Fahamu vitu vinavyotofautisha gharama za ujenzi kwenye majengo yenye kufanana mchoro

Fahamu vitu vinavyotofautisha gharama za ujenzi kwenye majengo yenye kufanana mchoro

Kuna kitu nmeona kinajadiliwa hapa kuhusu ground beam, wengi wanasema eneo lenye kichanga halihtji ground beam, lakini kama ukifanya soil investigation kawaida ya hali ya udongo huwa inabdlika kulingana na mda.. Pia udongo huwa ina tabia ya kujongea. Eneo unalojenga wewe inawezekana kukwa na mchanga lakini mita 10 toka ulipo kukwa na udongo wa aina nyingine.

Nini umuhimu wa ground beam. Kazi kubwa ya ground beam n kuzuia un equally settlements (kutitia kwa nyumba kusikokua sawa) unapoeka mkanda au ground beam unafanya nyumba yako ititie kwa pamoja hvo kuzuia nyufa zisitokee kwenye nyumba..


Ushauri wangu ni muhimu kueka ground beam regardless ya aina udongo sababu tabia ya udongo huwa haitabadiliki...
 
Hapa nitaelezea Sababu za msingi zinazosababisha majengo yanayofanana kujengwa kwa gharama tofauti.

Tuzungumzie mchoro wa nyumba ya vyumba vitatu vya Kulala kimoja kati ya hivyo ni master bedroom, sitting room, dining, kitchen ,public toilet na store.
Mchoro aliununua ndugu anaitwa Juma, baada ya Juma kununua Alitoa copy akawapa majirani zake wawili Hasani na John.

Hawa wote walijengewa na fundi mmoja ambae ni mimi. Lkn Kila mtu kutumia gharama tofauti kusimamisha boma.

SABABU ZA MSINGI ZA KUFANYA GHARAMA ZA UJENZI ZITOFAUTIANE :

1. location
2. Uimara
3.land type. (slop au tambalale)
4.soil type
5.nyakati.

HAPA NITAZUNGUMZIA UIMARA
Msingi wa nyumba imara utajengwa Kama ifuatavyo.
. Utachimbwa kwenda chini urefu WA mita moja au zaidi.
. Utaanza na zege yenye ratio nzuri kabla ya kujenga tofali
.Utajengwa kwa tofali imara
.Utawekewa Beam yenye kusukwa nondo na ratio nzuri
.Utamwagiliwa maji ya kutosha.
ILI HAYA YOTE YAFANYIKE LAZIMA UMPATE FUNDI MZURI.

Juma aliomba nyumba yake nimjengee kwa viwango hivyo, ndio maana nilitumia tofali nyingi,cement nyingi, nondo nyingi, mchanga mwingi, kokoto nyingi, ring za kutosha, maji mengi nk. Ktk kujenga msingi.

John alisema uwezo wake mdogo , yeye alihitaji tuchimbe futi moja kwenda chini baada ya hapo tujenge tofali, hakuishia hapo pia alisema tusiweke Beam.

Kilichotekea ni utofauti wa Tshs zaidi ya million nne kati ya hiyo misingi miwili.

Kiufupi Juma alitumia 6mil
John Tshs 2.8mil
Hasani Tshs 4mil.

Kilichotofautisha ni uimara WA kujenga msingi. Hawa wote ni majirani.

Mpaka tunamaliza boma Juma alitumia 18m
John 7m
Hasani 12m.
Nyumba zote hizi zikipigwa rangi vizuri hutoweza kujua madhaifu ya awali mpaka pale utakapoanza kuona nyufa (expansion joint)

Hoja yangu hapa ni kwamba unapotokea mjadala wa gharama za ujenzi LAZIMA tuzingatie vitu mhimu vinavyosababisha gharama kuwa kubwa au ndogo.

Ushauri.
1.Tusipende kukimbilia kununua nyumba wakati hujui ilijengwa kwa viwango vipi.
2.Jenga nyumba imara ogopa vya Bei cheee
3.Nyumba kuijenga si lelemama, ili kumudu anza mdogomdogo. Ukiwa na 5m anza hata msingi.

