Fahamu kuhusu vibali vya ujenzi, umuhimu wake na namna ya kuvipata

Fahamu kuhusu vibali vya ujenzi, umuhimu wake na namna ya kuvipata

Kulingana na sheria ya ujenzi wa majengo mijini si ruhusa kwa mtu yeyote kujenga au kuanza kujenga jengo bila ya kuwa na seti ya michoro ya jengo (architectural drawings), hivyo basi kuna vitu vya kuzingatia na ambavyo vinatakiwa kuwepo kwenye michoro hiyo ili kuepuka usumbufu utakaojitokeza wakati ukitafuta kibali cha kujenga jengo.

Vitu hivyo ni;

1. Namna jengo litakavyokuwa (plans section, elevation, and foundation and roof plan)
Ili kupata kibali cha ujenzi lazima kuwe na michoro itakayoonesha msingi(foundation) utakavyokuwa, mchoro wa kipande/sehemu ya jengo(section plan), paa, na mionekano ya mbele, nyuma, kushoto, na kulia. Michoro yote hii ya namna jengo litakavyokuwa inatakiwa iwe na vipimo vinavyoonekana vizuri.

2. Namba na eneo la kiwanja kilipo
Hivi huonekana sehemu ya chini au kulia Katika michoro ya namna jengo litakavyokuwa.

3. Jina la mmilikaji ardhi inayohusika
Pia sehemu hii huonekana katika michoro yote ya jengo upande wa kulia au chini.

4. Jina la mchoraji na anwani
Pia hii sehemu huonekana chini au kulia katika michoro ya jengo.

5. Ukubwa wa jengo kwa mita za mraba
Hii sehemu huonekana kwenye mchoro wa jengo(floor plan) au kwenye mchoro unaoonesha mpangilio kati ya kiwanja na jengo (site plan).

6. Ujazo wa kiwanja (plot coverage)
Hii sehemu hueleza ujazo utakao chukuliwa na jengo katika kiwanja, pia huonekana kwenye mchoro unaoonesha mpangilio kati ya jengo na kiwanja(site plan).

7. Uwiano (plot ratio)
Hii sehemu hueleza uwiano kati ya jengo na kiwanja, pia huonekana katika mchoro wa site plan.

8. Matumizi yanayokusudiwa
Hii sehemu hueleza kusudio la matumizi ya jengo, pia huonekana kulia au chini katika michoro yote ya jengo.

9. Idadi ya maegesho yatakayokuepo
Hii sehemu huonesha idadi ya maegesho ya magari na vitu vingine vinavyozunguka jengo ndani ya kiwanja husika, pia huonekana katika mchoro wa site plan.

10. Umbali wa jengo kutoka kwenye mipaka ya kiwanja (setbacks)
Hii sehemu hutumika kuonesha umbali uliopo kutoka katika mipaka ya kiwanja mpaka jengo husika, pia huonekana kwenye mchoro wa site plan.

11. Mfumo wa kutoa majitaka hadi kwenye mashimo
Hii sehemu huonesha jinsi ya kutoa majitaka kutoka kwenye jengo mpaka kwenye mashimo ya kuhifadhia,pia sehemu hii huonekana kwenye site plan.

Kutokana na maelezo hapo juu, kwa mtu yeyote anayehitaji kujenga jengo inabidi ahakikishe kila kitu nilichokielezea hapo juu kinaonekana katika seti ya michoro ya jengo (architectural drawings) kabla ya kuendelea na utaratibu mwingine unaofuata.

Mchoro wa jengo.png

Mchoro wa jengo (floor plan)

section plan.png

Mchoro wa sehemu ya jengo(section plan)

Paa.png

Mchoro wa paa (roof plan)

elevation.png

Mchoro unaoonesha mionekano ya jengo (elevation)
Chanzo: Ujenzi Elekezi Blog
 

Habari wataalam,

Nataka nijenge nyumba ndogo kwa mjengo wa stail ya ghorofa moja yaani floor moja kwa juu, kutokana taratibu za nchi na vibali vya ujenzi.

Naomba kwa anaejua hatua za kufanya ili kupata vibali na gharama za kupata hivo vibali, sitaki kujenga kienyeji nataka kufuata utaratibu ili wasije kuniandama.

Note: Eneo halijapimwa, ni squater tu.

