Familia tata

Familia tata

Nimeipenda kweli am waiting for the next episode!
 
iliyopita…
Mzee Komba akashauriwa
kurejea nyumbani ili
aweze kupumzisha akili
sambamba na kupokea
wageni, kazi ile ya
kushughulika na mwili wa
marehemu ikaachwa
mikononi mwa mzee Linus,
akishirikiana na vijana wa
familia zote mbili.
ENDELEA...
Nyumbani kwa mzee Komba,
watu walishaanza kujaa, kila
mmoja akizungumza kwa
jinsi alivyoona kuhusiana na
ajali ile. Mama yake Juddy,
alikuwa muda wote
akimtuliza shoga yake, dada
yake na jirani yake wa miaka
mingi, mama Tonny.
Uani, walikuwepo majirani
wawili, mama Rama na
mama Sabina, wamekaa
chini ya muarobaini
kujikinga na jua
wakizungumza.
“Mimi nina wasiwasi,” Mama
Rama alianza
“Wa nini na wewe shosti,
umeanza,” alijibu Mama
Sabina.
“Hii ajali, hivi unafikiri ni
bahati mbaya kweli?”
“Jamani hebu acha uchuro,
sasa wewe unadhani ni
makusudi?”
“Kabisa, akili yangu hainipi
kabisa, unakumbuka kifo cha
Juddy?”
“Jamani, kwani vipi mama
Rama?”
“Naona kama Bap kafanya
makusudi, hivi
unaendeshaje mwendo
mkali vile wakati umeshafika
nyumbani?”
“Usiseme hivyo, kwani wewe
ni mgeni na Bap, si kila siku
ndiyo mwendo wake
jamani?”
“Hata kama, naona kama
alikuwa anatafuta nafasi
alipize kisasi kwa kifo cha
dada yake, hivi unadhani
walifurahi kwa jinsi Tonny
alivyofanya?”
“Mmh, mi sidhani bwana,
naona ni ajali tu, mbona
Salum naye anaendeshaga
mwendo mkali, ingekuwa
yeye ndiyo kamgonga
ungesemaje,” Mama Sabina
alimwambia shoga yake,
akimzungumzia jirani yao
mwingine, Salum ambaye
pia anasifika kwa kuendesha
gari kwa mwendo kasi, hata
akiwa hatua mbili kutoka
nyumbani kwake…
***
Mzee Komba na vijana wake
walifanikiwa kuufikisha
mwili wa Santo katika
hospitali ya serikali ya
Mwananyamala, baada ya
kumaliza taratibu zote
wakarejea nyumbani
kujiunga na waombolezaji
wengine. Watu sasa
walishakuwa wengi.
Kila mmoja alizungumza
lake, lakini wengi wakilaumu
tabia ya uendeshaji wa
mwendokasi wa Bap,
