Familia tata

Familia tata

ndilo tatizo la wa tz mtu anangangania ni copy sawa kwani imekanushwa umeona haikufai waweza pita hivi..........siyo lazima usome

Mkuu ni anang'ang'ania na siyo anangangania.
Nakurekebisha tu maana nakipenda sana kiswahili.
Amani itawale leo jumapili.
 
SEHEMU YA 06



Lakini sifa yake kubwa ilikuwa ni tabia yake ya kuendesha magari kwa mwendo kasi. Hata kama alikuwa akienda sehemu ya karibu, alipenda kulikimbiza...
Sasa Endelea...
Mama yake Tonny alikuwa uani kwake akifua nguo za mtoto wake wa mwisho, Subby wakati akitaniana na kaka yake Tonny aliyeitwa Santo. Santo alikuwa akisoma darasa la saba katika Shule ya Msingi Bunge na siku hiyo ya Jumamosi, hakwenda shule.
Mama Tonny alikuwa akimpenda sana Santo na mara nyingi walikuwa wakitaniana. Leo, wakiwa hapa, mama alikuwa akimshambulia Tonny kwamba ni lazima atafeli kwa sababu ya kupenda sana filamu. Na kweli, Santo alikuwa shabiki mkubwa wa filamu, hasa za Kizungu, ingawa pia alivutiwa na zile za Kihindi na Kibongo.
Baada ya kuzidiwa utani na mama yake, Santo akaamua kuondoka lakini akamvizia akiwa amejisahau, akamtekenya kwenye mbavu. Mama alipata mshtuko mkubwa na akiwa na hasira, aliinuka na kuanza kumfukuza kijana wake aliyekuwa anakimbilia nje ya geti!
***
Baptist alikuwa anakata kona maarufu mtaani kwao iitwayo Kwa Kipira, akiwa katika mwendo wa kasi kama kawaida yake. Mtaa ulikuwa kimya na hakukuwa na mtu barabarani. Akiwa anakaribia kwenye geti la nyumba ya Mzee Komba, ghafla akamuona mtu akitokeza kwa kasi na kuingia barabarani.
Hakuweza kujizuia, hakuweza kulizuia gari, kishindo kikubwa kikasikika na mtu mmoja alionekana akirushwa juu na alipoanguka chini, akabakia kuwa mtulivu pale chini alipofikia.
Alikuwa ni Santo!
Kishindo kile kilileta kelele kubwa mtaani na mara moja, kila mtu aliyekuwepo alitoka nje ya nyumba ili kushuhudia kilichotokea. Bap alifanikiwa kusimamisha gari mita chache mbele, akatoka nje ya gari na kumkimbilia mtu aliyemgonga!
