Fahamu kuhusu Fao la Kukosa Ajira Tanzania (Unemployment Benefit)

Fahamu kuhusu Fao la Kukosa Ajira Tanzania (Unemployment Benefit)

Ni Faida/Msaada kwa maana ya kwamba, ukipata ajira utaendelea kuchangia pale ulipo ishia, na ikitokea amestaafu kile kiasi/kiwango ulicho lipwa hakita tolewa/punguzwa kwenye malipo ya pensheni.
Msaada kwenye Tuta..mfano nimechangia miezi 180 ambayo naona Ni miaka 15 nikaachishwa kazi...Je naweza kuingia kwenye mfumo Wa pension Hadi nakufa???
 
Hapana, baada ya kulipwa 33.3% ya mshahara wako wa mwisho, utasubiri miezi 18+ ukitafuta ajira, ukikosa ndio utaruhusiwa kuchukua kiasi kilichobaki
Je unaruhusiwa kuchukua kiasi chote baki I mean Kuchukua rumpsum
 
Fao la Kukosa Ajira ni faida/msaada wa kifedha unaotolewa kwa mwanachama wa mfuko wa pensheni aliyepoteza ajira kwa sababu zisizo za hiari, kama vile kufukuzwa kazi, kuisha kwa mkataba, au sababu nyingine za halali. Hata hivyo, fao hili halitolewi kwa mtu aliyeacha kazi kwa hiari, kwani kufanya hivyo humfanya apoteze sifa za kupata fao hili.

Sifa za Kupata Fao la Kukosa Ajira

Umri: Mtu anayestahili fao hili anatakiwa kuwa chini ya umri wa miaka 55, ikiwa umepoteza kazi na umri wako ni zaidi ya miaka 55 basi italazimika ulipwe fao la uzee (Old age pension)

Mchango: Fao hili ulipwa kwa Mwanachama aliye changia kwenye mfuko chini ya miezi 180, ikiwa umechangia zaidi ya miezi 180 na uko chini ya miaka 55 ukapoteza ajira, basi utalipwa pensheni iliyo cheleweshwa, (differed pension).

Sababu za Kupoteza Ajira: Ajira inatakiwa kuwa imekoma kwa sababu zisizo za hiari kama vile: kufukuzwa kazi, Mkataba kuisha, au kupunguzwa kazini (retrenchment).

Malipo ya Fao la Kukosa Ajira
Fao la kukosa ajira hulipwa kwa awamu mbili. Kwa Aliyechangia Zaidi ya Miezi 18: Malipo ya Awamu ya Kwanza: Unalipwa 33.3% ya mshahara wako wa mwisho kwa kipindi cha miezi 6. Baada ya Malipo ya Kwanza: utakuwa na kipindi cha miezi 18 (miaka miwili) cha kutafuta ajira, ukipata ajira, utaendelea kuchangia katika mfuko pale ulipoishia na ikitokea umekosa ajira ndani ya kipindi hiki, utaandika barua kwenda kwa Mkurugenzi mkuu wa mfuko kuhama uchangiaji, toka uchangiaji wa lazima kwenda hiari, baada ya kuhama uchangiaji unaweza endelea kujichangia mwenyewe au utaruhusiwa kuchukua kiasi kilichobaki kwenye mfuko.

Kwa Aliyechangia Chini ya Miezi 18: Malipo: Utalipwa nusu ya kiasi ulichochangia kwenye mfuko. Baada ya Malipo: utakuwa na kipindi cha miezi 18 (Miaka miwili) cha kutafuta ajira. Ukipata ajira, utaendelea kuchangia pale ulipoishia, na Ukikosa ajira ndani ya kipindi hiki, utaandika barua kwenda kwa Mkurugenzi mkuu wa mfuko kuhama uchangiaji, toka uchangiaji wa lazima kwenda hiari, baada ya kuhama uchangiaji unaweza endelea kujichangia mwenyewe kwa mfumo wa hiari au kuchukua kiasi kilichobaki kwenye mfuko.

