Fahamu kuhusu Fao la Kukosa Ajira Tanzania (Unemployment Benefit)

Fahamu kuhusu Fao la Kukosa Ajira Tanzania (Unemployment Benefit)

DOMINGO THOMAS

JF-Expert Member
Joined
Feb 16, 2023
Posts
365
Reaction score
365
Fao la Kukosa Ajira ni faida/msaada wa kifedha unaotolewa kwa mwanachama wa mfuko wa pensheni aliyepoteza ajira kwa sababu zisizo za hiari, kama vile kufukuzwa kazi, kuisha kwa mkataba, au sababu nyingine za halali. Hata hivyo, fao hili halitolewi kwa mtu aliyeacha kazi kwa hiari, kwani kufanya hivyo humfanya apoteze sifa za kupata fao hili.

Sifa za Kupata Fao la Kukosa Ajira

Umri: Mtu anayestahili fao hili anatakiwa kuwa chini ya umri wa miaka 55, ikiwa umepoteza kazi na umri wako ni zaidi ya miaka 55 basi italazimika ulipwe fao la uzee (Old age pension)

Mchango: Fao hili ulipwa kwa Mwanachama aliye changia kwenye mfuko chini ya miezi 180, ikiwa umechangia zaidi ya miezi 180 na uko chini ya miaka 55 ukapoteza ajira, basi utalipwa pensheni iliyo cheleweshwa, (differed pension).

Sababu za Kupoteza Ajira: Ajira inatakiwa kuwa imekoma kwa sababu zisizo za hiari kama vile: kufukuzwa kazi, Mkataba kuisha, au kupunguzwa kazini (retrenchment).

Malipo ya Fao la Kukosa Ajira
Fao la kukosa ajira hulipwa kwa awamu mbili. Kwa Aliyechangia Zaidi ya Miezi 18: Malipo ya Awamu ya Kwanza: Unalipwa 33.3% ya mshahara wako wa mwisho kwa kipindi cha miezi 6. Baada ya Malipo ya Kwanza: utakuwa na kipindi cha miezi 18 (miaka miwili) cha kutafuta ajira, ukipata ajira, utaendelea kuchangia katika mfuko pale ulipoishia na ikitokea umekosa ajira ndani ya kipindi hiki, utaandika barua kwenda kwa Mkurugenzi mkuu wa mfuko kuhama uchangiaji, toka uchangiaji wa lazima kwenda hiari, baada ya kuhama uchangiaji unaweza endelea kujichangia mwenyewe au utaruhusiwa kuchukua kiasi kilichobaki kwenye mfuko.

Kwa Aliyechangia Chini ya Miezi 18: Malipo: Utalipwa nusu ya kiasi ulichochangia kwenye mfuko. Baada ya Malipo: utakuwa na kipindi cha miezi 18 (Miaka miwili) cha kutafuta ajira. Ukipata ajira, utaendelea kuchangia pale ulipoishia, na Ukikosa ajira ndani ya kipindi hiki, utaandika barua kwenda kwa Mkurugenzi mkuu wa mfuko kuhama uchangiaji, toka uchangiaji wa lazima kwenda hiari, baada ya kuhama uchangiaji unaweza endelea kujichangia mwenyewe kwa mfumo wa hiari au kuchukua kiasi kilichobaki kwenye mfuko.

Pia malipo ya fao la kukosa ajira yanatofautina kwa mtu mwenye ujuzi (skilled) na Mtu asiye na ujuzi (Unskilled) kwa mtu asiye na ujuzi yeye hulipwa kiasi chote alicho changia kwenye mfuko na mwenye ujuzi yeye hulipwa kwa kufuata maelekezo hayo juu, hii ni kwasababu ni ngumu mtu asiye na ujuzi kupata ajira kwa urahisi ukilinganisha na mtu mwenye ujuzi

Kumbuka: Malipo ya fao la kukosa ajira yatakoma pale tu unapo pata ajira nyingine.

Sababu za Malipo Kufanyika kwa Awamu

Mfumo wa malipo kwa awamu una lengo la kuhakikisha mwanachama anaendelea kuwa na sifa za kupata pensheni ya uzee. Kama kiasi chote kingetolewa mara moja, kuna hatari ya mwanachama kufika umri wa kustaafu bila kufikia michango ya miezi 180 inayotakiwa kwa ajili ya pensheni ya uzee.

Hivyo, malipo kwa awamu yanasaidia kulinda michango iliyopo ili mwanachama awe na nafasi ya kufanikisha sifa za pensheni ya uzee.

Faida ya Fao la Kukosa Ajira

Hutoa msaada wa kifedha kwa kipindi cha mpito baada ya kupoteza ajira. Hakuna kupunguzwa kwa michango ya awali kwenye mfuko, Mfano: Ulikuwa na michango 20, ukalipwa fao la kukosa ajira, lakini hukuchukua kiasi chote. Ukipata ajira mpya, utaanza kuchangia kuanzia mchango wa 21 na kuendelea.

Kumbuka: Fao hili ni haki ya mwanachama aliyepoteza ajira kwa sababu halali zilizopo kwenye sheria, Mchakato wa kudai fao hili unahitaji nyaraka zinazothibitisha hali ya kuachishwa kazi kama barua ya kusitishwa kwa ajira.
 