Kishindo kile kilikuwa kama nyundo iliyopiga katika kichwa cha mama yake Tonny, alitambua kabisa kwamba aliyegongwa ni mtoto wake. Naye pasipo kutarajia alianguka na kupoteza fahamu muda uleule mwanaye alipogongwa.
Ndani ya dakika moja, watu wengi walijazana pale alipokuwa amelala Santo, mwili wake ulijaa damu na watu wakawa kama waliochanganyikiwa. Kwa muda wakawa hawajui wafanye nini hadi akili zilipowarejea.
Baptist alikuwa wa kwanza kumshika Santo, akamgeuza vizuri na kumtazama, akatoa ishara kwa wenzake wambebe, wakampakia kwenye gari alilomgonga nalo. Watu wengine wawili wakaingia ndani ya gari lile, kwa kasi ya ajabu, likaondoka kuelekea hospitalini!
Watu wengine nao mtaani wakawasha magari yao na kulifuatilia gari lililombeba Santo. Baptist aliendesha gari kwa kasi hadi alipofika katika Hospitali ya Mico iliyopo Tegeta Basihaya. Madaktari wakampokea haraka mgonjwa na moja kwa moja akapelekwa chumba cha upasuaji!
Nyumbani kwa akina Santo, baadhi ya majirani walishtuka baada ya kumuona mama yake Santo akiwa amelala chini, tena kwa namna ya kutisha. Walipomchunguza, wakagundua kwamba alikuwa amepoteza fahamu.
Wakamfanyia huduma ya kwanza, kisha wakambeba na kumwingiza ndani kwake. Alirejewa na fahamu baada ya nusu saa, akashangaa kuona watu wamemzunguka sebuleni alipolala kwenye kochi.
“Vipi?” aliwauliza wanawake wawili waliokuwa karibu yake, akiwemo mama yake Juddy.
“Tulia, tuliza akili kwanza, upo salama?” mama Juddy alimwambia mwenzake huku akimtengeneza vizuri kanga zake alizojifunga.
“Kuna nini kimetokea dada, niambie haraka,” mama yake Santo alimwambia mama Juddy huku akimshika mikono yake kwa nguvu kubwa.
“Tumekukuta umeanguka pale mlangoni kwako, ndiyo tukakubeba na kukuingiza ndani,” alijibiwa!
“Mnenikuta nimeanguka?” aliuliza tena na kuanza kuvuta kumbukumbu.
Je, nini kitatokea? Usikose kufuatilia simulizi hii katika toleo lijalo
 
