya kitaifa hasa jeshi mimi naliheshimu sana,unaandika hapo kwa sababu nchi ina amani kwa sababu ya jeshi letu unalolitusi,bora ungezungumzia jeshi la polisi kuliko JWTZ jeshi letu lililotukuka.

EAST AFRICA EAGLE naomba uje umpe shule Yeriko Nyerere na mods wapeleke uzi huu Jamii forum Intelgensia ambako kuna watu hawingii huku jukwaa la siasa,ili ajibiwe kwa weledi wa hali ya juu!

Kwa kumalizia wewe na mimi labda hatujui sawasawa kuhusu jeshi letu.Nashauri Ngome wamchukue Yeriko nyererer wakamhoji Pale Ngome upanga kwa nini analitusi jeshi letu tukufu.
Nmesikitishwa sana na ndugu Yeriko nyerere.

Ukana Shilungo.

Mbona povu Mkuu.
Yerick ametoa Mpaka na source,au unafikiri hii list kaandaa Yericko ?
 
Nivigumu siasa kuongoa mambo ya kitaalamu, hili hata wahenga walilinena, wakati wenzetu wakijenga mataifa yao kijeshi na kiulinzi yakawa imara na ya kisiasa zaidi, sisi tunaendelea kuonyeshana namna mwanajeshi anavyopasua tofari kwa kichwa, yani utafiki ni jeshi la enzi za akina Mkwawa.

Wakati wa miaka ya sitini mpaka miaka ya tisini, Tamzania ilikuwa ya kwanza barani Afrika kwakuwa na idara ya ujasusi imara ikifuatiwa na Zimbabwe, lakini leo Zimbabwe ni ya kwanza ikifuatiwa na Misri na Tanzania ni ya Tatu.

Hali kadhlika baada ya vita vya Uganda, Tanzania ilipanda kwenye viwango vya ubora na uimara wa kijeshi hasa sifa zikienda kwa kikosi cha ardhini kile kilichopambana na majeshi ya Nduli katika uwanda wenye maji ya kiuno kwa mda wa siku sita mfululizo mpaka kikashinda kikiongozwa na Brigedia Kiwelu ambae baada ya mapambano yale alibatizwa na kuitwa KAMBARE, jina hilo lilifuati uwezo wake wa kuzama mda mrefu majini huku akiji mapigo vikosi vya Nduli vilivyokuwa vimejichimbia mlimani katika mto Kagera,

Sifa hizi zilieneoa duniani kote na tafiti nyingi za mashirika ya kijasusi zikafanywa nakusema Tanzania ni nchi ya kwanza Barani Afrika kwakuwa na Jeshi imara la miguu,

Hivi sasa siasa zimeharibu sifa hizo na utafiti wa wakala wa usalam wa taifa wa Amerika umeweka takwimu hizi hapa mpya ambao Tanzania ni ya mwisho kati ya nchi 22 zilizofanyiwa utafiti.

ORODHA KAMILI.

1 Egypt

PwrIndx: 0.6122

2 Algeria

PwrIndx: 1.1698

3 Ethiopia

PwrIndx: 1.3229

4 South Africa

PwrIndx: 1.3467

5 Nigeria

PwrIndx: 1.5261

6 Kenya

PwrIndx: 1.7689

7 Morocco

PwrIndx: 1.8499

8 Tunisia

PwrIndx: 1.8635

9 Angola

PwrIndx: 2.2599

10 Libya

PwrIndx: 2.3353

11 Sudan

PwrIndx: 2.3465

12 Democratic Republic of the Congo

PwrIndx: 2.6642

13 Uganda

PwrIndx: 2.6895

14 South Sudan

PwrIndx: 2.7689

15 Ghana

PwrIndx: 2.9726

16 Zimbabwe

PwrIndx: 3.0955

17 Cameroon

PwrIndx: 3.3009

18 Zambia

PwrIndx: 3.5013

19 Somalia

PwrIndx: 3.5462

20 Mozambique

PwrIndx: 4.1026

21 Madagascar

PwrIndx: 4.2547

22 Tanzania

PwrIndx: 4.3423



Chanzo: Countries Ranked by Military Strength (2014)

Napenda nikusahihishe kidogo kuhusiana na maelezo niliyoweka red. Wakati wa vita vya Uganda, Division iliyopigana ikiwa ndani ya maji ya kiunoni iliongozwa na Brigedia (wakati huo) Mwita Marwa na ndiye alipewa hilo jina la Kamanda "KAMBALE"
 
Ukishaanza na kujiunga na Mafisadi na Mafia wa aina hii ya Victor Bout usitegemee masilahi ya Umma ndani ya Jeshi .
Mara zote malengo ya Jeshi yanapotea kabisa na badala yake Jeshi linageuka kuwa taasisi ya Makamanda wachache ambao wanakuwa Mabilionea ,na kuwa ingiza wanasiasa ndani yake au Kinyume chake,kwa maana ya Wanasiasa kuwa ingiza Makamanda kwenye madili kama hayo.

 
Back
Top Bottom