Faidika na darasa la FaizaFoxy; Uliza chochote utajibiwa

Faidika na darasa la FaizaFoxy; Uliza chochote utajibiwa

Shukran sana kwa ushauri mzuri.

1) Hivi Nchi za Rwanda, Congo, Burundi nk zilitawaliwa na France na Belgium kwa wakati mmoja au kwa nyakati tofauti au ikoje? Kwa nini ushawishi wa France kwa Mataifa hayo ni Mkubwa baada ya ukoloni kuliko Belgium kwa Mataifa hayo?

Naam, tuanze kwanza kuona kwa uchache historia ya karibuni ya ukoloni wa nchi hizo, tukianzia na Rwanda:

Rwanda

Ruanda- Urundi
Germany East Africa (Deutsch-Ostafrika) 1887-1914

Kumbukumbu za kihistoria zinaanza na utawala wa kifalme uliojulikana kama Ufalme wa Mwami (aka Mfalme) Rwabugiri .

Mzungu wa kwanza kufika Rwanda alikuwa ni Mjerumani, Count Von Gotzen ambae alitembelea medani ya Mwami Rwabugiri mnamo mwaka 1894, baada ya mwaka mfalme akafariki na kukaanza mvutano wa nani awe mrithi wa ufalme huo. Wakati Rwanda bado wapo kwenye kizazaa cha kushindania nani arithi, Wajerumani wakitokea Tanganyika, wakaingia nchini humo mwaka 1897 na kutangaza kuwa sasa huo ni utawala wa Kaiser wa Ujerumani.

Wakati huohuo wakatangaza (wakaamua) kuwa utawala wa Burundi nao ni wa Kaiser na ndipo pakajulikana kama Ruanda Urundi na kuwa Germany East Africa (Deutsch-Ostafrika), Rwanda, Burundi na Tanganyika.

Koloni la Ubelgiji (Belgium)

...Itaendelea
 
ANGALIA UNAVYOZUNGUKA KIVULI CHAKO MWENYEWE;
"lakini Kama unamaanisha shule za waislaam,basi nadhani zipo zinazofanya vizuri sana mojawapo ni feza"---HAPA NDIO NAANZA KUFAHAMU KUMBE KUNA SHULE ZA WAISLAAM ZINAZOFANYA VIZURI NA ZISIZO FANYA VIZURI.
"shule zisizofanya vizuri waende wakaone feza wanaweza vipi?"----OOH! KUMBE,SASA MBONA MNAWACHUKIA NECTA BURE TU,KUMBE TATIZO NI MANAGEMENT ZENU WENYEWE?.
MWISHO,KWAHIYO UNAWASHAURI WAMFUATE DK.MADATI ILI WASIWE WAMWISHO KILA MWAKA EEH! Basi msimchukie ndalichako na management yake wakati tiba ni kumfuata dk.madati wa feza awape mwongozo jinsi gani ya kupunguza div 0 na 4


Wa mwisho kila mwaka? tafadhali sana, kuwa mkweli wa nafsi yako, au dini yako inakufundisha kudanganya? (sidhani). Hebu nipe majina ya walioshika namba moja kitaifa mwaka jana, primary, O level na A level.
 
Wa mwisho kila mwaka? tafadhali sana, kuwa mkweli wa nafsi yako, au dini yako inakufundishi kudanganya? (sidhani). Hebu nipe majina ya walioshika namba moja kitaifa mwaka jana, primary, O level na A level.

Wewe umetahiriwa?
 
Mm ni msafr naweza kuzikusanya swala zot ktk muda 1?, mfano zot nikaziswali ktk muda wa dhuhr!
 
Kuna msichn mzr ambaye nimempend na kan pend, tatizo lake nkimtumia sms hajibu na akijbu hardish kw wakat.
Nifanyaj wadau
 
Naam, na mimi natazama hayo hayo kwa mwanamme atakae kuja kuoana na wa kwangu.
Madam umesema una degree ya kwanza katika maswala ya telecomunications na mara nyingi ulikua unamtetea sana JK na ccm kwa ujumla (japo sikuon ukiwa una mtetea makufuli)!!

Swali ni je kwa elimu yako ya canada je ulishiriki au ulitumika katika kuwahujumu chadema katika uchaguzi mkuu mwaka jana???
 
Madam umesema una degree ya kwanza katika maswala ya telecomunications na mara nyingi ulikua unamtetea sana JK na ccm kwa ujumla (japo sikuon ukiwa una mtetea makufuli)!!

Swali ni je kwa elimu yako ya canada je ulishiriki au ulitumika katika kuwahujumu chadema katika uchaguzi mkuu mwaka jana???

Hapana.

Chadema hawakuhujumiwa, walijihujumu wenyewe hususan pale mgombea wao alipoongea KKKT.

Si unakumbuka aliongea nini?
 
Hapana.

Chadema hawakuhujumiwa, walijihujumu wenyewe hususan pale mgombea wao alipoongea KKKT.

Si unakumbuka aliongea nini?
Si kweli. Je unakumbuka uchakachuzi wa kura? Je na wewe ulikuepo kwenye ku dukua matokeo?

Swali lingine...

Kuna tetesi zinasema wewe ulikua unapewa buku saba ili kumtetea kikwete humu je ni kweli???
 
207b65a26a318bb0aba30c22f8e9b527.jpg

KUNA WAKATI INABIDI MUONE HAIBU JAMANI.

= aibu
 
Si kweli. Je unakumbuka uchakachuzi wa kura? Je na wewe ulikuepo kwenye ku dukua matokeo?

Swali lingine...

Kuna tetesi zinasema wewe ulikua unapewa buku saba ili kumtetea kikwete humu je ni kweli???

 
Impeachment ilishafanyika miaka ya nyuma nadhani kwa Rais Nixon. Aliponea chupuchupu.

Tatizo kubwa linalomkabili Trump ni kwamba establishment(wenye Marekani) hawamtaki kabisa kwasababu mbalimbali.

Kwanza hatabiriki, kwahiyo ni vigumu kumshauri.

Pili ana nia ya dhati ya kuirudisha Marekani mikononi mwa Wamarekani wa kawaida na wa kati. Yuko against lile kundi dogo lenye nguvu sana(the Roschild and others) linaloitumia Marekani kwa maslahi yao binafsi. Katika hili John F. Kenedy alijaribu akaishia kuwa assassinated.

Vilivile, Trump ni mbaguzi kwa hiyo kuna hatari sera zake zikawa za kibaguzi pia. Ikumbukwe kuwa Trump ameshinda kura nyingi za wazungu kuliko watu wa rangi nyingine.
Nnakushauri ukiandika jambo la kihistoria tena kubwa kama la "impeachment" ujitulize na ufanye utafiti japo kiduchu kuliko kukurupuka na kuleta vitu vya kudhani.

Faidika na darsa la FaizaFoxy wa JF.

Rais Richard Nixon wa US hajawahi kuwa "impeached". Marais wa US waliowahi kuwa "impeached" na baraza la wawakilishi la US (House of Representatives) ni Rais Andrew Johnson na Rais Bill Clinton na wote wakaonekana na seneti (Senate) kuwa hawana hatia na kuendelea na kazi zao. Richard Nixon aliachia madaraka (resigned) kabla hajawa "impeached".
 
Back
Top Bottom