Fahamu zaidi kuhusu kinga ya Ukimwi iitwayo PEP

Fahamu zaidi kuhusu kinga ya Ukimwi iitwayo PEP

Hapo tatizo lako litakuwa ni kuona au kuambiwa lakini usijue au usielewe uhalisia wa kilichotokea.Maswali kama haya nilishaulizwa sana na usifikiri kwamba kuna utata hata kidogo.Cha msingi ni kujua kwa undani historia nzima na aina ya maisha ambayo wapenzi hao walikuwa wanaishi.

Sasa ili niweze kujibu swali lako,nahitaji mfano ulioshiba taarifa sahihi ili niweze kukwambia kwa nini hilo lilitokea,vinginevyo itakuwa ni hisia tu.Kuna uwezekano mkubwa watu hao watakuwa wametumia ARVs wote wawili.Pia umeshasahau kwamba vipimo vya HIV vinaweza pia kutoa majibu ya HIV+ kwa mtu yeyote yule hata kama hajawahi kushiriki ngono au kuchangamana damu na mtu mwingine,ndio maana nikakwambia vipimo ni mojawapo ya kanyaboya ambalo waliotudanganya wanatumia ili kurubuni akili zetu ili tuweze kutumia dawa zao zenye sumu ambazo ndio zinatuangamiza huku tukimsingizia HIV ambaye ni hewa.

Mimi pia kuna familia ninaifahamu,baba,mama na mtoto wao mchanga walikufa kwa dalili moja.Baada ya kuchunguza kumbe wote walikufa kwa TB.TB huambukizwa kwa njia ya hewa,baba,mama na mtoto hulala kwenye kitanda kimoja kila siku,nadhani unaelewa namaanisha nini.Mwenye TB ni rahisi kumpima HIV+ kutokana na sayansi ya vipimo vya HIV ilivyo.Hii ni case study moja tu ya mfano ambayo ninaijua kwa undani.Sasa inabidi ulete case study ambayo una taarifa za kutosha ili tuijadili,vinginevyo utakuwa unatumia hisia tu,na hapo ndipo maana ya HIV/AIDS kuitwa mindset disease inapokuja.

Mfano wa hao watu niliowasemea ni kipindi cha nyuma sana kabla ya ujio wa ARV's na watu walikufa kwa vipindi vinavyokaribiana, kuna mtu alikuwa anatuhumiwa kuambukiza watu kwa makusudi.
 
Mfano wa hao watu niliowasemea ni kipindi cha nyuma sana kabla ya ujio wa ARV's na watu walikufa kwa vipindi vinavyokaribiana, kuna mtu alikuwa anatuhumiwa kuambukiza watu kwa makusudi.

Bado hujatoa case study iliyoshiba taarifa sahihi,ni hisia tu hizo ambazo zinasababishwa na ukosefu wa uelewa sahihi.Kumbuka kwamba TB nayo ina dalili zinazofanana kabisa na zile ulizoambiwa kwamba ni za ukimwi,pia TB inaua.Na nilishakwambia kwamba TB ni mojawapo ya condition ambayo inaweza ika trigger vipimo kutoa majibu ya HIV+ kama ulinifuatilia vizuri,hivyo mtu anaweza asile ARVs lakini akafa kwa dalili kama zile ulizoambiwa kwamba ni ukimwi kwa sababu TB nayo inaua,na pia anaweza kumuambukiza mtu mwingine kama atalala naye kitanda kimoja(mfano akifanya ngono na mtu mwingine).

Mambo haya ninayoyaeleza huwa watu wengi wanaya bypass kutokana na kasumba(mindset) ya muda mrefu tangu mwaka 1984 HIV/AIDS ilipotangazwa,hivyo kasumba(mindset) hii imeshakomaa kwenye vichwa vya watu kiasi cha kuwa vigumu sana kuelewa jambo lingine tofauti na hilo wanaloelewa tangu kipindi kile.Fungua akili yako na ufuatilie taratibu utauona mwanga tu,ninakuhakikishia hilo.

Mimi nimeshawaachisha watu ARVs na wako vyema hadi leo hii hawatumii ARVs kwa muda mrefu,walioendelea kutumia walishakufa.Think about that.Hii ni nafasi yako ya muhimu sana kuelewa ukweli huu,na hutajuta kukutana na mimi humu JF.Ninakupenda ndio maana napoteza muda wangu kwa ajili yako na watu wako wa karibu.

