Familia ya GSM ilivyotembea kwa magoti korido za Ikulu kuomba Hayati Magufuli asiwafunge

Familia ya GSM ilivyotembea kwa magoti korido za Ikulu kuomba Hayati Magufuli asiwafunge

Huwezi kuwamakiza viroboto kwa siku moja,wako wengi sana bandani
Ukifukazana na mmoja mmoja hawataisha. Alichotakiwa kufanya ni kuufumua mfumo wa uongozi wa nchi na 2020 tuwe tumeanza na mfumo mpya. Viroboto wangekufa kifo kwa kukosa mazalio.
 
Ukifukazana na mmoja mmoja hawataisha. Alichotakiwa kufanya ni kuufumua mfumo wa uongozi wa nchi na 2020 tuwe tumeanza na mfumo mpya. Viroboto wangekufa kifo kwa kukosa mazalio.
Sio rahisi kihivyo maana ni process ya miaka mingi,kabla hujatimiza azma wanakuwahi wewe labda uwe mafia kwelikweli kama Kagame au Putin
 
Sio rahisi kihivyo maana ni process ya miaka mingi,kabla hujatimiza azma wanakuwahi wewe labda uwe mafia kwelikweli kama Kagame au Putin
Kabisa. Ni process ndefu ndiyo maana nimesema alitakiwa aanze mapema kwa kuufumua mfumo. Rais huwezi kufanya haya kwa awamu moja ila ukifanya vizuri wakati wa awamu yako unakuwa umeweka msingi imara kwa awamu inayofuata.
 
Sasa wamerudi upyaaaaaa!
Na Yanga juu, ukiona raisi au kiongozi mkuu ana urafiki mkubwa na wafanyabiashara jua huku nyuma kuna kitu, namkubuka baba wa taifa alisema Ikulu isigeuzwe pango la Wafanyabiashara enzi za mzee rukhsa wafanyabiashara hasa hawa wasio wamatumbi walikuwa wanaenda kumsalimia mzee na vifuko vya sandarusi, duniani kote wafanyabiashara wakubwa na wadogo, magenge ya maharamia wanataka kuwa karibu na viongozi wakuu ili wafanye mambo wanvyotaka, si tunawakumbuka akina Zuma, ndio shida ya hizi banana republic ,waacha niishie hapa nisijesekwa ndani kwa kudai naichonganisha serikali na wananchi, wakubwa hawataki na hawapendi kuambiwa ukweli wa madudu wanayoyafanya. Tutamkumbuka sana JPM
 
I doubt kama kuna ukweli wowote katika hili....

1. Ambao walikumbana na mkono wa JPM ama hawakuinuka tena au wali-struggle sana kuinuka!

Kinyume chake, GSM hawakutetereka kabisa... na hata kama watu mnajisahaulisha, GSM waling'ara zaidi kipindi cha JPM pengine kuliko hata wakati wa JK!

Minoti ya GSM ikaanza kuonekana wazi wazi hadharani kipindi cha JPM pale walipoanza kujihusisha moja kwa moja na Yanga!!

2. Ukimhusisha GSM na JK hapo ndo unavuruga kila kitu!!

Pamoja na mambo yake yote, JPM aliwakumbatia sana Vigogo wa CCM na Watendaji Wakuu wa Serikali.

Ni kutokana na ukweli huo, ndo maana hadi siku Mwenyezi Mungu anamchukua, JPM hakuwahi kumgusa any high profile CCM Politician and Top Govt Executive!

JPM alisimamisha miradi mingi ya ujenzi kama sio yote ya NSSF kwa madai kwamba kuna ufisadi mkubwa!

Kama kuna ufisadi mkubwa, vipi kuhusu wahusika wa huo ufisadi?! DG wa NSSF akampa Ubalozi Malaysia!!!

Hata hasimu wake mkuu Bernard Membe, aliishia tu kuongea kwa mafumbo kwamba "...kule Lindi watu wametafuna Sh 20B" lakini hakumtaja hata kwa jina!

And guess what... mwaka jana nilienda nyumbani kwao Membe! Kwa hali niliyoikuta pale, kuna kila dalili kwamba Magu aliongea ukweli kuhusu "watu kutafuna 20B kule Lindi"!

Je, alimfanya nini?!

Sasa ikiwa hata Membe hakumfanya kitu zaidi ya kumwadhibu kisiasa, ndo aguse maslahi ya JK?! Au hizi habari za JK na GSM hazina ukweli wowote?

