Fahamu Kuhusu Retirement Planning(Kujipanga kwa ajili ya Kustaafu)

Fahamu Kuhusu Retirement Planning(Kujipanga kwa ajili ya Kustaafu)

Masokotz

JF-Expert Member
Joined
Nov 26, 2018
Posts
3,713
Reaction score
6,121
Habari za wakti huu;
Ni matumaini yangu kwamb mnaendelea salama na Shughuli zenu za upambanaji na utafutaji wa Riziki;

Leo nimeona nilete mada ambayo kwa wajasiriamali wengine inaweza kuwa na faida sana na kuwasaidi katika kufanya mipango kuhusu maisha yao ya sasa na ya baada.

Leo nataka kuzungumza kuhusu kitu kinaitwa Retirement Planning au kujipanga kwa maisha baada ya kustaafu.

Kwanza nianze kusema kwamba Kustaafu sio suala la umri au uwezo ni suala la uamuzi.Ninaposema ni suala la uamuzi ninamaanisha kwamba Sio kila mstaafu afikie umri wa miaka 55 au 60 hata hivyo ktika mjadala wetu wa leo tunaweka utaratibu kwamba Mstaafu atastaafu akiwa na umri wa miaka 60 kwa mujibu wa sheria zetu.

Sasa nitaomba sana andiko lolote ambalo nitaliweka hapa ambalo linazungumzia masuala ya kisheria na iwapo litakuwa na makosa basi mwenye utaalamu anaweza kuweka marekebisho nami nitajitahidi kufuatili zaidi na kufanya maboresho.

Kwa mujibu wa taarifa nilizonazo kwa mifuko Rasmi ya hifadhi ya Jamii,Mstaafu anaweza kulipwa Pensheni pale tu ambapo anakua amechangia angalau michango 180 au michango ya miaka 15 mfululizo au zaidi ya hapo.Michango inakuwa mfululizo bila kujitoa wala kuruka kuchangi.HIvyo Basi iwapo wewe ni majsiriamali na unataka kujindaa kwa ajili ya kustaafu ni lazima uangali Umri wako wa sasa na umri wa kustaafu imebaki miaka mingapi.Iwapo imebaki chini ya miaka 15 basi usijaribu kushawishia na fao la kujitoa.Ila Pia inabidi uanze kuangalia kiwango chako cha mchango unachotoa uone iwapo kinaweza kuendana na mipango yako baada ya kustaafu ili auweze kujipanga


Jambo lingine ambalo unapaswa kufahamui ni kwamba Mstaafu hulipwa kiinuo mgongo(Lumpsum Pension) ambayo ni kama theluthi moja ya michango yake yote na kisha kila mwezi hulipwa mafao ya kila mwenzi amabyo ni sawa pia kama theluthi moja ya pato lake la wastani wa mwaka wake wa mwisho wa ajiraa.Hii ina maana kwamba kama Mshahara wako kwa miezi 12 kabla ya kustaafu ni Milioni 1 basi pensheni yako ya kila mwenzi itakuwa ni theluthi moja hivi aua kama laki 330,000.Hii inamaana kwamba katika mwaka wako wa mwisho wa ajira ni lazima kabisa ujiandae kwa kuongeza pato lako la mshahara ili upandishe kiwango chakeo cha Lumpsum na kiwango cha Pensheni.

Baada ya maelezo hayo sasa nieleze namna mjasiriamali anavoweza kufanya mipango ya kujiandaa kustaafu na wakti sahihi wa kuanza kufanya hivyo.Kwa kuanza tufahamu kwamba Michango ya Hifadhi ya Jamii ni Tax exempted na hivyo basi kama wewe ni Mjasiriamali ambaye unamiliki Kampuni au biashara yako uanweza kabisa kuchangia na malipo yale yakatoka kwenye Kampuni yako na kuipa nafuu ya kikodi.Ila usisahu kwamba kiwango utakachotumia Pia ndicho kitatumika katika kukotoa kodi ya Payrol Tax(Kodi ya Mshahara )Hivyo bsi unapopiga hesabu zako zingatia PIA Hilo;

Pembeni ya Hii mifuko ya hifadhi ya jamii(Kwa sasa NSSF Pekee) uanweza kuwa na Mipango mingine ya kustaafu kama vile kununua BIMA za Maisha ambazo nyingi hazina kiwango kikubwa sana cha michango.Unaweza kuchukua Bima ya Maisha ya Wafanyakazi ambayo kimsingi nayo ina faida.Inabidi uzungumze na kampuni za BIMA vizuri ili uweze kupata aina ya BIMA ambayo itawanufaisha warithi wa wafanyakazi wako iwapo watafia kazini,na Pia itwainufaisha kampuni iwapo wataishi mpaka wastaafu au kuwanufaisha wote.