wakisema kama isingekuwa
vile, angeweza kunusuru
maisha ya Santo. Hata
hivyo, hali ilikuwa tofauti
sana kwa mama yake
marehemu, mama Tonny.
Akiwa amejikunyata chini
alipolala kwenye mkeka
akifarijiwa na mama Juddy,
picha ya tukio lile ilijirudia.
Alimuona mtoto wake
akimtekenya, akajiona
mwenyewe akiinuka kwa
hasira na kuanza kumfukuza
mwanaye.
“Mwanangu nimemuua
mwenyewe dada,” alijikuta
akimwambia mama Juddy,
aliyekuwa na majirani
wengine wawili sebuleni
kwake, ambao nao
walishtushwa na kauli ile.
“Kivipi shoga,” Mama Juddy
alimuuliza mwenzake kwa
namna ya kushangaa kidogo,
maana alijua ni mtoto wake
ndiye alimuua Santo kwa
kumgonga na gari.
“Bila mimi asingeweza
kugongwa na gari. Tulikuwa
tunataniana na mwanangu
hapa ndani, nisingeinuka na
kuanza kumfukuza wala haya
yasingetokea. Hivi ni gari ya
nani imemgonga?” alisema
na kumalizia na swali!
Mama Juddy alisita kidogo
kujibu swali hilo,
akawatazama majirani zake
kuwaashiria wamjibu. Wote
walionekana kusita kujibu
hali iliyomfanya mama
Tonny kurudia kuuliza.
“Ni nani aliyemgonga
Santo?”
“Kagongwa na kaka yake,
Bap!” mama Juddy hatimaye
alisema, huku akimshika
mkono mfiwa katika namna
ya kumtuliza.
“Nani? Bap? No!” Mama
Tonny alijikuta akisema kwa
sauti iliyowashtua wote
waliokuwepo sebuleni.
Ghafla akainuka, akakaa
katika mkeka, akamtazama
shoga yake mama Juddy,
akamuegemea na kujikuta
akiangua kilio kwa sauti
huku akizungumza maneno
yasiyoeleweka!
***
Nje, chini ya mti, watu
kadhaa walikuwa wamekaa
wakizungumza taratibu. Kila
mmoja alikuwa na majonzi,
wakiomboleza msiba wa
ghafla wa Santo, kijana
mdogo aliyekuwa na umri
wa miaka tisa tu!
Mzee Linus alikuwa
amejiinamia, kichwani
mwake akiwaza mambo
mengi, kifo kile cha kijana
wake kilimuumiza sana,
lakini alimshukuru Mungu
kwa kila jambo. Kama
aliyekumbuka kitu,
akamshika mkono mzee
Komba na kumnong’oneza
jambo!
Je, nini kitatokea? Usikose
kusoma sehemu
inayofuata katika toleo
lijalo.
 