3. Hivi mlilifuatilia vizuri Sakata la Makinikia? Wakati mambo yapo HOT, watu wakanza kumhusisha JK na mikataba ya madini wakati akiwa waziri Wizara ya Nishati na Madini!

Katika kutekeleza "mahaba" ya JPM kwa Wastaafu kwamba waachwe wapumzike, Ripoti ya 2 ya Makinikia (Ripoti ya Profesa Oroso) ikaja na hili:-
JK na Mikataba ya Madini.png


Kwa wasiofahamu, huyo Waziri anayetajwa kwenye Ripoti ya Makinikia 2 kwamba "alipambana kwa jasho na damu kuhakikisha maslahi ya taifa yanalindwa" ni Jakaya Kikwete!

Ukiisoma ripoti ile, utaona mikataba YOTE ya madini ambayo ilisainiwa tangu enzi za Mwinyi ilikuwa na kasoro EXCEPT, mikataba iliyosainiwa na JK!!

Na kule bungeni, Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Hassan Zungu akapiga marufuku mijadala ya kibunge iliyokuwa inataka wastaafu wahojiwe!

Magu alimaanisha alipokuwa anasema waacheni wazee wapumzike!

Hakutaka kabisa kuwagusa Vingunge wa CCM! Ni kutokana na ukweli ndo maana napata shaka sana kuamini haya unless kama HAKUNA UKWELI wowote kuhusu JK kuhusika na GSM!

4. JK pamoja na tuhuma zake nyingi lakini mwishowe akaona Rostam Azizi na Swahibu ake Lowassa ni liability!!

Baada ya JK kuasisi "Kujivua Gamba", RA akasusa siasa za Bongo na akapotea kabisa kwenye mainstream politics!

Hivi nchi hii kuna mtu alikuwa na tuhuma nyingi kumzidi RA?!

Je, RA alifanywa nini zaidi ya kuanza tena kujipenyeza serikalini kipindi cha JPM?! Au pia tukumbushane kwamba ni JPM ndie--

JPM.png


Narudia, JPM aliwalinda sana Vigogo wa CCM, na kama mnaamini GSM ni mkono wa kuume wa JK, basi JPM asingewagusa!

5. Watu mnadanganyana kwamba JK hakumtaka JPM bali alimtaka swahibu ake Membe!

Ukweli ni kwamba, ni janja janja ya Membe ndiyo iliwafanya watu waamini yeye ndo chaguo la JK! Membe ni mpole lakini ni mjanja sana! Kama umepata kukaa pamoja na Membe na kuongea nae utalifahamu hili!

Binafsi, nimewahi kukaa na Membe face to face, tena at a comfort zone, living room kwake! The guy is CLEVER!

Ni ujanja ujanja wake huu akafikia hadi kuaminisha watu kwamba yeye ndo Chaguo #1 la Mr. President! Watu wakafikia hadi kusema eti Membe na JK ni ndugu wa damu wakati hakuna ukweli wowote!!

Na wengi mnaaminishana ni Mkapa ndie ka-influence JPM kuwa Rais kinyume na matakwa ya sitting president!

Hapa nawakumbusha tu kwamba kutokana na mifumo mibovu, nchi hii Rais ndo kila kitu! Kama Jk angemtaka Membe basi hakuna ambae angemzuia!

Rais: Yeye ndo Mwenyekiti wa Chama Tawala! Yeye ndo Amiri Jeshi Mkuu, yeye ndo Mwenyekiti wa Baraza la Usalama, yeye ndo "Jaji Mkuu", yeye ndo "Askofu Mkuu", yeye ndo "Mufti na Kadhi" etc etc etc!

Atakacho, HAKUNA WA KUMZUIA!

Mambo nyeti yanajadiliwa kwenye National Security Council ambayo, unless Sheria ya 2010 iwe imebadilishwa, Rais Mstaafu sio Mjumbe wa NSC ingawaje anaweza kuwepo kwenye kikao kwa MWALIKO!

Sasa huyo Rais Mstaafu influence ya kuweka rais amtakaye yeye ataitoa wapi?!

Kikao pekee nyeti ambacho Rais Mstaafu ni mjumbe ni Kamati ya Maadili na Usalama ya CCM! Hiki ndicho kikao ambacho, kinadharia, ndicho kinafanya mchujo!