Mambo ya kuzingatia unapofanya Mipango ya kustaafu ni kuhakikisha kwamba Unatumia Kiwango kidogo kabisa cha uwekezaji ili kupata faida kubwa mbeleni hasa kwa kuzingatia halihalisi ya uchumi wako binafsi na hali ya uchumi wa taifa.Usiishi maisha ya dhiki katiki kipindi unapojiandaa kustaafu ili ustaafu na mafao makubwa bali tafuta namna ya kubalance Mapato yako ya sasa yakupa maisha ya Furaa na wakti huo huo ya kupe nafasi ya kuishi maisha mazuri utakapo staafu.

Je unafikiri ni kiwango gani ni kizuri cha kuweka kama akiba kwa ajili ya kujiandaa kustaafu ambayo itakupa Kiwango kizuri cha maisha baada ya kustaafu?

Tujadili kwa pamoja huku tukiboresha mjadala huu na kuweka taarifa ambazo zitakusaidia katika kupanga kustaafu
 
Vijana changamkeni kustaafu kunakuja na kujipanga ni lazima. Sisi wengine huko hatuko tena tumestaafu miaka mingi kabla na Alhamdulillah tulijipanga hata bila ya kuwa na mpango maalumu.
 
Habari za wakti huu;
Ni matumaini yangu kwamb mnaendelea salama na Shughuli zenu za upambanaji na utafutaji wa Riziki;

Leo nimeona nilete mada ambayo kwa wajasiriamali wengine inaweza kuwa na faida sana na kuwasaidi katika kufanya mipango kuhusu maisha yao ya sasa na ya baada.

Leo nataka kuzungumza kuhusu kitu kinaitwa Retirement Planning au kujipanga kwa maisha baada ya kustaafu.

Kwanza nianze kusema kwamba Kustaafu sio suala la umri au uwezo ni suala la uamuzi.Ninaposema ni suala la uamuzi ninamaanisha kwamba Sio kila mstaafu afikie umri wa miaka 55 au 60 hata hivyo ktika mjadala wetu wa leo tunaweka utaratibu kwamba Mstaafu atastaafu akiwa na umri wa miaka 60 kwa mujibu wa sheria zetu.

Sasa nitaomba sana andiko lolote ambalo nitaliweka hapa ambalo linazungumzia masuala ya kisheria na iwapo litakuwa na makosa basi mwenye utaalamu anaweza kuweka marekebisho nami nitajitahidi kufuatili zaidi na kufanya maboresho.

Kwa mujibu wa taarifa nilizonazo kwa mifuko Rasmi ya hifadhi ya Jamii,Mstaafu anaweza kulipwa Pensheni pale tu ambapo anakua amechangia angalau michango 180 au michango ya miaka 15 mfululizo au zaidi ya hapo.Michango inakuwa mfululizo bila kujitoa wala kuruka kuchangi.HIvyo Basi iwapo wewe ni majsiriamali na unataka kujindaa kwa ajili ya kustaafu ni lazima uangali Umri wako wa sasa na umri wa kustaafu imebaki miaka mingapi.Iwapo imebaki chini ya miaka 15 basi usijaribu kushawishia na fao la kujitoa.Ila Pia inabidi uanze kuangalia kiwango chako cha mchango unachotoa uone iwapo kinaweza kuendana na mipango yako baada ya kustaafu ili auweze kujipanga


Jambo lingine ambalo unapaswa kufahamui ni kwamba Mstaafu hulipwa kiinuo mgongo(Lumpsum Pension) ambayo ni kama theluthi moja ya michango yake yote na kisha kila mwezi hulipwa mafao ya kila mwenzi amabyo ni sawa pia kama theluthi moja ya pato lake la wastani wa mwaka wake wa mwisho wa ajiraa.Hii ina maana kwamba kama Mshahara wako kwa miezi 12 kabla ya kustaafu ni Milioni 1 basi pensheni yako ya kila mwenzi itakuwa ni theluthi moja hivi aua kama laki 330,000.Hii inamaana kwamba katika mwaka wako wa mwisho wa ajira ni lazima kabisa ujiandae kwa kuongeza pato lako la mshahara ili upandishe kiwango chakeo cha Lumpsum na kiwango cha Pensheni.

