Fanya haya mambo 5 ili uzeeke kijana

Fanya haya mambo 5 ili uzeeke kijana

Watu wengi ni wazee lakini vibogoyo, wamepinda, hawaoni, hawanusi, wanatembea na chupa za mikojo na vidonge vya rangi mbalimbali. Huu uzee unagharama sana. Kuna mambo ukianza kufanya leo yanaweza kukusaidia ukazeeka huku huku ukiwa unanguvu na kila kitu kiko vzr.

1: Asilimia kubwa ya vyakula vyako viwe mzao wa ardhi (plant based), Maana mwili wako ulikuwa designed kutumia mazao ya ardhi sio wanyama wenzako.

2: Epuka magomvi na mafarakano. Pima jambo kama halina manufaa kubali kushindwa. Simba ni mfalme wa Pori lakini anazeeka akiwa na miaka 14, wakati kobe mchovu wa pori anazeeka akiwa na miaka 100+. Kwa sababu simba ni mkali na muda wote anafokafoka hovyo.

3: Fanya mazoezi ya kawaida. Wanaokimbia mabio umbali mreefu huzeeka vibaya. Tembea tu kwa miguu mara nyingi. Hili ndio zoezi salama na la bei nafuu.

4: Kuwa na mke mmoja mnayependana. Pia tafuta marafiki na watu au baadhi ya ndugu mnaoendana muwe na muda wa chakula cha pamoja na kuenjoy.

5: Amini katika Mungu anayekuongoza wewe binasi sio kama kanisa au kikundi cha dini au kupitia mtu flani wa kiroho. Hata kama unasali hii ya Mungu binafsi itakupa faida kubwa kiafya na kiuwekevu.

Hizi ni baadi ya sababu kwa nini ni shemu tatu tu duniani ndio kuna idadi kubwa ya wazee ambao hawaumwiumwi wala kuomba kufa kila muda (okinawa, roma linda na kisiwa kimoja huko Italia). Wazee wengi duniani ni wagonjwa na wamejaa masumbufu mengi wanajiombea kufa.
Shukran
 
Ukiishi kijijini automatically utafanya mazoezi ya kutembea, kula kiasili, kuwa na mke mmoja kwa Wakristu, n.k
Ujumbe huu utufikie sisi wenye maisha yafuatayo
1. tunaojiita matajiri wenye nyumba za mageti na ka-gari ka kuendea kazini
2. tukifika kazini tunakalia viti vya kuzunguka 4.saa nne tunakula supu, chapati na Coca-Cola.
3. Mchana tunakula makaange na pepsi baridiiiii
4.jioni kabla ya kufika nyumbani tunapiga Serengeti baridiiii
5. Wenye hasira na tusiokuwa wavumilivu kwa mawazo ya watu wengine
6. Tunaotumbua fedha ya mshahara mnono bila kuwekeza tukisubiri fedha za pensheni kuanzisha Miradi ya uzalishaji mali
7. Tunaozaa ovyo na kumwachia mke ndo alee watoto sisi tuko bize na safari za ulaya. Utakuta una fedha lakini mitoto ni mapapai.
 
Natembeza viatu, maisha ni magumu , mke anakaanga maandazi, watoto wanasoma shule za kidumu na fagio, nyumba ya kupanga.
Kufokafoka katika mazingira haya ni lazima, maisha yenyewe tu ni zaidi ya mazoezi.
Ushauri wako utafaa kwa wale wenye maisha fulani ya kati au ya juu, kwetu sisi huku magoloka ni ngumu sana.
 
Watu wengi ni wazee lakini vibogoyo, wamepinda, hawaoni, hawanusi, wanatembea na chupa za mikojo na vidonge vya rangi mbalimbali. Huu uzee unagharama sana. Kuna mambo ukianza kufanya leo yanaweza kukusaidia ukazeeka huku huku ukiwa unanguvu na kila kitu kiko vizuri.

1: Asilimia kubwa ya vyakula vyako viwe mzao wa ardhi (plant based), Maana mwili wako ulikuwa designed kutumia mazao ya ardhi sio wanyama wenzako.

2: Epuka magomvi na mafarakano. Pima jambo kama halina manufaa kubali kushindwa. Simba ni mfalme wa Pori lakini anazeeka akiwa na miaka 14, wakati kobe mchovu wa pori anazeeka akiwa na miaka 100+. Kwa sababu simba ni mkali na muda wote anafokafoka hovyo.

3: Fanya mazoezi ya kawaida. Wanaokimbia mabio umbali mreefu huzeeka vibaya. Tembea tu kwa miguu mara nyingi. Hili ndio zoezi salama na la bei nafuu.

4: Kuwa na mke mmoja mnayependana. Pia tafuta marafiki na watu au baadhi ya ndugu mnaoendana muwe na muda wa chakula cha pamoja na kuenjoy.

5: Amini katika Mungu anayekuongoza wewe binasi sio kama kanisa au kikundi cha dini au kupitia mtu flani wa kiroho. Hata kama unasali hii ya Mungu binafsi itakupa faida kubwa kiafya na kiuwekevu.

