Fahamu kuhusu vibali vya ujenzi, umuhimu wake na namna ya kuvipata

Fahamu kuhusu vibali vya ujenzi, umuhimu wake na namna ya kuvipata

Nadhani hizo Sheria ipo kwa waliopo ndani ya na wale wanaojenga majengo makubwa au magorofa,lakini kwa walio nje ya mji ambaye amenunua eneo lilipopimwa na halmashauri na anajenga nyumba ya kawaida sidhani Kama ni tatizo
Kibali cha ujenzi ni sheria ya Tanzania nzima popote pale kinahitajika
 
safiiii,je hii inaweza kuzuia watu kutapeliwa viwanja?? au mtu kuuza kiwanja kisicho chake/ watu wawili kuuziwa kiwanja kimoja??
Ndio maana tunasisitiza kununua viwanja vilivyopimwa na kuvipatia hati miliki kuwa na uhakika...Ushauri zaidi tupigie au fika ofisin kwetu MBEZI BEACH TANGI BOVU JENGO LA TEVI COMMERCIAL PARK
 
mleta mada mwizi tu
Then karibu ofisin Mbezi Beach Tangi Bovu jengo la Tevi commercial park (NBC HOUSE),Ghorofa ya tatu au ukifika chini waulize askari wanaolinda bank waambie nataka kwenda SUSTAINABLE CITIES COMPANY LIMITED.

Kwa ushauri zaidi kuhusu masuala ya ardhi kama upimaji,utafutaji wa hati miliki au kununua kiwanja au kama una eneo kubwa unaliuza tuone mana tunayanunua na tunayakata viwanja vilivyopimwa then tunauza.
 
Kibali cha ujenzi(Building permit), ni moja ya kanuni muhimu sana ya upangaji wa miji nchini Tanzania. kila anaehitaji kujenga anapaswa kufuata kanuni za kibali cha ujenzi atakachopewa, mara nyingi kwa mujibu wa sheria kibali cha ujenzi hutolewa na mamlaka za serikali ambazo ni halmashauri kupitia idara ya mipango miji na mazingira.

Kulingana na sheria ya ujenzi wa majengo mijini Na 101 ya mwaka 2009 si ruhusa kwa mtu yeyote kujenga au kuanza kujenga jengo bila ya kuwa na;

- Uhalali wa umiliki wa ardhi mahali unapojenga.

- Kibali cha ujenzi kutoka mamlaka husika.

1. UMUHIMU WA KIBALI CHA UJENZI

- Kutimiza matakwa ya kanuni za ujenzi mijini.

- Kuwezesha kujenga majengo ya nyumba kama yaliyoelekezwa katika mipango miji ya sehemu husika.

- Kudhibiti ujenzi holela.

2. JINSI YA KUPATA KIBALI CHA UJENZI

- Kuwasilisha michoro ya ramani ya jengo kwa ajili ya uchunguzi.

- Kulipia malipo stahiki ya uchunguzi wa ramani hizo.

- Kulipia malipo ya kiwanja kwa mwaka husika.

3. JINSI YA KUWASILISHA MAOMBI MICHORO YA MAJENGO MAALUMU.

Michoro ya majengo maalumu(Maghorofa, kumbi, Taasisi mbalimbali, Bar, Vituo vya mafuta, Viwanda, Hospital na majengo mengine ya jinsi hiyo iwasilishwe kwa kuanza na michoro ya awali ya kisanifu(Preminary Drawings) ambayo itahusisha.

- Michoro ya sakafu(Floor plan) 1:100

- Sura ya jengo(Elevations) 1:100

- Mkato wa jengo(Section) 1:100

Baada ya uchunguzi wa michoro ya awali kukamilika itawasilishwa michoro ya michoro(Final Drawings) ambayo ni michoro ya kisanifu na ya kihandisi(Architectural and structural drawings) kwa ajili ya uchunguzi.