Ukitaka kujua kwamba sibahatishi,subiri uone mtu aje kupinga kwa hoja anazozijua yeye halafu ujionee mwenyewe kitakachotokea.Hata madaktari nawakaribisha kama wanaona mimi napotosha waje hapa.Tunaenda hoja kwa hoja,sayansi kwa sayansi,vithibitisho kwa vithibitisho.Hakuna siasa.
 
huna uelewa wowote wa HIV/AIDS nadoupt kiwango chako cha elimu,mimi nipo katika maswala ya afya najua vizuri kila kitu kuhusu UKIMWI...

Kuwepo kwenye masuala ya afya haina maana kwamba unajua vizuri kuhusu ukimwi.Sasa mimi nataka kukuthibitishia kwamba wewe hujui kuhusu HIV/AIDS na kile unachokijua umedanganywa.

.. ila nashindwa nikusaidie vipi maana si ajabu una matatizo ya kisaikolojia,may be upo kwenye denial stage after HIV positive results....

Tayari umeshaanza kuji miss direct kwenye hoja zako.Kumwambia mwenzako ana matatizo ya kisaikolojia na mambo mengine ya hovyo unayoongea bila uthibitisho wowote inanipa picha kamili wewe ni mtu wa aina gani.

....naomba usiendelee maana mtu kama wewe unatakiwa ushtakiwe kwa kosa la kujaribu kusababish vifo vya watanzania wanaoishi na virusi vya ukimwi kwa u.j.i.nga wako...

Ungejua ukweli ulivyo kwenye suala hili ndio ungejua kwamba wanaotetea kuhusu HIV/AIDS ukiwemo na wewe,ndio walipaswa si kushtakiwa tu bali kunyongwa hadi kufa kutokana na mamilioni ya vifo walivyosababisha tangu kutangazwa kwa upumbavu huu mwaka 1984.Wewe ni mjinga kuhusu suala hili lakini hujijui kwamba ni mjinga,na kutojijua kwamba ni mjinga ndio ujinga mkubwa zaidi ya ujinga wowote.

...huna elimu ACHA KABISA.sorry nilikusudia kumqoute huyo deception.

Wewe mwenye elimu hebu tuletee evidence kwamba HIV anasababisha AIDS na HIV/AIDS inaambukizwa kwa njia ya ngono na kwamba AIDS haina tiba.Lete uthibitisho huo hapa jukwaani watu wauone.Pia utuletee na electronics micrographs za HIV ili tumuone HIV anafananaje,usilete picha ya mchoro bali lete micrographs za HIV kama unazo.Ukifanya haya yote tutalinganisha na uhalisia wa mambo yanayotokea katika maisha yetu ya kila siku tuone kama kweli sayansi unayoijua wewe inaendana na kinachotokea mtaani.Hapo basi wewe ndio utakuwa na elimu na mimi nitakuwa mijinga kuliko wote duniani.

Vinginevyo kwa kukusaidia,kuna thread nyingi sana humu JF nilishazungumzia mambo haya,mojawapo ni hiyo hapo chini,ina page zaidi ya 60,kama kweli unataka kujua ukweli basi soma hiyo thread taratibu sana usiwe na haraka.Nataka uone kwamba sio kila kitu ambacho kiko tofauti na kile unachokijua wewe basi ni uongo,kumbe unaweza ukawa umedanganywa pia.Nimekuchagulia thread hii moja uisome hapo chini;

https://www.jamiiforums.com/jf-doct...ye-ukimwi-tena-peku-na-asipate-ukimwi-62.html
 
Deception naomba mawasiliano yko kuna ndugu yng anahtaj ushaur
 
Vipi Kwa hapa tz ,ma-nurse wanaopata virusi wakati wa kutoa huduma,wanapatiwa hii treatment???

