Mr George Francis
JF-Expert Member
- Jun 27, 2022
- 234
- 376
FAHAMU KUHUSU MAKOSA YA RUSHWA NA ADHABU ZAKE KWA MUJIBU WA SHERIA
SEHEMU YA NNE (4)
mr.georgefrancis21@gmail.com
Ni siku nyingine tena tunakutana katika muendelezo wa mada yetu ambapo hapa tunapata elimu kuhusu makosa ya rushwa na adhabu zake kama kichwa cha somo kinavyoeleza.
Sasa bila kupoteza muda tuendelee na mada yetu kwa kuangazia makosa yafuatayo:
11. Umiliki wa mali ambazo upatikanaji wake haueleweki. Ni kosa kwa Mtumishi wa umma kuwa na mali au pesa nyingi zaidi kuliko kipato chake halali cha sasa au kilichopita na hana maelezo ya kuridhisha kuhusu alivyozipata.
Mahakama ikijiridhisha kuwa kuna mtu anamiliki mali au pesa fulani kwa niaba ya mtuhumiwa au alipewa hizo mali ambazo upatikanaji wake haueleweki kama zawadi kutoka kwa mtuhumiwa na kama hakuna ushahidi unaojitoshereza kuhalalisha umiliki wake basi mali hizo zitachukuliwa kuwa ni mali zinazomilikiwa na mtuhumiwa hivyo kuwa sehemu ya kesi husika inayomkabili mtuhumiwa.
✓ADHABU:
Mtu atakayekutwa na hatia ya kutenda kosa hili adhabu yake ni faini isiyozidi shilingi milioni kumi (10,000,000/=) au kifungo kisichozidi miaka saba (7) au vyote kwa pamoja.
• Lakini pamoja na adhabu hiyo Mahakama inaweza kuamuru mali hizo za mtuhumiwa zitaifishwe na kuwa mali za serikali. Kuhusiana na kosa hili kuna maelezo mengi muhimu, siwezi kuelezea kilakitu lakini ili kuongeza maarifa zaidi kuhusu kosa hili soma kifungu cha 27(1) hadi (9) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.
12. Matumizi mabaya ya mali za umma. Mtumishi wa umma au mtumishi katika taasisi binafsi ambaye kwa kukosa uaminifu au kwa udanganyifu akafuja mali za umma zilizowekwa chini yake au akabadilisha umiliki wa mali hizo na kuwa mali zake au akaruhusu mtu mwingine kufanya hivyo atakuwa anatenda kosa.
✓ADHABU:
Mtu yeyote anayekutwa na hatia ya kutenda kosa hili adhabu yake faini isiyozidi shilingi milioni kumi (10,000,000/=) au kifungo kisichozidi miaka saba (7) au vyote kwa pamoja.
• Pamoja na adhabu hii lakini pia Mahakama inaweza kuamuru kuwa mali zilizofujwa ama kubalidilishwa umiliki wake na mtuhumiwa zirejeshwe kwa mmiliki wake halali au mtuhumiwa kuamriwa kulipa fidia kama mali hizo hazipatikani.
Hapa pia kuna options nyingine ambazo Mahakama inaweza kuamua. Lakini ili kuongeza maarifa zaidi kuhusiana na kosa hili, hunabudi kusoma kifungu cha 28(1)(2)(3) &(4)(a)(b)(c)&(d) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.
13. Kubadilisha matumizi. Mtumishi wa umma au mtumishi wa taasisi binafsi anayebadilisha mali za serikali au idara ya serikali taasisi binafsi kutoka katika matumizi ya vile ilivyokusudiwa kuwa na kufanya kutumika kwa matumizi yake binafsi au kwa faida ya mtu mwingine kupitia nafasi yake atakuwa ametenda kosa.
✓ADHABU:
Mtu yeyote anayekutwa na hatia ya kutenda kosa hili adhabu yake ni faini isiyozidi shilingi milioni mbili (2,000,000/=) au kifungo kisichozidi miaka miwili (2) au vyote kwa pamoja. Hii ni kwa mujibu wa kifungu cha 29 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.
14. Kusaidia au kufadhili kutenda kosa. Mtu yeyote anayemsaidia au kufadhili mtu mwingine kutenda kosa la rushwa kinyume cha sheria hii ya kuzuia na Kupambana na Rushwa naye pia atakuwa ametenda kosa la rushwa.
✓ADHABU:
Ukikutwa na hatia ya kutenda kosa hili adhabu yake ni faini isiyozidi shilingi milioni mbili (2,000,000/=) au kifungo kisichozidi miaka miwili (2) au vyote kwa pamoja. Hii ni kwa mujibu wa kifungu cha 30 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.
Ahsante kwa kuendelea kuwa nami, tukutane katika sehemu inayofuata ya mada hii ili tumalizie mada yetu.
