Fahamu kuhusu VPN

Hapana, si lazima VPN hapo. Kuna mifumo mingi siku hizi ya kumuwezesha mtu kuitumia system/ computer ya ofisini kwake akiwa nyumbani/ akiwa popote. Lakini umuhimu wa VPN unakuja pale ambapo mfumo huo unaruhusu kutumika kwenye location fulani tu na pia kulinda data.

Ili VPN ifanye kazi unachohitaji kikubwa ni internet tu. Zaidi ya hapo ni kufuata malekezo ya VPN provider unayemtumia juu ya namna ya ku-connect na kuchagua location. Wamerahisisha sana siku hizi kiasi ambacho huhitaji kuumiza kichwa kufanya vitu manual - sehemu kubwa vitu vinafanya kazi automatically; just click and go!
 


Mdau kauliza VPN kama VPN wewe umemjibu kuhide location and so so!!! Hizo ulizotaja ni App za VPN za kuhide location ila IT wa Kampuni husika wanatumia pia VPN(Sio Apps wanakupa Public IP na credentials) kuweza kuaccess system zao ili waweze kufanya kazi wakiwa home.

 
Naambiwa ukitumia VPN network inakuwa slow sana. Limekaaje hili
VPN INAPUNGUZA KASI YA NETWORK?

Ndio na hapana - yote inategemea na mambo kadhaa. Unaweza kutumia VPN halafu network ikaenda kwa kasi ileile, au unaweza uka-connect kwenye VPN halafu ghafla ukaona network inaangukia pua. Kwa ujumla, ni vizuri kutarajia mabadiliko ya kasi ya mtandao unapotumia VPN, lakini usitarajie kila unapotumia VPN basi network inapungua kasi papo kwa papo. Wakati mwingine unaweza usigundue kama spidi imepungua.

SASA KWANINI VPN INAPUNGUZA SPEED YA NETWORK?

Nakupa sababu 7 za kwanini VPN inaivuta shati network yako;

1. Location ya Server.
Umbali halisi kati yako wewe na VPN server unayotumia unachangia sana kuamua ni kasi kiasi gani ya network utapata. Kwanini? Kwasababu inachukua muda mrefu zaidi kwa zile data packets kusafiri kati yako na VPN server. Kadiri unavyokuwa mbali na server ndivyo speed ya network inayokuwa slower.

2. Ukomo wa Server Bandwidth.
Kama VPN server unayotumia ina kitu tunaita bandwidth limitations, basi speed ya network lazima ipungue pale unapogonga limit au server ikizidiwa (Mkiwa watu wengi mnaitumia kwa wakati mmoja). Pia server kama server yenyewe ina impact kwenye speed ya network kulingana na aina yake; kama ni server ya ubora mdogo basi na kasi itaathirika kulinganisha na High quality servers.

3. Aina ya Encryption.
Inategemea aina ya encryption ya VPN protocol unayotumia - kama unatumia stronger encryption basi kasi ya network inaangukia pua. Lakini si mara zote, na wakati mwingine huwezi kugundua kabisa. Kwa ujumla encryption aina ya OpenVPN protocol ndo mara nyingi inapunguza kasi ya network, wakati PPTP ina kasi kubwa. Lakini PPTP ni hatari zaidi kwasababu haina reliable encryption. Aina zingine ni IKEv2, L2TP/IPSec na SoftEther protocol.

4. Firewall.
Firewalls mara nyingi haziathiri kasi ya VPN lakini huwa zinaweza kuharibu mambo kama imesetiwa kuingilia traffic ya VPN au performance ya CPU yako. Niongezee hapa kuwa kasi ya CPU yako pia ni sababu inayochangia mabadiliko ya kasi ya network. Kama unatumia CPU za kizamani badi ni sababu mojawapo ya kukuchelewesha.

5. Network Setup
Kuna watumiaji wa VPN wamegundua kuwa kuna utofauti ukiwa unatumia internet ambayo connection yake ni ya router ambayo ina LAN cable ukilinganisha na kutumia WiFi. Jaribu kubadilisha connection yako, hamia kwenye kutumia WiFi, utaona utofauti.

6. VPN Routing Algorithms
Kuna uwezekano VPN provider wako ana-route connection yako kati ya server nyingi, na wakati mwingine ana-route data zako pia. Hiyo safari ndo sababu mojawapo ya ku-slow down kwa VPN speed. Hii ni kawaida sana kwa FREE VPNs... vya bure vina gharama zake.

7. Kasi ya netwrok yako.
Mwisho wa siku, unatumia mtandao gani? TTCL, Halotel, Voda, Tigo au Zantel. Hakikisha unatumia mtandao ambao una kasi, tunaongelea angalau ya 3G kwenda juu. Siwezi sema mtandao gani una kasi zaidi - inategemea uko wapi.

Bila shaka nimejibu swali lako mkuu.
 
Shukrani kwa kuniweka sawa mkuu. Umetisha.
 
Ume-connect?
Mkuu nimeeka hiyo hoxx VPN ila nitajuaje inafanya kazi muda huu ??
Ume-connect? Itakuonesha kuwa upo connected. Na pia kama ulienda sawa basi ulichagua location mwanzo kabisa kabla ya ku-connect.
 

Tayari nimesha install kwenye Computer then what next?
 
Asante. Wewe umenielewa vizuri swali langu. Kwa hiyo hizo credential na public ip pekee ndio zatakiwa? Kuset hizo Credential na hiyo public ip unaenda wapi ? Hii pic ulioweka ni app gani? Ya kwenye simu au pc?
 
Asante. Wewe umenielewa vizuri swali langu. Kwa hiyo hizo credential na public ip pekee ndio zatakiwa? Kuset hizo Credential na hiyo public ip unaenda wapi ? Hii pic ulioweka ni app gani? Ya kwenye simu au pc?

Hiyo ni window app inaitwa cisco anyconnect(VPN connection zipo apps nyingi mostly used ni Anyconnect ya cisco) ,ukiifungua kwenye blank space unaweka hiyo Public IP kisha unaclick connect then inakuja sehemu ya kujaza hizo credentials ambazo unapewa na VPN provider(IT wa kampuni yako) then unaclick Ok fter that Unakuwa tayari connected na VPN ,ukishakuwa succesffully connected na VPN ina maana unakuwa upo kama kwenye Local Network yako(LAN) hapo kama wamekupa access the server zako unaweza uka RDP(Remote Desktop IP ya Server yako kisha ukaingia na kufanya kazi zako)!!

Note:Lazima uwe na internet ili kukuwezesha kuconnect VPN via Public IP.
 
Shukrani sana
 
Uzi makini sana shukrani mleta mada
 
Hii list bila Nord VPN & Express VPN ni batili! I'm sorry usinielewe vibaya...
 
mkuu kuna kitu nimekutana nacho kinaitwa intranet..ni nn hasa? Na kazi yake je?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…