Huduma ya PEP iko katika vituo vyote vinavyotoka huduma za VCT na PCT (provider initiatec counselling and testing). Kinachotakiwa ni kufuata mwongozo

Kwanini pia wasitafute Chanjo pia,mie naona hiyo ni.mbinu tu ya kuwaweka sawa kisaikolojia waliobakwa na manesi wanaokuwa katika mazingira hatarishi.Ndo hapa naona kuwa wale jamaa wanaosema HIV ni nadharia ya uongo huenda wapo sahihi

Unajua unachokiongelea mkuu?

kupimwa ni lazima.. maana kama na wewe una maambukizi hizo dawa zinakua hazina maana. i've been to this dosage wakati fulani baada ya kuwa kwenye mazingira yenye utata katika kutekeleza majukumu yangu ya kikazi.. hizi dawa ni balaa, tujali sana afya zetu vijana wenzangu maana UKIMWI is real na unaua maukwelii.

Nakubalina na wewe. Hizi dawa zina matatizo makubwa na kweli ni mateso mtu kuzitumia. Hata hivyo ni muhimu kwani zinatoa kinga ya uhakika.

zinatesa. unakunywa kwa kengele alafu kipindi cha mwanzoni zinasumbua sana., zina maudhi kama kichwa kuuma, kichefuchefu na mwili kujisikia vibaya. shida kubwa ni kuwa zinataka chakula cha maana. hakwambii mtu kula ila utatafuta chakula mwenyewe maana zina njaa kama antibiotics. huwezi kula chipsi alafu ukameza hizi dawa. kama ulichagua muda wa kumeza kuwa saa tatu basi utameza saa tatu asubuhi na saa tatu usiku bila kuchelewa siku zooote za dozi yako mpaka hizo wiki nne ziishe.

Kweli kabisa. Kuna jamaa yangu alikuwa anazitumia, alifika wakatia akakaribia kuziacha. Hata hivyo, alimaliza dozi na ni mzima kabisa.

huna uelewa wowote wa HIV/AIDS nadoupt kiwango chako cha elimu,mimi nipo katika maswala ya afya najua vizuri kila kitu kuhusu UKIMWI ila nashindwa nikusaidie vipi maana si ajabu una matatizo ya kisaikolojia,may be upo kwenye denial stage after HIV positive results.naomba usiendelee maana mtu kama wewe unatakiwa ushtakiwe kwa kosa la kujaribu kusababish vifo vya watanzania wanaoishi na virusi vya ukimwi kwa u.j.i.nga wako.huna elimu ACHA KABISA.sorry nilikusudia kumqoute huyo deception.

Nimesikitika sana kuona kwamba kuna mtu anaweza kutoa maneno kama hayo anayoyaandika Deception. Ningeshauri afuatilie kilichompata Thabo Mbeki alipojifanya kuwa na misimamo ya ajabu dhidi ya VVU/UKIMWI.
 
Last edited by a moderator:
Huduma ya PEP iko katika vituo vyote vinavyotoka huduma za VCT na PCT (provider initiatec counselling and testing). Kinachotakiwa ni kufuata mwongozo



Unajua unachokiongelea mkuu?



Nakubalina na wewe. Hizi dawa zina matatizo makubwa na kweli ni mateso mtu kuzitumia. Hata hivyo ni muhimu kwani zinatoa kinga ya uhakika.



Kweli kabisa. Kuna jamaa yangu alikuwa anazitumia, alifika wakatia akakaribia kuziacha. Hata hivyo, alimaliza dozi na ni mzima kabisa.



Nimesikitika sana kuona kwamba kuna mtu anaweza kutoa maneno kama hayo anayoyaandika Deception. Ningeshauri afuatilie kilichompata Thabo Mbeki alipojifanya kuwa na misimamo ya ajabu dhidi ya VVU/UKIMWI.

Mkuu hoja inapingwa kwa hoja, tiririka kitaalamu kama alivyofanya deception ili na sisi tuelewe na tujue ukwel upo wapi.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu hoja inapingwa kwa hoja, tiririka kitaalamu kama alivyofanya deception ili na sisi tuelewe na tujue ukwel upo wapi.

Siwezi kupoteza muda wangu ku-debate na watu wanaoongea bila ushahidi wa kisayansa. Masuala ya tiba hayafanywi kwa hisia wala mahaba. Yanafanyika baada ya tafiti zinazotoa ushahidi wa kuridhisha.