Ilipoishia wiki iliyopita..
Mzee Linus alikuwa
amejiinamia, kichwani
mwake akiwaza mambo
mengi, kifo kile cha kijana
wake kilimuumiza sana,
lakini alimshukuru Mungu
kwa kila jambo. Kama
aliyekumbuka kitu,
akamshika mkono mzee
Komba na kumnong’oneza
jambo!
SASA ENDELEA…
“Kaka!”
“Niambie,” Mzee Komba
alimuitikia rafiki yake,
kichwa chake kikiwa na
mawazo mengi.
“Hivi nini kitatokea kwa
Bap?” aliuliza tena
“Kivipi?” naye akajikuta
akiuliza.
“Hii kwake itakuwa ni kesi ya
mauaji au kitu gani,?”
“Sidhani, ni traffic case,”
alisema mzee Komba.
“Ila itabidi lazima
tumwambie Bap, tabia yake
ya kuendesha gari kwa kasi
si nzuri, atamgonga mtu
sehemu wasiyomfahamu,
wanaweza kumfanyia kitu
kibaya sana,” alisema mzee
Linus.
“Kila siku ninamkataza,
lakini hasikii. Kuna wakati
niliamua hata kumzuia
kuendesha gari, lakini
nikashindwa, hebu
tumuache, tuamini kwamba
atabadilika mwenyewe, hasa
baada ya tukio hili.”
“Lakini hatujafuatilia Polisi,
nini kimemtokea?”
“Amewekwa mahabusu,
katika jambo kama hili,
hatuna sababu ya
kuhangaika hivi sasa, hebu
hili tulijadili kesho, mwache
alale leo,”
Watu wakaendelea kujaa
pale nyumbani kwa mzee
Komba, msiba ulikuwa wa
ghafla sana. Mama yake
Tonny baada ya kuambiwa
aliyemgonga na kumuua
mwanawe ni Bap, akili yake
ikachanganyikiwa. Mambo
mengi yalipita kichwani
mwake, akajikuta akihusisha
tukio hilo na kile
kilichotokea mwaka mmoja
na nusu uliopita!
“Atakuwa amefanya
makusudi?” alijiuliza, lakini
sauti asiyoifahamu,
ikamtaarifu kuwa ni bahati
mbaya, naye kwa moyo
mkunjufu kabisa, akainua
mikono yake juu
akimshukuru Mungu na
kumuombea Baptist!
Baada ya kuwasiliana na
ndugu zake wa karibu
ambao walikuja msibani
pale siku ile ile, mzee
Komba akawatangazia
majirani na waombolezaji
wengine kuwa mazishi ya
mtoto wake yatafanyika siku
tatu baadaye, wakisubiri
watu wengine waliokuwa nje
ya Dar es Salaam wafike.
Hakutaka kwenda kumzika
mtoto wake nyumbani kwao
Mbinga, alitaka azikwe Dar
kwa kuwa ndipo yalipo
maisha yake!
Asfat aliwasili Dar es Salaam
saa tano na nusu asubuhi,
akakodi teksi iliyomtoa
uwanja wa ndege wa Julius
Nyerere na kumfikisha
Nakasagwe saa saba
mchana. Alipokelewa kwa
vilio kutoka kwa ndugu,
jamaa na marafiki. Baada ya
kuingiza begi lake chumbani
kwake, akaingia bafuni na
alipomaliza kuoga,
akamfuata mama yake na
kumuomba waongee kidogo.
Wakatoka nje kabisa ya
nyumba, ambako watu
walikuwa wametapakaa.
Wakatafuta eneo la peke
yao, wakakaa chini ya
matofali na kuanza
kuzungumza. Asfat akamtaka
mama yake amueleze ukweli
juu ya tukio lile, kwa sababu
alimwambia wazi kuwa yeye
binafsi, haamini kama ile
ilikuwa ni ajali kama ajali
zingine.
Mama akamtazama, macho
yake yakaanza kujaa
machozi, akajifuta kwa
khanga aliyokuwa
amejifunga na baadaye
akamwambia;
“Hata mimi mwanzo
nilikuwa na mawazo kama
yako, sikuamini mara moja,
lakini kadiri nikirejea tukio
zima, sioni ni wapi Bap
alikusudia. Kama kuna mtu
wa kumlaumu, nilaumuni
mimi, nisingemfukuza,
asingetoka nje.”
Kwa mara nyingine, Asfat
akakubali, lakini
hakuridhika!
Baada ya kumaliza
mazungumzo hayo, akarejea
chumbani kwake,
akaikumbuka albamu yake
ya picha, akaichukua na
kuanza kuziangalia picha
zake, zikiwemo za zamani
enzi za utoto hadi
ukubwani.
Akakutana na picha
aliyoipenda sana, alikuwa
amepiga na marehemu
Juddy, wakati flani wa
sikukuu ya Krismas, miaka
kadhaa iliyopita, aliipenda
picha hiyo kwa vile
ilimkumbusha mambo ya
siku hiyo, ambayo hawezi
kusahau.
Nini kitatokea? Usikose
kufuatilia simulizi hii ya
kusisimua katika toleo
lijalo.
 
