Faidika na darasa la FaizaFoxy; Uliza chochote utajibiwa

Hawavai kwa ajili ya waarabu bali wanavaa kwa ajili ya dini yao.

Kwa hvyo hata wakiwachukia bado wanasonga mbele kwa sababu hawamfuati muarabu wanaifuata dini
Kwanini watu kama nyie wavaaji magunia kichwani mnajifanya waarab wakati hao waarab hawana issue nanyi? Tena wanawachukia ile mbaya.

ukiacha kuchagua jua umechagua kuacha
 
Reactions: bbc
Nioneshe hiyo aya. Siwezi kukubaliana na kitu kutoka kichwani mwako tu.

Halafu naona unakwepa maswali yangu, hauna majibu au haufahamu? Pia umekwepa kuchambua maswali yako na kuja na mojamoja umeamua kuja na lingine jipya kabisa kila post.

Kwa ugeni wa majadiliano namna hii, kweli ni mimi ni mgeni, nilianza kujadiliana mtandao wa yahoo groups mwaka 2005 na Jambo forums mwaka 2007 na Jamii forums toka ianzishwe. Uzoefu wangu ni mdogo sana kama uonavyo.

Wewe mwenzangu mwenye uzoefu naona unarukia hili unaacha njiani kabla hatujamalizana unarukia lile unaacha, ukiulizwa maswali hujibu.

Unaonesha ni mzoefu sana wewe wa mijadala.
 
Umesoma hiyo article na kuelewa? Vua hilo gunia lako kichwani, unajitwika haibu bure, wenyewe wanaona dharau kuigwa kila kitu na nyie.
Ukiona mtu anaacha hoja iliyopo na kukujadili wewe ujuwe kisha shindwa kwa hoja huyo. Naomba kwanza tuelewane, tafadhali usinijadili mimi zijadili hoja.

Jibu maswali niliyokuuliza kabla hatujaendelea na mada yako.
 
Aya inayoashiria mkono na sio kiganja hii apa

وَالسَّارِقُ وَالسَّارِقَةُ فَاقْطَعُوا أَيْدِيَهُمَا جَزَاءً بِمَا كَسَبَا نَكَالًا مِّنَ اللَّهِ ۗ وَاللَّهُ عَزِيزٌ حَكِيمٌ

[ AL - MAIDA - 38 ]
Na mwizi mwanamume na mwizi mwanamke, ikateni mikono yao, hayo ni malipo ya waliyo yachuma, ndiyo adhabu ya mfano itokayo kwa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye hikima.

Aya imetaja AYDIYAHUMAA ni jam'u Ya YADU
na wala aya haikuitaja KAFFUN kwa maana ya kiganja.

Sasa hii aya mtume aliwakata watu viganja na Qurani imesema Mkono,unasemaje hapo my mother?

Kuhusu maswali yako.nilijibu labda hukuona.
Narudia kwa kurekebisha zaidi.

Kuhusu KUKUsanywa kwa hadithi wakati wa uhai wa mtume wA Allah.kwanza kabisa hadithi ni mafundisho ya mtume iwe vitendo,ama maneno yake.kwa maana akisema neno mtume kwa sisi tunaita hadithi .

Sasa kukusanywa kwa hadithi wakati wa mtume kams unakusudia kuzikusanya zote basi haiwezekani kuzikusanya zote kwa sababu bado mafundisho yalikuwa yanaendelea kwa kuwa mtume alikuwa hajafa.sasa ilikuwa likisemwa neno la mtume wapo ambao waliandika katika masahaba.

Mfano tu
Kulikiwa kuna Kitabu cha Hadiyth kilichoandikwa na Ibn ‘Amr (Radhiya Allaahu ‘anhuma) kinajulikana kama Swaadiqah الصادقة . Khalifah ‘Aliy (Radhiya Allaahu ‘anhu) pia alikuwa na nyaraka zilizoandikwa Hadiyth za Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu hukumu za Sheria.

Hawa ni masahaba ambao walimuona mtume na wakachukua mafundisho kutoka kwake.lakini haina maana walizikusanya hadithi zote kwa sababu kila sahaba alisuhubiana na mtume kwa namna yake,kwa hyo kila sahaba alikuwa ana zijua hadithi huwenda sahaba mwingine asiijue hadithi hiyo.

Wakati wa kutekwa Makkah kwa amani, Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alitoa hotuba. Al-Bukhaariy anaripoti kuwa kwa maombi ya Abu Shah (Radhiya Allaahu ‘anhu), Swahaba kutoka Yemen, Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliamuru hotuba hiyo aandikiwe.

Mtume wa Allah aliamuruhu hotuba hiyo iandikwe kuonyesha kwamba suala la kuandika lilikuepo wakati huo.

Lakini pia katika sulhu ya udaybiya ile mikataba iliandikwa katika makaratasi.na barua mbali mbali ambazo alizituma mtume kwenda kwa viongozi mbali mbali pia ziliandikwa.

Sasa unaposema kukusanya zilikusanywa lini naweza kukuambia zilianza kukusanywa tokea wakati wa Mtume huo huo kwa kuwepo baadhi ya masahaba wakiandika maneno yake na huko ni kukusanya.

Ama unakusudia kusema kwamba kukusanywa kulikamilika lini?