Nasema kinadharia kwa sababu, practically, sitting president anaenda kwenye hicho kikao akiwa tayari na watu wake.

Anaenda pale kutetea tu wale alioona wanastahili kuingia kwenye Top 5!

Wakati wa Uchaguzi Mkuu 2015 Mark Mwandosya aliwahi kulalamika kwamba "Mwenyekiti alikuwa anatembea na majina yake mfukoni"!

He's damn right!

JK alifika kwenye Kamati ya Maadili na Usalama akiwa na majina yake 5 huku EL na wenzake wakiwa wamekatwa juu kwa juu, na sio kwamba walikatwa na Kamati...

...kamati ili-rubber stamp tu maamuzi ya rais!

JK alivyo mjanja, akampeleka Membe Top 5 huku akiwa amemchinja EL! Unadhani JK ni stupid na hakufahamu kwamba hasira za Watu wa Lowassa zingekuwa ni kutompa kura Membe?!

Anyway, Rais Mstaafu pekee ambae alikuwa na ubavu wa ku-influence maamuzi ya sitting president ni Nyerere ambae alimtaka Mkapa awe Rais, na akawa!

But look... huyo huyo Nyerere baada ya kumpa urais Mkapa, baada ya hapo akashindwa kumdhibiti coz' Rais ndo kila kitu!

Siku NBC inaingizwa mnadani Nyerere alibaki kunung'unika tu lakini hakuwa na ubavu wa kumzuia Mkapa!!

So, always JPM alifahamu kama JK asingetaka, basi hata yeye huo Urais asingeupata! Na ni kutokana na hilo, ndo maana mara zote JPM alikuwa anasisitiza "waacheni wazee wapumzike"!

Hapo aliyekuwa analengwa aachwe apummzike ni JK kwa sababu ndie alikuwa anaandamwa sana!

Sema ndo vile tu, zikifika siku za mwezi mchanga, unakuta JPM huyo huyo anapiga vijembe wazee!

JPM aliendelea kuwabeba hata watu wa JK. Mchukulie Said Mtanda kwa mfano! Yule alikuwa hafahamiki kabisa kwenye system.

Lakini kwavile babake Said Mtanda alistaafia B'moyo na kuishi jirani na familia ya JK, bond kati ya JK and Mtanda Family ikaanza hapo!

Said Mtanda na Rizimoko na wenyewe wamekua pamoja!

So, kwavile Said Mtanda hakuwa na issue ya maana mjini, Membe na JK wakampeleka Mchinga kugombea ubunge in 2010 lakini 2015 akatoswa na Wananchi!

JPM hadi anaingia kaburini hakumtupa Said Mtanda! "Mtu wa JK" ambae alimpiga chini ni yule ambae alikuwa DC wa Geita enzi za JK!

Huyu alipigwa chini na Magu kwa sababu basically, hakuwa mtu wa JK bali alikuwa mtu wa Membe!!

Hivi tukumbushane kwamba hata Salma alipewa ubunge kwa heshima ya Mstaafu!!
 
Sikiliza nikuambie kitu kijana kutumia jina feki haimaanishi ukose adabu,kwataarifa yako nina elimu ya uhakika kuliko wewe ila hauwezi hata siku moja najisifu mbele za watu kwasababu katika harakati zangu za maisha nimekutana na watu wenye uelewa wa hali ya juu mno ila hawakwenda shule kama mimi, kwahiyo nikajifunza kumbe kwenda shule sio kujua kila kitu
Aliyeenda shule hachangiagi udedere kama wewe bogus! Walioenda shule maoni na michango yao inaonekana tu na hata kwa kusoma na kuchambua kwa haraka haraka utajua ni mtu wa aina gani... we bogus!
 
Chukulia ni kweli kilichondikwa, mzalendo gani anakiuka sheria na kutoa maamuzi mwenyewe tena Ikulu? Huoni alifanya makosa makubwa na sasa hivi ndiyo wamerudi upya? Angesema sheria ichukuwe mkondo wake huoni tatizo lingekuwa limeisha? Magufuli tatizo lake, miongoni mwa madhambi mengi ni kuwa alikuwa anaendesha nchi kama familia binafsi. Alikuwa anaamua nani akamatwe, nani asamehewe, nani auawe na nani afungwe. Wazalendo hawako hivyo.
Na ndo uongozi wa Dictatorship unataka hivyo... tulipofikia tunataka dictatorship mambo yaende sio usengeusenge tu
 