Tatizo lako mkuu Luthar hutabiriki siku wala saa.
 
Last edited by a moderator:
11 Ilipoishia wiki iliyopita..
Mzee Linus alikuwa
amejiinamia, kichwani
mwake akiwaza mambo
mengi, kifo kile cha kijana
wake kilimuumiza sana,
lakini alimshukuru Mungu
kwa kila jambo. Kama
aliyekumbuka kitu,
akamshika mkono mzee
Komba na kumnong’oneza
jambo!
SASA ENDELEA…
“Kaka!”
“Niambie,” Mzee Komba
alimuitikia rafiki yake,
kichwa chake kikiwa na
mawazo mengi.
“Hivi nini kitatokea kwa
Bap?” aliuliza tena
“Kivipi?” naye akajikuta
akiuliza.
“Hii kwake itakuwa ni kesi ya
mauaji au kitu gani,?”
“Sidhani, ni traffic case,”
alisema mzee Komba.
“Ila itabidi lazima
tumwambie Bap, tabia yake
ya kuendesha gari kwa kasi
si nzuri, atamgonga mtu
sehemu wasiyomfahamu,
wanaweza kumfanyia kitu
kibaya sana,” alisema mzee
Linus.
“Kila siku ninamkataza,
lakini hasikii. Kuna wakati
niliamua hata kumzuia
kuendesha gari, lakini
nikashindwa, hebu
tumuache, tuamini kwamba
atabadilika mwenyewe, hasa
baada ya tukio hili.”
“Lakini hatujafuatilia Polisi,
nini kimemtokea?”
“Amewekwa mahabusu,
katika jambo kama hili,
hatuna sababu ya
kuhangaika hivi sasa, hebu
hili tulijadili kesho, mwache
alale leo,”
Watu wakaendelea kujaa
pale nyumbani kwa mzee
Komba, msiba ulikuwa wa
ghafla sana. Mama yake
Tonny baada ya kuambiwa
aliyemgonga na kumuua
mwanawe ni Bap, akili yake
ikachanganyikiwa. Mambo
mengi yalipita kichwani
mwake, akajikuta akihusisha
tukio hilo na kile
kilichotokea mwaka mmoja
na nusu uliopita!
“Atakuwa amefanya
makusudi?” alijiuliza, lakini
sauti asiyoifahamu,
ikamtaarifu kuwa ni bahati
mbaya, naye kwa moyo
mkunjufu kabisa, akainua
mikono yake juu
akimshukuru Mungu na
kumuombea Baptist!
Baada ya kuwasiliana na
ndugu zake wa karibu
ambao walikuja msibani
pale siku ile ile, mzee
Komba akawatangazia
majirani na waombolezaji
wengine kuwa mazishi ya
mtoto wake yatafanyika siku
tatu baadaye, wakisubiri
watu wengine waliokuwa nje
ya Dar es Salaam wafike.
Hakutaka kwenda kumzika
mtoto wake nyumbani kwao
Mbinga, alitaka azikwe Dar
kwa kuwa ndipo yalipo
maisha yake!
Asfat aliwasili Dar es Salaam
saa tano na nusu asubuhi,
akakodi teksi iliyomtoa
uwanja wa ndege wa Julius
Nyerere na kumfikisha
Nakasagwe saa saba
mchana. Alipokelewa kwa
vilio kutoka kwa ndugu,
jamaa na marafiki. Baada ya
kuingiza begi lake chumbani
kwake, akaingia bafuni na
alipomaliza kuoga,
akamfuata mama yake na
kumuomba waongee kidogo.
Wakatoka nje kabisa ya
nyumba, ambako watu
walikuwa wametapakaa.
Wakatafuta eneo la peke
yao, wakakaa chini ya
matofali na kuanza
kuzungumza. Asfat akamtaka
mama yake amueleze ukweli
juu ya tukio lile, kwa sababu
alimwambia wazi kuwa yeye
binafsi, haamini kama ile
ilikuwa ni ajali kama ajali
zingine.
Mama akamtazama, macho
yake yakaanza kujaa
machozi, akajifuta kwa
khanga aliyokuwa
amejifunga na baadaye
akamwambia;
“Hata mimi mwanzo
nilikuwa na mawazo kama
yako, sikuamini mara moja,
lakini kadiri nikirejea tukio
zima, sioni ni wapi Bap
alikusudia. Kama kuna mtu
wa kumlaumu, nilaumuni
mimi, nisingemfukuza,
asingetoka nje.”
Kwa mara nyingine, Asfat
akakubali, lakini
hakuridhika!
Baada ya kumaliza
mazungumzo hayo, akarejea
chumbani kwake,
akaikumbuka albamu yake
ya picha, akaichukua na
kuanza kuziangalia picha
zake, zikiwemo za zamani
enzi za utoto hadi
ukubwani.
Akakutana na picha
aliyoipenda sana, alikuwa
amepiga na marehemu
Juddy, wakati flani wa
sikukuu ya Krismas, miaka
kadhaa iliyopita, aliipenda
picha hiyo kwa vile
ilimkumbusha mambo ya
siku hiyo, ambayo hawezi
kusahau.
Nini kitatokea? Usikose
kufuatilia simulizi hii ya
kusisimua katika toleo
lijalo.
 
