Familia ya Rais Magufuli mkiliachia hili jambo lipite bila ya kumburuza mahakamani Kabendera itakuwa ni usaliti wa karne!

Familia ya Rais Magufuli mkiliachia hili jambo lipite bila ya kumburuza mahakamani Kabendera itakuwa ni usaliti wa karne!

Familia yenyewe wana ushahidi wa kuthibitisha kuwa Magufuli hakuua?.
 
Ila @ Nyani Ngabu wewe ni nani kutaka Kabendera aburuzwe mahakamani? What if ana ushahidi? Utareconmend auawe?
I’m all for it. Ila Kabendera naye ni lazima atoe ushahidi na awataje waliomwambia.m
 
Hata nchi zenye vita wanalima na kuzaliana. Kama hauamini kaangalie DRC Congo, kisha tazama idadi ya watu na sisi watanzia tunaoongozwa na chama kimoja kwa shuruti.
Wanalima halafu WANYAMULENGE wanayachoma moto mazao ....

Wanazaliana kwa wale wanawake na wanaume WASIOUAWA kila uchao....

CCM haiongozi kwa shuruti.....watanzania hawaoni mbadala nje ya CCM....
 
Kama anao ndo vizuri sasa.
Wewe ni mtu mwenye heshima zako ndani ya Jf ...tena muda mrefu,hudhani bandiko lako linaweza kumnyima haki anayepaswa na kuyapa majangili ushindi? Magufuli alikua malaika?
 
Familia yenyewe wana ushahidi wa kuthibitisha kuwa Magufuli hakuua?.
Familia haiwajibiki kuthibitisha hakuua.

Mwenye wajibu wa kuthibitisha ni anayetoa tuhuma.

Kuna watu bado mna ujinga wa kutisha na kusikitisha sana.
 
Vitu vya kuambiwa sio ushahidi, ninashangaa kusikia msomi wa fani ya sheria anasema "niliambiwa na mtu mkubwa " huo ukubwa sio ushahidi. Fikiria kuwa mtu kuuwawa tena ikulu, ofisi ya serikali, huyu jamaa ana ujasiri gani wa kuchafua ikulu? Sasa tunaomba uchunguzi wa kisayansi kuhusu hilo jambo.
 
Wewe ni mtu mwenye heshima zako ndani ya Jf ...tena muda mrefu,hudhani bandiko lako linaweza kumnyima haki anayepaswa na kuyapa majangili ushindi? Magufuli alikua malaika?
Hahahaaa! Mimi nina heshima gani hapa JF jamani? 🤣

Ulichokiandika hata sijakielewa na wewe mwenyewe sidhani hata unakielewa.
 
Katika madai yote dhidi ya Rais Magufuli, hili dai la huyu mwandishi Eric Kabdendera, kuwa Rais Magufuli alimuua Ben Saanane kwa kumpiga risasi ya kichwa hapo Ikulu [nasadiki ni Ikulu ya Dar], ni dai kubwa na zito sana.

Ni kashfa kubwa sana. Kwa mtu tu wa kawaida, kutuhumiwa kuua mtu mwenzio si jambo dogo. Seuze Rais wa nchi?

Wengi wetu kwa sasa tutakuwa tumeshaiona hii excerpt ya hicho kitabu:
View attachment 3190381

Napata wakati mgumu sana kuamini kuwa Rais Magufuli anaweza kumuua kijana wa Kitanzania, ambaye ni mtu mdogo sana, in the grand scheme of things, kwa mikono yake mwenyewe tena kwenye nyumba ya wananchi, Ikulu.

Tumeshawazoea akina Lissu na wenzake kuropoka na kutoa tuhuma za ajabu ajabu bila kutoa wala kuonyesha ushahidi wowote ule zaidi ya kusema ‘nimeambiwa’ au ‘niliambiwa’.

Lissu keshawahi kusema mara kadhaa kuwa baada ya Magufuli kufariki, eti nyumbani kwake yalikutwa mabulungutu ya mahela, dola za Kimarekani, kwenye mamilioni.

Bila ushahidi wowote ule zaidi ya ‘kuambiwa’, tuhuma hizo zinabaki kuwa ni porojo tu za Lissu.