● Michoro inayowasilishwa izingatie kanuni na taratibu zote muhimu za kiuchoraji(Architectural and Engineering Aspects) na iwe imesainiwa na msanifu majengo/Mhandisi anayetambuliwa(Architectural and Structural Endorsement).

● Michoro hiyo iambatane na nakala ya cheti cha uchunguzi wa athari za kimazingira(Environment Impact Assessment EIA).

● Michoro iambatane na nakala za nyaraka zote halali za umiliki wa kiwanja husika pamoja na stakabadhi ya malipo ya kiwanja kwa mwaka husika.

● Michoro yote iwasilishwe ikiwa na maandishi yanayosomeka(Readable text).

● Michoro yote iwasilishwe kwenye ukubwa wa karatasi(paper size) A0,A1,A2 au A3.

4. JINSI YA KUWASILISHA MAOMBI YA MICHORO YA MAJENGO YA KAWAIDA.

Michoro ya majengo ya kawaida itawasilishwa kwa kuzingatia maelezo ya hapo juu isipokuwa haitatangiliwa na michoro ya awali(Preminary Drawing) kama ilivyo katika michoro ya majengo maalumu.

- MICHORO ILIYOANDALIWA IONYESHE NINI.
●Litakavyokuwa(Plans,Sections,Elevations,Foundation,Roof plan,Site plan).

●Ramani ya kiwanja(Location plan).

●Namba na eneo la kiwanja kilipo.

●Jina la mmilikaji ardhi inayohusika.

●Jina la mchoraji, ujuzi na anuani.

●Ukubwa wa jengo kwa mita za mraba.

●Ujazo wa kiwanja(Plan ratio).

●Urefu wa jengo(Height).

●Matumizi yanayokusudiwa.

●Idadi ya maegesho yatakayokuwepo.

●Umbali kwa jengo kutoka kwenye mipaka ya kiwanja(Setbacks).

●Mfumo wa kutoa majitaka hadi kwenye mashimo.

- VIAMBATANISHO UNAVYOTAKIWA KUWA NAVYO

● Fomu moja ya maombi iliyojazwa kwa usahihi.

● Hati ya kumiliki kiwanja au barua ya toleo.

● Kumbukumbu zingine zinazohusu kiwanja hicho kama hati za mauzo makabidhiano na mengine.

● Nakala ya risiti ya kodi ya kiwanja na kodi za majengo.

● Mabadiliko ya matumizi ya ardhi.

● Ramani ya kiwanja iliyosajiliwa.

- UMUHIMU WA KIBALI CHA UJENZI

● Kutimiza matakwa ya kanuni za ujenzi mijini.

● Kuwezesha kujenga majengo na nyumba kama yaliyoelekezwa katika mipango miji ya sehemu husika.

● Kudhibiti ujenzi holela.

- MUDA WA UPATIKANAJI WA KIBALI CHA UJENZI.

● Endapo mwombaji atakamilisha hatua zote muhimu kwa wakati atapata kibali cha ujenzi ndani ya majuma mawili(2) hadi manne(4).

● Hii ni pamoja na uwasilishaji wa ramani zilizoidhinishwa na wataalamu husika na hati za umiliki zilizo sahihi.

- WAJIBU WA MWANANCHI

Ni wajibu wa kila mwananchi kujenga au kukarabati nyumba yake iliyo ndani ya mji/jiji kwa kibali kutoka halmashauri.

- TAHADHARI

● Endapo mwananchi yeyote atajenga au kukarabati nyumba bila kibali cha ujenzi toka halmashauri,atapewa ilani ya kusimamisha ujenzi au ukarabati na kushauriwa kufuata taratibu za kuomba kibali cha ujenzi ndani ya siku saba(7).

● Kama mwombaji atakaidi ilani ya kusimamisha jiji au miji litampa ilani ya kubomoa jengo lake mwenyew na akishindwa jiji litabomoa jengo husika na kudai mmiliki gharama za utekelezaji wa ubomoaji.

Imeandaliwa na; UTUKUFU CLEMENT MWANJISI
(Planning officer wa kujitegemea).
Squatter areas nazo zinahusika na haya hasa kwenye majengo ya kawaida?
 
