Tafuta biblia zilizo halali utajua maana ya Tunda, achana na hizo nakala za kihuni walizotafsiri VATICAN kwa kuficha ficha mambo kwa maslahi yao.
Mtu wa kwanza hakuitwa Adam wala mkewe hakuitwa eve maana hawakuwa na asili ya Uzungu, pili hawakuishi huko walikotuaminisha hawa wachungaji na wanasayansi uchwara.
Tatu Tunda maana yake ilikuwa ni maarifa/Neno la ujuzi wa kutambua mambo fulani hapa dunian, na Mti ulito toa hayo matunda ni Malaika ambao waliishi dunian na walikuwa na mission zao hapa hapa dunian.
Mtu wa kwanza alipewa ONYO asiwasiliane na hao malaika wala kuwaomba wampe/wamwambie Habari za maarifa waliyonayo ambayo walukatazwa kuyajua maana yalikuwa nje ya uelewa wao(Tunda).
Baada ya kuumbwa kwa mwanamke ambaye biblia za uongo zinamuita eva/hawa huyu hakuumbwa kwa udongo kama Adam bali aliumbwa kutokana na Imagination+mawazo ya Adamu kuhusu uwepo wa kiumbe kitakachofanana nayeye kitakachomtoa upweke hivyo eva aliumbwa kwa staili hii.
Kwakuwa Eva hakuwa na Uelewa sawa ama nguvu sawa na adamu bali alishawishika na kiumbe ambacho biblia zenu zinasema ni nyoka(Dragon) ambaye ndiye alimshawishi eva na eva ndiye wa kwanza kuyasikiliza maarifa ya wale malaika walioambiwa wasiyasikie na baadae akamueleza Adam, hapa ndipo chanzo cha maovu kilipoanza.
Adam hakufa kama tunavyodanganywa bali alipewa laana kwa wazawa wake na hata eva hakufa tafuta ktk biblia yako hutoona maala wanaeleza hili jambo zaid ya kudanganya kuwa adam alikufa na umri wa miaka fulan which is nonsense.
Unatakiwa ujuwe kuwa Adam mission yake aliyoletwa dunian ilikuwa ni kuongeza idadi ya malaika waliosaliti ambao idadi yao ilitakiwa kuwa replaced na wana wa adam atakao wazaa na mkewe maana Adamu nae kabla ya kuumbiwa mwili alikuwa ni sehemu ya malaika, baada ya anguko la shetan na wenzie ndipo ikaja sababu ya adamu kushushwa dunian na akafanyiwa mwili ili aweze kuendeleza uumbaji wa malaika wapya(wanadamu).
Idadi inayotakiwa kwa wana wa adamu kureplace idadi ya malaika waliosaliti mbingu inajulikana na huenda ikatimia muda ukifika.
Shida za dunia hazitokwisha na hizo raha mnazotamani hazitopatikana maana huyo kiumbe anaeitwa shetan hataki idadi ya wana wa adamu itimie maana ikitimia na ule mwisho utafika na hukumu kwa shetan na wafuasi wake itafika.
Shetan si mjinga kuwapotosha watu na kuwafanya wamsaliti Muumba ili tu idadi isifikie na malengo ya shetani kuutawala ulimwengu yaendelee uku idadi ya wana wa adamu ikiendelea kudhorota na anguko la wengi liwepo.
Tutafute elimu nje ya box, Hilo kanisa la kizungu la Katolic wakishirikiana na madhehebu yote na dini zote hawa ndio wahuni nambari moja waliopotosha Biblia ya kweli kwa kufuta baadhi ya vitabu na vingine kuvipotosha kwa kuedit na kuweka uongo mwingi maana hawa wote wako chini ya shetan kuhakikisha wana wa Adamu hatuijui kweli na hatuifikii ile idadi inayotakiwa kureplace jeshi la shetani.
Tuendeleeni kushabikia mamipira, maushenzi ya kubishiana dini ya nani ndio sahihi, kuuwana sisi kwa sisi, kujadiri uwepo wa Mungu na ujinga mwingne tunajichelewesha sisi wenyewe