Chukulia ni kweli kilichondikwa, mzalendo gani anakiuka sheria na kutoa maamuzi mwenyewe tena Ikulu? Huoni alifanya makosa makubwa na sasa hivi ndiyo wamerudi upya? Angesema sheria ichukuwe mkondo wake huoni tatizo lingekuwa limeisha? Magufuli tatizo lake, miongoni mwa madhambi mengi ni kuwa alikuwa anaendesha nchi kama familia binafsi. Alikuwa anaamua nani akamatwe, nani asamehewe, nani auawe na nani afungwe. Wazalendo hawako hivyo.
Sasa mbonq singer hakufungwa na Rugemalila?,, Tatizo wabongo mna mentality za kijamaa,, kila tajiri mnamuona bepari,, huu ujinga na majungu dhidi ya watu matajiri huwezi kuuona katika nchi zilizostaarabika kama kenya😂.
Nchi zinafight kutengeza mabilionea ili watoe ajira, kwa bongo matajiri ni wahaini,, huu ni ufala
 
Tunaendelea na visa na mikasa ya hayati JPM..

Hakuna siri JPM hakuwa chaguo la wana CCM mwaka 2015, hata mwenyekiti wa chama hakumtaka awe Rais bali alizidiwa na nguvu ya asili.

Mwenyekiti alimkusudia kumrithisha kijiti rafiki yake wa kitambo Bernard Membe,lakini wana CCM walimtaka Edward Lowassa.

Baada ya jina la Magufuli kuibuka kidedea kuna watu hawakulala siku hiyo. Tena sio wapinzani, bali wafanyabiashara na mafisadi ndani ya CCM, walijua kiama chao kimefika.

Mojawapo wa wafanyabiashara hao ni familia ya Bwana Ghalib almaarufu kama GSM.

Tukirudi nyuma kidogo hii familia ina asili ya mkoa wa Tanga na mzee wao marehemu Said Mohamed ambaye alifariki mapema mwaka huu alihamia huko Kusini mwa Tanzania na kujikita na kilimo na biashara ya korosho, alipozeeka akawaachia biashara vijana wake waziendeleze.

Pia hii familia imekuwa na ukaribu na familia ya mstaafu JK kwa miaka mingi.
Tufahamu kuwa JK aliwapenda sana watu wa mkoa wa Tanga kuliko watu wa mkoa wowote uli, labda ni kwa sababu alisoma Tanga School au kwa sababu wilaya anayotokea iko jirani na mkoa wa Tanga sielewi.

Nikikupa hapa orodha ya watu wa mkoa wa Tanga ambao walibebwa na JK kipindi cha utawala wake utashangaa,wengine hakuna aliyekuwa akiwafahamu wakalama post kubwa za ukuu wa mkoa,wilaya hata uwaziri ,achilia mbali post zingine za juu.

Kipindi hiki cha JK ndipo familia hii ya GSM nayo ikaibuka kama uyoga, kupitia kampuni zao za HSC na Silent Ocean wakaigeuza Kariakoo kuwa Dubai ya Afrika au China ya Afrika, wafanyabiashara toka nchi jirani wakawa hawaendi tena China kufuata mzigo mambo yote yaliiishia kariakoo.

Umafia wa kiwango cha juu uliofanyika bandarini na TRA na kampuni hizi ulivutia wateja wengi, mzigo ulikombolewa bandarini fasta na kwa gharama ndogo.

Kumbe nyuma yake kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa taratibu za bandari na kodi za TRA, mabilioni ya shilingi yalihujumiwa na hii familia.

Baada ya hii jina la JPM kupenya sasa ikawa patashika nguo kuchanika wakawata na kuwazua wakaamua kuiua kampuno ya HSC wakijua tu ikibaki hewani JPM atowaacha salama.

Kupitia kampuni ya Law Domain Adocate tarehe 19 oct 2015 siku chache kabla ya uchaguzi mkuu,wakafile A notice of resolution to wind up voluntarily. Hii kwa wasiojua sheria, wind up ni kusimamisha shughuli za kampuni kisheria.

Walisahau kitu kimoja ila wakaja kukikumbuka baadae kuwa jinai huwa haifi, pamoja na kuwind up HSC kisheria bado wangekamatwa na kujibu tuhuma hata kama kampuni haipo.

Ile Silent Ocean ilibaki kuoparate kwa sababu inasemekana haikusajiliwa Tanzania japo iliwakenga wafanyabiashara wa Tanzania.