SEHEMU YA 07


“Tumekukuta umeanguka pale mlangoni kwako, ndiyo tukakubeba na kukuingiza ndani,” alijibiwa!
“Mmenikuta nimeanguka?” aliuliza tena na kuanza kuvuta kumbukumbu…!!!
Sasa endelea...
Baada ya kumfikisha hospitalini alikopokelewa, Baptist akachukua simu yake na kumpigia baba yake mzazi, mzee Linus.
“Shikamoo baba,” Baptist aliongea mara tu ilipopokelewa.
“Marahaba, tunakaribia hapa hospitali, vipi hali yake,” mzee Linus alijibu, kauli ambayo ilimshangaza sana Baptist, hakutegemea kama mzee wake alishataarifiwa. Ukweli ni kwamba mama yake, alimpigia simu na kumweleza kilichotokea mara tu walipoondoka nyumbani kuelekea hospitali.
Naye mzee Linus aliwasiliana na rafiki yake. Bahati nzuri, mzee Komba alikuwa Bahari Beach Hotel alikokuwa na kikao cha kikazi na washirika wake kibiashara, wakati mzee Linus alikuwa akirejea kutoka shambani kwake Mapinga, alikuwa akikaribia Bunju, njia ya kuelekea Bagamoyo!
Wakakubaliana kukutana hospitali.
***
Mama Tonny alivuta kumbukumbu zake vizuri akiwa amejiinamia chini. Kwa mbali akakumbuka kuhusu kilichotokea. Kishindo cha kugongwa na gari mtoto wake kikajirudia tena akilini mwake, akapiga ukulele..
“Mamaaaaaa!”
Watu wote waliokuwa sebuleni hapo wakashtuka, mama yake Juddy akawahi kumshika mkono na kumtuliza.
“Vipi mwenzangu?” aliuliza
“Santoo, Santooo, mwanangu Santooo jamani,” mama Tonny alianza kuangua kilio, Mama Juddy akamshika vizuri na kumtuliza, akazidi kupiga kelele na kuuliza alipo mwanae.
“Amepelekwa hospitali.”
“Wamempeleka yeye au maiti yake?” aliuliza huku akiuma meno kwa uchungu, hakuamini kama mwanae alikuwa mzima.
“Mzima kabisa dada, wala usiogope,” mama Juddy alijitahidi kumfariji.
“Nataka kwenda, nataka kwenda, sasa hivi,” alisema na kuinuka, wanawake wenzake walijaribu kumzuia, lakini akawashinda nguvu, asijue hospitali waliyokwenda, akatoka nje ya geti na kuanza kutimua mbio akiwa pekupeku bila viatu.
Bahati nzuri kulikuwa na vijana wa kiume mtaani hapo ambao bado walikuwa katika vikundi wakijadili tukio hilo, wakaambiwa wamkamate asije kupata madhara zaidi.
Zoezi lile halikuwa kubwa, vijana kadhaa wenye ubavu walimkimbiza mama kidogo, na kumkamata na kumsihi atulie, kwani tayari akina baba walikuwa wameshafika hospitalini, na taarifa zilizoletwa muda huo zilisema Santo alikuwa bado chumba cha upasuaji.
Kwa unyonge mama akakubali kurudi nyumbani, lakini akiwa anatoa kilio kikubwa. Vijana wale walimuongoza nyumbani wakijaribu kumpa matumaini.
***
Baptist aliwafuata mzee Komba na baba yake waliokuwa wamekaa kwenye benchi wakizungumza kwa huzuni.
“Inabidi niende polisi kutoa taarifa za ajali,” aliwaambia huku naye akionekana kuwa mwenye huzuni kubwa.
“Sawa, nenda kituo cha Wazo, halafu kitakachotokea utatuambia,” alisema mzee Linus.
Baptist akaendesha gari kwa kasi kama kawaida yake hadi Kituo Kidogo cha Polisi Wazo. Alijua haitakuwa rahisi kutoka wakati ule, akatafuta sehemu nzuri na kuegesha, akasogea kaunta ya polisi na kueleza tatizo lake kwa askari aliyekuwa zamu.
“Zunguka, vua viatu, saa, mkanda, afande, mfungulie mlango huyu, kaua,” askari aliyekuwepo kaunta alisema kwa sauti kubwa, hali iliyosababisha watu wote waliokuwa jirani kumtazama Baptist aliyekuwa sasa anazunguka kuingia kaunta.
“Kwani imekuaje?” alisema askari mwingine aliyekuwa ndani, ambaye alionekana kama ndiye mkubwa, kuliko yule aliyekaa kaunta. Akataka kijana yule aingie ofisini kwake.
Baptist akaingia, akakisogelea kiti kilichokuwa kinatazamana na kile cha ofisa wa polisi, akakaa. Ofisa huyo akataka kupata maelezo ya nini hasa kimetokea.
Baptist akamuelezea kuanzia mwanzo hadi mwisho. Askari akatingisha kichwa. Akachukua mkono wa simu ya mezani, akabonyeza namba kadhaa kisha akauweka sikioni.
itaendelea
 
