Fahamu kinachojiri kuhusiana na kirusi cha Corona (Coronavirus)

Umetia chumvi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama upo moshi ni siku kadhaa utakua Chuga. Ngoja nikusanye muvi na series kibao niwe naangalia tu karatini
mkuu chukua fash yangu nenda kona ya nairobi mwambie Murphy ai-format afu ajaze muvi mpya mpya🎥🎥🎥🎥



then tukutane karantini😂😂😂😂😅😅😅
 
Siangaliagi za kutafsiriwa mkuu. Kuna mshikaji kona nairobi juu ya ofisi yake kuna poster ta Creed II ndio hua naenda ananiwekea
ukihitaji ambazo hazijatafsiriwa pia hua zipo





tukutane karantini😷😷😷😷
 
Vipi ukipata hivyo virus unaweza kupona?. Wapo waliopitia hiyo madhira amepona?

Sent using Jamii Forums mobile app
Matibabu hufanyika kwa wenye dalili za virusi hivyo.

Dalili hizo hutibiwa kwa usaidizi maalumu katika mifumo ya mwili hususani mfumo wa upumuaji pamoja na viungo vya mwili vyenye dalili za kushindwa kufanya kazi vizuri.

Kwa lugha nyingine matibabu hayo hujulikana kama 'supportive care'.

Tiba kamili ya COVID-19 bado haijapatikana.
 
Watanzania inabidi tujielimishe kadiri tunavyoweza...

Kwa mnaowezq ifikia youtube, tafute documentaries zinazoonesha namna watu waliopo sehemu zenye maambukizi wanavyojiepusha...

Juzi nilikuwa natazama blogger mmoja Mrusi kaweka vblogg yake akiwa Wuhan, namna ambavyo mji umegeuka kuwa ghost town, watu wana hofu ya kugusa hadi buttons za elevators kiasi kwamba wanatumia vijiti vya toothpick...
 
UPDATE: Wizara ya afya ya China imeripoti visa vipya 11 sanjari na vifo vipya 13 nchini humo.

Hubei pekee, kumeripotiwa visa vipya 7 huku vifo vyote 13 vikitokea pia mkoani humo.

Mpaka sasa, China imeripoti visa 80,824 vikiwemo vifo 3,189.

Wagonjwa wapatao 65,541 mpaka sasa wametibiwa dalili za COVID-19 na kupata ahueni.

Hivi sasa, wagonjwa wapatao 3,610 wako katika hali mbaya zaidi.
 
Vipi ukipata hivyo virus unaweza kupona?. Wapo waliopitia hiyo madhira amepona?

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuwa na exposureya virusi hivyo sio kuwa ni ugonjwa, isipokuwa dalili za magonjwa yanayofanana na hali ya mafua mtu ataanza yapata pale kinga za mwili zitapoanza kupambana na uvamizi wa virus...

Kwa watu wenye kinga nzuri, baada ya muda mfupi unarudi kuwa sawa...

Kwa walio na kinga ya chini, hawa virusi hupelekea mtu kuwa na 'nimonia' (pneumonia) na wanaofika stage hii na kuendelea ndio wanaopoteza maisha...
 
UPDATE: Iran

Visa vipya 1,365 vimeripotiwa hivi punde nchini humo sanjari na vifo vipya 97.

Ongezeko hilo linapelekea idadi ya visa vyote nchini humo kufikia 12,729 huku idadi ya vifo ikifikia 611 hadi sasa.

Waliopata ahueni wafikia 4,339 huku kukiwa na uwezekano wa visa vipya kuongezeka zaidi.
 
Bado hujanijibu mkuu. “ukiwa na kinga nzuri baada ya muda unakuwa sawa”. Unakuwa sawa ndio kusemaje? Kupona ama kuacha mafua,lakini virus bado unavyo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa hiyo huo usaidizi una maana gani mkuu?. Ni sawa na kuongeza kinga mwilini tu,lakini utakufa au ikoje?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bado hujanijibu mkuu. “ukiwa na kinga nzuri baada ya muda unakuwa sawa”. Unakuwa sawa ndio kusemaje? Kupona ama kuacha mafua,lakini virus bado unavyo?

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuwa sawa/timamu maana yake kinga ya mwili imeweza kuvikabili virusi na mtu kupona kabisa...

Kuna watu ambao wanapona kabisa, maambukizi yanaondoka mwilini mwao...

Kuna kitu kimoja sijajua vizuri bado, naendelea kufuatilia. Nacho ni iwapo mtu aliyepona je mwili utatengeneza kinga ya kudumu au maambukizi yanaweza mrudia tena akiwa exposed!
 
Asante mkuu. Fuatilia mpaka mwisho nijulishe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kutokana na report kamaili ni yanaweza kukurudia
Na yakikurudia ni hatari zaid
Ni kama mafua, inaweza kukurudia kama kawaida
Sent using Jamii Forums mobile app
 
UPDATE: Uhispania

Visa vipya 609 pamoja na vifo vipya 58 vimeripotiwa nchini humo hivi punde.

Mpaka sasa, idadi ya visa vyote nchini humo imefikia 5,841 huku vifo vikifikia 191.

Serikali ya nchi hiyo imepanga kufungwa kwa nchi nzima kuanzia Jumatatu asubuhi wiki ijayo ili kupunguza na kukabiliana na mlipuko wa virusi vya Corona nchini humo, vyombo vya habari vya ndani vimeripoti.
 
Kwa hiyo huo usaidizi una maana gani mkuu?. Ni sawa na kuongeza kinga mwilini tu,lakini utakufa au ikoje?

Sent using Jamii Forums mobile app
Huo usaidizi ama kwa kitaalamu 'Supportive care' unafanyika kwa wagonjwa wenye dalili za COVID-19 na hujumuisha mambo yafuatayo;

1. Uongezwaji wa maji ndani ya mwili ili kukabiliana na upungufu wa maji mwilini.

2. Usaidizi wa kupumua kwa kutumia vifaa maalumu (oksijeni).

3. Usaidizi katika viungo ama ogani za mwili (vital organs) zenye dalili za kushindwa kufanya kazi; mapafu, figo, ini, moyo n.k. kwa kutumia vifaa maalumu vya kitabibu.

4. Mchanganyiko wa dawa mbalimbali ili kutibu hizo dalili. Dawa zinazotumika ni zile zitumikazo kutibu maradhi mengine kama vile Ebola n.k.

Kinachotibiwa ni dalili tu ila kirusi kinaendelea kuwepo ndani ya mwili maana bado hakuna dawa ya kuweza kukiangamiza kabisa isipokuwa ni uwezo wa mwili wa mgonjwa kuweza kuvithibiti virusi hivyo ili visishambulie mwili na kuleta tena dalili.

Pia, kuna wanaopona dalili hizo lakini kwa mujibu wa tafiti zilizopo, wanaweza kubakia na matatizo mengine ya kudumu katika mifumo yao ya mwili ama ogani zao kutokana na madhara yaliyosababishwa na virusi hivyo isitoshe pia kuna visa vya watu kuambukizwa tena ama kwa mara nyingine.

Bado utafiti zaidi unaendelea kuhusiana na kirusi hiki pamoja na tabia zake maana kuna mambo mengi yahusuyo kirusi hiki bado hayajafahamika kitaalamu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…