Fahamu zaidi kuhusu Mr Kuku

Fahamu zaidi kuhusu Mr Kuku

Wanaomjua Sasa Ndiyo Wanakuja Sasa Kutupa Data
 
Hoja kama hizi utawadanganya nazo hao wajinga wajinga wanaowaletea ninyi fedha zao na siyo mimi! Maisha yangekuwa rahisi namna hii mnayodanganya hii dunia isingekuwa na maskini. Ni suala la muda tu lakini ukweli utajulikana na wajinga wanaowapa fedha zao watabaki wanalia na kuomboleza.
Definition of Risk Takers
Certain types of people enjoy taking risks, while others prefer stability and are averse to any type of risk. A risk taker is someone who risks everything in the hope of achievement......
 
Definition of Risk Takers
Certain types of people enjoy taking risks, while others prefer stability and are averse to any type of risk. A risk taker is someone who risks everything in the hope of achievement......
Did you think that I dont know the meaning of risk taker! I do dude! BTW the difference between lazy, fools who embrace imposibles and risk takers is bigger that our universal. Those who are investing their money in the Kuku project are fools.
 
Jamaa anaidea nzur sana hasaa kma ataamua kuliboresha wazo lake. Au kma atatokea mtu mwenye mtaji mkubwa ambae hana nia ya kufanya utapeli akaamua kufanya hyo kitu.

Unaweza kujiuliza kitu simple kabis kama ikiwa anayo hio plani ya biashara inayoweza kukupa return on investment ya 100% kwa miez 3 yaani 180000 ikupe 360000, kwanin asiende bank kuchukua mkopo ili afinance hio biashara yake manake bank watamchaji riba ambayo haitafika 20% kwamwaka?? Jibu nikua hawez kwenda kuitapeli bank

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah mimi sijui tunakwama wapi.

Huyu mtu anajinadi kuwa ana biashara ya kuku na anawaalika watu waende kwenye mashamba yake kuona uwekezaji, wanaenda na wanashawishika na wanawekeza, mtu mmoja ninayefahamiana naye amewekeza huko 5,000,000. Sasa maswali ya kujiuliza ni haya:

1. Ikiwa Mr Kuku Farms ana biashara ambayo inakua kwa kasi na kuweza kurejesha mtaji na faida kubwa ndani ya muda mfupi, NI IPI RAHISI KWA MWEKEZAJI HUYU KATI YA KUCHUKUA 700,000 KWA RIBA YA 100% KWA MUDA WA MIEZI 6 KUTOKA KWA INDIVIDUALS au KUCHUKUA MKOPO BENKI KWA RIBA TUNAZOZIJUA

2. Iikiwa investment ya Mr Kuku Farms ina return kubwa kiasi hiki, kwa nini anaendelea kuchukua fedha kwa watu wengine?

Mimi umaskini wangu huwa unaletwa na roho ya kusita sita, ndio maana hata utajiri wa Namaingo Business Agency ulinikosa. Niliuliza maswali nikafukuzwa kwenye semina na wamama wenye ushungi walinizodoa. Naamini sasa watakuwa matajiri wakubwa kwa ufugaji wa sungura kuku na samaki huko kijiji cha Mbawa ikiwa hakikuota mbawa
 
Habari wana chamvi, nimesoma uzi kuhusu mada tajwa hapo juu nami nataka kushirikishana uzoefu wangu kuhusu huyo 'mwekezaji".

Huyo bwana anaitwa Tariq, mwaka juzi 2018 nilisoma bandiko lake fb kuhusu mradi wa kilimo cha nyanya cha umwagiliaji, ahadi ilikuwa nzuri kuhusu faidi ambapo kiwango cha chini cha hisa ilikuwa 36 na kila hisa 5000/= hivyo unapata 180,000 /=

Baada ya miezi mitatu unapata 360,000/= nilitamani kuwekeza japo nilikuwa na shaka, niliongea nae akanielewesha kwamba uwekezaji ni kupitia vikundi vya watu 15, hivyo akaniunganisha na wadau tukawa na kikundi cha What App tulikuwa mikoa tofauti ila mm niliiona na advantage kwa kuwa mradi ungefanyika jirani.