Ukihitaji fundi, usisite kunitafuta, Hakina utaenjoy service yangu.
0655173113


UPDATES
tuendelee na mjadala wetu. Hapo awali tulijadili jinsi namna gani uimara wa nyumba unavyoathiri gharama za ujenzi. Leo tujadili namna location inavyoathiri gharama za ujenzi.

NAMNA LOCATION INAVYOSABABISHA GHARAMA ZA UJENZI KUWA TOFAUTI.

Mungu aliumba ardhi ktk mionekano tofauti. Kuna tambalale, milima na mabonde.
Ujenzi ktk Eneo tambalale unagharama nafuu kulinganisha na Eneo lenye slope . Lakini pia ujenzi wa Eneo tambalale lililoko Chanika mkoni DSM Unaweza kuwa na gharama tofauti na ujenzi wa Eneo tambalale lililoko msasani mkoani DSM. Hivyo hivyo ujenzi wa DSM unagharama kubwa kuliko ujenzi wa Mbeya.

SABABU ZA KUTOFAUTISHA GHARAMA KATI YA ENEO TAMBALALE NA LENYE SLOP.

sanasana hapa kimbembe huwa ktk kujenga msingi wa nyumba.

Msingi uliotumia tofali 1500 katika eneo tambalale, msingi huohuo ukitaka kuujenga ktk eneo lenye slope unaweza kutumia tofali 2300 au zaidi kulingana na ukali wa slope.
Tukumbuke kwamba Kwa kadri tofali zinavyoongezeka ndivyo na material mengine yanavyozidi kuongezeka kitu ambacho hupelekea kuongezeka kwa gharama za fundi. Si ajabu kumalizia 10mil ktk msingi wa nyumba ya Vyumba vitatu ktk Eneo LA slope.

Hivyo basi kama hutaki kutumia gharama kubwa kwenye ujenzi epuka kununua viwanja vilivyo na slope.

Jambo lingine linaloathiri ktk location ni upatikanaji wa material.
Mfano mtu anaejenga mbezi beach atanunua tani 18 Za mchanga zaidi ya 450.000 Tshs wakati mtu wa Chanika atanunua Kwa 220,000tshs.

Pia boma utakalojenga kwa 8mil Mbeya, DSM utalijenga Kwa zaidi ya 15mil. Sababu Mbeya tofali ni cheap, labour ni cheap nk.

Kwa ujenzi imara na wakisasa tutafutane 0655173113
Hapa ndiyo tutaelewa concept ya Jenga Uza. Ni nyumba za kiwango duni sana. Mjenzi amatumia minimum amount ili aje apate faida kubwa akiuza. Likipita tetemeko dogo tu,nyumba yote inageuka kifusi.
 
Mleta mada nakupongeza kwa kuipenda kazi yako. Ila nakuomba pia uwe unatumia ushauri wa wataalamu wa ujenzi. Namaanisha uchote maarifa kwa Architects, Engineer na Quantity Surveyor. Mie nimesoma ujenzi na nimepitia maelezo yako naona kama hayajajitosheleza pengine ni kutokana na ufahamu wa kitaalamu. Kwa mfano, nyumba sio lazima iwe na ground beam, kuna sababu hupelekea iwepo au isiwepo.kwa hiyo wakati mwingine mnaongezea gharama za ujenzi zisizokuwa za lazima kwa kigezo/kauli mbiu ya nyumba imara

Sent using Jamii Forums mobile app
Nami pia nimo katika tasnia hii ya ujenzi, mtoa maada kaeleza vizuri ingawa vipo ambavyo kateleza kidgo lakini kwa vile anasema yeye ni fundi basi anahitaji pongezi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanini nyumba zetu huwa zina majiko ndani lakini hazina sehemu za kutolea moshi nje?! Tangu kwa archtecture mpaka kwa civil engineer.
Kwanini mjenzi haachi maeneo ya kuweka vyoo, anamwaga zege kisha anakuja kutindua zege, wakati alifahamu tangu mwanzo kutawekwa mfumo wa maji machafu, na hata maji masafi, kwanin yasiwekwe wakati wa ujenzi wanasubiri jadi nyumba inaisha wanaanza gharama za kutindua zege na ukuta?!
Mnaposoma huwa hamfundishwi au ni ujinga wa wataalam wetu?!
Hilo ni kosa la Architecture na Mara nyingi hua inatokea kwa mtu ambaye anajenga vitu vikubwa lakini anataka mafundi wa bei rahisi.

