Fatma Karume aondolewa kwenye orodha ya mawakili (Permanent removal), akutwa na hatia ya kukiuka maadili

Fatma Karume aondolewa kwenye orodha ya mawakili (Permanent removal), akutwa na hatia ya kukiuka maadili

Mmonyoko wa maadili, na inasikitisha sana kwa mtu unayejitambua kuandika kauli mbaya kama hii. I hope kizazi kama wewe mnapaswa mfundishwe uzalendo.
Unajua Uzalendo lkn Maadili hujui...

Hairuhusiwi kuiba research ya mtu na kujidai ni ya kwako - plagiarism is a crime..

Hairuhusiwi kufanya biashara ukiwa Ikulu...haiwezekani familia inaanzisha Kampuni ya Ujenzi na inajipa tender za kujenga Uwanja wa ndege wa Kimataifa kijijini kwao na kununua Ndege za familia kwa Fedha za Umma, huo ni Ujinga tu amechuma Majanga atakula na nduguze na wanae
 
Hope hawajafanya hivyo kumuondolea sifa ya kuweza kuteuliwa kushika madaraka makubwa baadaye kama ya AG! DPP!
 
Lakini shangazi alikuwa mwisho wake Ina majibu yake haonyeshi kuchukua , hata hivyo mawakili waupande mmoja ukute ndio walikaa wawili tu jiwe kawagiza nao wamefuata
 
Kikao cha kamati ya maadili ya Mawakili kilichokaa leo tarehe 23/9/2020 kimemkuta na hatia ya kukiuka maadili kwa kiwango cha juu, wakili Fatma Karume mwenye roll namba 848 na hivyo kuamuru jina lake liondolewe (permanent removal) katika orodha ya mawakili Tanganyika.

September mwaka 2019, wakili Karume alisimamishwa kufanya kazi ya uwakili Tanzania Bara, maamuzi yaliyotolewa na Jaji Feleshi kwenye kesi iliyofunguliwa na Ado Shaibu akipinga uteuzi wa mwanasheria mkuu wa serikali kuteuliwa kimakosa na Rais Magufuli na kesi iliondolewa.

Mahakama kuu iliamuru Fatma apelekwe kamati ya maadili ya mawakili kwa kosa la kushambulia ofisi ya mwanasheria mkuu ambae ndiye alikuwa wakili wa Ado Shaibu katika kesi hiyo.

Pia, soma=> Fatma Karume asimamishwa kufanya kazi za Uwakili

===
Akijibu hoja ya mdau kwenye mtandao wa twitter aliyemuomba akate rufaa dhidi ya uamuzi huo, Fatma amesema hatafanya hivyo kwa maelezo kwamba muamuzi wa rufaa yake sio huru.

"Ukiingia kwenye mapambano unahitaji kujua nani unapambana nae, kanuni za mpambano na uhuru wa muamuzi. Iwapo kanuni haziko wazi na muamuzi hayuko huru, huo sio mpambano bali upotevu wa muda. Hifadhi nguvu zako kwa mpambano unaoweza kushinda". Yalinukuliwa majibu ya Fatma Karume.

Asubiri rais mpya, rais wa watu aingie ofisini.

Mengi yaliyo fyongo na sheria fyongo kama za yule rubani wa Chopa zitakwenda naye kupumzika Chatto.

Ni jambo la kufurahisha kuwa Tanzania mpya iko njiani!
 
Hana kosa lolote lile zaidi ya udikteta chuki na roho mbaya ya huyo anayejiita MWENDAWAZIMU kwa sababu tu Shangazi yuko mstari wa mbele kumkosoa hadharani bila woga. Maria Sarungi pia kampuni yake Kwanza TV imefungiwa nadhani kwa mwaka kwa makosa ya kubambikiwa.

Makosa yake ni yepi? Huyu mama mwaka huu analo, kule Imma advocates wamemtimua na huku nako pia
 
Asubiri rais mpya, rais watu aingie ofisini.

Mengi yaliyo fyongo na sheria fyongo kama za yule rubani wa Chopa zitakwenda naye kupumzika Chatto.

Ni jambo la kufurahisha kuwa Tanzania mpya iko njiani!
Kwani JPM ataapishwa tarehe ngapi?
 
Naona wanamlazimisha aingie siasa. Hata hivyo kuna uwezekano wa hali ya hewa kubadilika.
 
Kikao cha kamati ya maadili ya Mawakili kilichokaa leo tarehe 23/9/2020 kimemkuta na hatia ya kukiuka maadili kwa kiwango cha juu, wakili Fatma Karume mwenye roll namba 848 na hivyo kuamuru jina lake liondolewe (permanent removal) katika orodha ya mawakili Tanganyika.

September mwaka 2019, wakili Karume alisimamishwa kufanya kazi ya uwakili Tanzania Bara, maamuzi yaliyotolewa na Jaji Feleshi kwenye kesi iliyofunguliwa na Ado Shaibu akipinga uteuzi wa mwanasheria mkuu wa serikali kuteuliwa kimakosa na Rais Magufuli na kesi iliondolewa.

Mahakama kuu iliamuru Fatma apelekwe kamati ya maadili ya mawakili kwa kosa la kushambulia ofisi ya mwanasheria mkuu ambae ndiye alikuwa wakili wa Ado Shaibu katika kesi hiyo.

Pia, soma=> Fatma Karume asimamishwa kufanya kazi za Uwakili

===
Akijibu hoja ya mdau kwenye mtandao wa twitter aliyemuomba akate rufaa dhidi ya uamuzi huo, Fatma amesema hatafanya hivyo kwa maelezo kwamba muamuzi wa rufaa yake sio huru.

"Ukiingia kwenye mapambano unahitaji kujua nani unapambana nae, kanuni za mpambano na uhuru wa muamuzi. Iwapo kanuni haziko wazi na muamuzi hayuko huru, huo sio mpambano bali upotevu wa muda. Hifadhi nguvu zako kwa mpambano unaoweza kushinda". Yalinukuliwa majibu ya Fatma Karume.
Tuko wapi "Uhuru na Haki"?
 
Kila anae ongea ukweli CCM lazima wamfanyie figisu ili aharibikiwe. Huyu mama kosa lake lilikua ni kutetea na kuongea maovu yanayofanywa na serikali.

Lissu asiposhinda uchaguzi huu, basi na yeye atafanyiwa figisu ili aondolewe kwenye Advocate Roll. Ila Tundu Lissu akiwa Rais basi Fatma Karume atakuwa Waziri Wa Sheria au Mwanasheria Mkuu Wa Serikali (Hapa ndio mahakama na wanasheria wanaotumikia na kuwaabudu CCM watakapo juta).
Natamani Mungu atusaidie watz hili litokee yaani Lissu awe rais wa Jamhuri ya Tanzania tutakuwa tumepata uhuru wa kweli
 
Kosa lake ni kumshambulia Mwanasheria Mkuu wa serikali kuwa hana sifa hiyo na kwamba Rais alikosea kumteua.
Sio uongo mbona yule jamaa anapwaya kweny ile nafasi alowekwa
 
Kama hii sheria / kosa la kushambulia ofisi ya mwanasheria mkuu ipo basi haifai na ifutwe..., haya mambo ya kusema taasisi fulani / watu fulani hawawezi kushambuliwa au kukosolewa ni nzuri mpaka pale taasisi hizo zinapokosea au kufanya makosa...., sasa hapo ni nani wa kuwashambulia na kuwakosoa?
Hao ni miungu watu utawasemaje mkuu hawaguswi hao
 
Back
Top Bottom