Fanya haya mambo 5 ili uzeeke kijana

Fanya haya mambo 5 ili uzeeke kijana

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
Watu wengi ni wazee lakini vibogoyo, wamepinda, hawaoni, hawanusi, wanatembea na chupa za mikojo na vidonge vya rangi mbalimbali. Huu uzee unagharama sana. Kuna mambo ukianza kufanya leo yanaweza kukusaidia ukazeeka huku huku ukiwa unanguvu na kila kitu kiko vizuri.

1: Asilimia kubwa ya vyakula vyako viwe mzao wa ardhi (plant based), Maana mwili wako ulikuwa designed kutumia mazao ya ardhi sio wanyama wenzako.

2: Epuka magomvi na mafarakano. Pima jambo kama halina manufaa kubali kushindwa. Simba ni mfalme wa Pori lakini anazeeka akiwa na miaka 14, wakati kobe mchovu wa pori anazeeka akiwa na miaka 100+. Kwa sababu simba ni mkali na muda wote anafokafoka hovyo.

3: Fanya mazoezi ya kawaida. Wanaokimbia mabio umbali mreefu huzeeka vibaya. Tembea tu kwa miguu mara nyingi. Hili ndio zoezi salama na la bei nafuu.

4: Kuwa na mke mmoja mnayependana. Pia tafuta marafiki na watu au baadhi ya ndugu mnaoendana muwe na muda wa chakula cha pamoja na kuenjoy.

5: Amini katika Mungu anayekuongoza wewe binasi sio kama kanisa au kikundi cha dini au kupitia mtu flani wa kiroho. Hata kama unasali hii ya Mungu binafsi itakupa faida kubwa kiafya na kiuwekevu.

Hizi ni baadi ya sababu kwa nini ni sehemu tatu tu duniani ndio kuna idadi kubwa ya wazee ambao hawaumwiumwi wala kuomba kufa kila muda (okinawa, roma linda na kisiwa kimoja huko Italia). Wazee wengi duniani ni wagonjwa na wamejaa masumbufu mengi wanajiombea kufa.
 
Kama unapesa lakini huna akili ya kula na kujidhibiti. zitakungoa meno, zitakupa presha na kisukari, wasiwasi na magomvi hadi zikuue ukakosa hata uzee wa mateso.
ukiwa na pesa utakula vizuri, mlo kamili, pale protini, hapa vaitamini, pale faiba, na kadhalika
huna pesa utashindia carbs kila siku, kwashakoo anakua rafiki yako
 
Watu wengi ni wazee lakini vibogoyo, wamepinda, hawaoni, hawanusi, wanatembea na chupa za mikojo na vidonge vya rangi mbalimbali. Huu uzee unagharama sana. Kuna mambo ukianza kufanya leo yanaweza kukusaidia ukazeeka huku huku ukiwa unanguvu na kila kitu kiko vz...
Bila kuzungumzia pombe uchambuzi wako ni batili.
 
Nina over 60 na sasa hivi nimetoka kutembea kwa mda wa saa moja
Namshukuru Mungu sina maradhi yoyote yale hata tezi dume
Sijisifii ila najitahidi kwa kula vizuri na kazi nyingi sio mvivu wa kukaa kaa na kupiga soga kijiweni
Wazee wenzangu wananishangaa nikiwapita na baiskeli 😄
 
Watu wengi ni wazee lakini vibogoyo, wamepinda, hawaoni, hawanusi, wanatembea na chupa za mikojo na vidonge vya rangi mbalimbali. Huu uzee unagharama sana. Kuna mambo ukianza kufanya leo yanaweza kukusaidia ukazeeka huku huku ukiwa unanguvu na kila kitu kiko vzr.

1: Asilimia kubwa ya vyakula vyako viwe mzao wa ardhi (plant based), Maana mwili wako ulikuwa designed kutumia mazao ya ardhi sio wanyama wenzako.

2: Epuka magomvi na mafarakano. Pima jambo kama halina manufaa kubali kushindwa. Simba ni mfalme wa Pori lakini anazeeka akiwa na miaka 14, wakati kobe mchovu wa pori anazeeka akiwa na miaka 100+. Kwa sababu simba ni mkali na muda wote anafokafoka hovyo.

3: Fanya mazoezi ya kawaida. Wanaokimbia mabio umbali mreefu huzeeka vibaya. Tembea tu kwa miguu mara nyingi. Hili ndio zoezi salama na la bei nafuu.

4: Kuwa na mke mmoja mnayependana. Pia tafuta marafiki na watu au baadhi ya ndugu mnaoendana muwe na muda wa chakula cha pamoja na kuenjoy.

5: Amini katika Mungu anayekuongoza wewe binasi sio kama kanisa au kikundi cha dini au kupitia mtu flani wa kiroho. Hata kama unasali hii ya Mungu binafsi itakupa faida kubwa kiafya na kiuwekevu.

Hizi ni baadi ya sababu kwa nini ni shemu tatu tu duniani ndio kuna idadi kubwa ya wazee ambao hawaumwiumwi wala kuomba kufa kila muda (okinawa, roma linda na kisiwa kimoja huko Italia). Wazee wengi duniani ni wagonjwa na wamejaa masumbufu mengi wanajiombea kufa.
-Kufanya mazoezi inahitaji mlo mzuri, -Kutoka na kula na mke pamoja na marafiki muenjoy yahitaji pesa
  • Mlo wa veggies unahitaji pesa
  • Mafarakano mara nyingine husababishwa na umasikini

Tutafute pesa, pesa inaondoa stress
 
Tafuta pesa tu, ukiwa na pesa utazeeka vizuri
Pesa ni kitu kimoja akili ya kuzitumiq hapo pia zinagawa watu katika makundi mawili. Moja wanatumia pesa zao kujiua kidogokidogo bioa kujua, na wengine kutumia pesa kujiimarishia uzee mwema.
Pesa ni muhimu, ila bila umakini utajikuta unakufa kwa kosa la kutafuta pesa badala ya kutumia chache ulizonazo zikupe maisha marefu.
 
Back
Top Bottom