Faida na athari za Mwanaume kuwepo katika chumba wakati mwenza wake akijifungua

Faida na athari za Mwanaume kuwepo katika chumba wakati mwenza wake akijifungua

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Hivi karibuni Rais Samia Suluhu Hassan alizungumzia kuhusu mpango wa Wanaume kuruhusiwa kuingia katika vyumba vya kujifungulia wakati wenza wao wanapokuwa katika mchakato wa kujifungua.

Kuna mambo ambayo yanaweza kutajwa kuwa ni faida au hasara za suala hilo kama ambavyo inafafanuliwa na wataalam wa afya:

Baadhi ya wataalamu wa Afya na Wanasaikolojia wamefafanua faida za wanaume kuwepo pamoja na wenza wao wakati wa kujifungua kwamba kutaongeza upendo, kuondoa upweke na kutamsaidia mwanamke kisaikolojia kupata faraja ya kupunguza uchungu wa kujifungua.

Wanasema uwepo wa mume utamsaidia mwanamke kupata hisia chanya na kujiona anathaminiwa na kujiamini zaidi kuwa mwenza wake yuko naye katika shida na raha.

Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dkt. Shedrack Mwaibambe anasema suala la mimba ni la wote wawili, uwepo wa wote katika chumba cha kujifungua utasaidia kuongeza uhusiano zaidi kati ya mume na mke na pia kuondoa hofu endapo kutatokea tatizo mume wake atakuwa pale kutoa taarifa kwa urahisi.

"Hii ni nzuri sana kama kweli unampenda mwenza wako utatamani umsindikize na itaongeza uaminifu, mwanamke anakuwa na imani kuwa hata kama nikichanika vibaya mume wangu yupo ataenda kutoa taarifa," amesema.

Wataalam: Kushuhudia mke akijifungua kumeathiri wengi

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake na Uzazi, Matilda Ngarina amewahi kunukuliwa akisema: “Hatua ya kujifungua inatisha. Ni wanaume wachache ambao wanaweza kushuhudia wenzi wao wakijifungua kisha wakaendelea kuwa katika hali ya kawaida kisaikolojia.

“Ni tukio la kuogopesha. Linahitaji ujasiri wa ziada. Wanaume waliojaribu kushuhudia wenzi wao wakijifungua 90% wameathirika kisaikolojia.”

Dkt Ngarina anaeleza baadhi ya athari za kisaikolojia walizopata wanaume hao, zimesababisha wengine kujikuta hawatamani tena kutungisha mimba.

“Wapo wanaume wengine waliochukua uamuzi wa kuomba wake zao wafungwe kizazi, ili kuwaepusha kuzaa tena na wengine walipoteza hamu ya kushiriki kwenye tendo la ndoa,” anasema.

Anasema wapo wengine ambao baada ya kukumbwa na athari hizo walijisalimisha kwa madaktari kuomba msaada, ambapo walikutanishwa na wataalamu wa masuala ya saikolojia na wakarejea katika hali yao ya kawaida.

Dkt. Ngarina anasema uamuzi wa kuzungumza na wataalamu wa afya mtu anapopatwa na matatizo, ni jambo muhimu kuliko kuruhusu athari ziendelee kutawala.

“Ukweli ni kwamba wanaume wengi hawana desturi ya kushiriki kwenye kliniki ili wapate elimu ya masuala ya afya na uzazi jambo ambao ni muhimu kusaidia kuwa na familia bora,” anasema.
 
unaingia leba mkeo akijifungua mtoto wa ndege joni
 
hahaha na hata ingekua ni lazima wangu sjui kama angeweza binafsi hata sitaki anione yeye asubirie tu taarifa nitakapotoka salama
 
We jiulize kwanini manesi wengi hawana watoto hili jambo sio zuri hata kidogo
 
Sioni Faida Zaidi ya Hasara tu
Kwanza Kumsikia Mkewangu Akilia tu Nywele Zina Sisimka Ndio Kusikia nipo nje
Nikiona Ndio mtihani Kabisa!
 
Hivi karibuni Rais Samia Suluhu Hassan alizungumzia kuhusu mpango wa Wanaume kuruhusiwa kuingia katika vyumba vya kujifungulia wakati wenza wao wanapokuwa katika mchakato wa kujifungua.

Kuna mambo ambayo yanaweza kutajwa kuwa ni faida au hasara za suala hilo kama ambavyo inafafanuliwa na wataalam wa afya:

Baadhi ya wataalamu wa Afya na Wanasaikolojia wamefafanua faida za wanaume kuwepo pamoja na wenza wao wakati wa kujifungua kwamba kutaongeza upendo, kuondoa upweke na kutamsaidia mwanamke kisaikolojia kupata faraja ya kupunguza uchungu wa kujifungua.

Wanasema uwepo wa mume utamsaidia mwanamke kupata hisia chanya na kujiona anathaminiwa na kujiamini zaidi kuwa mwenza wake yuko naye katika shida na raha.

Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dkt. Shedrack Mwaibambe anasema suala la mimba ni la wote wawili, uwepo wa wote katika chumba cha kujifungua utasaidia kuongeza uhusiano zaidi kati ya mume na mke na pia kuondoa hofu endapo kutatokea tatizo mume wake atakuwa pale kutoa taarifa kwa urahisi.

"Hii ni nzuri sana kama kweli unampenda mwenza wako utatamani umsindikize na itaongeza uaminifu, mwanamke anakuwa na imani kuwa hata kama nikichanika vibaya mume wangu yupo ataenda kutoa taarifa," amesema.

Wataalam: Kushuhudia mke akijifungua kumeathiri wengi

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake na Uzazi, Matilda Ngarina amewahi kunukuliwa akisema: “Hatua ya kujifungua inatisha. Ni wanaume wachache ambao wanaweza kushuhudia wenzi wao wakijifungua kisha wakaendelea kuwa katika hali ya kawaida kisaikolojia.

“Ni tukio la kuogopesha. Linahitaji ujasiri wa ziada. Wanaume waliojaribu kushuhudia wenzi wao wakijifungua 90% wameathirika kisaikolojia.”

Dkt Ngarina anaeleza baadhi ya athari za kisaikolojia walizopata wanaume hao, zimesababisha wengine kujikuta hawatamani tena kutungisha mimba.

“Wapo wanaume wengine waliochukua uamuzi wa kuomba wake zao wafungwe kizazi, ili kuwaepusha kuzaa tena na wengine walipoteza hamu ya kushiriki kwenye tendo la ndoa,” anasema.

Anasema wapo wengine ambao baada ya kukumbwa na athari hizo walijisalimisha kwa madaktari kuomba msaada, ambapo walikutanishwa na wataalamu wa masuala ya saikolojia na wakarejea katika hali yao ya kawaida.

Dkt. Ngarina anasema uamuzi wa kuzungumza na wataalamu wa afya mtu anapopatwa na matatizo, ni jambo muhimu kuliko kuruhusu athari ziendelee kutawala.

“Ukweli ni kwamba wanaume wengi hawana desturi ya kushiriki kwenye kliniki ili wapate elimu ya masuala ya afya na uzazi jambo ambao ni muhimu kusaidia kuwa na familia bora,” anasema.

Watoto wangu wote watatu wamezaliwa ninawaona. Huu ni utaratibu wangu, lazima niwepo mtoto wangu anapozaliwa, sikuwahi kushurutishwa na sijawahi kuwa na athari yoyote hasi kisaikolojia zaidi ya kuwa na kumbukumbu mzuri na hisia chanya kwa wanangu na mama zao.

Najiandaa mwezi wa kumi kuingia tena labour kushuhudia mtoto wangu wanne anazaliwa.
 
SAFI SANA
Baadhi ya wanaume wanaogopa kuona mke akijifungua

Sasa unaogopa nini, tunapimaje uanaume wako kama sio kuvumilia mambo magumu kama hayo?

Watoto wangu wote watatu wamezaliwa ninawaona. Huu ni utaratibu wangu, lazima niwepo mtoto wangu anapozaliwa, sikuwahi kushurutishwa na sijawahi kuwa na athari yoyote hasi kisaikolojia zaidi ya kuwa na kumbukumbu mzuri na hisia chanya kwa wanangu na mama zao.

Najiandaa mwezi wa kumi kuingia tena labour kushuhudia mtoto wangu wanne anazaliwa.
 
Mi sioni faida yake, binafsi siogopi ila sioni faida.

Labda wanawake waliojifungua watuambie wao hupenda nn!?
 
UJue wakat wa kujifungua kwa njia ya ku push kawaida, wanawake kuachia haja kubwa ni ktu common sana ( hapa sijazungumzia wale wanaofukuliwa mitaro, no). ni part of the process.

Sasa haya mambi yanaoswa kutoonwa na mweza, kwanza unakua kama una invade privacy yake.
 
Watoto wangu wote watatu wamezaliwa ninawaona. Huu ni utaratibu wangu, lazima niwepo mtoto wangu anapozaliwa, sikuwahi kushurutishwa na sijawahi kuwa na athari yoyote hasi kisaikolojia zaidi ya kuwa na kumbukumbu mzuri na hisia chanya kwa wanangu na mama zao.

Najiandaa mwezi wa kumi kuingia tena labour kushuhudia mtoto wangu wanne anazaliwa.
Bongo hii hii?? Labda private hospitals
 
Subirieni watoto nyumbani/ nje ya wodi mtafaint huko leba nani atawapepea manesi wapo bize na mzazi.
 
Sioni Faida Zaidi ya Hasara tu
Kwanza Kumsikia Mkewangu Akilia tu Nywele Zina Sisimka Ndio Kusikia nipo nje
Nikiona Ndio mtihani Kabisa!
Sasa wewe siku ukimsikia analia akikazwa na njemba utaweza kufamania kwel.? Kama kulia tu kwake ,wewe unapata shida!!
 
tunapenda kuiga umagharibi mpaka kwenye mambo ya kipuuzi
 
Back
Top Bottom