SEHEMU YA 08


Baptist akamuelezea kuanzia mwanzo hadi mwisho. Askari akatingisha kichwa. Akachukua mkono wa simu ya mezani, akabonyeza namba kadhaa kisha akauweka sikioni.
Sasa endelea...
“ Hebu askari watatu waje ofisini mara moja, wanatakiwa kwenda kupima ajali Nakasangwe na halafu kuangalia maendeleo ya majeruhi hospitalini haraka..,” ofisa yule wa polisi aliongea kwenye simu na kisha kurudisha mkonga sehemu yake.
Dakika moja baadaye, askari watatu, akiwemo mwanamke mmoja walikuwa ofisini hapo, wakapewa maelekezo, kisha wakainuka pamoja na Baptist na kuelekea kwenye gari la Polisi aina ya Toyota Land Cruiser, maarufu kama Difenda. Wakakanyaga moto hadi eneo la tukio. Wakachukua vipimo pamoja na kupata vidokezo kutoka kwa majirani ambao sasa walikuwa wengi wamejikusanya ilipotokea ajali na nyumbani kwao mzee Komba, wengi wakiulizia maendeleo ya majeruhi.
Baada ya kumaliza shughuli hiyo, wakawasha gari wakiwa na Baptist na kuondoka kuelekea hospitali alikolazwa majeruhi. Wakaomba kukutana na daktari aliyempokea mgonjwa na kutaka kujua hali yake.
“Ana hali mbaya sana afande, sidhani kama atapona,” daktari aliyempokea na kumshughulikia Santo aliwaambia askari wale alipowakaribisha ofisini kwake na wao kujitambulisha.
“Ameumia kwa kiasi gani,?” askari kiongozi wa msafara aliuliza. Kabla daktari huyo hajajibu chochote, simu yake ya mezani ikaita. Akatoa ishara ya kumtaka radhi, akainua mkonga wa kuongelea na kuuweka sikioni, alisikiliza kwa sekunde chache kabla ya kuurudisha mahali pale.
“He is dead (amefariki),” alisema huku akitoa miwani yake na kuifuta kwa kitambaa chake cheupe!
***
Vilio viliripuka nyumbani kwa mzee Komba mara tu taarifa za kifo hicho zilipopelekwa. Alikuwa ni mzee huyo aliyempigia simu mtoto wake mkubwa wa kiume, akimfahamisha tukio hilo la kusikitisha. Mama yake Tonny alipoteza fahamu mara tu alipofuatwa na mtoto wake na kumweleza kuwa kule hospitalini, Santo amefariki dunia!
Taarifa za kifo hicho zilisambaa kwa kasi kubwa, ndugu mbalimbali wa ndani na nje ya nchi waliarifiwa na zilipomfikia Asfat, ambaye sasa alikuwa ameshamaliza masomo na akijiandaa kwa safari ya kurejea nyumbani Tanzania, hakuamini.
“What?” aliuliza wakati alipopokea simu ya kaka yake, Amani, aliyemtaarifu juu ya msiba huo.
“Ndiyo hivyo sista, bahati mbaya,” Amani alisema kwa upole.
Asfat hakutaka kuamini kirahisi kama kifo kile kilikuwa bahati mbaya, akilini mwake aliona huenda kilikuwa ni kisasi, hivyo akataka maelezo ya kutosha kutoka kwa kaka yake.
“Kaka Amani, slowly please (taratibu tafadhali), hebu niambie vizuri, una uhakika kaka Baptist kamgonga Santo kwa bahati mbaya? Sitaki kuamini, naona kama kisasi fulani hivi, wewe unaonaje?” Asfat aliongea huku akiwa ameuma meno.
“Hapana dada Asfat, ni ajali. Santo alikuwa na mama uani, wanataniana, si unawajua walivyo, sijui ilikuwaje wakaanza kufukuzana, Santo akakimbilia nje, sasa ile anatokeza tu mlangoni na Baptist anapita, si unajua anavyoendeshaga, hakujua, hakumuona, hakuna hata mtu mmoja anayemlaumu Bap, ni ajali dada, amini ninachokuambia, ambacho najua hata mama atakuambia hicho hicho,” Amani alijaribu kumtuliza dada yake.
Asfat akakubali, lakini hakuridhika!!!!…
...Baptist akaondoka na askari wale kurejea kituoni Wazo, ambako aliwekwa mahabusu na baadaye kufunguliwa jalada la ajali iliyosababisha kifo.
Pale hospitalini, mzee Komba na mzee Linus wakaanza taratibu za kuutoa mwili ili uende kuhifadhiwa hospitali yenye majokofu ya kuhifadhia maiti. Majirani wengine kadhaa nao walikuwa wameshawasili hospitalini hapo kwa msaada wowote unaoweza kuhitajika.
Mzee Komba akashauriwa kurejea nyumbani ili aweze kupumzisha akili sambamba na kupokea wageni, kazi ile ya kushughulika na mwili wa marehemu ikaachwa mikononi mwa mzee Linus, akishirikiana na vijana wa familia zote mbili
 
