Fahamu kuhusu Fao la Kukosa Ajira Tanzania (Unemployment Benefit)

Unampa mtu 33.3% ya mshahara wake wa mwisho laki 3, sasa pesa itamfikisha wapi? Huu si uhuni , mtu anateseka wakati pesa yake wamekalia NSSF wanatumia tu
Dhima na madhumuni ya kufanya hivyo yalikuwa ni mazuri tu, kumlinda mwanachama asipoteze sifa ya kuwa pensioner
 
Kama nimechangia miezi 180 plus nikafukuzwa kazi nikiwa chini ya umri wa miaka 55,,hapo stahiki zangu zitakuaje? Maelezo tafadhari.
Kama umechangia miaka 15+ (Miezi 180) kazi ikifika Ukomo na una miaka 55+ wewe utalipwa kiinua mgongo na pensheni ya Kila mwezi mpaka kufa, lakini ukiwa chini ya miaka 55 utalipwa kwanza kiinua mgongo alafu utasubiri utaratibu wa pensheni ya Kila mwezi ukifika miaka 55
 
Je naweza kuchukua hiyo 33.3% Kwa mkupuo wa miezi 6 au ni mpaka Kila mwezi ndani ya miezi hiyo 6?
Kama uliomba fao la kukosa ajira baada ya miezi 6 kupita toka ajira yako ifike ukomo, hiyo 33.3% utalipwa kwa mkupuo
 
Natarajia kufanya vituko Ili niachishwe kazi 2035,by that time nitakuwa below 50 lakini nitakuwa nimechangia zaidi ya miezi 180.
 
Ni somo zuri sana lakini sijaelewa kwa nini kuna watu wame-dislike!
 
Hii sheria inawaumiza watu wa Mkataba.Nimewahi fanya kazi kampuni binafsi kabla ya mambo kuvurugika awamu ya 5 ,baada ya kazi kuisha walinilipa hela zangu zote ndani ya mwezi 1 tuu ,ilikuwa PPF saizi haipo.
Kivipi inawaumiza.....!?
 
Kivipi inawaumiza.....!?
Sasa unaanzaje kulipwa mdogo mdogo harafu unasubiria miezi 18 uanze upya kutafutiza huoni huo ni usumbufu na lolote linaweza tokea hapo katikati?

PPF waliwahi nipa hela yote Kwa mkupuo na ndio ulikuwa utaratibu wa awali.

Uzembe wa mifumo kukosa hela ndio umewashishia mzigo walioko kwenye Ajira za mkataba.

Harafu Serikali imerekwbisha sheria ya kikokotoo iliyolalamikiwa na wale permanent employee,Kwa nini wasirekebishe na Kwa temporary contract employees? Hapo unaona ni sawa?
 
Kitu ambacho unatakiwa kufahamu wabunge, madiwani, wakuu wa mikoa na wilaya sio wanachama wa PSSSF/NSSF na hawalipwi na hiyo mifuko
 
Dhima na madhumuni ya kufanya hivyo yalikuwa ni mazuri tu, kumlinda mwanachama asipoteze sifa ya kuwa pensioner
Mwanachama yupi wakati mikataba yenyewe uko private haieleweki? mkisha kuwa serikalini mnasahu kuwa waajiri huku ni wahindi na wachina, wanakutumia wanakupa laki 3 au 4 hakuna mikopo wala bonus, mtu anapotaka pesa yake apewe acheni usumbufu wakati ni pesa yake
 
Utaratibu wa kuomba mafao unaweza omba ukiwa mkoa wowote ule kwenye ofisi za mfuko husika, fika na barua yako ya ukomo wa mkataba na namba yako ya uanachama, utapewa utaratibu na fomu za kujaza.
 
Kitu ambacho unatakiwa kufahamu wabunge, madiwani, wakuu wa mikoa na wilaya sio wanachama wa PSSSF/NSSF na hawalipwi na hiyo mifuko
Kama wabunge wanalipwa kiinua mgongo chote, na mishahara yao ni mikubwa sana, sasa kona kona za nini kwa huyu mtoto wa masikini anaetaka kujikwamua kutoka kwenye kifungo cha wahindi? mnashangaa wagonjwa wa akili kuongezeka wakati nyie ndio tatizo, wapeni watu pesa zao wafanye biashara waokoe familia zao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…