1. ARVs zinapunguza VVU na maambukizi.... huu ni ukweli usiopingikwa kwa nadharia na theolojia

2. ARVs zikitolowe kama PEP zinakinga maambukizi kwa kiwango kikubwa sana....Hili nalo halina utata!

3. ART imesaidia kupunguza vifo kwa kiwango kikubwa sana ingawa dawa zinazotumika zinaambatana na madhara makubwa (side effects)... Hakuna pia mjadala hapa.

Sasa unataka nijadili porojo?
 
Mimi sio mtaalamu wa afya lakini kati ya watu ambao siwaamini hapa duniani ni WAZUNGU! Hawa jamaa kwa jinsi wanavyopenda pesa hawashindwi "kugundua" ugonjwa, kuusambaza halafu baadae wakatengeneza dawa za "kuutuliza" ili tu wapate pesa. Kwao hawajali ni watu wangapi watateseka na kufa ilimradi tu pesa inapatikana!

Kuna siku niliongea na daktari mmoja mzungu akaniambia magonjwa mengi yanayotutesa hapa duniani hasa Afrika kama kisukari, ukimwi, maleria n.k yana CHANJO / DAWA ambazo mtu ukitumia unapona kabisa..! Ila akasema "There is no money in the treatment/prevention of deseases!" Pesa inapatikana kwa kutengeneza dawa za kupunguza makali, ambazo mtu atalazimika kunywa maisha yake yote hivyo kuwa mteja wa kudumu!

Kuna mambo mengi sana ambayo nadhani ukweli wake ungejulikana ingekuwa shida sana.
 
...........Kuna mambo mengi sana ambayo nadhani ukweli wake ungejulikana ingekuwa shida sana.

Moja kati ya mambo ambayo ukweli wake umeshajulikana ni hili la HIV/AIDS.Watu wanasubiri Obama au Bush ndio aje aseme ili waamini kwamba HIV/AIDS ni ugonjwa feki/haupo na HIV hasababishi AIDS,ARVs hazina faida yoyote mwilini zaidi ya hasara na ndio hizo zinazosababisha AIDS kwa wale wanaozitumia baada ya kuzitumia kwa muda mrefu.

Kama watu wangejua ukweli huu basi ingekuwa shida sana kama unavyosema.Lakini si wengi watakaojua ukweli huu kwa kuwa mimi sio Obama au Bush,sio Faucci au Gallo, hivyo watanzania wengi wanaosoma haya watadharau.
 
....Nakubalina na wewe. Hizi dawa zina matatizo makubwa na kweli ni mateso mtu kuzitumia.....

Ni bora hata wewe unalijua hilo kwamba zina matatizo tena makubwa,hizi ni ARVs,na najua pia unajua kwamba ARVs ndizo zinazosababisha matatizo yafuatayo kwa wale waliozitumia kwa muda mrefu,na ndizo zinazoua,HIV haui.

Matatizo yanayosababishwa na ARVs/PEP;

1.Matatizo ya moyo/presha
2.Matatizo ya ini
3.Matatizo ya figo
4.Anaemia/upungufu wa damu
5.Cancer
6.Kisukari

Matatizo yote haya yanaua.Sasa kama side effects hizi zinaua,watu wanaogopa nini kiasi cha kuwafanya wakimbilie kula ARVs?

Kama unapinga kwamba matatizo haya hayasababishwi na ARVs basi lete hoja zako ili watu wajionee wenyewe ukweli uko wapi kati ya yale usemayo wewe na yale nisemayo mimi.Siasa tuziweke pembeni.

...Kweli kabisa. Kuna jamaa yangu alikuwa anazitumia, alifika wakatia akakaribia kuziacha. Hata hivyo, alimaliza dozi na ni mzima kabisa.....

Najua utasema PEP ndizo zimemnusuru jamaa yako.Ninakuhakikishia kwamba hata kama huyo jamaa yako asingekunywa PEP,asingelikufa kwa Ukimwi,maana PEP haziwezi kuzuia Ukimwi.Hakuna mantiki ya kuua kitu ambacho hakina madhara,dawa huua vijidudu vyenye madhara,HIV hana madhara,hivyo PEP ni upuuzi tu na ulimbukeni wa kifikra.