Mfano katika majengo kama hayo lazima uweke duct za kufanya yote hayo...
Ushawahi kujiuliza kwann maghorofa mengi ya uswahilini yanaonyesha bomba za maji kwa nje, bomba hazipaswi kuonekana kwa nje ya jengo iwe ni storm water, grey water n.k

Sent using Jamii Forums mobile app
 
We muongo mafundi wote mnajenga na kutindua, kuhusu chimney inahitajika kwenye majiko yote popote sio lazima kuwe na baridi, sema hamjui lakini sio kusingizia baridi.
Architecture anachora nyumba haweki chimney, ok unawrza kusema ni kazi ya structure engineer lakini naye haweki.
Masaki zile nyumba zilijengwa na wazungu zina chimney, wao hawana joto pale?!
Siyo kwamba muongo, jengo ili likamilike inabidi watu wote washirikishwe
Architecture
Engineer
Electrical
Plumber
M.E.P n.k
Wengi wanajenga lakini hawashirikishi hao watu, hii naongelea majengo ya ghorofa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuongezea nyama hapo( kwa idhini ya mleta mada) hiyo issue huja kutokana na type ya udongo wa eneo husika. Bila shaka akifika kwenye kipengele hicho ataelezea kwa undani, naamin huwezi mwaga mchanga 75mm sehem yenye mchanga ili uanze ujenzi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Naam,
Kwenye mchango 75mm ni nyingi mno, Sifa moja ya Mchanga hua ukifanya settlement basi hua mara moja tuu,
Tofauti na clay soil
Ndo maana treatment za kujenga sehemu yenye clay soil ni tofauti na sehemu yenye sand

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nylon ni kwaajili ya kuzuia unyevunyevu.

Kujenga sehemu yenye mfinyanzi yahitaji umakini sana. Ogopa sana ule Udongo unaopasuka ukiwa mkavu, ndiyo chanzo cha nyufa.

Kichanga ni udongo ambao hauna madhara na unaweza hata usiweke beam
Hapa niko tofauti na wew me nimesurvey maeneo mengi ya pwani kuanzia Kibaha kuja hadi Dar ambako kuna udongo wa kichanga, nyumba nyingi zikijengwa huwa naona zina ufa inaweza isiwe kubwa sana ila lazima unakuta kuna viufa kwenye msingi lakin maeneo ya Kaskazin kama K'njaro na arusha sijawahi kuoa hivyo viufa kama nakosea nirekebishwe
 
nondo ndogo za kufunga nondo kubwa au bangili hizo ndo zina kazi ya kuzuia cracking kitaalam
Nimekusoma mkuu. Naomba unishauri au maoni ktk hili;
Kuna nyumba ndogo yenye chumba na sebule na choo/bafu. Urefu m8 na upana m5, msingi wake umewekewa nondo 2 (zimelazwa)pamoja na hizo stirrups. Udongo wa eneo ni aina ya kichanga.
 
Nimekusoma mkuu. Naomba unishauri au maoni ktk hili;
Kuna nyumba ndogo yenye chumba na sebule na choo/bafu. Urefu m8 na upana m5, msingi wake umewekewa nondo 2 (zimelazwa)pamoja na hizo stirrups. Udongo wa eneo ni aina ya kichanga.
Nondo mbili?? Nondo mbili wamezifungaje hao mafundi..
Kitaalamu ground beam au beam yoyote inahtaji angalau nondo 4 za kuanzia mm 12,kwenda mbele.. Kwa nn ziwe nondo 4..
Beam nyingi znazosukwa huwa ni mstatili au mraba.. Na mara nyingi hayo maumbo huwa yana pembe 4,kitaalamu kwenye pembe ya beam ndo eneo ambalo linakua zaidi lipo hatarini kwenye kupatwa na nyufa. Hvo wataalam wanshauri angalau kwenye kila pembe ya Beam ipate nondo moja. Hvo ukiwa na beam ya mstatili, au Mraba lazma uwe na nondo 4 znazocover eneo lote la beam..