Pia malipo ya fao la kukosa ajira yanatofautina kwa mtu mwenye ujuzi (skilled) na Mtu asiye na ujuzi (Unskilled) kwa mtu asiye na ujuzi yeye hulipwa kiasi chote alicho changia kwenye mfuko na mwenye ujuzi yeye hulipwa kwa kufuata maelekezo hayo juu, hii ni kwasababu ni ngumu mtu asiye na ujuzi kupata ajira kwa urahisi ukilinganisha na mtu mwenye ujuzi

Kumbuka: Malipo ya fao la kukosa ajira yatakoma pale tu unapo pata ajira nyingine.

Sababu za Malipo Kufanyika kwa Awamu

Mfumo wa malipo kwa awamu una lengo la kuhakikisha mwanachama anaendelea kuwa na sifa za kupata pensheni ya uzee. Kama kiasi chote kingetolewa mara moja, kuna hatari ya mwanachama kufika umri wa kustaafu bila kufikia michango ya miezi 180 inayotakiwa kwa ajili ya pensheni ya uzee.

Hivyo, malipo kwa awamu yanasaidia kulinda michango iliyopo ili mwanachama awe na nafasi ya kufanikisha sifa za pensheni ya uzee.

Faida ya Fao la Kukosa Ajira

Hutoa msaada wa kifedha kwa kipindi cha mpito baada ya kupoteza ajira. Hakuna kupunguzwa kwa michango ya awali kwenye mfuko, Mfano: Ulikuwa na michango 20, ukalipwa fao la kukosa ajira, lakini hukuchukua kiasi chote. Ukipata ajira mpya, utaanza kuchangia kuanzia mchango wa 21 na kuendelea.

Kumbuka: Fao hili ni haki ya mwanachama aliyepoteza ajira kwa sababu halali zilizopo kwenye sheria, Mchakato wa kudai fao hili unahitaji nyaraka zinazothibitisha hali ya kuachishwa kazi kama barua ya kusitishwa kwa ajira.
Kama nimechangia miezi 180 plus nikafukuzwa kazi nikiwa chini ya umri wa miaka 55,,hapo stahiki zangu zitakuaje? Maelezo tafadhari.
 
Hapana, baada ya kulipwa 33.3% ya mshahara wako wa mwisho, utasubiri miezi 18+ ukitafuta ajira, ukikosa ndio utaruhusiwa kuchukua kiasi kilichobaki
Je naweza kuchukua hiyo 33.3% Kwa mkupuo wa miezi 6 au ni mpaka Kila mwezi ndani ya miezi hiyo 6?
 
Elimu nzuri ila hapo tu kwenye "msaada" ndo mgogoro, zile hela ni za mwanachama na si msaada na ikipita miezi 18 unalipwa kiasi ulichochangia na wanatoa hiyo 33% ya mshahara wako waliokulipa miezi 6.
Wanaita Msaada Kwa sababu ukipata Ajira hawazikati kwamba eti ulishalipwa bali itaendelea ulipoishia.
 
Okay ......hii ela iliniumiza aisee sintosahau yaani nilikuwa apeche alolo 2019 nikatia timu NSSF nikakutana na hii dhahama ya fao la kukosa ajira wakati mie nataka nivute yote. Mwisho wa siku ikabidi nichukue fao la kukosa ajira na nilivyomaliza nikawa napambana nilipwe zilizobaki hata kwa kujifanya mgonjwa lakini wapi, kumbuka kipindi hicho hata staffs wa NSSF hawakuwa na maelezo ya what next ukishalipwa fao la kukosa ajira miezi sita. Nimekuja kugundua kwamba baada ya miezi 18 unalipwa baada ya kusota sana ndo kuna staff akanambia maana wengine walikuwa wanarukaruka the si unajua enzi zile mzee baba Magu alikuwepo.

Nikasubiri miezi 18 nikavuta mkwanja wangu nikaacuana nao
Hela uliyovuta baada ya miezi 18 walikata Yale malipo ya awali ya 33.3% ndio ukalipwa kilichobaki ama ilikuaje?
 