11 Ilipoishia wiki iliyopita..
Mzee Linus alikuwa
amejiinamia, kichwani
mwake akiwaza mambo
mengi, kifo kile cha kijana
wake kilimuumiza sana,
lakini alimshukuru Mungu
kwa kila jambo. Kama
aliyekumbuka kitu,
akamshika mkono mzee
Komba na kumnong’oneza
jambo!
SASA ENDELEA…
“Kaka!”
“Niambie,” Mzee Komba
alimuitikia rafiki yake,
kichwa chake kikiwa na
mawazo mengi.
“Hivi nini kitatokea kwa
Bap?” aliuliza tena
“Kivipi?” naye akajikuta
akiuliza.
“Hii kwake itakuwa ni kesi ya
mauaji au kitu gani,?”
“Sidhani, ni traffic case,”
alisema mzee Komba.
“Ila itabidi lazima
tumwambie Bap, tabia yake
ya kuendesha gari kwa kasi
si nzuri, atamgonga mtu
sehemu wasiyomfahamu,
wanaweza kumfanyia kitu
kibaya sana,” alisema mzee
Linus.
“Kila siku ninamkataza,
lakini hasikii. Kuna wakati
niliamua hata kumzuia
kuendesha gari, lakini
nikashindwa, hebu
tumuache, tuamini kwamba
atabadilika mwenyewe, hasa
baada ya tukio hili.”
“Lakini hatujafuatilia Polisi,
nini kimemtokea?”
“Amewekwa mahabusu,
katika jambo kama hili,
hatuna sababu ya
kuhangaika hivi sasa, hebu
hili tulijadili kesho, mwache
alale leo,”
Watu wakaendelea kujaa
pale nyumbani kwa mzee
Komba, msiba ulikuwa wa
ghafla sana. Mama yake
Tonny baada ya kuambiwa
aliyemgonga na kumuua
mwanawe ni Bap, akili yake
ikachanganyikiwa. Mambo
mengi yalipita kichwani
mwake, akajikuta akihusisha
tukio hilo na kile
kilichotokea mwaka mmoja
na nusu uliopita!
“Atakuwa amefanya
makusudi?” alijiuliza, lakini
sauti asiyoifahamu,
ikamtaarifu kuwa ni bahati
mbaya, naye kwa moyo
mkunjufu kabisa, akainua
mikono yake juu
akimshukuru Mungu na
kumuombea Baptist!
Baada ya kuwasiliana na
ndugu zake wa karibu
ambao walikuja msibani
pale siku ile ile, mzee
Komba akawatangazia
majirani na waombolezaji
wengine kuwa mazishi ya
mtoto wake yatafanyika siku
tatu baadaye, wakisubiri
watu wengine waliokuwa nje
ya Dar es Salaam wafike.
Hakutaka kwenda kumzika
mtoto wake nyumbani kwao
Mbinga, alitaka azikwe Dar
kwa kuwa ndipo yalipo
maisha yake!
Asfat aliwasili Dar es Salaam
saa tano na nusu asubuhi,
akakodi teksi iliyomtoa
uwanja wa ndege wa Julius
Nyerere na kumfikisha
Nakasagwe saa saba
mchana. Alipokelewa kwa
vilio kutoka kwa ndugu,
jamaa na marafiki. Baada ya
kuingiza begi lake chumbani
kwake, akaingia bafuni na
alipomaliza kuoga,
akamfuata mama yake na
kumuomba waongee kidogo.
Wakatoka nje kabisa ya
nyumba, ambako watu
walikuwa wametapakaa.
Wakatafuta eneo la peke
yao, wakakaa chini ya
matofali na kuanza
kuzungumza. Asfat akamtaka
mama yake amueleze ukweli
juu ya tukio lile, kwa sababu
alimwambia wazi kuwa yeye
binafsi, haamini kama ile
ilikuwa ni ajali kama ajali
zingine.
Mama akamtazama, macho
yake yakaanza kujaa
machozi, akajifuta kwa
khanga aliyokuwa
amejifunga na baadaye
akamwambia;
“Hata mimi mwanzo
nilikuwa na mawazo kama
yako, sikuamini mara moja,
lakini kadiri nikirejea tukio
zima, sioni ni wapi Bap
alikusudia. Kama kuna mtu
wa kumlaumu, nilaumuni
mimi, nisingemfukuza,
asingetoka nje.”
Kwa mara nyingine, Asfat
akakubali, lakini
hakuridhika!
Baada ya kumaliza
mazungumzo hayo, akarejea
chumbani kwake,
akaikumbuka albamu yake
ya picha, akaichukua na
kuanza kuziangalia picha
zake, zikiwemo za zamani
enzi za utoto hadi
ukubwani.
Akakutana na picha
aliyoipenda sana, alikuwa
amepiga na marehemu
Juddy, wakati flani wa
sikukuu ya Krismas, miaka
kadhaa iliyopita, aliipenda
picha hiyo kwa vile
ilimkumbusha mambo ya
siku hiyo, ambayo hawezi
kusahau.
Nini kitatokea? Usikose
kufuatilia simulizi hii ya
kusisimua katika toleo
lijalo.

Umerudia episode
 
Umerudia episode

Karudia mara mbili, ndo ujue kuna sehemu ana copy na kupest. Lakini mpenzi wangu ndo lazima uquote mpost mzima jamani? Haka kasimu nakokatumia kanawaka moto jamani.
 
Karudia mara mbili, ndo ujue kuna sehemu ana copy na kupest. Lakini mpenzi wangu ndo lazima uquote mpost mzima jamani? Haka kasimu nakokatumia kanawaka moto jamani.

Ha ha haaaaaaaa, ndo apate ajue na afaham eti.

Km vp tumpatie dozi ya aspirin
 
Ha ha haaaaaaaa, ndo apate ajue na afaham eti.

Km vp tumpatie dozi ya aspirin

Njoo nikugaie umpelekee. kangekua kabinti ningekapelekea mwenyewe. Hebu nambie, hii valentine, haka kamwaga mkojo kako kalipita salama?
 
Njoo nikugaie umpelekee. kangekua kabinti ningekapelekea mwenyewe. Hebu nambie, hii valentine, haka kamwaga mkojo kako kalipita salama?

Lols, hayo ya Valentine mi hata siyajui. So jana imepita kama ilivopita juzi na leo
 
iyopita
Akakutana na picha
aliyoipenda sana, alikuwa
amepiga na marehemu
Juddy, wakati flani wa
sikukuu ya Krismas, miaka
kadhaa iliyopita, aliipenda
picha hiyo kwa vile
ilimkumbusha mambo ya
siku hiyo, ambayo hawezi
kusahau.
SASA ENDELEA…
Ni siku ambayo alimjua
mwanaume kwa mara ya
kwanza. Alifanya tendo hilo
katika vyoo vya ukumbi wa
disco, katika ufukwe wa
Coco, jijini Dar es Salaam.
“Ninahitaji kuongea na
Festo,” alijisemea
mwenyewe, akimkumbuka
mvulana ambaye alifanya
naye kitendo hicho, ambaye
walikuwa bado
wakiwasiliana, ingawa urafiki
wao wa kimapenzi ulikuwa
umefifia sana!
Festo baada ya kumaliza
shule, alienda India
kusomea udaktari, mara ya
mwisho walipowasiliana, ni
wakati alipompigia simu
akiwa Mumbai, akimtaka
ampokee uwanja wa ndege
wa Heathrow, jijini London
alipokwenda kwa shughuli
zake. Hiyo ilikuwa mara yake
ya kwanza kufika Uingereza
na hakutaka kuhangaika.
Alimpokea na kumwelekeza
sehemu anayoweza kufikia.
Baada ya hapo waliwasiliana
tu kwa simu hadi Festo
aliporejea Dar es Salaam na
kuajiriwa katika hospitali ya
Taifa Muhimbili. Asfat
akaitoa simu yake ya
mkononi, akatafuta jina
alilolihitaji, alipolipata
akabonyeza kupiga.
“Mambo?” Asfat alizungumza
mara baada ya upande wa
pili kupokea.
“Poa, umekuja lini mbona
kimya kimya,” upande wa
pili nao ukajibu.
“Nimepata msiba ghafla,
mdogo wangu Santo
amefariki juzi kwa kugongwa
na gari,”
“Dah, pole sana aisee,
mipango ikoje,”
“Tunategemea kuzika
keshokutwa hapa hapa Dar,”
alisema Asfat.
Baada ya kimya kidogo
kupita, Asfat akarudi tena
simuni.