Sasa basi baada ya JPM kuingia madarakani, naweza kusema mwezi mzima alikuwa akishinda kama sio bandarini basi ni TRA, mabosi wa taasisi hizo mbili vitambi viliporomoka.

Vijana wake wakamletea ripoti ya wakwepa kodi maarufu,jina la HSC na Silent Ocean likiwa kidedea pale juu.

Matumbo moto wakajua hapa Segerea inawahusu, kama Manji alilala Segerea who is GSM?

Kwa kutumia ushawishi wa vijana wa mstaafu wakaomba apointment mara kadhaa kuonana na JPM.

Appointment ikawa approved wakaitwa Ikulu, kwa makosa yao walitembea kwa magoti kwenye korido mpaka ofisini kwa JPM. Akiwa na sura iliyokasirika akawaambia sitaki maelezo lipeni hizo arreas au Segerea inawasubiri

Yakalipwa mabilioni kimyakimya GSM dhambi zao zikasamehewa.

Plea bargain kwa wasiojua ilianza na hawa mabwana ila yao ilikuwa ya kimya kimya.

Kuanzia siku hiyo JK na JPM wakawa watu wa kutupiana vijembe hadharani kama utani vile kumbe wanajua kinachoendelea, ukitaka kula lazima uliwe.

Ikulu kutamu jamani
JPM alikua komesha. Mungu amlaze pema
 
Aliyeenda shule hachangiagi udedere kama wewe bogus! Walioenda shule maoni na michango yao inaonekana tu na hata kwa kusoma na kuchambua kwa haraka haraka utajua ni mtu wa aina gani... we bogus!
Waswahili kwakweli mna kazi sana nikwamba wewe haunizidi chechote kile maishani kuanzia pesa,elimu na mafanikio kiujumla.........mitandaoni kuna mambo sana eti nawewe una elimu ya hgk ambayo unakaa unajisifia tena kwa mtu ambaye usikute ni umri wa baba yako
 
Na ndo uongozi wa Dictatorship unataka hivyo... tulipofikia tunataka dictatorship mambo yaende sio usengeusenge tu
Umaskini unakusumbua sana na pia kutokana tangu jana upo period basi unachangia kwahasira mno hebu nikuambie kitu kimoja hamna uzalendo unaofundishwa darasani ila uzalendo unaanzia moyoni bila kujali dini,kabila wala elimu.....ewe mwanamke wa kisukuma fikiria kauli ya mumeo magufuli alipokiwaambia watu kuwa jimbo fulani sileti maendeleo kwasababu mumemchagua mbunge wa upinzani je hii ni sawa? Fikiria wale waliokavunjiwa nyumba dar halafu na mwanza nao wakaachiwa kwa kauli kuwa walimchagua je kwako ni sawa hata kama magufuli alikuwa mumeo?
 
Tunaendelea na visa na mikasa ya hayati JPM..

Hakuna siri JPM hakuwa chaguo la wana CCM mwaka 2015, hata mwenyekiti wa chama hakumtaka awe Rais bali alizidiwa na nguvu ya asili.

Mwenyekiti alimkusudia kumrithisha kijiti rafiki yake wa kitambo Bernard Membe,lakini wana CCM walimtaka Edward Lowassa.

Baada ya jina la Magufuli kuibuka kidedea kuna watu hawakulala siku hiyo. Tena sio wapinzani, bali wafanyabiashara na mafisadi ndani ya CCM, walijua kiama chao kimefika.

Mojawapo wa wafanyabiashara hao ni familia ya Bwana Ghalib almaarufu kama GSM.

Tukirudi nyuma kidogo hii familia ina asili ya mkoa wa Tanga na mzee wao marehemu Said Mohamed ambaye alifariki mapema mwaka huu alihamia huko Kusini mwa Tanzania na kujikita na kilimo na biashara ya korosho, alipozeeka akawaachia biashara vijana wake waziendeleze.

Pia hii familia imekuwa na ukaribu na familia ya mstaafu JK kwa miaka mingi.
Tufahamu kuwa JK aliwapenda sana watu wa mkoa wa Tanga kuliko watu wa mkoa wowote uli, labda ni kwa sababu alisoma Tanga School au kwa sababu wilaya anayotokea iko jirani na mkoa wa Tanga sielewi.

