Ujinga huu sijui barca utaisha lini?. Thomas Lemar yuko poa tu kwa sababu Coutihno inaonekana hatutampata alafu atasababisha tukose hata kusajili wengine kwani muda utatuishia.
Tulikuwa tumeshaelekea kupata wachezaji wazuri tu hako nyuma kama vile Jean Michael Seri na Martinez, kwakua uongozi hauna msimamo eti baadae ukagaili.
Sasa dirisha linaenda kufungwa usiku wa Leo alafu eti bado Coutihno ni kipaumbele namba1!!!. Kama uongozi ulitakiwa ujiwekee kikomo (deadline) cha kutaka kumsajili kabla ya dirisha kufungwa then baada ya hapo tungehamishia nguvu za kusajili wachezaji wengine sehemu zingine.
Tutabaki na timu legelege na kuungaunga kama msimu uliopita hasa kwa kukosa mbadala wa Xavi na Iniesta. Bad enough tumekuwa na bench (sub) bovu/lisiloaminika kiasi ambacho hatukuwa hivo huko nyuma. Tumebahatika kupata mbadala wa Dani Alves (Semedo) na Neymar (Dembele) hata kama hawataonesha uwezo mkubwa kwa sasa lakini watakuwa vizuri zaidi kadiri muda unavoenda.
"Life+time"....
Sent using
Jamii Forums mobile app