Na ndo maana pengine hata familia ya Rais Magufuli haijawahi kusema wala kufanya chochote dhidi ya madai hayo.

Ila hili la Magufuli kutuhumiwa kuwa ni cold-blooded murderer, si la kawaida na halipaswi kupuuziwa.

If not true, what Kabendera did is libelous and should sued.

Mimi si mtaalamu wa sheria za Tanzania. Lakini naamini sheria za libel zipo.

Licha ya kwamba Rais Magufuli alikuwa ni public figure, kuna vitu huwezi kuvisema dhidi yake bila ushahidi.

Tuhuma za mauaji kwa mtu yeyote yule, humtia doa kubwa sana kwenye jamii, mtu huyo.

Majuzi hapa tumeona kituo cha televisheni cha Marekani, ABC, kilikubali kumlipa Rais Trump $15 milioni kwa sababu mmoja wa watangazaji wake alisema kimakosa kuwa Trump alipatikana na hatia ya ubakaji wakati si kweli.

Kubaka ni moja ya makosa yanayompa mtu doa la maisha.

Uuaji, kwangu mimi, ni kosa lililo juu ya ubakaji.

Sasa huyu jamaa Kabendera anakuja na tuhuma nzito namna hiyo tena kwa Rais mzima bila hata ushahidi wowote ule zaidi ya kusema kaambiwa na vyanzo vyake.

Hapana kwa kweli. Tuhuma kama hizo ni nzito sana kuachwa hivi hivi tu, la sivyo kama ni za ukweli.

Familia ya Rais Magufuli ikimwacha huyu jamaa bila kumburuza mahakani akatoe testimony yake huko under the penalty of perjury, itakuwa ni usaliti mkubwa sana kuwahi tokea nchini.

Yaani kabisa Rais Magufuli ampige risasi ya/za kichwa huyo Ben Saanane hapo Ikulu, halafu watu wa Magufuli waichukue maiti yake na kwenda kuitupa kwenye moto Rufiji?

Vigumu sana kuamini hilo.

Familia ya Rais Magufuli ni lazima ichore mstari mchangani na kuchukua hatua.

La sivyo, mtatufanya watu kama mimi tuamini kuwa yanayosemwa ni ya kweli.
Magufuli aliacha Familia!?
 
Familia haiwajibiki kuthibitisha hakuua.

Mwenye wajibu wa kuthibitisha ni anayetoa tuhuma.

Kuna watu bado mna ujinga wa kutisha na kusikitisha sana.
Mzee Kibao aliuawa na Polisi,Nondo alitekwa na polisi...ulitaka waje FBI kuthibitisha tuhuma dhidi ya polisi au ulitaka waliokuwepo kwenye eneo la uhalifu wakahojiwe na waliofanya uhalifu ?
 
Vitu vya kuambiwa sio ushahidi, ninashangaa kusikia msomi wa fani ya sheria anasema "niliambiwa na mtu mkubwa " huo ukubwa sio ushahidi. Fikiria kuwa mtu kuuwawa tena ikulu, ofisi ya serikali, huyu jamaa ana ujasiri gani wa kuchafua ikulu? Sasa tunaomba uchunguzi wa kisayansi kuhusu hilo jambo.
It strains credulity!

Yaani sitting president analetewa mtu Ikulu ili amuue yeye mwenyewe?

Hahahaa Kabendera is full of it.
 
Mzee Kibao aliuawa na Polisi,Nondo alitekwa na polisi...ulitaka waje FBI kuthibitisha tuhuma dhidi ya polisi au ulitaka waliokuwepo kwenye eneo la uhalifu wakahojiwe na waliofanya uhalifu ?
Sijaelewa ulichokiandika.
 
Katika watu hao mimi niko msitari wa mbele kabisa. Kwa bahati mbaya sidhani kama yuko mwenye ujasiri wa kufanya hivyo!
Natamani sana waende mahakamani, tutajua wapi panuvuja.

Unajua mtu anayeandika hadi ''mto rufiji'' ana kila kitu. Akiulizwa ushahidi atamtaja dereva aliyepeleka mzigo siyo source yenyewe.
Dereva kwasababu ni weak na hana pesa ndiye atafungua '' can of worms''
 
Back
Top Bottom