Wapo watu wengi sana wanaishi kwenye ndoa zao ambao wameambiwa ni HIV- wakati wenza wao ni HIV+ tena kwa miaka mingi sana,je, hawa nao wametumia PEP?Watu hawa hata humu JF wapo kuweka msisitizo.Tuache kuwa rigid/wagumu wa kubadili fikra na mitazamo yetu,watu wengi bado wanaishi katika dunia ya zamani/primitive.Hebu tu stretch bongo zetu basi kidogo.

....Nimesikitika sana kuona kwamba kuna mtu anaweza kutoa maneno kama hayo anayoyaandika Deception. Ningeshauri afuatilie kilichompata Thabo Mbeki alipojifanya kuwa na misimamo ya ajabu dhidi ya VVU/UKIMWI.

Hebu tujuze wenzako,nini kilimpata Thabo Mbeki,na alikuwa na msimamo gani dhidi ya VVU/UKIMWI,na huo msimamo aliupata wapi kiasi cha kujiamini.
 
....... hizi dawa ni balaa, tujali sana afya zetu vijana wenzangu maana UKIMWI is real na unaua maukwelii.

Hizi ndizo basics/misingi ambayo watu kama ninyi hawana.Ili uelewe kwamba HIV/AIDS ni feki inabidi kwanza uwe na basic knowledge ya vitu kama hivi.

Watu wengi ukiwemo na wewe hamuwezi kutofautisha kati ya VVU na UKIMWI.Kwenye akili zenu mmeshajiwekea kasumba kwamba VVU ndio UKIMWI na UKIMWI ndio VVU.Ni vigumu sana kuelewa kile ninachozungumzia mimi kama huna uelewa wa mambo madogo kama haya.

1.VVU na UKIMWI ni vitu viwili tofauti
2.Hukuna mtu aliyepinga kwamba UKIMWI haupo.UKIMWI upo ila hausababishwi na VVU.
3.UKIMWI=Upungufu wa Kinga Mwilini,Kumbe kama hiki ndicho kirefu cha Ukimwi,basi kila mtu aliwahi na anaweza kuwa na ukimwi katika maisha yake bila ya kuwa na huyo VVU(feki),kama hali vizuri,hanywi maji safi na salama,anakunywa sana pombe bila kula vizuri,anatumia sana madawa ya hospitali mara kwa mara,anatumia sana madawa ya kulevya,anatumia sana madawa ya kuhamasisha kujamiiana,ana msongo mkali wa mawazo nk.Na specifically kile tunachokiona kwa watu wanaoumwa sana mitaani/mahospitalini ambao wanatumia ARVs ni wazi kwamba kimesababishwa na ARVs na si VVU kama wengi wanavyodhani.

4.UKIMWI unapona tena wakati mwingine hata bila muathirika kujijua.Kama muathirika atabadili style yake ya maisha na kuepukana na mambo tajwa hapo juu basi kinga yake itapanda na kurudi katika hali ya kawaida.Watu huumwa mara nyingi kwa kuwa kinga zao huwa zimeshuka,yaani wana UKIMWI,lakini hawana VVU.Ndio maana ukisambaza vijidudu vya TB hewani kwenye kundi la watu 10,pengine 2 au 3 ndio watapata TB,hii ni kwa sababu kinga zao ziko chini,yaani wana UKIMWI(lakini hawana VVU),na wale 7 au 8 hawajapata TB kwa kuwa kinga zao ziko juu.Ukiwatibia watu hawa 2 au 3 wanapona kabisa TB na wanarudi katika hali yao ya kawaida bila ya kutumia ARVs.

5.UKIMWI hauui,kinachoua ni ugonjwa ambao unajulikana kama vile malaria au TB ambao unamwingia mtu kama mtu huyo kinga yake iko chini,yaani ana UKIMWI(lakini hana VVU).Watu wengi wamejazwa kasumba hii kwenye bongo zao kwa kusikia au kuona matangazo mbalimbali mara kwa mara bila ya hata kujiuliza,ndio maana sasa hivi nikisema UKIMWI hauui watu wanashangaa.

Hebu jiulize kidogo tu.Kama kinga yako imeshuka,yaani una UKIMWI(huna VVU).Halafu ukawekwa kwenye mazingira ambayo ni 'disease free',Je, UKIMWI(upungufu wa kinga) utakuua?