Mungu akubariki sana.
NAME: Mr George Francis
EMAIL: mr.georgefrancis21@gmail.com
SEHEMU YA NNE (4)
mr.georgefrancis21@gmail.com
Ni siku nyingine tena tunakutana katika muendelezo wa mada yetu ambapo hapa tunapata elimu kuhusu makosa ya rushwa na adhabu zake kama kichwa cha somo kinavyoeleza.
Sasa bila kupoteza muda tuendelee na mada yetu kwa kuangazia makosa yafuatayo:
11. Umiliki wa mali ambazo upatikanaji wake haueleweki. Ni kosa kwa Mtumishi wa umma kuwa na mali au pesa nyingi zaidi kuliko kipato chake halali cha sasa au kilichopita na hana maelezo ya kuridhisha kuhusu alivyozipata.
Mahakama ikijiridhisha kuwa kuna mtu anamiliki mali au pesa fulani kwa niaba ya mtuhumiwa au alipewa hizo mali ambazo upatikanaji wake haueleweki kama zawadi kutoka kwa mtuhumiwa na kama hakuna ushahidi unaojitoshereza kuhalalisha umiliki wake basi mali hizo zitachukuliwa kuwa ni mali zinazomilikiwa na mtuhumiwa hivyo kuwa sehemu ya kesi husika inayomkabili mtuhumiwa.
✓ADHABU:
Mtu atakayekutwa na hatia ya kutenda kosa hili adhabu yake ni faini isiyozidi shilingi milioni kumi (10,000,000/=) au kifungo kisichozidi miaka saba (7) au vyote kwa pamoja.
• Lakini pamoja na adhabu hiyo Mahakama inaweza kuamuru mali hizo za mtuhumiwa zitaifishwe na kuwa mali za serikali. Kuhusiana na kosa hili kuna maelezo mengi muhimu, siwezi kuelezea kilakitu lakini ili kuongeza maarifa zaidi kuhusu kosa hili soma kifungu cha 27(1) hadi (9) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.
12. Matumizi mabaya ya mali za umma. Mtumishi wa umma au mtumishi katika taasisi binafsi ambaye kwa kukosa uaminifu au kwa udanganyifu akafuja mali za umma zilizowekwa chini yake au akabadilisha umiliki wa mali hizo na kuwa mali zake au akaruhusu mtu mwingine kufanya hivyo atakuwa anatenda kosa.
✓ADHABU:
Mtu yeyote anayekutwa na hatia ya kutenda kosa hili adhabu yake faini isiyozidi shilingi milioni kumi (10,000,000/=) au kifungo kisichozidi miaka saba (7) au vyote kwa pamoja.
• Pamoja na adhabu hii lakini pia Mahakama inaweza kuamuru kuwa mali zilizofujwa ama kubalidilishwa umiliki wake na mtuhumiwa zirejeshwe kwa mmiliki wake halali au mtuhumiwa kuamriwa kulipa fidia kama mali hizo hazipatikani.
Hapa pia kuna options nyingine ambazo Mahakama inaweza kuamua. Lakini ili kuongeza maarifa zaidi kuhusiana na kosa hili, hunabudi kusoma kifungu cha 28(1)(2)(3) &(4)(a)(b)(c)&(d) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.
13. Kubadilisha matumizi. Mtumishi wa umma au mtumishi wa taasisi binafsi anayebadilisha mali za serikali au idara ya serikali taasisi binafsi kutoka katika matumizi ya vile ilivyokusudiwa kuwa na kufanya kutumika kwa matumizi yake binafsi au kwa faida ya mtu mwingine kupitia nafasi yake atakuwa ametenda kosa.
✓ADHABU:
Mtu yeyote anayekutwa na hatia ya kutenda kosa hili adhabu yake ni faini isiyozidi shilingi milioni mbili (2,000,000/=) au kifungo kisichozidi miaka miwili (2) au vyote kwa pamoja. Hii ni kwa mujibu wa kifungu cha 29 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.
14. Kusaidia au kufadhili kutenda kosa. Mtu yeyote anayemsaidia au kufadhili mtu mwingine kutenda kosa la rushwa kinyume cha sheria hii ya kuzuia na Kupambana na Rushwa naye pia atakuwa ametenda kosa la rushwa.
✓ADHABU:
Ukikutwa na hatia ya kutenda kosa hili adhabu yake ni faini isiyozidi shilingi milioni mbili (2,000,000/=) au kifungo kisichozidi miaka miwili (2) au vyote kwa pamoja. Hii ni kwa mujibu wa kifungu cha 30 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.
Ahsante kwa kuendelea kuwa nami, tukutane katika sehemu inayofuata ya mada hii ili tumalizie mada yetu.
Mungu akubariki sana.
NAME: Mr George Francis
EMAIL: mr.georgefrancis21@gmail.com