BAADHI YA MASWALI YA WADAU WENGINE

======

======

======

======

======


BAADHI YA MAJIBU YA WADAU

======



PIA, SOMA:
Kulingana na sheria ya ujenzi wa majengo mijini si ruhusa kwa mtu yeyote kujenga au kuanza kujenga jengo bila ya kuwa na seti ya michoro ya jengo (architectural drawings), hivyo basi kuna vitu vya kuzingatia na ambavyo vinatakiwa kuwepo kwenye michoro hiyo ili kuepuka usumbufu utakaojitokeza wakati ukitafuta kibali cha kujenga jengo.

Vitu hivyo ni;

1. Namna jengo litakavyokuwa (plans section, elevation, and foundation and roof plan)
Ili kupata kibali cha ujenzi lazima kuwe na michoro itakayoonesha msingi(foundation) utakavyokuwa, mchoro wa kipande/sehemu ya jengo(section plan), paa, na mionekano ya mbele, nyuma, kushoto, na kulia. Michoro yote hii ya namna jengo litakavyokuwa inatakiwa iwe na vipimo vinavyoonekana vizuri.

2. Namba na eneo la kiwanja kilipo
Hivi huonekana sehemu ya chini au kulia Katika michoro ya namna jengo litakavyokuwa.

3. Jina la mmilikaji ardhi inayohusika
Pia sehemu hii huonekana katika michoro yote ya jengo upande wa kulia au chini.

4. Jina la mchoraji na anwani
Pia hii sehemu huonekana chini au kulia katika michoro ya jengo.

5. Ukubwa wa jengo kwa mita za mraba
Hii sehemu huonekana kwenye mchoro wa jengo(floor plan) au kwenye mchoro unaoonesha mpangilio kati ya kiwanja na jengo (site plan).

6. Ujazo wa kiwanja (plot coverage)
Hii sehemu hueleza ujazo utakao chukuliwa na jengo katika kiwanja, pia huonekana kwenye mchoro unaoonesha mpangilio kati ya jengo na kiwanja(site plan).

7. Uwiano (plot ratio)
Hii sehemu hueleza uwiano kati ya jengo na kiwanja, pia huonekana katika mchoro wa site plan.

8. Matumizi yanayokusudiwa
Hii sehemu hueleza kusudio la matumizi ya jengo, pia huonekana kulia au chini katika michoro yote ya jengo.

9. Idadi ya maegesho yatakayokuepo
Hii sehemu huonesha idadi ya maegesho ya magari na vitu vingine vinavyozunguka jengo ndani ya kiwanja husika, pia huonekana katika mchoro wa site plan.

10. Umbali wa jengo kutoka kwenye mipaka ya kiwanja (setbacks)
Hii sehemu hutumika kuonesha umbali uliopo kutoka katika mipaka ya kiwanja mpaka jengo husika, pia huonekana kwenye mchoro wa site plan.

11. Mfumo wa kutoa majitaka hadi kwenye mashimo
Hii sehemu huonesha jinsi ya kutoa majitaka kutoka kwenye jengo mpaka kwenye mashimo ya kuhifadhia,pia sehemu hii huonekana kwenye site plan.

Kutokana na maelezo hapo juu, kwa mtu yeyote anayehitaji kujenga jengo inabidi ahakikishe kila kitu nilichokielezea hapo juu kinaonekana katika seti ya michoro ya jengo (architectural drawings) kabla ya kuendelea na utaratibu mwingine unaofuata.

View attachment 1356883
Mchoro wa jengo (floor plan)

View attachment 1356884
Mchoro wa sehemu ya jengo(section plan)

View attachment 1356885
Mchoro wa paa (roof plan)

View attachment 1356886
Mchoro unaoonesha mionekano ya jengo (elevation)
Chanzo: Ujenzi Elekezi Blog
Thax sana mkuu barikiwa sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari wana Jf

Niliwahi kupata kuishi morogoro na kupata kujenga sehemu ya kujisitiri katika kiwanja ambacho hakijapimwa japo nimekuwa nikilipia jengo hill hapo manispaa.

Nimepata taarifa kunatakiwa kibari cha ujenzi kwa sale tulio wahi kujenga bila vibali naomba kujua hatua za kufuata ili kutimiza hili jambo ila ramani ya nyumba nilitumia ya mtu na hata pia sikumbuki ilipo.mnaojua nisaidieni niko nje ya mkoa.

Asanteni
 
Kama kiwanja hakijapimwa,taratibu za kupata kibali cha ujenzi zikoje?
 
Nenda ofisi za halimashauri utapewa ushauri unaohitaji.
 
Back
Top Bottom