- Thread starter
- #21
5 iliyopita
Mzee Komba na familia
yake walishiriki kila hatua
ya tukio lile na mzee Linus
na familia yake nao
hawakuonyesha kinyongo
chochote, wote waliamini
kilichotokea ilikuwa ni
mipango ya Mungu.
SASA ENDELEA...
Juddy alizikwa siku nne
baada ya kufariki katika
tukio lililokusanya umati
mkubwa wa watu, kwenye
makaburi ya Nakasangwe!
Watoto wa familia zote
mbili walishiriki kikamilifu
shughuli ile ya msiba na
walikaa nyumbani kwa mzee
Linus kwa siku zote, hadi ya
saba, wakati walipokaa kikao
cha pamoja kujadili
kilichotokea na mzee Komba
ndiye alikuwa mwenyekiti wa
kikao kile.
Rafiki, kaka yangu, shemeji
yangu na wanangu wote wa
nyumba hii, kwa niaba ya
familia yangu, tunaomba
kuwaomba radhi kwa yote
yaliyotokea, lakini tunaamini
ni kazi ya Mungu ambayo
siku zote haina makosa,
Mzee Komba alisema huku
akijifuta machozi, kitendo
ambacho pia kilifanywa na
watu wote, hasa Asfat,
aliyesafiri kutoka Ulaya kuja
kuhudhuria mazishi ya rafiki
yake mkubwa!
Usijali kaka, rafiki, jirani na
wanangu wote. Kama
ulivyosema, hili ni tukio
ambalo hakuna
aliyelitegemea, huu msiba
ni wetu wote kama ambavyo
tumeshuhudia, wote
mmeshiriki kikamilifu tokea
mwanzo hadi sasa. Nyinyi ni
sisi na sisi ni nyinyi, haya
yamepita, sasa tujitahidi
kumnusuru Tonny, ni kijana
mdogo aliyetaka
kuwachekesha wenzake
lakini matatizo yakatokea,
Mzee Linus naye alisema,
huku watu wote wakiendelea
kujifuta machozi!
Walijadili mambo mengi
sana kama familia marafiki
na hatimaye baadaye
wakakubaliana kuondoa aina
yoyote ya chuki baina yao.
Wakasimama na kushikana
mikono. Wakati wa tendo
hili, wote waliendelea
kutokwa na machozi.
Tonny alikaa polisi kwa siku
tatu, baadaye akapelekwa
katika mahakama ya watoto
Kisutu jijini Dar es Salaam
ambako alisomewa shtaka la
mauaji ya bila kukusudia. Na
baada ya kusomewa
mashtaka yake ambapo
hakutakiwa kujibu chochote
kwa kuwa mahakama ile
haikuwa na uwezo wa
kusikiliza kesi hiyo,
akapelekwa Segerea.
Wazazi walimtafuta
mwanasheria aliyekuwa
akitamba sana jijini Dar es
Salaam, Bennedict ili aweze
kumsimamia Tonny. Kazi
hiyo hata hivyo haikuwa
ngumu sana kutokana na
wazazi wa marehemu nao
kupigana kwa nguvu zote
kuhakikisha kijana huyo
anaachiwa!
Tonny aliachiliwa huru
baada ya miezi mitatu tu na
alipotoka mahakamani,
alikwenda moja kwa moja
nyumbani kwa akina Juddy
akiwa analia!
Kilio chake kiliashiria majuto
aliyokuwa nayo. Hata hivyo,
wote walionyesha moyo wa
huruma dhidi yake na
akaomba apelekwe kaburini
kwa Juddy ili akaweke shada
la maua.
Ombi hilo likakubaliwa na
familia zote zikapanga
kitendo hicho kifanyike
kesho yake ambayo ilikuwa
ni Jumapili ili wengine pia
wahudhurie.
Makaburini, Tonny alipiga
magoti katikati ya kaburi la
Juddy, akachukua mshumaa
na kuuwasha, akalibusu
shada lake la maua na
kuliweka, kisha machozi
yakaanza kumtoka.
Wanafamilia wengine
waliomsindikiza nao
waliweka mashada yao na
kupiga magoti. Mwishowe
wote kwa pamoja walisali na
kuondoka!
Asfat akarejea zake shuleni
Ulaya na ndugu wa familia
zingine wakaendelea na
maisha yao ya kila siku.
Hakukuwa na tofauti yoyote
kati ya familia hizi kwa
kipindi kirefu.
Mwaka mmoja na miezi sita
baada ya kifo cha Juddy,
maisha yalikuwa katika
mtindo wake wa kawaida
kabisa kwa familia hizi
rafiki.
Baptist, ambaye alimuachia
ziwa Juddy, alikuwa akitoka
mjini kutengeneza gari lao
lililokuwa limeharibika
mfumo wake wa umeme
eneo moja la Gerezani, jijini
Dar es Salaam. Wakati
akirejea nyumbani alikuwa
na mawazo mengi.
Katika umri wake wa miaka
25, alikuwa mtu wa
kujirusha sana katika
maeneo ya starehe. Ilikuwa
ni lazima aende klabu kila
mwisho wa wiki na hii
ilimfanya kuwa na marafiki
wengi wa kike na kiume.
Lakini sifa yake kubwa
ilikuwa ni tabia yake ya
kuendesha gari kwa mwendo
kasi. Hata kama alikuwa
akienda sehemu ya karibu,
alipenda kulikimbiza...
Je, kitu gani kilitokea?
Usikose kufuatilia simulizi
hii ya kusisimua katika
toleo lijalo.
