Familia yake wanataka kunitolea mahari

Familia yake wanataka kunitolea mahari

Ironbutterfly

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2023
Posts
3,042
Reaction score
8,227
Habari za eid pili waungwana,

Iko hivi, nimejaliwa kuzaa watoto wawili wa kiume na bwana mmoja. Kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo, hatukuoana na huyo bwana. Watoto wote nilikuwa naishi nao kwangu, huku tukisaidizana malezi. Yeye alishaoa kama miaka mitatu nyuma.

Kama miaka miwili nyuma nilipata changamoto kazini na mambo mengi yalitokea upande wangu hivyo sikuwa stable kuendelea kuishi na watoto. Tulipojadiliana pande zote, wazazi wake wakasema niwakabidhi watoto wawalee hadi hapo nitakapo kuwa sawa.

Basi watoto nikawapeleka kwao, nikawa na still huwa naenda kuwatembelea pindi nipatapo nafasi pamoja na kuchangia gharama za ada na mahitaji mengine ya watoto.

Muda umeenda, nimerudi kwenye fomu, na nimeona nahitaji kuwachukua watoto niwalee sasa, yaani niishi nao huku nilikohamia kikazi. Wazazi wake bwana yule wamekuja na wazo kuwa, familia yao imeamua jamaa anitolee mahari kwa mujibu wa mila zao, so wamenambia niifahamishe wazee wangu ili taratibu zifanyike.

Binafsi sijaafiki suala hilo, kwani jamaa alishaoa na kashazaa watoto wengine wawili kwa mkewe. Hata mila za kwetu haziafiki jambo hilo, isitoshe mimi niko na mtu wangu ambaye tuna plan zetu za hapo baadae kidogo, naona kama ni mbinu ya kunizuia kuchukua wanangu.

Hebu mnipe ushauri wadau, namna gani naweza kuwachukua watoto bila kuleta mikwaruzano?
 
Unaweza chukua watoto ila kama ulivyosema una Bwana mpya 🙃 kama huyu bwana mpya atakubali kuishi na wewe ukiwa na watoto wawili kama kiongozi wa wanaume JF nakushauri huyo jamaa hakufai hata kidogo kimbia...
 
Habari za eid pili waungwana.
Iko hivi,nimejaliwa kuzaa watoto wawili wa kiume na bwana mmoja.Kutokana na sababu zilizokuwa nje ya
Hiyo kukutolea Mahari kisheria ni kuwahalalisha ( Legitimize) hao watoto watambulike katika familia yao.
Kama hao wazazi wana mtazamo kama wangu, ikiwa wanataka kutoa mahari ili uolewe na jamaa hiyo ni issue nyingine.
So rudi waulize wanakutolea mahari kwa minajili gani?
 
Hiyo kukutolea Mahari kisheria ni kuwahalalisha ( Legitimize) hao watoto watambulike katika familia yao.
Kama hao wazazi wana mtazamo kama wangu, ikiwa wanataka kutoa mahari ili uolewe na jamaa hiyo ni issue nyingine.
So rudi waulize wanakutolea mahari kwa minajili gani?
Ili watambulike kwao na hata sasa wanaishi kwao bwana yule🙏
 
Hakuna mwanaume akiyekamilika akataka kulea watoto w mwanaume mwingine

Pili kwa sisi waafrica mtoto anachukua ubini wa baba. Kuchanganya family mbili zenye damu na koo tofauti huwa zinaleta shida sana. I have experienced this. .
Yeye pia anaye mtoto mmoja alomzaa na mwanamke mwingine,na huyo mwanamke alishaolewa🙏
 
Yeye pia anaye mtoto mmoja alomzaa na mwanamke mwingine,na huyo mwanamke alishaolewa🙏
Ndio mwanamke anaweza leo mtoto wa Bwana ila mwanaume hawezi leo mtoto w Bwana mwingine. Mwanae bado atabaki na ubini wake.

Kwanza unawanyima haki watoto kukua kwao Haimanishi kuwa hawakutambui kama mama yao

Uchagan hata ukienda ukaolew mara kumi kama umelipiw mahari unarudi nyumbani. Ukipokea mahari maana yake watoto watatambulika rasmi kwa baba. .
 
Kwa upande wangu itaniharibia,we mtu wangu akijua nimetolewa mahari na baby dady atajisikiaje?
Issue ni hivi umetolewa mahari ili kuhalalisha watoto uliozaa na huyo wa kwanza watambulike kwenye familia (ukoo) wake, ili kesho akifa watoto wawe na haki.
Tafuta Mwanasheria awaeleweshe.
Au muhulize jinsi ya kuhalalisha watoto wa nje ya ndoa ni vipi?
 
Ndio mwanamke anaweza leo mtoto wa Bwana ila mwanaume hawezi leo mtoto w Bwana mwingine. Mwanae bado atabaki na ubini wake.

Kwanza unawanyima haki watoto kukua kwao Haimanishi kuwa hawakutambui kama mama yao

Uchagan hata ukienda ukaolew mara kumi kama umelipiw mahari unarudi nyumbani. Ukipokea mahari maana yake watoto watatambulika rasmi kwa baba. .
Lol mila gani hizo,na wahaya nao wana hizo mila eeh,manake bwana yule ni mhaya 🤔
 
Back
Top Bottom