“Festo,nina shida sana ya
kuonana na wewe, ni
muhimu sana katika maisha
yangu kwa kweli,”
“Nitakuja msibani kesho,
tutaongea.”
“Hapana, sitaki tuzungumzie
huku, iwe sehemu nyingine,”
Asfat alisema na kumfanya
Festo ahamishe hisia zake,
akadhani mwenzake alihitaji
mazungumzo ya kimapenzi.
“Wapi sasa, hoteli?”
akajikuta akiuliza.
“Hapana, sehemu tu tulivu,
ninahitaji kuongea na wewe,
nina ishu ya muhimu sana
kwangu,”
Baada ya kujibishana kwa
muda wakakubaliana siku na
muda wa kuonana!
Shughuli ya msiba
iliendelea, maneno ya hapa
na pale yaliendelea kama
kawaida ya misiba ya
uswahilini. Kwa muda wote,
mama Juddy hakubanduka
karibu na mama Tonny,
alikaa naye na kumfariji kwa
kila kilichoendelea. Hali
kama hiyo pia ilikuwa kwa
mzee Linus na rafiki yake
mzee Komba.
Watoto wa familia zote nao
walikuwa kitu kimoja,
hakuna mtu aliyeonyesha
tofauti. Walishirikiana kama
kawaida hadi msiba ule
ukaonekana wa familia zote.
Hatimaye mazishi
yakafanyika katika makaburi
ya Nakasangwe, karibu
kabisa na sehemu aliyozikwa
Juddy, mwaka mmoja na
nusu uliopita. Wiki mbili
baada ya mazishi hayo,
maisha yaliendelea kama
kawaida.
***
“Ndiyo hivyo Festo, nataka
kulipiza kisasi, nisaidie jinsi
ya kuipata hiyo sumu,” Asfat
alimalizia kwa kumwambia
mpenzi wake wa zamani,
baada ya kumweleza mkasa
wa familia zao na jinsi
ambavyo hakuridhishwa na
kifo cha mdogo wake,
akiamini Baptist alifanya
makusudi.
Walikuwa wamekaa pembeni
katika ufukwe wa Kawe,
wakiwaangalia watu
mbalimbali wakipunga
upepo na kuogelea.
Asfat alitaka kulipiza kisasi
kwa kumuua ye yote katika
familia ya mzee Linus,
ilimuuma sana.
“Hapana Asfat, siwezi
kukusaidia kutimiza lengo
lako, sisi tumeapa kumsaidia
mgonjwa na siyo kummaliza,
isitoshe, kwa jinsi watu
walivyokuwa wakizungumza
siku ile pale msibani,
inaonekana kabisa ni ajali,”
Festo alimwambia Asfat,
aliyetoa macho kwa
mshangao.
Je, nini kitatokea? Fuatilia
katika toleo lijalo.
 
Karudia mara mbili, ndo ujue kuna sehemu ana copy na kupest. Lakini mpenzi wangu ndo lazima uquote mpost mzima jamani? Haka kasimu nakokatumia kanawaka moto jamani.

Mkuu kasimu gani hako au mkorea? Pole
 
ndilo tatizo la wa tz mtu anangangania ni copy sawa kwani imekanushwa umeona haikufai waweza pita hivi..........siyo lazima usome
 
ndilo tatizo la wa tz mtu anangangania ni copy sawa kwani imekanushwa umeona haikufai waweza pita hivi..........siyo lazima usome

Endelea na story kwanza mkuu, wengine tunafatilia
 
Back
Top Bottom