Fahamu kinachojiri kuhusiana na kirusi cha Corona (Coronavirus)

Fahamu kinachojiri kuhusiana na kirusi cha Corona (Coronavirus)

Taarifa zisizo rasmi zinadai wanajeshi takribani 180 wa Korea Kaskazini wamekufa kutokana na virusi vya Corona katika mwezi wa Januari na Februari huku wengine maelfu wakiwa karantini.

Serikali bado haijatoa ripoti yeyote ile kuhusiana na visa wala vifo nchini humo.
Aisee!
 
Na kama hii Corona ilikuwa ni engineered virus, hakika walioitengeneza watajuta mpaka basi!!
 
NEWS ALERT: Man City's Benjamin Mendy is self-isolating as a precaution. A member of his family was admitted to hospital displaying symptoms of coronavirus. [BBC]

1584082919842.png
 
Wachina inaelekea wameamua kila siku ipitayo waripoti visa vichache vichache ili kuuaminisha umma wao na ulimwengu kuwa wameuthibiti ugonjwa.

Huu ugonjwa uliathiri sana heshima na utu wa mchina duniani, sasa nadhani serikali yao imeamua kushusha data ili kuuonyesha ulimwengu kuwa this is not China virus but Whole world virus.
 
UPDATE: Australia

Visa vyote nchini humo vimefikia 156 hadi sasa huku wagonjwa 26 wakiripotiwa kupata ahueni.

Hadi sasa, Australia imeripoti vifo vitatu (3) vinavyohusishwa na ugonjwa wa virusi vya Corona (COVID-19).

Waziri wa mambo ya ndani wa nchi hiyo, Peter Dutton, amebainika kuwa na maambukizi ya virusi vya Corona.
 
Weka data kuthibitisha hilo......
Wachina inaelekea wameamua kila siku ipitayo waripoti visa vichache vichache ili kuuaminisha umma wao na ulimwengu kuwa wameuthibiti ugonjwa.

Huu ugonjwa uliathiri sana heshima na utu wa mchina duniani, sasa nadhani serikali yao imeamua kushusha data ili kuuonyesha ulimwengu kuwa this is not China virus but Whole world virus.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
UPDATE: Barani Afrika

1. Misri imeripoti visa vipya 13 nchini humo pamoja na kifo kipya kimoja (1). Idadi ya visa vyote nchini humo imefikia 80 hadi sasa.

2. Ivory Coast imeripoti kisa cha kwanza nchini humo. Raia wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 45 ambaye alisafiri kuelekea nchini Italia hivi karibuni.

3. Gabon imeripoti kisa cha kwanza nchini humo. Kisa hicho ni raia wa Gabon mwenye miaka 27 aliyerejea nchini humo mnamo Machi 8 akitokea nchini Ufaransa.

4.Ghana imeripoti visa vya kwanza viwili (2) nchini humo. Wawili hao walirejea nchini humo wakitokea katika mataifa ya Norway na Uturuki.

Hadi saa nchi zipatazo kumi (10) za kusini mwa jangwa la Sahara zimekwisha ripoti visa vya COVID-19 katika nchi zao; Ivory Coast, Nigeria, Senegal, Cameroon, Togo, Afrika Kusini, Burkina Faso, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Gabon pamoja na Ghana.
 
BREAKING: Kisa cha kwanza nchini Kenya

Wizara tya afya ya nchi hiyo imethibitisha kisa cha kwanza cha virusi vya Corona nchini humo.

Kisa hicho ni raia wa Kenya aliyerejea nchini humo mnamo Machi 5 akitokea nchini Marekani kupitia London, Uingereza.

Mgonjwa yuko katika hali nzuri.
 
NEWS ALERT: Kenya's Ministry of health has confirmed the first coronavirus case in Kenya. The Kenyan citizen returning from the US to Nairobi via London on 5th March. She was confirmed positive by the national influenza lab. However, the patient is stable. [Citizen TV]
 
Back
Top Bottom