Fao la Kukosa Ajira ni faida/msaada wa kifedha unaotolewa kwa mwanachama wa mfuko wa pensheni aliyepoteza ajira kwa sababu zisizo za hiari, kama vile kufukuzwa kazi, kuisha kwa mkataba, au sababu nyingine za halali. Hata hivyo, fao hili halitolewi kwa mtu aliyeacha kazi kwa hiari, kwani kufanya hivyo humfanya apoteze sifa za kupata fao hili.

Sifa za Kupata Fao la Kukosa Ajira

Umri: Mtu anayestahili fao hili anatakiwa kuwa chini ya umri wa miaka 55, ikiwa umepoteza kazi na umri wako ni zaidi ya miaka 55 basi italazimika ulipwe fao la uzee (Old age pension)

Mchango: Fao hili ulipwa kwa Mwanachama aliye changia kwenye mfuko chini ya miezi 180, ikiwa umechangia zaidi ya miezi 180 na uko chini ya miaka 55 ukapoteza ajira, basi utalipwa pensheni iliyo cheleweshwa, (differed pension).

Sababu za Kupoteza Ajira: Ajira inatakiwa kuwa imekoma kwa sababu zisizo za hiari kama vile: kufukuzwa kazi, Mkataba kuisha, au kupunguzwa kazini (retrenchment).

Malipo ya Fao la Kukosa Ajira

Fao la kukosa ajira hulipwa kwa awamu mbili.
Kwa Aliyechangia Zaidi ya Miezi 18: Malipo ya Awamu ya Kwanza: Unalipwa 33.3% ya mshahara wako wa mwisho kwa kipindi cha miezi 6. Baada ya Malipo ya Kwanza: utakuwa na kipindi cha miezi 18 (miaka miwili) cha kutafuta ajira, ukipata ajira, utaendelea kuchangia katika mfuko pale ulipoishia. na ikitokea umekosa ajira ndani ya kipindi hiki, utaandika barua kwenda kwa Mkurugenzi mkuu wa mfuko kuhama uchangiaji, toka uchangiaji wa lazima kwenda hiari, baada ya kuhama uchangiaji unaweza endelea kujichangia mwenyewe au utaruhusiwa kuchukua kiasi kilichobaki kwenye mfuko.

Kwa Aliyechangia Chini ya Miezi 18: Malipo: Utalipwa nusu ya kiasi ulichochangia kwenye mfuko. Baada ya Malipo: utakuwa na kipindi cha miezi 18 (Miaka miwili) cha kutafuta ajira. Ukipata ajira, utaendelea kuchangia pale ulipoishia, na Ukikosa ajira ndani ya kipindi hiki, utaandika barua kwenda kwa Mkurugenzi mkuu wa mfuko kuhama uchangiaji, toka uchangiaji wa lazima kwenda hiari, baada ya kuhama uchangiaji unaweza endelea kujichangia mwenyewe kwa mfumo wa hiari au kuchukua kiasi kilichobaki kwenye mfuko.

Pia malipo ya fao la kukosa ajira yanatofautina kwa mtu mwenye ujuzi (skilled) na Mtu asiye na ujuzi (Unskilled) kwa mtu asiye na ujuzi yeye hulipwa kiasi chote alicho changia kwenye mfuko na mwenye ujuzi yeye hulipwa kwa kufuata maelekezo hayo juu, hii ni kwasababu ni ngumu mtu asiye na ujuzi kupata ajira kwa urahisi ukilinganisha na mtu mwenye ujuzi

Kumbuka: Malipo ya fao la kukosa ajira yatakoma pale tu unapo pata ajira nyingine.

Sababu za Malipo Kufanyika kwa Awamu

Mfumo wa malipo kwa awamu una lengo la kuhakikisha mwanachama anaendelea kuwa na sifa za kupata pensheni ya uzee. Kama kiasi chote kingetolewa mara moja, kuna hatari ya mwanachama kufika umri wa kustaafu bila kufikia michango ya miezi 180 inayotakiwa kwa ajili ya pensheni ya uzee.

Hivyo, malipo kwa awamu yanasaidia kulinda michango iliyopo ili mwanachama awe na nafasi ya kufanikisha sifa za pensheni ya uzee.

Faida ya Fao la Kukosa Ajira

Hutoa msaada wa kifedha kwa kipindi cha mpito baada ya kupoteza ajira. Hakuna kupunguzwa kwa michango ya awali kwenye mfuko, Mfano: Ulikuwa na michango 20, ukalipwa fao la kukosa ajira, lakini hukuchukua kiasi chote. Ukipataujui hii kitu ajira mpya, utaanza kuchangia kuanzia mchango wa 21 na kuendelea.

Kumbuka: Fao hili ni haki ya mwanachama aliyepoteza ajira kwa sababu halali zilizopo kwenye sheria, Mchakato wa kudai fao hili unahitaji nyaraka zinazothibitisha hali ya kuachishwa kazi kama barua ya kusitishwa kwa ajira.
Nilikuwa sijui leo umenifundishaa kitu
 
Back
Top Bottom