Nah, I'll never do this kind of shit.
Mwizi ni Mwizi tu sababu tayari yeye alishaamua kuona kudhuru wengine ni jambo la kawaida hivyo kumuogopa na kumsaidia sio kitu sahihi.
Njia pekee ya kumsaidia ni kumfanya aache wizi na sio kujipendekeza kwake ili akuache huku akiendelea kufanya uovu kwa wengine.
Kumsaidia ni kumreport polisi akitoka awe raia mwema au kumpa kipigo mpaka ajute kwanini aliamua kuwa mwizi.
Au kama kila mtu akiwa hivi kama wewe basi wizi hautoisha na wataona fahari kuendeleza hizo tabia mbovu sababu wanajua watu watajipendekeza kwao kwa uoga hivyo wao kuwa na power kwenu.
Kuishi namna hii ni uoga wa maisha yaani unaishi jinsi jamii inavyotaka na sio unavyotaka wewe now huo ni utumwa wa kisaikolojia wa kujitakia.
Maisha ni mafupi mno kuishi jinsi kima fulani anataka sababu ya uoga na kuogopa vitu ambavyo huna uhakika navyo kama vitatokea.
Na wanasema asilimia 99 ya vitu unavyoviogopa vitatokea havitatokea so hapa ni kujipa tabu, stress zisizo na msingi na kujichosha bure na kupoteza muda tu kufanya maisha yako na mambo yako ya maana ya maendeleo.
Unless na wewe unaendana na hao wezi walivyo na ndio maana unaweza kukaa kijiweni kuongea pumba na wezi. ndege wafananao huruka pamoja.
Iko hivi, mimi naishi ninavyotaka kama siku utaibiwa basi utaibiwa au kama hautaibiwa basi hautoibiwa na hakuna cha kufanya kuzuia hicho hicho kitu especially kama hujui kitatokea au lah.
Mimi katika maisha yangu nina kanuni moja yanapokuja mambo ya fujo, ukilianzisha ni eidha nikupige au tupigane au wewe unipige mimi na kama ukishindwa kunipiga basi mimi nitakupiga wewe.
Ukiondoa majambazi wenye silaha za moto siku mwizi au kibaka atakapo jaribu kuvunja ndani kwangu basi nondo lazima ihusike na ni lazima mmoja aende chini hakuna kulialia na bila shaka hatorudia tena.