Hapo watakuwa wamekupa ya mwezi wa 11 na 12, I guess walichelewa kuchakata maana kama uliondoka kazini tarehe 30 Sept maana yake huwa inachukua mwezi process yote kukamilika....hivyo kifuatapo hapo utakuwa unalipwa mwezi mmoja mmoja mpaka hiyo miezi 6 iishe
Kwa nini wasilipe ya miezi 6 yote badala ya mwezi mmja mmja manake Haina Tija
 
Hii sheria inawaumiza watu wa Mkataba.Nimewahi fanya kazi kampuni binafsi kabla ya mambo kuvurugika awamu ya 5 ,baada ya kazi kuisha walinilipa hela zangu zote ndani ya mwezi 1 tuu ,ilikuwa PPF saizi haipo.
 
Serikali haina huruma kabisa wabunge wanalipana mafao zaidi ya 200M wakimaliza tu miaka yao 5, lakini Mtanzania anae lipwa laki 5 anaambiwa apewe 33.3% nyingine asubiri miezi 18, hii nchi hii ina viongozi wa hovyo sana , vitu vingine hata mtoto wa darasa la 7 anaweza kuwazidi akili
 
Fao la Kukosa Ajira ni faida/msaada wa kifedha unaotolewa kwa mwanachama wa mfuko wa pensheni aliyepoteza ajira kwa sababu zisizo za hiari, kama vile kufukuzwa kazi, kuisha kwa mkataba, au sababu nyingine za halali. Hata hivyo, fao hili halitolewi kwa mtu aliyeacha kazi kwa hiari, kwani kufanya hivyo humfanya apoteze sifa za kupata fao hili.

Sifa za Kupata Fao la Kukosa Ajira

Umri: Mtu anayestahili fao hili anatakiwa kuwa chini ya umri wa miaka 55, ikiwa umepoteza kazi na umri wako ni zaidi ya miaka 55 basi italazimika ulipwe fao la uzee (Old age pension)

Mchango: Fao hili ulipwa kwa Mwanachama aliye changia kwenye mfuko chini ya miezi 180, ikiwa umechangia zaidi ya miezi 180 na uko chini ya miaka 55 ukapoteza ajira, basi utalipwa pensheni iliyo cheleweshwa, (differed pension).

Sababu za Kupoteza Ajira: Ajira inatakiwa kuwa imekoma kwa sababu zisizo za hiari kama vile: kufukuzwa kazi, Mkataba kuisha, au kupunguzwa kazini (retrenchment).

Malipo ya Fao la Kukosa Ajira
Fao la kukosa ajira hulipwa kwa awamu mbili. Kwa Aliyechangia Zaidi ya Miezi 18: Malipo ya Awamu ya Kwanza: Unalipwa 33.3% ya mshahara wako wa mwisho kwa kipindi cha miezi 6. Baada ya Malipo ya Kwanza: utakuwa na kipindi cha miezi 18 (miaka miwili) cha kutafuta ajira, ukipata ajira, utaendelea kuchangia katika mfuko pale ulipoishia na ikitokea umekosa ajira ndani ya kipindi hiki, utaandika barua kwenda kwa Mkurugenzi mkuu wa mfuko kuhama uchangiaji, toka uchangiaji wa lazima kwenda hiari, baada ya kuhama uchangiaji unaweza endelea kujichangia mwenyewe au utaruhusiwa kuchukua kiasi kilichobaki kwenye mfuko.

Kwa Aliyechangia Chini ya Miezi 18: Malipo: Utalipwa nusu ya kiasi ulichochangia kwenye mfuko. Baada ya Malipo: utakuwa na kipindi cha miezi 18 (Miaka miwili) cha kutafuta ajira. Ukipata ajira, utaendelea kuchangia pale ulipoishia, na Ukikosa ajira ndani ya kipindi hiki, utaandika barua kwenda kwa Mkurugenzi mkuu wa mfuko kuhama uchangiaji, toka uchangiaji wa lazima kwenda hiari, baada ya kuhama uchangiaji unaweza endelea kujichangia mwenyewe kwa mfumo wa hiari au kuchukua kiasi kilichobaki kwenye mfuko.