Niongezee tu hata kupaka rangi nyumba yako unahitaji kibali vinginevyo faini! Usifanye shughuri yoyote ya badiliko bila kibali.
 
Kibali cha ujenzi(Building permit), ni moja ya kanuni muhimu sana ya upangaji wa miji nchini Tanzania. kila anaehitaji kujenga anapaswa kufuata kanuni za kibali cha ujenzi atakachopewa, mara nyingi kwa mujibu wa sheria kibali cha ujenzi hutolewa na mamlaka za serikali ambazo ni halmashauri kupitia idara ya mipango miji na mazingira.

Kulingana na sheria ya ujenzi wa majengo mijini Na 101 ya mwaka 2009 si ruhusa kwa mtu yeyote kujenga au kuanza kujenga jengo bila ya kuwa na;

- Uhalali wa umiliki wa ardhi mahali unapojenga.

- Kibali cha ujenzi kutoka mamlaka husika.

1. UMUHIMU WA KIBALI CHA UJENZI

- Kutimiza matakwa ya kanuni za ujenzi mijini.

- Kuwezesha kujenga majengo ya nyumba kama yaliyoelekezwa katika mipango miji ya sehemu husika.

- Kudhibiti ujenzi holela.

2. JINSI YA KUPATA KIBALI CHA UJENZI

- Kuwasilisha michoro ya ramani ya jengo kwa ajili ya uchunguzi.

- Kulipia malipo stahiki ya uchunguzi wa ramani hizo.

- Kulipia malipo ya kiwanja kwa mwaka husika.

3. JINSI YA KUWASILISHA MAOMBI MICHORO YA MAJENGO MAALUMU.

Michoro ya majengo maalumu(Maghorofa, kumbi, Taasisi mbalimbali, Bar, Vituo vya mafuta, Viwanda, Hospital na majengo mengine ya jinsi hiyo iwasilishwe kwa kuanza na michoro ya awali ya kisanifu(Preminary Drawings) ambayo itahusisha.

- Michoro ya sakafu(Floor plan) 1:100

- Sura ya jengo(Elevations) 1:100

- Mkato wa jengo(Section) 1:100

Baada ya uchunguzi wa michoro ya awali kukamilika itawasilishwa michoro ya michoro(Final Drawings) ambayo ni michoro ya kisanifu na ya kihandisi(Architectural and structural drawings) kwa ajili ya uchunguzi.

● Michoro inayowasilishwa izingatie kanuni na taratibu zote muhimu za kiuchoraji(Architectural and Engineering Aspects) na iwe imesainiwa na msanifu majengo/Mhandisi anayetambuliwa(Architectural and Structural Endorsement).

● Michoro hiyo iambatane na nakala ya cheti cha uchunguzi wa athari za kimazingira(Environment Impact Assessment EIA).

● Michoro iambatane na nakala za nyaraka zote halali za umiliki wa kiwanja husika pamoja na stakabadhi ya malipo ya kiwanja kwa mwaka husika.

● Michoro yote iwasilishwe ikiwa na maandishi yanayosomeka(Readable text).

● Michoro yote iwasilishwe kwenye ukubwa wa karatasi(paper size) A0,A1,A2 au A3.

4. JINSI YA KUWASILISHA MAOMBI YA MICHORO YA MAJENGO YA KAWAIDA.

Michoro ya majengo ya kawaida itawasilishwa kwa kuzingatia maelezo ya hapo juu isipokuwa haitatangiliwa na michoro ya awali(Preminary Drawing) kama ilivyo katika michoro ya majengo maalumu.

- MICHORO ILIYOANDALIWA IONYESHE NINI.
●Litakavyokuwa(Plans,Sections,Elevations,Foundation,Roof plan,Site plan).

●Ramani ya kiwanja(Location plan).

●Namba na eneo la kiwanja kilipo.

●Jina la mmilikaji ardhi inayohusika.

●Jina la mchoraji, ujuzi na anuani.