SEHEMU YA 09


Mzee Komba akashauriwa kurejea nyumbani ili aweze kupumzisha akili sambamba na kupokea wageni, kazi ile ya kushughulika na mwili wa marehemu ikaachwa mikononi mwa mzee Linus, akishirikiana na vijana wa familia zote mbili. ENDELEA...
Nyumbani kwa mzee Komba, watu walishaanza kujaa, kila mmoja akizungumza kwa jinsi alivyoona kuhusiana na ajali ile. Mama yake Juddy, alikuwa muda wote akimtuliza shoga yake, dada yake na jirani yake wa miaka mingi, mama Tonny.
Uani, walikuwepo majirani wawili, mama Rama na mama Sabina, wamekaa chini ya muarobaini kujikinga na jua wakizungumza.
“Mimi nina wasiwasi,” Mama Rama alianza
“Wa nini na wewe shosti, umeanza,” alijibu Mama Sabina.
“Hii ajali, hivi unafikiri ni bahati mbaya kweli?”
“Jamani hebu acha uchuro, sasa wewe unadhani ni makusudi?”
“Kabisa, akili yangu hainipi kabisa, unakumbuka kifo cha Juddy?”
“Jamani, kwani vipi mama Rama?”
“Naona kama Bap kafanya makusudi, hivi unaendeshaje mwendo mkali vile wakati umeshafika nyumbani?”
“Usiseme hivyo, kwani wewe ni mgeni na Bap, si kila siku ndiyo mwendo wake jamani?”
“Hata kama, naona kama alikuwa anatafuta nafasi alipize kisasi kwa kifo cha dada yake, hivi unadhani walifurahi kwa jinsi Tonny alivyofanya?”
“Mmh, mi sidhani bwana, naona ni ajali tu, mbona Salum naye anaendeshaga mwendo mkali, ingekuwa yeye ndiyo kamgonga ungesemaje,” Mama Sabina alimwambia shoga yake, akimzungumzia jirani yao mwingine, Salum ambaye pia anasifika kwa kuendesha gari kwa mwendo kasi, hata akiwa hatua mbili kutoka nyumbani kwake…
***
Mzee Komba na vijana wake walifanikiwa kuufikisha mwili wa Santo katika hospitali ya serikali ya Mwananyamala, baada ya kumaliza taratibu zote wakarejea nyumbani kujiunga na waombolezaji wengine. Watu sasa walishakuwa wengi.
Kila mmoja alizungumza lake, lakini wengi wakilaumu tabia ya uendeshaji wa mwendokasi wa Bap, wakisema kama isingekuwa vile, angeweza kunusuru maisha ya Santo. Hata hivyo, hali ilikuwa tofauti sana kwa mama yake marehemu, mama Tonny.
Akiwa amejikunyata chini alipolala kwenye mkeka akifarijiwa na mama Juddy, picha ya tukio lile ilijirudia. Alimuona mtoto wake akimtekenya, akajiona mwenyewe akiinuka kwa hasira na kuanza kumfukuza mwanaye.
“Mwanangu nimemuua mwenyewe dada,” alijikuta akimwambia mama Juddy, aliyekuwa na majirani wengine wawili sebuleni kwake, ambao nao walishtushwa na kauli ile.
“Kivipi shoga,” Mama Juddy alimuuliza mwenzake kwa namna ya kushangaa kidogo, maana alijua ni mtoto wake ndiye alimuua Santo kwa kumgonga na gari.
“Bila mimi asingeweza kugongwa na gari. Tulikuwa tunataniana na mwanangu hapa ndani, nisingeinuka na kuanza kumfukuza wala haya yasingetokea. Hivi ni gari ya nani imemgonga?” alisema na kumalizia na swali!
Mama Juddy alisita kidogo kujibu swali hilo, akawatazama majirani zake kuwaashiria wamjibu. Wote walionekana kusita kujibu hali iliyomfanya mama Tonny kurudia kuuliza.
“Ni nani aliyemgonga Santo?”
“Kagongwa na kaka yake, Bap!” mama Juddy hatimaye alisema, huku akimshika mkono mfiwa katika namna ya kumtuliza.
“Nani? Bap? No!” Mama Tonny alijikuta akisema kwa sauti iliyowashtua wote waliokuwepo sebuleni.
Ghafla akainuka, akakaa katika mkeka, akamtazama shoga yake mama Juddy, akamuegemea na kujikuta akiangua kilio kwa sauti huku akizungumza maneno yasiyoeleweka!
***
Nje, chini ya mti, watu kadhaa walikuwa wamekaa wakizungumza taratibu. Kila mmoja alikuwa na majonzi, wakiomboleza msiba wa ghafla wa Santo, kijana mdogo aliyekuwa na umri wa miaka tisa tu!
Mzee Linus alikuwa amejiinamia, kichwani mwake akiwaza mambo mengi, kifo kile cha kijana wake kilimuumiza sana, lakini alimshukuru Mungu kwa kila jambo. Kama aliyekumbuka kitu, akamshika mkono mzee Komba na kumnong’oneza jambo!
Je, nini kitatokea? Usikose kusoma sehemu inayofuata katika toleo lijalo.
 
SEHEMU YA 10

Mzee Linus alikuwa amejiinamia, kichwani mwake akiwaza mambo mengi, kifo kile cha kijana wake kilimuumiza sana, lakini alimshukuru Mungu kwa kila jambo. Kama aliyekumbuka kitu, akamshika mkono mzee Komba na kumnong’oneza jambo!
SASA ENDELEA…
“Kaka!”
“Niambie,” Mzee Komba alimuitikia rafiki yake, kichwa chake kikiwa na mawazo mengi.
“Hivi nini kitatokea kwa Bap?” aliuliza tena
“Kivipi?” naye akajikuta akiuliza.
“Hii kwake itakuwa ni kesi ya mauaji au kitu gani,?”
“Sidhani, ni traffic case,” alisema mzee Komba.
“Ila itabidi lazima tumwambie Bap, tabia yake ya kuendesha gari kwa kasi si nzuri, atamgonga mtu sehemu wasiyomfahamu, wanaweza kumfanyia kitu kibaya sana,” alisema mzee Linus.
“Kila siku ninamkataza, lakini hasikii. Kuna wakati niliamua hata kumzuia kuendesha gari, lakini nikashindwa, hebu tumuache, tuamini kwamba atabadilika mwenyewe, hasa baada ya tukio hili.”
“Lakini hatujafuatilia Polisi, nini kimemtokea?”
“Amewekwa mahabusu, katika jambo kama hili, hatuna sababu ya kuhangaika hivi sasa, hebu hili tulijadili kesho, mwache alale leo,”
Watu wakaendelea kujaa pale nyumbani kwa mzee Komba, msiba ulikuwa wa ghafla sana. Mama yake Tonny baada ya kuambiwa aliyemgonga na kumuua mwanawe ni Bap, akili yake ikachanganyikiwa. Mambo mengi yalipita kichwani mwake, akajikuta akihusisha tukio hilo na kile kilichotokea mwaka mmoja na nusu uliopita!
“Atakuwa amefanya makusudi?” alijiuliza, lakini sauti asiyoifahamu, ikamtaarifu kuwa ni bahati mbaya, naye kwa moyo mkunjufu kabisa, akainua mikono yake juu akimshukuru Mungu na kumuombea Baptist!
Baada ya kuwasiliana na ndugu zake wa karibu ambao walikuja msibani pale siku ile ile, mzee Komba akawatangazia majirani na waombolezaji wengine kuwa mazishi ya mtoto wake yatafanyika siku tatu baadaye, wakisubiri watu wengine waliokuwa nje ya Dar es Salaam wafike. Hakutaka kwenda kumzika mtoto wake nyumbani kwao Mbinga, alitaka azikwe Dar kwa kuwa ndipo yalipo maisha yake!
Asfat aliwasili Dar es Salaam saa tano na nusu asubuhi, akakodi teksi iliyomtoa uwanja wa ndege wa Julius Nyerere na kumfikisha Nakasagwe saa saba mchana. Alipokelewa kwa vilio kutoka kwa ndugu, jamaa na marafiki. Baada ya kuingiza begi lake chumbani kwake, akaingia bafuni na alipomaliza kuoga, akamfuata mama yake na kumuomba waongee kidogo.
Wakatoka nje kabisa ya nyumba, ambako watu walikuwa wametapakaa. Wakatafuta eneo la peke yao, wakakaa chini ya matofali na kuanza kuzungumza. Asfat akamtaka mama yake amueleze ukweli juu ya tukio lile, kwa sababu alimwambia wazi kuwa yeye binafsi, haamini kama ile ilikuwa ni ajali kama ajali zingine.
Mama akamtazama, macho yake yakaanza kujaa machozi, akajifuta kwa khanga aliyokuwa amejifunga na baadaye akamwambia;
“Hata mimi mwanzo nilikuwa na mawazo kama yako, sikuamini mara moja, lakini kadiri nikirejea tukio zima, sioni ni wapi Bap alikusudia. Kama kuna mtu wa kumlaumu, nilaumuni mimi, nisingemfukuza, asingetoka nje.”
Kwa mara nyingine, Asfat akakubali, lakini hakuridhika!
Baada ya kumaliza mazungumzo hayo, akarejea chumbani kwake, akaikumbuka albamu yake ya picha, akaichukua na kuanza kuziangalia picha zake, zikiwemo za zamani enzi za utoto hadi ukubwani.
Akakutana na picha aliyoipenda sana, alikuwa amepiga na marehemu Juddy, wakati flani wa sikukuu ya Krismas, miaka kadhaa iliyopita, aliipenda picha hiyo kwa vile ilimkumbusha mambo ya siku hiyo, ambayo hawezi kusahau.
 
Back
Top Bottom