May Day
JF-Expert Member
- May 18, 2018
- 6,311
- 9,027
Mimi ninavyodhani kumpendekeza JPM wakati ule ilikuwa zaidi kutafuta imani ya Wananchi kwa Chama, maana ilishapungua sana wakaona walau huyo Jamaa atarudisha hali kwenye mstari.
Na huenda ilikuwa ni maamuzi ya Mtu au Watu wachache sana na ni baada ya kushauriana sana, bila shaka wapo walioiona hatari ya Jamaa kuwageuka.
Ambacho hawakutarajia Wakubwa hao ni kwamba Jamaa kweli atatoka kwenye mstari....ndio maana kukazuka lile jina "Mshamba". hopefully na kila walipokutana walimtambulisha kama "ona sasa huyu Mshamba.....".
Kuhusu Wafanyabiashara wao kupata matumbo joto kwa JPM kuingia kwenye usukani sidhani, maana utaogopaje kitu kabla ya kukijua? labda useme wasiwasi tu wa kuona huyu kweli ataendelea kutulinda ama?.
Ingekuwa inatokea kwa situation kama ile ya Marehemu Mzee Mrema wakati ule angepata kushika hatamu na kuipiga chini CCM hapo sasa lazima na wa kukimbia nchi wangekimbia...lakini hii ya kukabidhiana kwa amani wengi hutarajia mambo yataenda kama kawa, maana wanaona Kanzu ndio mpya ila Sheikh ni yule yule.
Mimi nadhani kilichowatokea ilikuwa ni suprise kwa kila mmoja ingawa walihisi ingeweza kutokea, kuanzia kwa waliompa kijiti, Wafanya Biashara n.k.
Na huenda ilikuwa ni maamuzi ya Mtu au Watu wachache sana na ni baada ya kushauriana sana, bila shaka wapo walioiona hatari ya Jamaa kuwageuka.
Ambacho hawakutarajia Wakubwa hao ni kwamba Jamaa kweli atatoka kwenye mstari....ndio maana kukazuka lile jina "Mshamba". hopefully na kila walipokutana walimtambulisha kama "ona sasa huyu Mshamba.....".
Kuhusu Wafanyabiashara wao kupata matumbo joto kwa JPM kuingia kwenye usukani sidhani, maana utaogopaje kitu kabla ya kukijua? labda useme wasiwasi tu wa kuona huyu kweli ataendelea kutulinda ama?.
Ingekuwa inatokea kwa situation kama ile ya Marehemu Mzee Mrema wakati ule angepata kushika hatamu na kuipiga chini CCM hapo sasa lazima na wa kukimbia nchi wangekimbia...lakini hii ya kukabidhiana kwa amani wengi hutarajia mambo yataenda kama kawa, maana wanaona Kanzu ndio mpya ila Sheikh ni yule yule.
Mimi nadhani kilichowatokea ilikuwa ni suprise kwa kila mmoja ingawa walihisi ingeweza kutokea, kuanzia kwa waliompa kijiti, Wafanya Biashara n.k.