●Ukubwa wa jengo kwa mita za mraba.

●Ujazo wa kiwanja(Plan ratio).

●Urefu wa jengo(Height).

●Matumizi yanayokusudiwa.

●Idadi ya maegesho yatakayokuwepo.

●Umbali kwa jengo kutoka kwenye mipaka ya kiwanja(Setbacks).

●Mfumo wa kutoa majitaka hadi kwenye mashimo.

- VIAMBATANISHO UNAVYOTAKIWA KUWA NAVYO

● Fomu moja ya maombi iliyojazwa kwa usahihi.

● Hati ya kumiliki kiwanja au barua ya toleo.

● Kumbukumbu zingine zinazohusu kiwanja hicho kama hati za mauzo makabidhiano na mengine.

● Nakala ya risiti ya kodi ya kiwanja na kodi za majengo.

● Mabadiliko ya matumizi ya ardhi.

● Ramani ya kiwanja iliyosajiliwa.

- UMUHIMU WA KIBALI CHA UJENZI

● Kutimiza matakwa ya kanuni za ujenzi mijini.

● Kuwezesha kujenga majengo na nyumba kama yaliyoelekezwa katika mipango miji ya sehemu husika.

● Kudhibiti ujenzi holela.

- MUDA WA UPATIKANAJI WA KIBALI CHA UJENZI.

● Endapo mwombaji atakamilisha hatua zote muhimu kwa wakati atapata kibali cha ujenzi ndani ya majuma mawili(2) hadi manne(4).

● Hii ni pamoja na uwasilishaji wa ramani zilizoidhinishwa na wataalamu husika na hati za umiliki zilizo sahihi.

- WAJIBU WA MWANANCHI

Ni wajibu wa kila mwananchi kujenga au kukarabati nyumba yake iliyo ndani ya mji/jiji kwa kibali kutoka halmashauri.

- TAHADHARI

● Endapo mwananchi yeyote atajenga au kukarabati nyumba bila kibali cha ujenzi toka halmashauri,atapewa ilani ya kusimamisha ujenzi au ukarabati na kushauriwa kufuata taratibu za kuomba kibali cha ujenzi ndani ya siku saba(7).

● Kama mwombaji atakaidi ilani ya kusimamisha jiji au miji litampa ilani ya kubomoa jengo lake mwenyew na akishindwa jiji litabomoa jengo husika na kudai mmiliki gharama za utekelezaji wa ubomoaji.

Imeandaliwa na; UTUKUFU CLEMENT MWANJISI
(Planning officer wa kujitegemea).

Nimesoma post na comments zote lakini kuna hoja za msingi naona hazijibiwi.
Kuna wadau wameuliza, vipi walio vijijini ambapo watu wapo mashambani mwao na hayajapimwa?
Watanzania wengi wanaishi vijijini na wanajenga na kuishi, tena na umeme wamewekewa. Vipi mnasemaje kuhusu watu hawa sheria inasemaje?
 
Tutakupa elimu bure ili ukafuatilie mwenyew labda kukusaidia tutakupatia watu waliopo katika wilaya husika wakusaidie kwa haraka zaidi mana tunafahamiana kutokana na mwingiliano wa kazi zetu
Mkuu wewe kazi yako mama ni nini? Ebu weka wazi kama kuna kazi tukupe.
 
Mkuu wewe kazi yako mama ni nini? Ebu weka wazi kama kuna kazi tukupe.
Sisi tuna kampuni mkuu tunafanya shughuli zote zinazohusu ardhi kama urasimishaji,upimaji maeneo,uuzaji viwanja tulivopima wenyew na ununuaji maeneo makubwa tunayakata viwanja then tunaviuza,ukihitaj kutafutiwa hati miliki,ukihitaji kucholewa ramani za majengo karibu.


