Fahamu utajiri uliopo kwenye uwekezaji wa dhamana za Serikali (Treasury Bills & Bonds)

kwa hii govt inayolia kila siku haina hela, hatutazinguana mbeleni? mf pension funds, kandarasi, wazabuni, local bank nk
hamna mkuu zoezi Zima linasimamiwa ki uadilifu sana banki kuu. Hivo ni ngumu serikali Ita default katika kulipa.

Endapo uchumi ukilega lega kama yaliyowakuta ugiriki ndo serikali inaweza kushindwa kulipa. Ila so far kwa Tanzania tupo safe.

Lakini ulichosema ni sahihi kabisa kwamba endapo nchi ikifilisika basi inaweza kushindwa kulipa. Hiyo ni kweli na ndicho kinachotokea ugiriki sasahiv. Lakini kwa Tanzania hilo sio rahisi sana maana hata banki kuu nadhani wapo makini sana kwenye Hili.
 
Mkuu Davion Delmonte Jr. samahani kama nitakua narudia kuuliza kile ulichoelezea ningependa kujua kwa ufasaha zaidi ni namna gani au utaratibu ukoje ile uweze kununu hizo bonds (yaani kama kuna kujisajili kwanza mambo yakoje).
swali la pili ni je mfumo huu ni tofaut na ule wa UTT na mifuko yao au ni sawa??
 
Last edited by a moderator:
kama unataka kununua bonds pindi BOT wanavo announce kuna form zinaitwa BOT-FORM GBI ambazo utadownload kwenye website yao. Maelezo yote yapo pale namna ya kuijaza. Kama unaona inachanganya kidogo unaweza ukapitia kwa ma broker japo yaweza kuwa na charges lakini kama ukiamua mwenyewe inawezekana pia.

suala lingine ni kwamba UTT na bonds ni vitu tofauti kabisa ntalielezea hilo kwa mapana kwani kunachapisho la uelewa juu ya UTT.
 

Your calculation looks good and attractive on paper, but I'm afraid in real world kweli unaweza kununua treasury bills ya miez mitatu ya face value of 100 million, ukanunua kwa 75million..... Actually sijawahi kununua dhamana za serikali mimi ni graduate wa finance ndo nimemaliza mwaka huu but niko very interested kwenye financial securities nitakapokuwa vizuri nitahusika sana DSE, nimefurahi sana kuona huu uzi wako... Yan umeundikika kimadesamadesa hadi raha... Ila tu nimeshangaa kuona mfano wako wa treasury bill ambayo ni risk free and short-term hlf inatoa return kubwa... Wengi watavutika ila in real word inaweza isiwe profitable sana kama mfano wako maana from wat I know watu huwa wanainvest kwenye bonds(defensive securities) ili kupunguza risk iliyoko kwenye stocks(aggressive securities), hivyo sikutarajia sana kuona return kubwa kiasi hicho inatoka kwenye treasury bills... Ila inawezekana ikawa sahihi maana mimi ni mgeni sana kwenye soko la dse
 
Sema vile watu hawajui.. Lakini faida za kuwa na hizi financial assets ni kubwa mno. Kuliko unavoweza kufikiri

Mkuu nimezoea kuona nmb...crdb...swala...kenya airway wakiuza hisa...je hizi hisa sijui unaziita bond za serikali zinatofautiana vipi na hizi za nmb...crdb and the alike???
Je nikitaka nunu hisa za serikal ntazipata wapi??? Wapi wanatangaza...ntajua vipi kwamba mda flani wanauza???
 
ulichosema ni sahihi kwamba inflation na kupanda kwa dola kunaweza kushusha thamani ya uwekezaji wako. Lakini ukiangalia kwa upande mngine hiyo milioni 10 kama ungeiacha bank ungeumia zaidi kwa sababu hiyo faida ya 3 milioni siyo haba.

Japo nipo nje ya mada....kwa ujuzi wako kwa nn hisa za NMB zinaporomoka kwa kasi??? Tokea 4000 mpaka 2700 !!! Nini sababu??? Na kipind hiki ni kipindi rafiki kwa ununuzi wa hisa??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…