Familia ya Rais Magufuli mkiliachia hili jambo lipite bila ya kumburuza mahakamani Kabendera itakuwa ni usaliti wa karne!

Familia ya Rais Magufuli mkiliachia hili jambo lipite bila ya kumburuza mahakamani Kabendera itakuwa ni usaliti wa karne!

Awataje wa nini, yeye amemtaja aliyempiga risasi Ben Saanane. Kama vipi kawasaidie familia ya Magufuli kufungua kesi ya kupinga huo ukweli.
Kuna kitu kinaitwa pandora box, je familia ya jiwe ina ujasiri wa kubariki na kutaka lifunguliwe?

Hiyo kesi haitakuwa tu ya kitaifa, itakuwa ya kimataifa. Dunia yote itafuatilia yanayojiri.

Be careful of what you wish for Nyani Ngabu! Je unajua kwa nini hakuna uchunguzi wowote ule ulifanyika?

Unachowashauri wana familia wakifanye ni ujinga, ndiyo ni ushauri wa kijinga.

Juhudi gani zilifanywa na jemadari mkuu kumlinda raia wake Ben Saanane? Hakuna!
 
MTUME KATIKA MASWALA KAMA HAYA
Tukio katika maisha ya Mtume:

Katika tukio moja, kipindi cha Mtume, mtu mmoja kutoka kabila fulani aliuawa bila haki. Mtume aliagiza uchunguzi wa haraka ufanyike na kuhakikisha waliotekeleza mauaji wanawajibika. Katika tukio hili, Mtume aliwaonya viongozi wa jamii dhidi ya upendeleo au kuchelewesha haki, akisema:


(Bukhari, Muslim)
Mtume alisisitiza kuwa kuchelewesha haki au kuzembea katika kushughulikia dhuluma kunaweza kusababisha Mtaarufuku mkubwa katika jamii
Cc
Nyani Ngabu
Nakubaliana na wewe kwani laiti Serikali ingekubali kuwaomba Scotland Yard au FBI kusaidia upelelezi na mhusika kukamatwa leo hii kashfa hii isingekuwepo.
 
Magufuli alikuwa kichaa na mlevi wa madaraka aliyependa kusifiwa sana. Hizi tuhuma sio mpya na kwa mtu anayemjua vizuri huyo shetani wa Chato, hilo tukio alilifanya na mengine mengi kama hilo
Una maana hata mrithi wake ni kichaa? Mbona naye anapenda kusifiwa hadi kuwaita watu machawa kama mwendaze alivyozoea kuwaita wanyonge?
 
I’m all for it. Ila Kabendera naye ni lazima atoe ushahidi na awataje waliomwambia.
Kabendera ni Mwandishi , kuna sheria ya kulinda 'source'
Anaweza kushtakiwa kwa 'madai ' aliyotoa siyo 'source'' . Kumbuka alifahamu uzito wa hoja na aliwasiliana na Wanasheria kabla . Kumburuza mahakamani kunaweza kuzua mazito zaidi. Jiulize kwanini ameandika ''boldly''

Jenerali Ulimwengu na gazeti Rai walimtuhumu Hans Kitime kuhusu matibabu ya milioni 60 wakati huo.
Walitakiwa kutoa ushahidi, wakaweka kila kitu hadharani, hawakushinikizwa kutaja ''source''
Mkapa hakuwa na uwezo wa kumshtaki akadai si Raia
 
Katika madai yote dhidi ya Rais Magufuli, hili dai la huyu mwandishi Eric Kabdendera, kuwa Rais Magufuli alimuua Ben Saanane kwa kumpiga risasi ya kichwa hapo Ikulu [nasadiki ni Ikulu ya Dar], ni dai kubwa na zito sana.

Ni kashfa kubwa sana. Kwa mtu tu wa kawaida, kutuhumiwa kuua mtu mwenzio si jambo dogo. Seuze Rais wa nchi?

Wengi wetu kwa sasa tutakuwa tumeshaiona hii excerpt ya hicho kitabu:
View attachment 3190381

Napata wakati mgumu sana kuamini kuwa Rais Magufuli anaweza kumuua kijana wa Kitanzania, ambaye ni mtu mdogo sana, in the grand scheme of things, kwa mikono yake mwenyewe tena kwenye nyumba ya wananchi, Ikulu.

Tumeshawazoea akina Lissu na wenzake kuropoka na kutoa tuhuma za ajabu ajabu bila kutoa wala kuonyesha ushahidi wowote ule zaidi ya kusema ‘nimeambiwa’ au ‘niliambiwa’.

Lissu keshawahi kusema mara kadhaa kuwa baada ya Magufuli kufariki, eti nyumbani kwake yalikutwa mabulungutu ya mahela, dola za Kimarekani, kwenye mamilioni.

Bila ushahidi wowote ule zaidi ya ‘kuambiwa’, tuhuma hizo zinabaki kuwa ni porojo tu za Lissu.

Na ndo maana pengine hata familia ya Rais Magufuli haijawahi kusema wala kufanya chochote dhidi ya madai hayo.

Ila hili la Magufuli kutuhumiwa kuwa ni cold-blooded murderer, si la kawaida na halipaswi kupuuziwa.

If not true, what Kabendera did is libelous and should sued.

Mimi si mtaalamu wa sheria za Tanzania. Lakini naamini sheria za libel zipo.

Licha ya kwamba Rais Magufuli alikuwa ni public figure, kuna vitu huwezi kuvisema dhidi yake bila ushahidi.

Tuhuma za mauaji kwa mtu yeyote yule, humtia doa kubwa sana kwenye jamii, mtu huyo.

Majuzi hapa tumeona kituo cha televisheni cha Marekani, ABC, kilikubali kumlipa Rais Trump $15 milioni kwa sababu mmoja wa watangazaji wake alisema kimakosa kuwa Trump alipatikana na hatia ya ubakaji wakati si kweli.

Kubaka ni moja ya makosa yanayompa mtu doa la maisha.

Uuaji, kwangu mimi, ni kosa lililo juu ya ubakaji.

Sasa huyu jamaa Kabendera anakuja na tuhuma nzito namna hiyo tena kwa Rais mzima bila hata ushahidi wowote ule zaidi ya kusema kaambiwa na vyanzo vyake.

Hapana kwa kweli. Tuhuma kama hizo ni nzito sana kuachwa hivi hivi tu, la sivyo kama ni za ukweli.

Familia ya Rais Magufuli ikimwacha huyu jamaa bila kumburuza mahakani akatoe testimony yake huko under the penalty of perjury, itakuwa ni usaliti mkubwa sana kuwahi tokea nchini.

Yaani kabisa Rais Magufuli ampige risasi ya/za kichwa huyo Ben Saanane hapo Ikulu, halafu watu wa Magufuli waichukue maiti yake na kwenda kuitupa kwenye moto Rufiji?

Vigumu sana kuamini hilo.

Familia ya Rais Magufuli ni lazima ichore mstari mchangani na kuchukua hatua.

La sivyo, mtatufanya watu kama mimi tuamini kuwa yanayosemwa ni ya kweli.
Akiguswa mtu wenu mnakuja juu,nyie kutwa mnamtukana Samia lakini mbona hamshtakiwi popote?au kwann huwa mnafurahia wapuuzi wakimtusi Samia?unadhani familia ya samia inafurahia?!

Kabendera alichoandika kama kweli au uongo ni haki yake kikatiba uhuru wakutoa maoni.
 
Back
Top Bottom