Hizi ni baadi ya sababu kwa nini ni shemu tatu tu duniani ndio kuna idadi kubwa ya wazee ambao hawaumwiumwi wala kuomba kufa kila muda (okinawa, roma linda na kisiwa kimoja huko Italia). Wazee wengi duniani ni wagonjwa na wamejaa masumbufu mengi wanajiombea kufa.
Umenena vyema sana.

Umenukubusha bibi yangu mmoja alikuwa anamiaka 90+ ila mgumu haumwi chochote na anaingia shambani kulima
 
Kama hupigi stori na age mates wako Kuna shida mahali
Nina over 60 na sasa hivi nimetoka kutembea kwa mda wa saa moja
Namshukuru Mungu sina maradhi yoyote yale hata tezi dume
Sijisifii ila najitahidi kwa kula vizuri na kazi nyingi sio mvivu wa kukaa kaa na kupiga soga kijiweni
Wazee wenzangu wananishangaa nikiwapita na baiskeli 😄
A
 
Ukiishi kijijini automatically utafanya mazoezi ya kutembea, kula kiasili, kuwa na mke mmoja kwa Wakristu, n.k
Ujumbe huu utufikie sisi wenye maisha yafuatayo
1. tunaojiita matajiri wenye nyumba za mageti na ka-gari ka kuendea kazini
2. tukifika kazini tunakalia viti vya kuzunguka 4.saa nne tunakula supu, chapati na Coca-Cola.
3. Mchana tunakula makaange na pepsi baridiiiii
4.jioni kabla ya kufika nyumbani tunapiga Serengeti baridiiii
5. Wenye hasira na tusiokuwa wavumilivu kwa mawazo ya watu wengine
6. Tunaotumbua fedha ya mshahara mnono bila kuwekeza tukisubiri fedha za pensheni kuanzisha Miradi ya uzalishaji mali
7. Tunaozaa ovyo na kumwachia mke ndo alee watoto sisi tuko bize na safari za ulaya. Utakuta una fedha lakini mitoto ni mapapai.
Ni kweli mkuu tajiri mzungu anaishi kwenye nymba yenye eneo kubwa balaa. Upepo wa kutosha mazoezi golf etc.

Mfano kuna tajiri mmoja mchungaji anahekari 1000 US hadi uwanja wa ndege kwa private jets zake.

Huku tajiri amebuni ukuta mrefu, anaogopa wezi na watu wasimuombe pesa, mzunguko wa hewa sufri. Anashindia AC, Anakunywa kapombe ili asiwakwaze wadau. Nyumba eneo lote katandaza baving brocks badala ya nyazi za kuvutia na maua rangi tofauti na miti rafiki inayohamasisha uhai.
Huyu unakuta anapesa ambazo akiwa na mindset ya tajiri wa ulaya au china angechukua hkari mia na kuigeuza kuwa edeni na bado pesa yake ikabaki nyingi tu. Mimi mwenyewe kwa mindest zangu za kuungaunga siamini katika tuviwanjwa twa 20×20, hata nikiwa na makazi mjini lazima shamba langu niligeuze residential huku wanakijiji wenzangu wanaona ni shamba.
Tatizo wabongo ni kuigana.
 
Ukae saaaana ugundue nn hapa duniani.
Kuna jamaa anaitwa Methusela aliishi miaka zaidi ya 900. Kama 100 au80 unaona ni mingi au ni halali kufika ukiwa hoi ibn taabani utakuwa hujitendei haki. Ni suicidal mindset ambazo umemezeshwa na wajanja wa dunia.
 
Kama hupigi stori na age mates wako Kuna shida mahali

A
Kupiga story napiga nao sana don't get me wrong
Ila ule mda wa kukaa nao masaa ndio sina kwa sababu baadhi wamestaafu na wengine bado wana biashara zao wanazosimamia kwa juu, na hao ndio huwa jioni jioni tunakutana na kuongea au kuzunguka once in a week

Wazee na vijjana ni tofauti sana, utakuja kukumbuka hili
 
Natembeza viatu, maisha ni magumu , mke anakaanga maandazi, watoto wanasoma shule za kidumu na fagio, nyumba ya kupanga.
Kufokafoka katika mazingira haya ni lazima, maisha yenyewe tu ni zaidi ya mazoezi.
Ushauri wako utafaa kwa wale wenye maisha fulani ya kati au ya juu, kwetu sisi huku magoloka ni ngumu sana.
Maisha ni maamuzi na uchaguzi. Ukiona kuuza viatu na kugombana na watu kwa ukondakta hadi unakufa ndio kunakufaa uko sahihi. Ukifika sehemu ukasema sitaki ngoja niexplore mawimbi mengine ya maisha ambayo yataniletea amani shangwe uzima mrefu na vicheko pia utapata.

Hakuna aliyeandikiwa. Ni kuchagua. Hata haya maoni ni uchaguzi. Ila kumbuka pia wazee wengi wa kiafrika sio matajiri lakini kwa vidogo walivykuwa navyo waliishi maisha bora waliyoyachagua.
 
Back
Top Bottom