Fahamu kuhusu vibali vya ujenzi, umuhimu wake na namna ya kuvipata

Fahamu kuhusu vibali vya ujenzi, umuhimu wake na namna ya kuvipata

Niongezee tu hata kupaka rangi nyumba yako unahitaji kibali vinginevyo faini! Usifanye shughuri yoyote ya badiliko bila kibali.
Niliweke sawa hili;

kupaka rangi nalo linatokana na wilaya kama hapa Tanzania nadhani ni wilaya mbili ambazo unatakiwa uchukue kibali ni wilaya ya Ilala na Manispaa ya dodoma
 
Tutakupa elimu bure ili ukafuatilie mwenyew labda kukusaidia tutakupatia watu waliopo katika wilaya husika wakusaidie kwa haraka zaidi mana tunafahamiana kutokana na mwingiliano wa kazi zetu

Asante sana mkuu. Nitakutafuta soon kwa upande wa manispaa ya kinondoni. Blessed.
 
Kwa
Kibali cha ujenzi(Building permit), ni moja ya kanuni muhimu sana ya upangaji wa miji nchini Tanzania. kila anaehitaji kujenga anapaswa kufuata kanuni za kibali cha ujenzi atakachopewa, mara nyingi kwa mujibu wa sheria kibali cha ujenzi hutolewa na mamlaka za serikali ambazo ni halmashauri kupitia idara ya mipango miji na mazingira.

Kulingana na sheria ya ujenzi wa majengo mijini Na 101 ya mwaka 2009 si ruhusa kwa mtu yeyote kujenga au kuanza kujenga jengo bila ya kuwa na;

- Uhalali wa umiliki wa ardhi mahali unapojenga.

- Kibali cha ujenzi kutoka mamlaka husika.

1. UMUHIMU WA KIBALI CHA UJENZI

- Kutimiza matakwa ya kanuni za ujenzi mijini.

- Kuwezesha kujenga majengo ya nyumba kama yaliyoelekezwa katika mipango miji ya sehemu husika.

- Kudhibiti ujenzi holela.

2. JINSI YA KUPATA KIBALI CHA UJENZI

- Kuwasilisha michoro ya ramani ya jengo kwa ajili ya uchunguzi.

- Kulipia malipo stahiki ya uchunguzi wa ramani hizo.

- Kulipia malipo ya kiwanja kwa mwaka husika.

3. JINSI YA KUWASILISHA MAOMBI MICHORO YA MAJENGO MAALUMU.

Michoro ya majengo maalumu(Maghorofa, kumbi, Taasisi mbalimbali, Bar, Vituo vya mafuta, Viwanda, Hospital na majengo mengine ya jinsi hiyo iwasilishwe kwa kuanza na michoro ya awali ya kisanifu(Preminary Drawings) ambayo itahusisha.

- Michoro ya sakafu(Floor plan) 1:100

- Sura ya jengo(Elevations) 1:100

- Mkato wa jengo(Section) 1:100

Baada ya uchunguzi wa michoro ya awali kukamilika itawasilishwa michoro ya michoro(Final Drawings) ambayo ni michoro ya kisanifu na ya kihandisi(Architectural and structural drawings) kwa ajili ya uchunguzi.

● Michoro inayowasilishwa izingatie kanuni na taratibu zote muhimu za kiuchoraji(Architectural and Engineering Aspects) na iwe imesainiwa na msanifu majengo/Mhandisi anayetambuliwa(Architectural and Structural Endorsement).

● Michoro hiyo iambatane na nakala ya cheti cha uchunguzi wa athari za kimazingira(Environment Impact Assessment EIA).

● Michoro iambatane na nakala za nyaraka zote halali za umiliki wa kiwanja husika pamoja na stakabadhi ya malipo ya kiwanja kwa mwaka husika.

● Michoro yote iwasilishwe ikiwa na maandishi yanayosomeka(Readable text).

● Michoro yote iwasilishwe kwenye ukubwa wa karatasi(paper size) A0,A1,A2 au A3.

4. JINSI YA KUWASILISHA MAOMBI YA MICHORO YA MAJENGO YA KAWAIDA.

Michoro ya majengo ya kawaida itawasilishwa kwa kuzingatia maelezo ya hapo juu isipokuwa haitatangiliwa na michoro ya awali(Preminary Drawing) kama ilivyo katika michoro ya majengo maalumu.