Nikikupa hapa orodha ya watu wa mkoa wa Tanga ambao walibebwa na JK kipindi cha utawala wake utashangaa,wengine hakuna aliyekuwa akiwafahamu wakalama post kubwa za ukuu wa mkoa,wilaya hata uwaziri ,achilia mbali post zingine za juu.

Kipindi hiki cha JK ndipo familia hii ya GSM nayo ikaibuka kama uyoga, kupitia kampuni zao za HSC na Silent Ocean wakaigeuza Kariakoo kuwa Dubai ya Afrika au China ya Afrika, wafanyabiashara toka nchi jirani wakawa hawaendi tena China kufuata mzigo mambo yote yaliiishia kariakoo.

Umafia wa kiwango cha juu uliofanyika bandarini na TRA na kampuni hizi ulivutia wateja wengi, mzigo ulikombolewa bandarini fasta na kwa gharama ndogo.

Kumbe nyuma yake kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa taratibu za bandari na kodi za TRA, mabilioni ya shilingi yalihujumiwa na hii familia.

Baada ya hii jina la JPM kupenya sasa ikawa patashika nguo kuchanika wakawata na kuwazua wakaamua kuiua kampuno ya HSC wakijua tu ikibaki hewani JPM atowaacha salama.

Kupitia kampuni ya Law Domain Adocate tarehe 19 oct 2015 siku chache kabla ya uchaguzi mkuu,wakafile A notice of resolution to wind up voluntarily. Hii kwa wasiojua sheria, wind up ni kusimamisha shughuli za kampuni kisheria.

Walisahau kitu kimoja ila wakaja kukikumbuka baadae kuwa jinai huwa haifi, pamoja na kuwind up HSC kisheria bado wangekamatwa na kujibu tuhuma hata kama kampuni haipo.

Ile Silent Ocean ilibaki kuoparate kwa sababu inasemekana haikusajiliwa Tanzania japo iliwakenga wafanyabiashara wa Tanzania.

Sasa basi baada ya JPM kuingia madarakani, naweza kusema mwezi mzima alikuwa akishinda kama sio bandarini basi ni TRA, mabosi wa taasisi hizo mbili vitambi viliporomoka.

Vijana wake wakamletea ripoti ya wakwepa kodi maarufu,jina la HSC na Silent Ocean likiwa kidedea pale juu.

Matumbo moto wakajua hapa Segerea inawahusu, kama Manji alilala Segerea who is GSM?

Kwa kutumia ushawishi wa vijana wa mstaafu wakaomba apointment mara kadhaa kuonana na JPM.

Appointment ikawa approved wakaitwa Ikulu, kwa makosa yao walitembea kwa magoti kwenye korido mpaka ofisini kwa JPM. Akiwa na sura iliyokasirika akawaambia sitaki maelezo lipeni hizo arreas au Segerea inawasubiri

Yakalipwa mabilioni kimyakimya GSM dhambi zao zikasamehewa.

Plea bargain kwa wasiojua ilianza na hawa mabwana ila yao ilikuwa ya kimya kimya.

Kuanzia siku hiyo JK na JPM wakawa watu wa kutupiana vijembe hadharani kama utani vile kumbe wanajua kinachoendelea, ukitaka kula lazima uliwe.

Ikulu kutamu jamani
Hadithi bila picha hainogi. Hebu weka picha tuone jinsi GSM alivyotembea kwa magoti ikulu.
 
Wamjini wapo kazini cowboys tupo pembeni jamani. Ila lake zone Ni kiboko kwa uongozi. Hawatakigi utani Mana watu wao na wao Ni masikini so wanayo Ile feel yake.
Ila wengine wao Ni kujichotea ama kuiba hela za wananchi masikini kwa manufaa yao binafsi.cheki kwanza kwa taizi la malipo ya Arab contractor kinachoendelea,Mara Kuna 69bn za software ya kufuatilia umeme kukatika tu. Symbion wamefaulu kesi wanalipwa 300bn.
Yaani lake zone Ni Cuba ya Fidel ama Bolivia ya Che guavara, Thomas Sankara,jf Kennedy,Maduro,hugo Chavez ,Gadafi wa Libya,wale viongozi walio tayari kuifia nchi zao. Jamani msinishambulie Ila Kuna ukweli cheki uhalisia.
Lengo sio kufa kwa ajiili ya nchi yako
Bali kuua kwa ajiili ya nchi yako

Sent from my 220333QAG using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom