Fedha haiwezi kununua vitu hivi

Fedha haiwezi kununua vitu hivi

Joined
Jul 31, 2022
Posts
45
Reaction score
98
1. Muda. Pesa haiwezi kununua muda uliopoteza.

2. Uzoefu wa kihisia.(Furaha,huzuni,vifijo, nderemo,shangwe,hofu, ukumbusho)

3. Muunganiko wa kweli-Watu wanaokujali au kukukubali pasipo fidia ya chochote.

4. Afya. Unaweza kwenda kwa madaktari bingwa na wazuri lakini juhudi zako binafsi pekee ndizo zitakazo amua hali afya yako.

5.Hekima. Hii unajifunza kwa maisha yako yote.Hekima haziuzwi.

6.Shukrani-Shukrani ya kufurahia na kuenjoy vitu vidogo vidogo, haziuzwi.

7.Ukarimu-kumsaidia mtu mwitaji pasipo kutegemea chochote toka kwake.

8.Mtizamo wako-kuwa mtu unayeweza kuwaza njia za kutengeneza pesa.

9. Kujipenda. Hakuna kiasi cha pesa kitakachokufanya kukipenda kwani kujipenda huanzia ndani.

10.Usalama-Fedha hununua ulinzi na lakini haiwezi kununua uhakika wa usalama wako.

Asante kwa kusoma.

Je ,ni vitu gani vingine ambavyo kimsingi fedha haiwezi kununua......?
 
Siyo kweli, mkuu. Pesa inakupa opportunities zinazokufanya upate na kufurahia hivyo vitu vyote na zaidi! Pesa ina nafasi na heshima yake.
 
.
FB_IMG_16608026153791746.jpg
 
Huko nyuma jamii nyingi ziliweza kuishi bila hela, walikula walicholima na kufuga
 
Back
Top Bottom