Sababu ya pili ni kuwa ili uwezd kumaintain shape ya beam yako, pamoja na cover (uwazi unaoachwa kati ya outer surface ya beam na nondo) unatakiwa uekwe nondo 4 ili kila pande iwe na cover.. Sasa unapoeka nondo mbili inakua vigumu kuipata shape ya pembe 4 ya beam yako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nondo mbili?? Nondo mbili wamezifungaje hao mafundi..
Kitaalamu ground beam au beam yoyote inahtaji angalau nondo 4 za kuanzia mm 12,kwenda mbele.. Kwa nn ziwe nondo 4..
Beam nyingi znazosukwa huwa ni mstatili au mraba.. Na mara nyingi hayo maumbo huwa yana pembe 4,kitaalamu kwenye pembe ya beam ndo eneo ambalo linakua zaidi lipo hatarini kwenye kupatwa na nyufa. Hvo wataalam wanshauri angalau kwenye kila pembe ya Beam ipate nondo moja. Hvo ukiwa na beam ya mstatili, au Mraba lazma uwe na nondo 4 znazocover eneo lote la beam..

Sababu ya pili ni kuwa ili uwezd kumaintain shape ya beam yako, pamoja na cover (uwazi unaoachwa kati ya outer surface ya beam na nondo) unatakiwa uekwe nondo 4 ili kila pande iwe na cover.. Sasa unapoeka nondo mbili inakua vigumu kuipata shape ya pembe 4 ya beam yako

Sent using Jamii Forums mobile app
Shukrani mkuu kwa maelezo yako. Si unajua wa mafundi mtaani mambo yao.
Kama hutojali unaweza weka picha za hizo beam mkuu?
 
Nunua kiwanja tambalale, ikiwa Sehemu ya kichanga itapendeza zaidi.
Wakati unajenga msingi chimba mashimo ya vyoo ili kupunguza gharama za kifusi.
Kuwa na mahusiano mazuri na fundi ili asikununulishe vitu vya gharama bila Sababu.
Usimbane fundi Kuhusu malipo yake, atakupa Ushauri mzuri wa kupunguza gharama bila kupunguza ubora
Naomba kujua:-

1. mfuko mmoja cement ya kawaida unawezajengea tofali ngapi kupandisha boma kwa kutumia tofali za block za nchi 5?

2.Naomba pia kujua mfuko mmoja cement ya kawaida unawezajengea tofali ngapi za msingi za block za nchi 6?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nondo mbili?? Nondo mbili wamezifungaje hao mafundi..
Kitaalamu ground beam au beam yoyote inahtaji angalau nondo 4 za kuanzia mm 12,kwenda mbele.. Kwa nn ziwe nondo 4..
Beam nyingi znazosukwa huwa ni mstatili au mraba.. Na mara nyingi hayo maumbo huwa yana pembe 4,kitaalamu kwenye pembe ya beam ndo eneo ambalo linakua zaidi lipo hatarini kwenye kupatwa na nyufa. Hvo wataalam wanshauri angalau kwenye kila pembe ya Beam ipate nondo moja. Hvo ukiwa na beam ya mstatili, au Mraba lazma uwe na nondo 4 znazocover eneo lote la beam..

Sababu ya pili ni kuwa ili uwezd kumaintain shape ya beam yako, pamoja na cover (uwazi unaoachwa kati ya outer surface ya beam na nondo) unatakiwa uekwe nondo 4 ili kila pande iwe na cover.. Sasa unapoeka nondo mbili inakua vigumu kuipata shape ya pembe 4 ya beam yako

Sent using Jamii Forums mobile app
Vipi kuhusu beam yenye nondo 3 mtaalam?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom