Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,743
- 25,564
SEHEMU YA 11
Akakutana na picha aliyoipenda sana, alikuwa amepiga na marehemu Juddy, wakati flani wa sikukuu ya Krismas, miaka kadhaa iliyopita, aliipenda picha hiyo kwa vile ilimkumbusha mambo ya siku hiyo, ambayo hawezi kusahau.
SASA ENDELEA…
Ni siku ambayo alimjua mwanaume kwa mara ya kwanza. Alifanya tendo hilo katika vyoo vya ukumbi wa disco, katika ufukwe wa Coco, jijini Dar es Salaam.
“Ninahitaji kuongea na Festo,” alijisemea mwenyewe, akimkumbuka mvulana ambaye alifanya naye kitendo hicho, ambaye walikuwa bado wakiwasiliana, ingawa urafiki wao wa kimapenzi ulikuwa umefifia sana!
Festo baada ya kumaliza shule, alienda India kusomea udaktari, mara ya mwisho walipowasiliana, ni wakati alipompigia simu akiwa Mumbai, akimtaka ampokee uwanja wa ndege wa Heathrow, jijini London alipokwenda kwa shughuli zake. Hiyo ilikuwa mara yake ya kwanza kufika Uingereza na hakutaka kuhangaika. Alimpokea na kumwelekeza sehemu anayoweza kufikia.
Baada ya hapo waliwasiliana tu kwa simu hadi Festo aliporejea Dar es Salaam na kuajiriwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili. Asfat akaitoa simu yake ya mkononi, akatafuta jina alilolihitaji, alipolipata akabonyeza kupiga.
“Mambo?” Asfat alizungumza mara baada ya upande wa pili kupokea.
“Poa, umekuja lini mbona kimya kimya,” upande wa pili nao ukajibu.
“Nimepata msiba ghafla, mdogo wangu Santo amefariki juzi kwa kugongwa na gari,”
“Dah, pole sana aisee, mipango ikoje,”
“Tunategemea kuzika keshokutwa hapa hapa Dar,” alisema Asfat.
Baada ya kimya kidogo kupita, Asfat akarudi tena simuni.
“Festo, nina shida sana ya kuonana na wewe, ni muhimu sana katika maisha yangu kwa kweli,”
“Nitakuja msibani kesho, tutaongea.”
“Hapana, sitaki tuzungumzie huku, iwe sehemu nyingine,” Asfat alisema na kumfanya Festo ahamishe hisia zake, akadhani mwenzake alihitaji mazungumzo ya kimapenzi.
“Wapi sasa, hoteli?” akajikuta akiuliza.
“Hapana, sehemu tu tulivu, ninahitaji kuongea na wewe, nina ishu ya muhimu sana kwangu,”
Baada ya kujibishana kwa muda wakakubaliana siku na muda wa kuonana!
Shughuli ya msiba iliendelea, maneno ya hapa na pale yaliendelea kama kawaida ya misiba ya uswahilini. Kwa muda wote, mama Juddy hakubanduka karibu na mama Tonny, alikaa naye na kumfariji kwa kila kilichoendelea. Hali kama hiyo pia ilikuwa kwa mzee Linus na rafiki yake mzee Komba.
Watoto wa familia zote nao walikuwa kitu kimoja, hakuna mtu aliyeonyesha tofauti. Walishirikiana kama kawaida hadi msiba ule ukaonekana wa familia zote.
Hatimaye mazishi yakafanyika katika makaburi ya Nakasangwe, karibu kabisa na sehemu aliyozikwa Juddy, mwaka mmoja na nusu uliopita. Wiki mbili baada ya mazishi hayo, maisha yaliendelea kama kawaida.
***
“Ndiyo hivyo Festo, nataka kulipiza kisasi, nisaidie jinsi ya kuipata hiyo sumu,” Asfat alimalizia kwa kumwambia mpenzi wake wa zamani, baada ya kumweleza mkasa wa familia zao na jinsi ambavyo hakuridhishwa na kifo cha mdogo wake, akiamini Baptist alifanya makusudi.
Walikuwa wamekaa pembeni katika ufukwe wa Kawe, wakiwaangalia watu mbalimbali wakipunga upepo na kuogelea.
Asfat alitaka kulipiza kisasi kwa kumuua ye yote katika familia ya mzee Linus, ilimuuma sana.
“Hapana Asfat, siwezi kukusaidia kutimiza lengo lako, sisi tumeapa kumsaidia mgonjwa na siyo kummaliza, isitoshe, kwa jinsi watu walivyokuwa wakizungumza siku ile pale msibani, inaonekana kabisa ni ajali,” Festo alimwambia Asfat, aliyetoa macho kwa mshangao.