Pia malipo ya fao la kukosa ajira yanatofautina kwa mtu mwenye ujuzi (skilled) na Mtu asiye na ujuzi (Unskilled) kwa mtu asiye na ujuzi yeye hulipwa kiasi chote alicho changia kwenye mfuko na mwenye ujuzi yeye hulipwa kwa kufuata maelekezo hayo juu, hii ni kwasababu ni ngumu mtu asiye na ujuzi kupata ajira kwa urahisi ukilinganisha na mtu mwenye ujuzi

Kumbuka: Malipo ya fao la kukosa ajira yatakoma pale tu unapo pata ajira nyingine.

Sababu za Malipo Kufanyika kwa Awamu

Mfumo wa malipo kwa awamu una lengo la kuhakikisha mwanachama anaendelea kuwa na sifa za kupata pensheni ya uzee. Kama kiasi chote kingetolewa mara moja, kuna hatari ya mwanachama kufika umri wa kustaafu bila kufikia michango ya miezi 180 inayotakiwa kwa ajili ya pensheni ya uzee.

Hivyo, malipo kwa awamu yanasaidia kulinda michango iliyopo ili mwanachama awe na nafasi ya kufanikisha sifa za pensheni ya uzee.

Faida ya Fao la Kukosa Ajira

Hutoa msaada wa kifedha kwa kipindi cha mpito baada ya kupoteza ajira. Hakuna kupunguzwa kwa michango ya awali kwenye mfuko, Mfano: Ulikuwa na michango 20, ukalipwa fao la kukosa ajira, lakini hukuchukua kiasi chote. Ukipata ajira mpya, utaanza kuchangia kuanzia mchango wa 21 na kuendelea.

Kumbuka: Fao hili ni haki ya mwanachama aliyepoteza ajira kwa sababu halali zilizopo kwenye sheria, Mchakato wa kudai fao hili unahitaji nyaraka zinazothibitisha hali ya kuachishwa kazi kama barua ya kusitishwa kwa ajira.
MKUU MFANO,MTU ALIKUWA ANAFANYA KAZI YA KUFUNDISHA,MKATABA UKAISHA,NA HAKUPEWA MWINGINE,BALI AKAPEWA BARUA YA KUMALIZA MKATABA NA ALIKUWA ANACHANGIA,AKIWA LABDA MKOA X.

JE,AKITAKA KUOMBA STAHIKI HIZI MPAKA AOMBEE OFISI ZA MKOA HUOHUO X AU HATA AKIWA MKOA Y ANAWEZA KUOMBEA OFISI ZA HUKO?

NA UTARATIBU WA KUOMBA HIZI STAHIKI UKOJE YAANI UNAANZIA WAPI?
 
Msaada kwenye Tuta..mfano nimechangia miezi 180 ambayo naona Ni miaka 15 nikaachishwa kazi...Je naweza kuingia kwenye mfumo Wa pension Hadi nakufa???
Kama umechangia miaka 15+ (Miezi 180) kazi ikifika Ukomo na una miaka 55+ wewe utalipwa kiinua mgongo na pensheni ya Kila mwezi mpaka kufa, lakini ukiwa chini ya miaka 55 utalipwa kwanza kiinua mgongo alafu utasubiri utaratibu wa pensheni ya Kila mwezi ukifika miaka 55
 
Kama umechangia miaka 15+ (Miezi 180) kazi ikifika Ukomo na una miaka 55+ wewe utalipwa kiinua mgongo na pensheni ya Kila mwezi mpaka kufa, lakini ukiwa chini ya miaka 55 utalipwa kwanza kiinua mgongo alafu utasubiri utaratibu wa pensheni ya Kila mwezi ukifika miaka 55
 
Back
Top Bottom