Faida za mkopo wa muda mrefu na mfupi

Faida za mkopo wa muda mrefu na mfupi

Ifike mahali tuelewe jamani, biashara ni kipaji kama vipaji vingine na sio kila mtu anacho hicho kipaji. Hao hao wataalamu wanatuambia kwamba katika kila biashara 10 zinazoanzishwa, 7 hua zinakufa kabla ya miezi 6! Kama huna kipaji cha biashara, kuliko ukatumbukize hela ya mkopo kwenye biashara ya majaribio ni heri mara 100 ujenge nyumba ya kuishi, au ununue gari ya kutembelea angalau utakua unaiona...!
Mballi ya kuwa ni kipaji, kosa letu kubwa ni kuanzisha biashara bila ya kuwa na a b c za ujasiriamali. Inalipa sana kama utahudhuria zile kozi za wiki mbili za ujasiriamali ili angalau ujue kubalance mahesabu, lakini leo umeona jirani ana duka na wewe unakwenda kuanzisha duka basi ujue huko mbele ni matatizo tu.
 
Mballi ya kuwa ni kipaji, kosa letu kubwa ni kuanzisha biashara bila ya kuwa na a b c za ujasiriamali. Inalipa sana kama utahudhuria zile kozi za wiki mbili za ujasiriamali ili angalau ujue kubalance mahesabu, lakini leo umeona jirani ana duka na wewe unakwenda kuanzisha duka basi ujue huko mbele ni matatizo tu.
Upo sahihi kabisa. Watu hua wanachukulia kama biashara ni kitu rahisi saana, kwamba we ukiwa na hela tu ukianzisha biashara baasi unakua tajiri..!😀 Hawaoni mjini huko kila ukipita unakuta biashara zimekufa, zingine ziko vile vile miaka nenda rudi hakuna maendeleo... Hao wenye abc za biashara wenyewe kuna wakati hua wanakula za uso wengine mpaka wanafilisika na kufunga biashara, sembuse wewe umekurupuka tena na mkopo juu aisee utakimbia mji peku 😆😆
 
Ongea mkuu... tuko hapa kuelimishana.
Bora nyumba ya kuishi kwamba uta save Kodi lakini gari ya kutembelea ina faida gani zaidi ya kukuongezea umaskini tu mafuta, service, bima, bado wazee wa kazi hujakutana nao wapate za kubrush viatu n.k
 
Sasa hio
Wataalam wa mikopo wanakwambia usikope kununua gari ya kutembelea maana gari liability haliingizi chochote Bali litakufanya pia utoe hela mfukoni ili kulihudumia kwa hiyo litakunyonya zaidi, kama unataka kununua gari basi nunua ya biashara eg hiace, coaster, kirikuu, tipper etc ili ilete hesabu pia hata kujenga nyumba ya kuishi kwa mkopo hawashauri pia labda ujenge ya biashara let say guest house, vyumba vya biashara n.k. Jana niliiona video moja ya MO anasema watu wanakosea kwa kukopa hela then wanajenga nyumba ya kuishi kwa nin hiyo hela usiifanyie biashara na wewe ukaendelea kupanga nyumba yenye gharama ndogo then biashara ikikua na kuanza kuingiza faida ya kutosha ndio unajenga nyumba kwa kutumia faida unayoipata

Sasa hio elimu ya biashara ya kufanya na ni biashara gani afanye na vipi apate faida kubwa ya kujenga nyumba hapo ndo kipengele mkuu!

Biashara nyingi zinafungwa within 5 years

Only few makes it

Business is not for everyone

Wanaoweza fanya hivo wafanye

Wasioweza basi wanunue gar na kujenga nyumba ni afadhali pia!
 
Sasa hio


Sasa hio elimu ya biashara ya kufanya na ni biashara gani afanye na vipi apate faida kubwa ya kujenga nyumba hapo ndo kipengele mkuu!

Biashara nyingi zinafungwa within 5 years

Only few makes it

Business is not for everyone

Wanaoweza fanya hivo wafanye

Wasioweza basi wanunue gar na kujenga nyumba ni afadhali pia
Point mkuu Asante sana
 
Usiogope kukopa, tajiri yeyote anakopa.
Faida ya mkopo wa muda mrefu, utakuwa unakatwa kidogo kidogo; ila hasara yake, kama ulichukua milioni 15, unaweza kujikuta jumla ya marejesho ni milioni 27+ , kutegemeana na muda.
 