Mfano tukisema siku ya kusmza kukusanya kura za wananchi na siku zimekamilika kukusanywa hayo ni mambo tofauti.

Nadhani nimekujibu kama sijssahau.

ukiacha kuchagua jua umechagua kuacha
 
Hizi pesa tunazozishika siku zote kwani hakuna zinazopita kwa wauza "kiti moto"?

Naam, nnaweza. Si imeoshwa.

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?
[emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Swali:

Nipo safarini natoka ugenini naelekea nyumbani, nilinuia kuswali swala ya msafiri, nafika myumbani dhuhr, al asr , magharib na al ishaa zimepita.

Je nitaswali kwa kupunguza ama nitatimiza idadi ya rakaa kwa swala husika?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umeshafika nyumbani kwa hiyo siyo msafiri. Utasali kamili.
 
Kuhusu hiyo aya,

umeshafika nyumbani kwa hiyo siyo msafiri. Utasali kamili.
Nimeshakujibu

Sasa kwa mujibu wa aya je mtume alikuwa anakosea kukata watu viganja badala ya mkono kama isemavyo Qurani?

ukiacha kuchagua jua umechagua kuacha
 
Vipi kuhusu maisha ya kaburini, kuna kuonana kama tunavyoonana kwa hapa duniani, hiyo baada ya kufa?, na kutembeleana ?

Na mwili wako utakuwa unauona kama unavyouona ukiwa hai?

Shukralaki.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa mantiki hiyo unalipa sasa, manake swala imewekewa muda maalumu

Sent using Jamii Forums mobile app
Ilikuwa uswali hsta ukiwa kwenye basi umekaa kuliko kipindi kikupite mkuu.

Mm siku moja natoka home naenda dar maghribi ilinikuta njiani nikaimslizia kwenye siti khalas

ukiacha kuchagua jua umechagua kuacha
 
Ilikuwa uswali hsta ukiwa kwenye basi umekaa kuliko kipindi kikupite mkuu.

Mm siku moja natoka home naenda dar maghribi ilinikuta njiani nikaimslizia kwenye siti khalas

ukiacha kuchagua jua umechagua kuacha
Ni kweli, shida ni udhu tu ukiwa kwenye chombo cha moto unaupataje!

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Ungemleta huyo binti nimfunde mimi na wewe ungetafuta wanaume wenzio wakufunde.
 
Ni kweli, shida ni udhu tu ukiwa kwenye chombo cha moto unaupataje!

Sent using Jamii Forums mobile app
Ikiwa gari ipo kwenye mwendo na huwezi kusimama basi unatayammamu kwenye KOCHI la gari kwa dharula na wala hakuna ubaya katika hilo.

Kwa sababu katika misingi ya fiqhi kuns msingi usemao

لا محرم مع الضرورة،ولا واجب مع العجز
Hakuna uharamu wa jambo kwa mwenye dharula,na hakuna uwajibu wa jambo kwa asiyeweza.

Kwa maana upo safarini huwezi kupata maji wala kusimama kusali,hio ni dharula kwa kweli na hapo huwezi kupata maji wala mswala wala huwezi kusimama kwenye basi ukasali.kwa hyo uwajibu wa kutafuta maji na kutawadha na kusimama uwajibu huo unadondoks kwa sababu huwezi kuvipata na kuvifanys vitu hivyo.

Hapo unatayammam kwenye kochi na unasali,na hsuna uwajibu wa kuelekea kibls kwa sababu huwenda gari kibla imekiacha nyums na yale makona makona utapoteza kibla.hivyo utaelekea pale linapoenda gari hapo kikubwa nia.



ukiacha kuchagua jua umechagua kuacha
 
Kwa mantiki hiyo unalipa sasa, manake swala imewekewa muda maalumu

Sent using Jamii Forums mobile app
Maulamaa wanakhitilafiana. Mimi nafata Qur'an kwenye hilo:

Qur'an 4:103. Mkisha sali basi mkumbukeni Mwenyezi Mungu mkisimama, na mkikaa, na mnapo jinyoosha kwa kulala. Na mtapo tulia basi shikeni Sala kama dasturi. Kwani hakika Sala kwa Waumini ni faradhi iliyo wekewa nyakati maalumu 103
 
Mbona hii aya haijajibu swali langu, imetoa tu maelezo ya swala!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe kabila gani au una asili ya wapi

Sent using Jamii Forums mobile app
Siwezi kujibu hili. Ukipitia posts za juu huko nilitoa darsa kuhusu maswali ambayo hayana tija na yenye vinasaba vya ubaguzi. Sivi entertain hivyo.

Mimi ni Mswahili wa Pwani kabisa ya Tanzania, Shungubweni, MKURANGA.
 
Mbona hii aya haijajibu swali langu, imetoa tu maelezo ya swala!

Sent using Jamii Forums mobile app
Naam imejibu labda hukuisoma yote kwa utuvu, sentensi ya mwisho kabisa hapo inasema Kwani hakika Sala kwa Waumini ni faradhi iliyo wekewa nyakati maalumu.

Kwa maana hiyo swala huswaliwa kwa wakati wake. Ikukipita wakati wake hailipiki. Bali uombe maghfirah na toba kws Allah.

Allahu 'allam
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…