Mkuu Black, suala la Messi kuondoka Barca sio la leo wala kesho. Messi angeweza kuondoka kipindi ambacho alizinguana na Luis Enrique ila kwa sasa haiwezekani, Messi akacheze EPL!!?? Impossible.
Mimi Neymar namkubali mno na namuona ndie Wing ya kushoto bora zaidi duniani, kama unaangalia vema mpira utagundua Neymar anakokota sana mpira kama Messi hayupo au endapo timu ina defence kali kama Madrids n.k
Angalia Classico iliyopita ambayo tulipigwa 2-1, Messi hakuweza kufurukuta sana upande wa kulia, ikabidi Neymar atembee kushoto. Tukubali kuwa Neymar kudribble anaweza na ni mzuri sehemu hiyo, tatizo lake ni nguvu miguuni.
Kubwa zaidi kuhusu Neymar ni fundi wa kuweka mpira wavuni, iwe faul au kawaida. Akipata chance nzuri hakuachi, sio kama halima benzema wa Madrid.