Uchaguzi 2020 Fadhila za Lissu kwa majasusi wa kibepari na kisingizio cha uwekezaji nchini

Lissu na Trippi hawawezi kufanikisha malengo yao, hii sio Zimbabwe hii ni nchi iliyokabidhiwa kwa Mungu siku moja kabla ya uhuru mwaka 1961.

Hao wenye nia zilizojificha kwa ufupi wasahau.
 
Endeleeni kuwaita mabeberu siku wakiamua msije kusema hatukuwaambia.
Waamue wao ni nani?hatutokubali taifa liangamie kwa tamaa za madaraka ya lissu,mataifa yote yaliokubali mabeberu kuingilia mambo yao ya ndani ndani hayajawai kukaa sawa mpaka leo.
 
Alitutishia miga kwenye madini yetu sasa ameamia ICC kamwe hatutakubali tamaa za fisi zimponze tanzania
 
Endeleeni kuwaita mabeberu siku wakiamua msije kusema hatukuwaambia.
Umekariri nyumbu wewe, kwenye mada neno mabeberu umeliona sehemu gani? Unawaza mabeberu tuu ukishaona jina Lissu
Mleta mada kasema mabepari wewe unakurupuka eti mabeberu!
 
Kwa sasa una uhuru gani? Kila siku "marufuku kufanya hiki,fungia fungia,kamata kamata ,vitisho na ujinga mwingine mwingi ndiyo uhuru unaotaka? Au ni mumiani wewe?
 

Lisu anapaswa kuongea kwa jeuri, na kama kweli wazungu wataingilia mambo yetu tutawaunga mkono. Tumechoka kuongozwa kwa shuruti na chama kinachonajisi box la kura. Kwa sasa hapa nchini tunaona viongozi wa ccm wakiongea kwa jeuri kisa wanaweza kuitumia tume ya uchaguzi, na kisha kuagiza vyombo vya dola kulinda ushindi haramu, acha hao wazungu waje kama ni kweli tuanze moja.

Hizo propaganda za kizee mkawape watu wa huko vijijini wasio na uelewa wowote wa mambo. Mpaka sasa hao wazungu wanatudai deni la 40t+ na hatuna uwezo wowote wa kuwalipa. Kama kuna chochote wanataka kwanini wasitumie kisingizio cha hilo deni lao kukichukua, mpaka wasubiri Lisu awe rais? Au ccm ndio mnajiona mnaaminika sana kwenye mali za nchi hii? Muhuni mkubwa wewe.
 
Mabeberu yakianua kuja kuchukua yakitakacho hayazuiwi na yeyote na wala hayahitaji kumtumia Lissu

Kwani mlipoyapa Uranium, yalimtumia Lissu?
Tulijikwaa lakini kwa sasa tumeamka na tumejitaidi kila namna ya kuamua kivyetuvyetu kupitia kiongozi wetu na hivi ndiyo mataifa yote duniani yaliweza kujikomboa kutoka kwenye utegemezi,lazima kama taifa tujue kwamba lazima mujiwezeshe karibia kila kitu,wakati rais anasema wawekezaji wazawa wapate fulsa ya kuzalisha na kupata soko ndani ya nchi alafu anatokea mtu anasema ataruhusu kila kitu kiingie na akijua wazi hatuwezi kushindanao kwa kuwa wao wamezalisha kwa gharama nafuu zaidi,ndio maana magufuli aliamua kujenga bwawa la umeme ambalo litasaidia kupunguza gharama za uzalishaji na kuweza kuleta ushindani wa bidhaa.
 

Lissu amekuwa akisema sana haya maneno. Kama hukusikia usipotoshe

Lissu
 
Hasemi mshindi atangazwe anasema nisipo tangazwa
 
Samahani "Shanta mine, Anglo Gold... Williamson Diamond... et al waliletwa na TL? Je ubinafshaji mashirika na kufa kwa vyama vya ushirika ni TL alihusika?"
 
amekuwa akitishia kuwa maamuzi yoyote ya kutokuwa yeye Rais yatawapeleka watu ICC.
Acha kupotosha. Unamsikiliza peke yako? Amesema "Ttume, Magufuli, wakuu wa vyombo vya dola wasifanye "mchezo" na uchaguzi huu"

"Mchezo" unaongelewa hapa ni kuhujumu. Acha uzwazwa.
 
Wewe una tofauti gani na mtu ambaye ni zero brain anayewaza baba yake afe ili apate urithi bila kuuliza zilipatikanaje na alikuwa anaziendeshaje kabla ya kuombea mabaya,ni kipi cha muhimu unachokikosa katika taifa hili mpaka uombe njaa na ukijua nawe haitakuacha salama kamwe nakushauri kitu kama umechoka na amani iliyopo nenda Libya au Kongo au ikiwezekana nenda ulaya.
 
Hasemi mshindi atangazwe anasema nisipo tangazwa
Ndio, "nikishinda kwa kura na nisipotangazwa kitawaka"
Na sisi tunasema tuko pamoja naye kwenye hilo
 
Mku kujiamini kwa Lisu ajulikana hajawahi kurudi nyuma ktk kile akisimamiacho fuatilia mambo yake tangu utawala Hayati Mzee wetu Mkapa.
Angalizo aliotupa kama chama tawala na Nec ni kutenda pasipo haki ataamua yy na wafuasi wake kwani anaamini ktk nguvu ya umma kama tunavyoshughudia kute anapopita anachokutana juu umma wenye kiu.
 
Ni bahati mbaya kwamba unashindwa kutumia ubongo katika kufikiri kama Mungu alivyokujali, badala yake umeamua kutumia kamasi.

Eti ametumwa, ametumwa na nani? Eti amesema asipotangazwa yeye kuwa mshindi amesema hapatakalika.

Yaani kwasababu ya chuki zako binafsi basi unaamua kumzushia mtu uongo mpaka hata shetani anakushangaa.

Bahati nzuri watanzania ni watu wenye uelewa mkubwa na wamemsikia Lissu alichosema na kukielewa hivyo kujaribu kutunga uwongo wako na kuwalisha watanzania ukifikiri watakuamini wewe unajidanganya.

Hivi tangu muanze kueneza huu uwongo umeleta impact gani chanya upande wenu?

Maana mi naona ndio kwanza kila mahali aendako Lissu anazidi kukibalika.

Hebu acha kuwa mjinga kama Inzi kila siju kuchenzea kinyesi, hebu siku moja nawewe tengeneza asali kama nyuki.

Sent from my A37f using JamiiForums mobile app
 
Acha kupotosha. Unamsikiliza peke yako? Amesema "Ttume, Magufuli, wakuu wa vyombo vya dola wasifanye "mchezo" na uchaguzi huu"

"Mchezo" unaongelewa hapa ni kuhujumu. Acha uzwazwa.
Kwani mwaka huu ndio Mara ya kwanza kufanya uchaguzi mbona wenzake hawakuwai kutoa mikwara ya namna hiyo na wala hawakuamasisha watu waingie barabarani, na hata huko marekani trump alipopita kuna mengi yalizungumzwa kuwa ameiba kura na hakuna mwananchi yeyote au mwanasiasa aliyeamasisha kuwa wavuruge nchi yao licha ya kwamba wapo wasiompenda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…