Ofisi zetu zipo Mbezi beach Tangi bovu jengo la TEVI COMMERCIAL PARK ghorofa ya tatu

au
Tupigie 0713132109,0752602988
 
Nimesoma post na comments zote lakini kuna hoja za msingi naona hazijibiwi.
Kuna wadau wameuliza, vipi walio vijijini ambapo watu wapo mashambani mwao na hayajapimwa?
Watanzania wengi wanaishi vijijini na wanajenga na kuishi, tena na umeme wamewekewa. Vipi mnasemaje kuhusu watu hawa sheria inasemaje?
Vijijini nyumba za ghorofa na zinazoeleweka kwa kupima kiwanja na hati na hizo ndizo hulipiwa kodi vinginevyo mababu zako walizaliwa nayo.
 
Kibali cha ujenzi(Building permit), ni moja ya kanuni muhimu sana ya upangaji wa miji nchini Tanzania. kila anaehitaji kujenga anapaswa kufuata kanuni za kibali cha ujenzi atakachopewa, mara nyingi kwa mujibu wa sheria kibali cha ujenzi hutolewa na mamlaka za serikali ambazo ni halmashauri kupitia idara ya mipango miji na mazingira.

Kulingana na sheria ya ujenzi wa majengo mijini Na 101 ya mwaka 2009 si ruhusa kwa mtu yeyote kujenga au kuanza kujenga jengo bila ya kuwa na;

- Uhalali wa umiliki wa ardhi mahali unapojenga.

- Kibali cha ujenzi kutoka mamlaka husika.

1. UMUHIMU WA KIBALI CHA UJENZI

- Kutimiza matakwa ya kanuni za ujenzi mijini.

- Kuwezesha kujenga majengo ya nyumba kama yaliyoelekezwa katika mipango miji ya sehemu husika.

- Kudhibiti ujenzi holela.

2. JINSI YA KUPATA KIBALI CHA UJENZI

- Kuwasilisha michoro ya ramani ya jengo kwa ajili ya uchunguzi.

- Kulipia malipo stahiki ya uchunguzi wa ramani hizo.

- Kulipia malipo ya kiwanja kwa mwaka husika.

3. JINSI YA KUWASILISHA MAOMBI MICHORO YA MAJENGO MAALUMU.

Michoro ya majengo maalumu(Maghorofa, kumbi, Taasisi mbalimbali, Bar, Vituo vya mafuta, Viwanda, Hospital na majengo mengine ya jinsi hiyo iwasilishwe kwa kuanza na michoro ya awali ya kisanifu(Preminary Drawings) ambayo itahusisha.

- Michoro ya sakafu(Floor plan) 1:100

- Sura ya jengo(Elevations) 1:100

- Mkato wa jengo(Section) 1:100

Baada ya uchunguzi wa michoro ya awali kukamilika itawasilishwa michoro ya michoro(Final Drawings) ambayo ni michoro ya kisanifu na ya kihandisi(Architectural and structural drawings) kwa ajili ya uchunguzi.

● Michoro inayowasilishwa izingatie kanuni na taratibu zote muhimu za kiuchoraji(Architectural and Engineering Aspects) na iwe imesainiwa na msanifu majengo/Mhandisi anayetambuliwa(Architectural and Structural Endorsement).

● Michoro hiyo iambatane na nakala ya cheti cha uchunguzi wa athari za kimazingira(Environment Impact Assessment EIA).

● Michoro iambatane na nakala za nyaraka zote halali za umiliki wa kiwanja husika pamoja na stakabadhi ya malipo ya kiwanja kwa mwaka husika.

● Michoro yote iwasilishwe ikiwa na maandishi yanayosomeka(Readable text).

● Michoro yote iwasilishwe kwenye ukubwa wa karatasi(paper size) A0,A1,A2 au A3.

4. JINSI YA KUWASILISHA MAOMBI YA MICHORO YA MAJENGO YA KAWAIDA.

Michoro ya majengo ya kawaida itawasilishwa kwa kuzingatia maelezo ya hapo juu isipokuwa haitatangiliwa na michoro ya awali(Preminary Drawing) kama ilivyo katika michoro ya majengo maalumu.

- MICHORO ILIYOANDALIWA IONYESHE NINI.
●Litakavyokuwa(Plans,Sections,Elevations,Foundation,Roof plan,Site plan).

