Familia ya marehemu Joe Mutaboyerwa yavamiwa. Mama na watoto wawili wauawa

Familia ya marehemu Joe Mutaboyerwa yavamiwa. Mama na watoto wawili wauawa

Wewe mtu mkubwa bna.naogopa kukudangia.
Yaani laiti ungelijua!, mimi nina ukubwa gani hadi uniogope?. Acheni roho mbaya tuu za uchoyo wa kuwanyima wenzenu company. Tena mimi ndio usiniogope kabisa, umri umeisha songa, sina hata meno ya kutafuna nyama, ni kunywa tuu kinywaji, hakuna kutafuna nyama.
P
 
Wanawake bhana!! Mume kafariki juzi tu keshapata HAWARA hadi anajua nyumbani kwake na hela zilipo!!!! Huyo hawara anayepajua home mume kafa juzi tu lazima alikuwepo kabla. Mjane anaishi mwenyeweee na wanawe tu very selfish utakuta hapo wakwe, mawifi na mashemeji aliwakatia laini wasiguse urithi alioachiwa akaamini mlinzi na kibenten.. Matokeo yake watoto malaika wanauwawa very sad!!!
Kwani Joe alikufaje!?
 
Binadamu wengine walipewa akili 1/2. Wewe utamshutumu vipi victim? Ni akili ya kawaida hiyo kweli? Nebuchadinezzer
Kwa hiyo ni kosa lake kuuawa yeye na wanawe? Yeye ndio amesababisha haya?
Unajuaje kama alikuwa "anatembea na wanaume hovyo hovyo"?

Ni sawa na kusema mwanamke akiwa barabarani usiku akabakwa ni kosa lake.

Hizi ni hukumu zenye double standards.
 
Wajameni, this is very sad!. Emmy Kaungamno, alikuwa jirani yetu next Door, enzi za udogoni pale Drive in Flats, "mafletini". Last Sunday nimesali Msasani Lutheran, nikasalimiana nae, na kujoke, how come, she looks so cute as if she is early twenties, na kusema lazima kuna watu wanatunza!, akasema thanks, hakuna mtu ni Almight God only!. Its as if alikuwa anatuaga!. So sad!.
Paskali
Huyu shadrak kapanga ana uhusiano na mzee kapanga baba yao akina ema yule wa Uk. Anaeishi tabata .
 
Inasikitisha sana,

FUNZO:
Wanawake wajane jieshimuni, jama unaona bado unaweza olewa, fanya hivyo na sio kutembea na wanaume hovyo hovyo.

Huyu mama amekufa na kusababisha wanae kufa kwa sababu ya uasherati wake. (Kwa lugha isiyoyakisanii)
Hata vitabu vya dini vinasema tamaa ni dhambi ya umauti.
 
Inasikitisha, wapumzike kwa amani....
Sasa boyfriend kashindwa kula hela za bibie kupitia mapenzi? Mbona ni rahisi kuliko hiyo njia ya kutumia manguvu/mauaji
I don’t believe kama boyfriend ndio kaua mchepuko na watoto kwa sababu hata wakifa yeye sio mrithi na angetaka hizo hela zinazoenda bank angemuua mke hata kwa sumu au angemlainisha kwa mapenzi akapewa hizo hela
Hii story ni kutunga
hapa kuna mkono wa ndugu wa mume
 
I don’t believe kama boyfriend ndio kaua mchepuko na watoto kwa sababu hata wakifa yeye sio mrithi na angetaka hizo hela zinazoenda bank angemuua mke hata kwa sumu au angemlainisha kwa mapenzi akapewa hizo hela
Hii story ni kutunga
hapa kuna mkono wa ndugu wa mume
Hilo nalo linawezekana kwa asilimia kubwa tu....
 
Familia ya mr Joe Mutaboyerwa imepigwa mapanga inawezekana ni mlinzi wao mama na watoto wawili wote wameuwawa [emoji33]
Very sad story!
Inasemekana ni njama ya boy friend wake aliyekuwa nae baada ya kifo cha Joe! Aligundua dada ana hela nyingi ambazo alikuwa apeleke bank next day, boy friend akapata tamaa, akapanga na mlinzi wakwakata mapanga wakawaua! Wakachukua pesa! Ila boyfriend akamzika mlinzi pesa! Mlinzi akatoa siri! Wote wamekamatwa!


Zaidi soma hapa
Dar Es Salaam. Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamshikilia Shadrack Kapanga (34) kwa tuhuma za mauaji ya mama na watoto wake wawili eneo la Masaki mtaa wa Maryknol.

Kapanga ambaye ni msaidizi wa kazi za ndani alikamatwa jana Ijumaa Juni 11, 2021 eneo la Magomeni akiwa kwenye harakati za kutoroka baada ya kuwaua Emilly Mutaboyerwa ambaye ni mama na Damita (13) na Daniela Mutaboyerwa (15).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Jumamosi Juni 12, 2021 na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, mtuhumiwa huyo alikamatwa akiwa na baadhi ya vitu alivyoviiba baada ya kufanya tukio hilo.

“Vitu alivyokutwa navyo wakati akitoroka ni simu za marehemu, televisheni, king’amuzi cha DSTV na rimoti,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Muliro ameeleza kuwa upelelezi wa awali umebaini kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo la mauaji Juni 9, 2021 baada ya kuwapiga kila mmoja kwa wakati tofauti kwa kitu kizito na kuwasababishia kuvuja damu nyingi na kupoteza maisha.

“ Baada ya kuwaua aliwafungia ndani na kutoroka. Upelelezi wa shauri hili unaendelea ili kujua sababu za msingi za mauaji hayo na mara utakapokamilika mhusika/wahusika watafikishwa Mahakamani haraka iwezekanavyo,” inaeleza.




View attachment 1816190

Sent using Jamii Forums mobile app
Mshana Jr:

Asante kwa taarifa mkuu ila taarifa hazijajitosheleza. 💔
 
Back
Top Bottom