Mzee Komba na familia
yake walishiriki kila hatua
ya tukio lile na mzee Linus
na familia yake nao
hawakuonyesha kinyongo
chochote, wote waliamini
kilichotokea ilikuwa ni
mipango ya Mungu.
SASA ENDELEA...
Juddy alizikwa siku nne
baada ya kufariki katika
tukio lililokusanya umati
mkubwa wa watu, kwenye
makaburi ya Nakasangwe!
Watoto wa familia zote
mbili walishiriki kikamilifu
shughuli ile ya msiba na
walikaa nyumbani kwa mzee
Linus kwa siku zote, hadi ya
saba, wakati walipokaa kikao
cha pamoja kujadili
kilichotokea na mzee Komba
ndiye alikuwa mwenyekiti wa
kikao kile.
Rafiki, kaka yangu, shemeji
yangu na wanangu wote wa
nyumba hii, kwa niaba ya
familia yangu, tunaomba
kuwaomba radhi kwa yote
yaliyotokea, lakini tunaamini
ni kazi ya Mungu ambayo
siku zote haina makosa,
Mzee Komba alisema huku
akijifuta machozi, kitendo
ambacho pia kilifanywa na
watu wote, hasa Asfat,
aliyesafiri kutoka Ulaya kuja
kuhudhuria mazishi ya rafiki
yake mkubwa!
Usijali kaka, rafiki, jirani na
wanangu wote. Kama
ulivyosema, hili ni tukio
ambalo hakuna
aliyelitegemea, huu msiba
ni wetu wote kama ambavyo
tumeshuhudia, wote
mmeshiriki kikamilifu tokea
mwanzo hadi sasa. Nyinyi ni
sisi na sisi ni nyinyi, haya
yamepita, sasa tujitahidi
kumnusuru Tonny, ni kijana
mdogo aliyetaka
kuwachekesha wenzake
lakini matatizo yakatokea,
Mzee Linus naye alisema,
huku watu wote wakiendelea
kujifuta machozi!
Walijadili mambo mengi
sana kama familia marafiki
na hatimaye baadaye
wakakubaliana kuondoa aina
yoyote ya chuki baina yao.
Wakasimama na kushikana
mikono. Wakati wa tendo
hili, wote waliendelea
kutokwa na machozi.
Tonny alikaa polisi kwa siku
tatu, baadaye akapelekwa
katika mahakama ya watoto
Kisutu jijini Dar es Salaam
ambako alisomewa shtaka la
mauaji ya bila kukusudia. Na
baada ya kusomewa
mashtaka yake ambapo
hakutakiwa kujibu chochote
kwa kuwa mahakama ile
haikuwa na uwezo wa
kusikiliza kesi hiyo,
akapelekwa Segerea.
Wazazi walimtafuta
mwanasheria aliyekuwa
akitamba sana jijini Dar es
Salaam, Bennedict ili aweze
kumsimamia Tonny. Kazi
hiyo hata hivyo haikuwa
ngumu sana kutokana na
wazazi wa marehemu nao
kupigana kwa nguvu zote
kuhakikisha kijana huyo
anaachiwa!
Tonny aliachiliwa huru
baada ya miezi mitatu tu na
alipotoka mahakamani,
alikwenda moja kwa moja
nyumbani kwa akina Juddy
akiwa analia!
Kilio chake kiliashiria majuto
aliyokuwa nayo. Hata hivyo,
wote walionyesha moyo wa
huruma dhidi yake na
akaomba apelekwe kaburini
kwa Juddy ili akaweke shada
la maua.
Ombi hilo likakubaliwa na
familia zote zikapanga
kitendo hicho kifanyike
kesho yake ambayo ilikuwa
ni Jumapili ili wengine pia
wahudhurie.
Makaburini, Tonny alipiga
magoti katikati ya kaburi la
Juddy, akachukua mshumaa
na kuuwasha, akalibusu
shada lake la maua na
kuliweka, kisha machozi
yakaanza kumtoka.
Wanafamilia wengine
waliomsindikiza nao
waliweka mashada yao na
kupiga magoti. Mwishowe
wote kwa pamoja walisali na
kuondoka!
Asfat akarejea zake shuleni
Ulaya na ndugu wa familia
zingine wakaendelea na
maisha yao ya kila siku.
Hakukuwa na tofauti yoyote
kati ya familia hizi kwa
kipindi kirefu.
Mwaka mmoja na miezi sita
baada ya kifo cha Juddy,
maisha yalikuwa katika
mtindo wake wa kawaida
kabisa kwa familia hizi
rafiki.
Baptist, ambaye alimuachia
ziwa Juddy, alikuwa akitoka
mjini kutengeneza gari lao
lililokuwa limeharibika
mfumo wake wa umeme
eneo moja la Gerezani, jijini
Dar es Salaam. Wakati
akirejea nyumbani alikuwa
na mawazo mengi.
Katika umri wake wa miaka
25, alikuwa mtu wa
kujirusha sana katika
maeneo ya starehe. Ilikuwa
ni lazima aende klabu kila
mwisho wa wiki na hii
ilimfanya kuwa na marafiki
wengi wa kike na kiume.
Lakini sifa yake kubwa
ilikuwa ni tabia yake ya
kuendesha gari kwa mwendo
kasi. Hata kama alikuwa
akienda sehemu ya karibu,
alipenda kulikimbiza...
Je, kitu gani kilitokea?
Usikose kufuatilia simulizi
hii ya kusisimua katika
toleo lijalo.