●Ramani ya kiwanja(Location plan).

●Namba na eneo la kiwanja kilipo.

●Jina la mmilikaji ardhi inayohusika.

●Jina la mchoraji, ujuzi na anuani.

●Ukubwa wa jengo kwa mita za mraba.

●Ujazo wa kiwanja(Plan ratio).

●Urefu wa jengo(Height).

●Matumizi yanayokusudiwa.

●Idadi ya maegesho yatakayokuwepo.

●Umbali kwa jengo kutoka kwenye mipaka ya kiwanja(Setbacks).

●Mfumo wa kutoa majitaka hadi kwenye mashimo.

- VIAMBATANISHO UNAVYOTAKIWA KUWA NAVYO

● Fomu moja ya maombi iliyojazwa kwa usahihi.

● Hati ya kumiliki kiwanja au barua ya toleo.

● Kumbukumbu zingine zinazohusu kiwanja hicho kama hati za mauzo makabidhiano na mengine.

● Nakala ya risiti ya kodi ya kiwanja na kodi za majengo.

● Mabadiliko ya matumizi ya ardhi.

● Ramani ya kiwanja iliyosajiliwa.

- UMUHIMU WA KIBALI CHA UJENZI

● Kutimiza matakwa ya kanuni za ujenzi mijini.

● Kuwezesha kujenga majengo na nyumba kama yaliyoelekezwa katika mipango miji ya sehemu husika.

● Kudhibiti ujenzi holela.

- MUDA WA UPATIKANAJI WA KIBALI CHA UJENZI.

● Endapo mwombaji atakamilisha hatua zote muhimu kwa wakati atapata kibali cha ujenzi ndani ya majuma mawili(2) hadi manne(4).

● Hii ni pamoja na uwasilishaji wa ramani zilizoidhinishwa na wataalamu husika na hati za umiliki zilizo sahihi.

- WAJIBU WA MWANANCHI

Ni wajibu wa kila mwananchi kujenga au kukarabati nyumba yake iliyo ndani ya mji/jiji kwa kibali kutoka halmashauri.

- TAHADHARI

● Endapo mwananchi yeyote atajenga au kukarabati nyumba bila kibali cha ujenzi toka halmashauri,atapewa ilani ya kusimamisha ujenzi au ukarabati na kushauriwa kufuata taratibu za kuomba kibali cha ujenzi ndani ya siku saba(7).

● Kama mwombaji atakaidi ilani ya kusimamisha jiji au miji litampa ilani ya kubomoa jengo lake mwenyew na akishindwa jiji litabomoa jengo husika na kudai mmiliki gharama za utekelezaji wa ubomoaji.

Imeandaliwa na; UTUKUFU CLEMENT MWANJISI
(Planning officer wa kujitegemea).

TUKUTANE MAHAKAMANI
 
Nimesoma post na comments zote lakini kuna hoja za msingi naona hazijibiwi.
Kuna wadau wameuliza, vipi walio vijijini ambapo watu wapo mashambani mwao na hayajapimwa?
Watanzania wengi wanaishi vijijini na wanajenga na kuishi, tena na umeme wamewekewa. Vipi mnasemaje kuhusu watu hawa sheria inasemaje?
kwa ufupi mkuu mana muda kidogo unabana;

kibali kinatakiwa kufwatwa nchi nzima ndio sheria inavotaka lakini Inatokana na wilaya husika una play vipi hili suala kwa wananchi wake ingawa wilaya nyingi ambazo ziko vijijin wameliacha kutokana na hari za kiuchumi za wananchi wao lakini wilaya za mijini lazima
 
Kwa maelekezo yako hakiwezi kosa kuwa na gharama ni kitu kinachohusisha taasisi na watu wenye taaluma mbalimbali
Kibali ukiwa na 150000 kwa wilaya kama ubungo unakipata haraka tu kikubwa uwe na michoro iliyochorwa na wataalamu
 
Back
Top Bottom