Si mantiki kusema timu ya mpira wa miguu haitafanikiwa kunyakua kombe kwa kuwa beki wake mmoja amepewa kadi nyekundu.Ili timu isinyakue kombe lazima ifungwe/ishindwe/ipoteze mchezo,kupoteza beki mmoja kwa kadi nyekundu si kigezo pekee cha kufungwa.

Hivyo basi,ni mantiki kusema kwamba,timu haitafanikiwa kunyakua kombe kama itafungwa/itashindwa/itapoteza mchezo.

Siku utakaporuhusu akili yako ianze kutumika ndipo utakapokuwa huru kutoka kwenye kifungo hiki cha muda mrefu cha VVU/UKIMWI.
 
Ishaniokoa hiyo kitu. Sitaisahau japo ni kama ARVs but ni uhakika. Nilijichanganya nikala mbunye mbovu yaani nlipagawa!
 
Ishaniokoa hiyo kitu. Sitaisahau japo ni kama ARVs but ni uhakika. Nilijichanganya nikala mbunye mbovu yaani nlipagawa!

PEP/ARVs hazina faida mwilini zaidi ya hasara.PEP hazina target.Je,unajua kwamba HIV ni feki?Huwezi ku target kitu kisichokuwepo.Wewe haujaokolewa na PEP,HIV ni kanya boya tu,hata usingetumia PEP ungekuwa safi tu.Kama hujui jipe muda kufuatilia,inaonekana hujui mambo mengi sana kuhusu HIV/AIDS,ninakusihi usidharau,jipe muda kufuatilia utagundua tu ukweli ulivyo,na utajua kwa nini waliotudanganya wameamua kutudanganya.
 
PEP (Post - Exposure Prophylaxis) ni matibabu anayopewa mtu after been exposed to HIV ili kukukinga kuwa HIV positive.

Matibabu haya yanatakiwa kutolewa as soon as possible baada ya mtu kuwa exposed na HIV (ndani ya masaa 72) i.e kama zishapita siku tatu( masaa 72) matibabu haya hayawezi kufanya kazi

Matibabu haya hutolewa kwa muda wa mwezi mmoja( 4weeks).

Swali: Mbona hiki kitu akizungumziwa sana na watoa huduma ya afya na wadau wanaohusika na mapambano dhidi ya ukimwi?

Je ni gharama ama kuna side effects kubwa?


PEP ipo kwa ajili ya wahudumu wa afya .. Hasa pale wanapopata ajali ya kujidunga sindano bahati mbaya... Inategemea na needle size pia

Nadhani pep is for needle prick injury only ...
 
ni ngumu kumeza ..tunaloweka.....mmedinyana jana hujui ka mwenzio anao...unakimbilia kupewa dawa ndani ya saa 72????
1. Unapima siku ya kwanza .....hakuna viashiria
2. Unarudi baada ya mwezi/miezi3 ...kuthibitisha

nahisi mnanichanganya kwa kusema masaa 72, vinginevyo uwe unatambua wazi umefanya na mwathirika

Kuna njia nyingi ambazo zinaweza kusababisha maambukizo ya UKIMWI, so nafikiri wenda hiyo tiba inatolewa kwa tahadhari pale unapokua exposed kwenye moja ya hizo njia regardless kuna proof kama umeshaathirika au la.
 
Kuna njia nyingi ambazo zinaweza kusababisha maambukizo ya UKIMWI, so nafikiri wenda hiyo tiba inatolewa kwa tahadhari pale unapokua exposed kwenye moja ya hizo njia regardless kuna proof kama umeshaathirika au la.

UKIMWI hauambukizwi kutoka mtu mmoja kwenda kwa mwingine ndugu yangu.Najua si wewe peke yako unayefikiri hivyo,mpo wengi sana.Jitahidi kidogo kuzinduka na kuhoji jambo hili ambalo watu wengi ukiwemo na wewe mnalichukulia kama 'trivial'.Ugumu wa kuelewa jambo hili unaanzia kwenye basics/misingi kama hii,kushindwa kujua kama UKIMWI hauambukizwi ni moja ya sababu kubwa za msingi zinazowafanya watu wengi wapinge hoja kwamba HIV/AIDS ni uongo mtupu.

Hebu jaribu kufikiri,Je,mtu mmoja anawezaje kumwambukiza mwingine upungufu wake wa kinga?Think about that.
 
UKIMWI hauambukizwi kutoka mtu mmoja kwenda kwa mwingine ndugu yangu.Najua si wewe peke yako unayefikiri hivyo,mpo wengi sana.Jitahidi kidogo kuzinduka na kuhoji jambo hili ambalo watu wengi ukiwemo na wewe mnalichukulia kama 'trivial'.Ugumu wa kuelewa jambo hili unaanzia kwenye basics/misingi kama hii,kushindwa kujua kama UKIMWI hauambukizwi ni moja ya sababu kubwa za msingi zinazowafanya watu wengi wapinge hoja kwamba HIV/AIDS ni uongo mtupu.

Hebu jaribu kufikiri,Je,mtu mmoja anawezaje kumwambukiza mwingine upungufu wake wa kinga?Think about that.
Sijakuelewa vizuri ndugu, ingawa kiukweli najua kinachoambukizwa ni virusi vinavyosababisha UKIMWI.
 
nahisi mnanichanganya kwa kusema masaa 72, vinginevyo uwe unatambua wazi umefanya na mwathirika
Si kila mkidinyana..ndo mana nikasema baada ya kuwa exposed na HIV( mf:umefanya mapenzi na muathirika na ukagundua mapema kabla ya hizo siku tatu).[/QUOTE]

Mi naona hata watu wanaopata ajali inawafaa kwasababu damu zinachanganyana kwenye ajali na ni rahisi kupata maambukizi, mfano mtu amekatika mguu kwenye ajali kazimia kalala kwenye dimbwi la damu za wengine ni hatari sana kwa afya yake katika kupata maambukizi ya vvu endapo kidonda chake kitakutana na damu iliyo na vvu
 
Sijakuelewa vizuri ndugu, ingawa kiukweli najua kinachoambukizwa ni virusi vinavyosababisha UKIMWI.

Ukifuatilia post zangu huku ukiwa na open mind utanielewa tu,cha msingi tenga muda wako kufuatilia,HIV/AIDS ni upuuzi wa watu fulani ambao wamepindua sheria za kisayansi ili kudanganya watu,hakuna ugonjwa kama huo kiuhalisia,unachoona wewe kwa watu wanaokufa sio kama ulivyoambiwa,kinachoua ni kitu kingine kabisa.Ukiwa na open mind kujifunza utajua hiko ni kitu gani.

Hakuna virusi vyovyote duniani vyenye uwezo wa kusababisha UKIMWI.Najua hiki ni kitu kigeni sana kwako,lakini vuta subira,jipe muda,utakuja kushangaa na kujionea wewe mwenyewe kwamba dunia uionayo sasa imejaa viini macho vingi sana kiasi cha kukufanya uone karibu kia kitu ni batili/uongo.

Nakusihi usiwe kama wana JF wengine ambao ni wepesi kupinga bila kuhoji,jipe muda,hoji,soma.Ukifanya haya hutajuta kukutana na changamoto hii humu JF.
 
Ukifuatilia post zangu huku ukiwa na open mind utanielewa tu,cha msingi tenga muda wako kufuatilia,HIV/AIDS ni upuuzi wa watu fulani ambao wamepindua sheria za kisayansi ili kudanganya watu,hakuna ugonjwa kama huo kiuhalisia,unachoona wewe kwa watu wanaokufa sio kama ulivyoambiwa,kinachoua ni kitu kingine kabisa.Ukiwa na open mind kujifunza utajua hiko ni kitu gani.

Hakuna virusi vyovyote duniani vyenye uwezo wa kusababisha UKIMWI.Najua hiki ni kitu kigeni sana kwako,lakini vuta subira,jipe muda,utakuja kushangaa na kujionea wewe mwenyewe kwamba dunia uionayo sasa imejaa viini macho vingi sana kiasi cha kukufanya uone karibu kia kitu ni batili/uongo.

Nakusihi usiwe kama wana JF wengine ambao ni wepesi kupinga bila kuhoji,jipe muda,hoji,soma.Ukifanya haya hutajuta kukutana na changamoto hii humu JF.

Duu! This is interesting. Hebu nipe mwangaza zaidi ili nijue wapi nianzie kupata huo uelewa mpya kuhusu hili jambo
 
Back
Top Bottom