Baada ya maelezo hayo sasa nieleze namna mjasiriamali anavoweza kufanya mipango ya kujiandaa kustaafu na wakti sahihi wa kuanza kufanya hivyo.Kwa kuanza tufahamu kwamba Michango ya Hifadhi ya Jamii ni Tax exempted na hivyo basi kama wewe ni Mjasiriamali ambaye unamiliki Kampuni au biashara yako uanweza kabisa kuchangia na malipo yale yakatoka kwenye Kampuni yako na kuipa nafuu ya kikodi.Ila usisahu kwamba kiwango utakachotumia Pia ndicho kitatumika katika kukotoa kodi ya Payrol Tax(Kodi ya Mshahara )Hivyo bsi unapopiga hesabu zako zingatia PIA Hilo;

Pembeni ya Hii mifuko ya hifadhi ya jamii(Kwa sasa NSSF Pekee) uanweza kuwa na Mipango mingine ya kustaafu kama vile kununua BIMA za Maisha ambazo nyingi hazina kiwango kikubwa sana cha michango.Unaweza kuchukua Bima ya Maisha ya Wafanyakazi ambayo kimsingi nayo ina faida.Inabidi uzungumze na kampuni za BIMA vizuri ili uweze kupata aina ya BIMA ambayo itawanufaisha warithi wa wafanyakazi wako iwapo watafia kazini,na Pia itwainufaisha kampuni iwapo wataishi mpaka wastaafu au kuwanufaisha wote.

Mambo ya kuzingatia unapofanya Mipango ya kustaafu ni kuhakikisha kwamba Unatumia Kiwango kidogo kabisa cha uwekezaji ili kupata faida kubwa mbeleni hasa kwa kuzingatia halihalisi ya uchumi wako binafsi na hali ya uchumi wa taifa.Usiishi maisha ya dhiki katiki kipindi unapojiandaa kustaafu ili ustaafu na mafao makubwa bali tafuta namna ya kubalance Mapato yako ya sasa yakupa maisha ya Furaa na wakti huo huo ya kupe nafasi ya kuishi maisha mazuri utakapo staafu.

Je unafikiri ni kiwango gani ni kizuri cha kuweka kama akiba kwa ajili ya kujiandaa kustaafu ambayo itakupa Kiwango kizuri cha maisha baada ya kustaafu?

Tujadili kwa pamoja huku tukiboresha mjadala huu na kuweka taarifa ambazo zitakusaidia katika kupanga kustaafu
Watu ambao siyo wafanyakazi, huwa mnakuwa mabingwa wa kushauri wastaafu na wafanyakazi kuhusu mishahara na akiba.

Yaani siku zote ninyi ndio mnajua na mnaona watu wengine hawajielewi na hawajui kutumia pesa zao.
 
Watu ambao siyo wafanyakazi, huwa mnakuwa mabingwa wa kushauri wastaafu na wafanyakazi kuhusu mishahara na akiba.

Yaani siku zote ninyi ndio mnajua na mnaona watu wengine hawajielewi na hawajui kutumia pesa zao.
Mkuu,kwanza fahamu kwamba huu ushauri sio kwa ajili ya wafanyakazi tu bali ni kwa ajili ya mtu yeyote mwenye kipato.Pili ushauri huu haumaanishi kwamba wafanyakazi hawajui nini cha kufanya na PESA zao na hata kama hawajui haihusiani na mjada huu.

All in all Kupanga ni kuchagua.NInakutakia kila la heri.
 
Mkuu,kwanza fahamu kwamba huu ushauri sio kwa ajili ya wafanyakazi tu bali ni kwa ajili ya mtu yeyote mwenye kipato.Pili ushauri huu haumaanishi kwamba wafanyakazi hawajui nini cha kufanya na PESA zao na hata kama hawajui haihusiani na mjada huu.

All in all Kupanga ni kuchagua.NInakutakia kila la heri.
Kama huu ni ushauri unawahusu wenye kipato, basi huu ushauri ni trash na theoretical.

Jifunze na experience mifumo ikoje kabla hujashauri watu kujiingiza kwenye mifumo ya kitapeli.
 
Kama huu ni ushauri unawahusu wenye kipato, basi huu ushauri ni trash na theoretical.

Jifunze na experience mifumo ikoje kabla hujashauri watu kujiingiza kwenye mifumo ya kitapeli.
Mkuu nafikiri ungeweka Mchango wako hapa maana uzuri Kichwa cha uzi kiko Open Kwamba ni kujipanga kustaafu na mm nimeweka Njia ya kawaida tu ya kupitia Social Security Insurance kama una njia nyingine ukaiweka utasaidia zaidi kuliko kuonesha Frustration za kiwango kikubwa kiasi hiki.Anyway any how Nmekuelewa
 
Mkuu nafikiri ungeweka Mchango wako hapa maana uzuri Kichwa cha uzi kiko Open Kwamba ni kujipanga kustaafu na mm nimeweka Njia ya kawaida tu ya kupitia Social Security Insurance kama una njia nyingine ukaiweka utasaidia zaidi kuliko kuonesha Frustration za kiwango kikubwa kiasi hiki.Anyway any how Nmekuelewa
Anyway, ushauri wangu ni kama ifuatayo:

Mishahara na vipato hazitishi, ukifanikiwa kupata kundi ka watu mnaowaza kwa usawa unganisheni nguvu.