Tukaanza taratibu za katiba usajili wa kikundi, kabla ya kusajili kikundi akasema tutume fedha ili mradi uanze kuendana na wakati ili kuwahi soko la nyanya.

Baada ya kutoa fedha tulipitia ubabaishaji mwingi sana, mara mradi wa arusha hauwezekani kuna shamba moro, wadau wakataka kwenda moro baada ya muda akasema kule eneo linapitiwa na reli mradi utakuwa Tanga akatutumia vi picha vya eneo na ka tank. Wadau wakalazimisha wakaenda Tanga kufika hakuna kinachendelea.

Tukaanza harakati za kukamilisha katiba na mkataba ili tujipange kwa hatua zaidi. Baada ya muda sana akasema amepata hasara hivyo fedha iliyobaki atawekeza mradi wa kuku uliopa kigamboni. Tukaendelea kupambana na kufuatilia.

Baada ya mwaka baada ya kuwa na maamuzi ya kwenda vgombo vya sheria ndo akaturudishia mitaji yetu na kuahidi faida baada ya muda. Baada tu ya kurudisha mitaji hakuwa anapokea simu wala kujibu hoja za group la What App ambalo tulianzisha. Baada ya kuanza tena harakati za kutaka kufuatilia faida akatoka katika kundi kwa jazba na kusema tufanye tunavyotaka hayupo tayari kuendelea na sisi.

Kama ambavyo mmeona tangazo lake ndivyo alivyo huwa hajibu wala kutoa ufafanuzi wa kina kuhusu hoja.

Pamoja na kwamba uoga wako ndo umaskini wako ila kwa wawekezaji wa kibongo bora kuwa mwoga. "invest on your own risk"

Nawatakia wakati mwema.
Haaaa mm nilishajua mda sana kuna dalili za Utapeli ndani yake.
 
Nna jamaa yangu yuko umo kwa mr kuku farm, jibu alilonipa ni kwamba wameruhusiwa kuendelea ila wameambiwa wabadili mfumo,, mfumo gani? Siujui huo mfumo ,

Ila kuna uwezekano ile KADANSEE isiwepo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo mnapenda vitu laini sana. Kama una pesa yako it's not proper kuwekeza sehemu bila kupewa kitu cha kuhalalisha huo uwezaji. Kaa chini fikiria anzisha biashara, kama huwezi nenda ukanunue hisa kule DSE au wekeza kwenye bonds itakulipa. Hii ya kuambiwa eti weka 100k upate 200k ni too good to be true.
 
Yaani mtu unampa tu pesa, yeye analisha kuku, anachanja dawa, ahangaike na changamoto za vifo, ahangaike kupata soko kwa wakati.
Mwisho ww unaenda tu kuzoa faida.

Hii kauli yangu ya kuwa hakuna pesa ya rahisi rahisi huwa inaniokoa sana.
 
Jamaa anaidea nzur sana hasaa kma ataamua kuliboresha wazo lake. Au kma atatokea mtu mwenye mtaji mkubwa ambae hana nia ya kufanya utapeli akaamua kufanya hyo kitu.

Unaweza kujiuliza kitu simple kabis kama ikiwa anayo hio plani ya biashara inayoweza kukupa return on investment ya 100% kwa miez 3 yaani 180000 ikupe 360000, kwanin asiende bank kuchukua mkopo ili afinance hio biashara yake manake bank watamchaji riba ambayo haitafika 20% kwamwaka?? Jibu nikua hawez kwenda kuitapeli bank

Sent using Jamii Forums mobile app

🤣🤣🤣🤣
"hawez kwenda kuitapeli bank"
 
Back
Top Bottom