Akakutana na picha aliyoipenda sana, alikuwa amepiga na marehemu Juddy, wakati flani wa sikukuu ya Krismas, miaka kadhaa iliyopita, aliipenda picha hiyo kwa vile ilimkumbusha mambo ya siku hiyo, ambayo hawezi kusahau.
SASA ENDELEA…
Ni siku ambayo alimjua mwanaume kwa mara ya kwanza. Alifanya tendo hilo katika vyoo vya ukumbi wa disco, katika ufukwe wa Coco, jijini Dar es Salaam.
“Ninahitaji kuongea na Festo,” alijisemea mwenyewe, akimkumbuka mvulana ambaye alifanya naye kitendo hicho, ambaye walikuwa bado wakiwasiliana, ingawa urafiki wao wa kimapenzi ulikuwa umefifia sana!
Festo baada ya kumaliza shule, alienda India kusomea udaktari, mara ya mwisho walipowasiliana, ni wakati alipompigia simu akiwa Mumbai, akimtaka ampokee uwanja wa ndege wa Heathrow, jijini London alipokwenda kwa shughuli zake. Hiyo ilikuwa mara yake ya kwanza kufika Uingereza na hakutaka kuhangaika. Alimpokea na kumwelekeza sehemu anayoweza kufikia.
Baada ya hapo waliwasiliana tu kwa simu hadi Festo aliporejea Dar es Salaam na kuajiriwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili. Asfat akaitoa simu yake ya mkononi, akatafuta jina alilolihitaji, alipolipata akabonyeza kupiga.
“Mambo?” Asfat alizungumza mara baada ya upande wa pili kupokea.
“Poa, umekuja lini mbona kimya kimya,” upande wa pili nao ukajibu.
“Nimepata msiba ghafla, mdogo wangu Santo amefariki juzi kwa kugongwa na gari,”
“Dah, pole sana aisee, mipango ikoje,”
“Tunategemea kuzika keshokutwa hapa hapa Dar,” alisema Asfat.
Baada ya kimya kidogo kupita, Asfat akarudi tena simuni.
“Festo, nina shida sana ya kuonana na wewe, ni muhimu sana katika maisha yangu kwa kweli,”
“Nitakuja msibani kesho, tutaongea.”
“Hapana, sitaki tuzungumzie huku, iwe sehemu nyingine,” Asfat alisema na kumfanya Festo ahamishe hisia zake, akadhani mwenzake alihitaji mazungumzo ya kimapenzi.
“Wapi sasa, hoteli?” akajikuta akiuliza.
“Hapana, sehemu tu tulivu, ninahitaji kuongea na wewe, nina ishu ya muhimu sana kwangu,”
Baada ya kujibishana kwa muda wakakubaliana siku na muda wa kuonana!
Shughuli ya msiba iliendelea, maneno ya hapa na pale yaliendelea kama kawaida ya misiba ya uswahilini. Kwa muda wote, mama Juddy hakubanduka karibu na mama Tonny, alikaa naye na kumfariji kwa kila kilichoendelea. Hali kama hiyo pia ilikuwa kwa mzee Linus na rafiki yake mzee Komba.
Watoto wa familia zote nao walikuwa kitu kimoja, hakuna mtu aliyeonyesha tofauti. Walishirikiana kama kawaida hadi msiba ule ukaonekana wa familia zote.
Hatimaye mazishi yakafanyika katika makaburi ya Nakasangwe, karibu kabisa na sehemu aliyozikwa Juddy, mwaka mmoja na nusu uliopita. Wiki mbili baada ya mazishi hayo, maisha yaliendelea kama kawaida.
***
“Ndiyo hivyo Festo, nataka kulipiza kisasi, nisaidie jinsi ya kuipata hiyo sumu,” Asfat alimalizia kwa kumwambia mpenzi wake wa zamani, baada ya kumweleza mkasa wa familia zao na jinsi ambavyo hakuridhishwa na kifo cha mdogo wake, akiamini Baptist alifanya makusudi.
Walikuwa wamekaa pembeni katika ufukwe wa Kawe, wakiwaangalia watu mbalimbali wakipunga upepo na kuogelea.
Asfat alitaka kulipiza kisasi kwa kumuua ye yote katika familia ya mzee Linus, ilimuuma sana.
“Hapana Asfat, siwezi kukusaidia kutimiza lengo lako, sisi tumeapa kumsaidia mgonjwa na siyo kummaliza, isitoshe, kwa jinsi watu walivyokuwa wakizungumza siku ile pale msibani, inaonekana kabisa ni ajali,” Festo alimwambia Asfat, aliyetoa macho kwa mshangao.