- MICHORO ILIYOANDALIWA IONYESHE NINI.
●Litakavyokuwa(Plans,Sections,Elevations,Foundation,Roof plan,Site plan).

●Ramani ya kiwanja(Location plan).

●Namba na eneo la kiwanja kilipo.

●Jina la mmilikaji ardhi inayohusika.

●Jina la mchoraji, ujuzi na anuani.

●Ukubwa wa jengo kwa mita za mraba.

●Ujazo wa kiwanja(Plan ratio).

●Urefu wa jengo(Height).

●Matumizi yanayokusudiwa.

●Idadi ya maegesho yatakayokuwepo.

●Umbali kwa jengo kutoka kwenye mipaka ya kiwanja(Setbacks).

●Mfumo wa kutoa majitaka hadi kwenye mashimo.

- VIAMBATANISHO UNAVYOTAKIWA KUWA NAVYO

● Fomu moja ya maombi iliyojazwa kwa usahihi.

● Hati ya kumiliki kiwanja au barua ya toleo.

● Kumbukumbu zingine zinazohusu kiwanja hicho kama hati za mauzo makabidhiano na mengine.

● Nakala ya risiti ya kodi ya kiwanja na kodi za majengo.

● Mabadiliko ya matumizi ya ardhi.

● Ramani ya kiwanja iliyosajiliwa.

- UMUHIMU WA KIBALI CHA UJENZI

● Kutimiza matakwa ya kanuni za ujenzi mijini.

● Kuwezesha kujenga majengo na nyumba kama yaliyoelekezwa katika mipango miji ya sehemu husika.

● Kudhibiti ujenzi holela.

- MUDA WA UPATIKANAJI WA KIBALI CHA UJENZI.

● Endapo mwombaji atakamilisha hatua zote muhimu kwa wakati atapata kibali cha ujenzi ndani ya majuma mawili(2) hadi manne(4).

● Hii ni pamoja na uwasilishaji wa ramani zilizoidhinishwa na wataalamu husika na hati za umiliki zilizo sahihi.

- WAJIBU WA MWANANCHI

Ni wajibu wa kila mwananchi kujenga au kukarabati nyumba yake iliyo ndani ya mji/jiji kwa kibali kutoka halmashauri.

- TAHADHARI

● Endapo mwananchi yeyote atajenga au kukarabati nyumba bila kibali cha ujenzi toka halmashauri,atapewa ilani ya kusimamisha ujenzi au ukarabati na kushauriwa kufuata taratibu za kuomba kibali cha ujenzi ndani ya siku saba(7).

● Kama mwombaji atakaidi ilani ya kusimamisha jiji au miji litampa ilani ya kubomoa jengo lake mwenyew na akishindwa jiji litabomoa jengo husika na kudai mmiliki gharama za utekelezaji wa ubomoaji.

Imeandaliwa na; UTUKUFU CLEMENT MWANJISI
(Planning officer wa kujitegemea).
Kitendo cha kubomoa jengo kisa mtu ajafuata utaratibu wa permit ni ukorofi,yawapasa kwenda kulitazama jengo na kama linakizi vigezo kuwe na faini ya kutofuata taratibu.kama halina vigezo ndio libomolewe.
 
Ingefaa process zote zicost hiyo 150000
Lakini kunahitajika hadi sign za msanifu majengo mtaalamu wa ramani cheti sijui cha nn
Malipo ya kila mwaka ya kiwanja
Mpaka uje kuitoa hiyo 150000 utakuta umetumia zaidi ya milion
Kibali ukiwa na 150000 kwa wilaya kama ubungo unakipata haraka tu kikubwa uwe na michoro iliyochorwa na wataalamu
 
Niliweke sawa hili;
kupaka rangi nalo linatokana na wilaya kama hapa Tanzania nadhani ni wilaya mbili ambazo unatakiwa uchukue kibali ni wilaya ya Ilala na Manispaa ya dodoma
Unachoongelea ni utekelezaji tu, Service Levy au ukitaka Kodi ya Maendeleo ipo miaka mingi na wengi walikuwa hawatozwi wakaisahau, sasa imekumbukwa na baadhi wameanza kutozwa, wanaishangaa wanadhani ni kodi mpya kumbe sivyo; Wilaya zote za Dar vibali hivyo vinahitajika kwani sheria na kanuni za Jiji ni moja.
 
