Fahamu kinachojiri kuhusiana na kirusi cha Corona (Coronavirus)

Mkuu FRANC THE GREAT umefanya kazi kubwa,nzuri na ya kutukuka sana ya kutupa taarifa mbali mbali ya nini kinachojiri kuhusiana na virusi vya korona tena kwa ufanisi mzuri tangu mwanzo.

Sasa basi binafsi yangu na kwa niaba ya wafuatiliaji wako,licha ya changamoto ya hapa na pale nakuomba uendelee kutuwekea updates ya nini kinachoendelea ili tuzidi kuhabarika na kupata elimu zaidi na zaidi ya nini kifanyike.

Natanguliza shukrani[emoji120]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwamtazamo wangu, Uhai ni kitu yenye thamani kubwa zaidi, na bila uhai hatuwezi kufanya lolote. Uhai napo toweka hauwezi kurudishwa kwa njia yoyote ya kibinadamu.

Uhai wetu ukiwa hatarini, tunafanya lolote tuwezalo kwa kufaa ili kuuhifadhi. Kwani, wengine hata wataomba msaada upitao uwezo wa kibinadamu wanapokuwa taabani.
 
Awali ya yote niwape pole wakazi wa Arusha kwa taharuki iliyowakumba pamoja na nchi yote kwa ujumla.
Tukio la kugundulika mgonjwa wa Corona ni pigo kubwa katika jamii yetu kiuchumi na kijamii, shughuli nyingi za kiuchumi na kijamii zimeanza kuyumba.
Hii ni kutokana na historia mbaya ya gonjwa hili la kutisha.

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza, nimesikitishwa sana na kiongozi/mwenyekiti wa ulinzi na usalama ambavyo hajaonyesha umakini na unyeti katika gonjwa hili.

Tizama video ili twende pamoja


Mh. Gambo alipokwenda kwenye tukio hotelini/Lodge ya Themi valley plot no 120, akiongozana na RPC na maafisa wengine wa jeshi, wameenda kama vile wanaenda kuigiza..location.
Hii ni kutokana na wao kutovalia vifaa vya kujikinga.

Maafisa wa Polisi pamoja na Gambo mwenyewe wengi wao aidha wamevaa mask pekee bila kuvaa gloves au kutokuvaa vyote kabisa.

Hii inasikitisha kwani wao ndio wanapaswa kuwa mfano kwa kizazi cha kibongo kisichojua chochote katika kujikinga na gonjwa hili.

NATOA RAI SI KWA GAMBO PEKEE BALI KWA VIONGOZI WOTE KUWA MFANO WA KUIGWA KWA KUVAA VIFAA MAHUSUSI VYA KUJIKINGA NA GONJWA HILI

Poleni Themi Valley lodge, mna mandhari nzuri, kuna wakati mlinifaa sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mh. Richard Kasesela amesema hakuna mgonjwa wa Corona mkoani kwake na kwamba taarifa zinazosikika ni uzushi mtupu.

Kasesela amesema ni kosa la jinai kwa mtu yoyote kutangaza kuwepo kwa mgonjwa wa Corona kwani hilo ni jukumu la Waziri wa Afya pekee.

Source: Channel Ten
 
Huyo nae ni mkuu wa wilaya? sasa taarifa itawafikiaje jamii kwa uharaka
 
Kosa la jinai kutangaza corona wakati tumetangaziwa dalili...utopolo mtupu
 
Kosa la jinai kutangaza corona wakati tumetangaziwa dalili...utopolo mtupu
 
Huo ujinga ndio ulio tufikisha hapa kujifanya wasiri wakati tatizo linatutafuna kuna haja ya viongozi kubadili mtazamo wao taarifa ikitolewa uchunguzwe na si kutoa vitisho,

Watu watakaa kimya na tatizo litakuwa kubwa zaid
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…