Pension schemes za TZ ni utapeli, kama kipato unachopata hulazimishwi kuchangia huko, achana nazo.

Siku zote elewa, Mwajiri anaangalia maslahi yake tu, atakulazimisha ufanye kazi mkoa au wilaya ambayo hutaki, na utashindwa kujiendeleza binafsi, hivyo kuwa makini.

Kama unafanya kazi mkoa mzuri kifursa na biashara, then wekeza kwenye assets, hasa ardhi na mashamba (location matter).
 
Anyway, ushauri wangu ni kama ifuatayo:

Mishahara na vipato hazitishi, ukifanikiwa kupata kundi ka watu mnaowaza kwa usawa unganisheni nguvu.

Pension schemes za TZ ni utapeli, kama kipato unachopata hulazimishwi kuchangia huko, achana nazo.

Siku zote elewa, Mwajiri anaangalia maslahi yake tu, atakulazimisha ufanye kazi mkoa au wilaya ambayo hutaki, na utashindwa kujiendeleza binafsi, hivyo kuwa makini.

Kama unafanya kazi mkoa mzuri kifursa na biashara, then wekeza kwenye assets, hasa ardhi na mashamba (location matter).
Hapa sasa umeutendea haki uzi wetu,Tunaweza tukajadili zaidi.Ushauri wangu hapo juu haujakataza kwamba Usiwekeze kwenye Assets na wala kushirikiana na wengine Ila as they say.Tumia kila Fursa unayopata ndio maana hata katika ushauri wangu kuna codes ndogo ndogo ambazo nimeziweka ambazo mtu akizifuatilia anaweza kujiandaa vizur zaidi kwa ajili ya kustaafu kwa heshima
 
Kustaafu kuzuri ni kuweka akiba kwenye personal account ambayo hugusi kabisa. Wazungu wanasema pay yourself first. Lakini pia usiogoppe kuinvest baada ya kufanya research ya kutosha kuhusu biashara. Pia unaweza kuwekeza kwenye real estate, au unaweza kuwa unanunua ngombe . Wakikuwa,, unauza unanunua tena hao ngombe
 
Watu ambao siyo wafanyakazi, huwa mnakuwa mabingwa wa kushauri wastaafu na wafanyakazi kuhusu mishahara na akiba.

Yaani siku zote ninyi ndio mnajua na mnaona watu wengine hawajielewi na hawajui kutumia pesa zao.
😁😬
 
Hapa sasa umeutendea haki uzi wetu,Tunaweza tukajadili zaidi.Ushauri wangu hapo juu haujakataza kwamba Usiwekeze kwenye Assets na wala kushirikiana na wengine Ila as they say.Tumia kila Fursa unayopata ndio maana hata katika ushauri wangu kuna codes ndogo ndogo ambazo nimeziweka ambazo mtu akizifuatilia anaweza kujiandaa vizur zaidi kwa ajili ya kustaafu kwa heshima
Nadhani pia watu wana maisha yao na maamuzi yao.

Kama mtu anatumia ovyo, kipato chake akifilisika hakuombi sioni sababu ya kukomaa naye. Ni kuachana naye na maisha yake
 
Inaskitisha mada hizi hakuna reply alafu majitu kwenye udaku simba na yanga..so sad taifa limekwama
ni kweli ni ngumu kuwapata watz kwenye mijadala kama hii. tunapenda mambo mepesimepesi ya udaku na umbea, michezo ya kiinimacho mipira hasa simba na yanga, kubeti
 
Vijana changamkeni kustaafu kunakuja na kujipanga ni lazima. Sisi wengine huko hatuko tena tumestaafu miaka mingi kabla na Alhamdulillah tulijipanga hata bila ya kuwa na mpango maalumu.

Ulifanya maandalizi gani Bibi/babu? Tufanye nini ili tuandae mazingira mazuri huko mbeleni??
 
Ulifanya maandalizi gani Bibi/babu? Tufanye nini ili tuandae mazingira mazuri huko mbeleni??
anza kuweka fedha kidogo kidogo kila mwezi. Ukisubiri upate fedha nyingi kwa wakati you may never get it.

Pia anza kuwekeza kama kwenye hisa (nunua kidogo kidogo) baada ya miaka unajikuta uko vizuri.

Usisahau na kujenga hata kajumba ka vyumba viwili kwanza.
 
Back
Top Bottom