Sisi tuna kampuni mkuu tunafanya shughuli zote zinazohusu ardhi kama urasimishaji,upimaji maeneo,uuzaji viwanja tulivopima wenyew na ununuaji maeneo makubwa tunayakata viwanja then tunaviuza,ukihitaj kutafutiwa hati miliki,ukihitaji kucholewa ramani za majengo karibu.


Ofisi zetu zipo Mbezi beach Tangi bovu jengo la TEVI COMMERCIAL PARK ghorofa ya tatu

au
Tupigie 0713132109,0752602988
Nikitaka kupimiwa kiwanja changu gharama yake inakuwaje gharama zenu?
 
Ahsante sana kwa muongozo...

Vinasumbua sana kupatikana hivyo... unaweza anza kujenga mpaka unamaliza bado hakijatoka... haswa nyumba za makazi...


Cc: mahondaw
 
Ingefaa process zote zicost hiyo 150000
Lakini kunahitajika hadi sign za msanifu majengo mtaalamu wa ramani cheti sijui cha nn
Malipo ya kila mwaka ya kiwanja
Mpaka uje kuitoa hiyo 150000 utakuta umetumia zaidi ya milion
Uoga wako mkuu lakini ukitaka kwa hela hiyo unachukua vizur tu
 
Nikitaka kupimiwa kiwanja changu gharama yake inakuwaje gharama zenu?
Inatakiwa tufike site tuangalie eneo then tukupe mahesabu yote na ushauri pia then siku hizi ukitaka kupunguza gharama mnaweza mkakaa kikao na majiran zako then mkachanga gharama mana peke yako naweza kukuambia mpaka kumaliza mchakato 5M lakin mkiwa wengi mnashare.....Mana sheria ya asaivi natengeneza ramani ya mpango mji sio peke yako bali na watu wa pembeni wataingia kivyovyote vile sasa kupunguza gharama washilikishe
 
5m????
Mh aya
Inatakiwa tufike site tuangalie eneo then tukupe mahesabu yote na ushauri pia then siku hizi ukitaka kupunguza gharama mnaweza mkakaa kikao na majiran zako then mkachanga gharama mana peke yako naweza kukuambia mpaka kumaliza mchakato 5M lakin mkiwa wengi mnashare.....Mana sheria ya asaivi natengeneza ramani ya mpango mji sio peke yako bali na watu wa pembeni wataingia kivyovyote vile sasa kupunguza gharama washilikishe
 
Huku mtaani kwa sasa kuna hii changamoto ya kuandikiwa maandishi haya kwenye kuta za nyumba nyingi zinazoendekea kujengwa.

"SIMAMISHA UJENZI, FIKA OFISI YA ARDHI NA VIBALI VYAKO".

Yasemekana ni kutokana na kujenga bila kibali cha ujenzi. Tatizo ni kwamba utaratibu wa kupata hicho kibali una konakona nyingi sana na upigaji ndani yake.

Kupata ramani tu ya architect sio chini ya 100,000/=
Hapo bado kulipia kibali chenyewe
Bado injinia anayeipitisha hajaomba chochote

Kwa kifupi masikini tunaojenga kwa kuungaunga, hizi konakona ndiyo zinatuumiza zaidi. Mnatumia mbinu mbadala ipi kukabiliana na hili kwa mnaojenga maeneo ya mjini?
 
Sisi wa huku vijijini ni kuporomosha tu vibanda bila tatizo lolote lile.
 
Hilo suala huwa linanishangaza sana. Kuna kero nyingi sana mitaani ikiwa ni pamoja na ubovu wa barabara za mitaani, miundombinu mibovu hasa ya uondoshaji maji taka na yale ya mvua.

Kero nyigi hazishughulikiwi kwa wakati kwasababu utaambiwa watendaji wachache, rasilimali fedha hakuna,au tatizo halijulikani kwenye ngazi ya Wilaya na urasimu mwiiingi.

Lakini jaribu kufanya kitu cha maendeleo kama ujenzi wa makazi biashara au anzisha mradi wa kuingiza pesa. Mamlaka zote zinazoitwa za "udhibiti" zitakuja siku hiyohiyo kila mtu akiwa na madai yake na yote yanahitaji uyalipie!
 
Back
Top Bottom