Usiogope kukopa, tajiri yeyote anakopa.
Faida ya mkopo wa muda mrefu, utakuwa unakatwa kidogo kidogo; ila hasara yake, kama ulichukua milioni 15, unaweza kujikuta jumla ya marejesho ni milioni 27+ , kutegemeana na muda.
Kweli mkopo wa muda mrefu una riba kubwa sana
 
Habari wakuu, mimi ni mtumishi wa Umma ambapo nina fursa za kukopa benki mkopo wa muda mrefu na mfupi na siku hizi benki nyingi zimeongeza muda wa mkopo hadi miaka 8.
Nilikuwa naomba mawazo yenu kuhusu faida za mkopo wa muda mrefu na muda mfupi ingawa nafahamu kuwa changamoto kubwa ya mkopo wa muda mrefu ni riba kuwa kubwa, Je zipi faida nyingine?
Habari za jioni wakuu

Nimeamua kuanzisha uzi huu ili iwe ni chanzo cha kujifunza mawili matatu kwa watumishi wa umma kuhusu mikopo inayotolewa na benki mbali mbali kwa watumishi wa umma.

Kumekuwa na malalamiko na vilio kwa watumishi wa umma kuhusu mikopo wanayopewa na benki. Wengi wao wanalaumu mikopo hiyo kuwa ni kandamizi na haipo kwa lengo la kuwa saidia bali ipo kuwakandamiza na kuyafanya maisha yao kuwa magumu.

Ukichunguza kwa undani zaidi utagundua tatizo sio mikopo inayotolewa na benki bali shida ipo kwa sisi watumishi kutokuwa na elimu juu ya namna bora ya kukopa.

Kwanza tufahamu ya kwamba benki za biashara zipo kutengeneza faida na kuzifanya ziendelee kuwepo sokoni.
Miongoni mwa bidhaa (products) zinazowafanya kupata faida na kuendelea kubaki sokoni ni hii mikopo kwa watumishi wa umma.

Kwa hiyo mtumishi wa umma unapokwenda kukopa benki afisa mikopo wa benki hiyo atakupa chaguo (option) ambayo itakuwa na faida zaidi kwa benki.

Chukulia mtumishi ana mshahara wa kuchukuwa nyumbani (take home) wa 700k, kwa mtumishi asiekuwa na elimu ya mikopo akifika benki atamuuliza afisa mikopo kwa mshahara wa 700k naweza kukopa kiasi gani??

Hapa afisa mikopo atakachoangalia kwanza ni option ipi itaingizia benki faida kubwa zaidi?

Ataanza kupiga mahesabu, kwanza ataangalia ni kiasi gani katika mshahara wa mtumishi kinakopesheka kwa kuzingatia sheria ya 1/3 ya mshahara ibaki kwa mtumishi , atagundua 2/3 ya 700k ni kama 460,000 hivi, kwa hiyo hapo mda wa chini atamuambia kwa miaka mitano una uweko wa kukopa hadi 19M, makatao yote itakuwa around 443,000 kwa mwezi.

Mtumishi aiekuwa na elimu ya milopo anaangalia mshahara wake wa 700k anajikuta inabakisha 270,000. Anamuuliza afisa mikopo nikichukuwa hiyo 19M kwa miaka nane je?

Anaambiwa ukichukuwa hiyo 19M kwa miaka nane kila mwezi utakatwa 325,000. Anakubali kuchukuwa 19M kwa miaka nane kwa sababu tu makato ni madogo.

Asicho kijuwa ni kuwa akichukuwa mkopo wa 19M kwa miaka mitano aliyotajiwa na afisa mikopo atakuwa ameipatia benki faida ya around 7,600,000 na akichukuwa kwa miaka nanae atakuwa ameipatia benki faida ya 12,160,000.

Kumbuka mtumishi huyu anachukuwa mkopo huu lengo lake kubwa ikiwa ni kuendeleza ujenzi wa kiawanja chake, kwa hiyo anachukuwa hiyo 19M ndani ya miaka nane anaishia kwenye kufunga linta.

Tunalopaswa kulielewa kwa sisi watumishi wa umma ni kuwa:
-Mkopo unaozidi miaka miwili na nusu hapo ni kujiumiza na unachokifanya ni kuinemeesha benki na kumfanya afisa mikopo kuongezwa cheo.
Ni vizuri kwa mtumishi wa umma kabla ya kwenda benki kwa ajili ya kukopa awe ameshatayarisha mpango wa mkopo. Usisubiri benki wakupangie wao, watakuumiza kwa kukupa option ya muda mrefu.

-Mtumishi wa umma jitahidi ukopebkwa awamu mgawanyiko zenye muda mfupi mfupi.

Chukulia hii 19M ambayo mtumishi mwenye take home ya 700k ambae alichagua kukopa kwa miaka nane, njia bora ni kuanza na 9.5M kwa miaka miwili na nusu tu ambapo atatakiwa kulipa 11.5M kwa makato ya 380,000 kwa mwezi. Riba ya miaka miwili na nusu atakuwa around 1,900,000.

Baada ya kuisha miaka miwili na nusa anachukuwa 9.5M nyengine. Hapo riba ya miaka mitano itakuwa ni 3,800,000 badala 7,600,000 kwa muda ule ule wa miaka mitano.

Mwisho tusiwe na tabia za kulalamika kwa matatizo tunayoyatengeneza wenyewe, tutafute elimu ya mambo tunayoyafanya ili kuwa na matikeo bora zaidi.
 
Back
Top Bottom