Felchesmi Mramba: Bwawa la JNHPP ni mara 10 ya bwawa la Kidatu lililojengwa kwa miaka 5

Felchesmi Mramba: Bwawa la JNHPP ni mara 10 ya bwawa la Kidatu lililojengwa kwa miaka 5

unataka Mama akope matrillion? Nimeeleza hapo juu unaweza kopa unavyotaka tatizo miaka 10 ijayo utakua na madeni yaliyo zaidi ya Pato la taifa mtaanza tena kumlaumu ukopaji awamu ya 6? Je unadhani ni sustainable kukopa zaidi ya trillion 20+ ndani ya miaka 10 kwa ajili ya Miradi miwili tu? Hapo Bado tuna Mradi wa zaidi ya trillion 20 wa kuvuna gesi huko Lindi.


Upigaji unakujaje sasa? Kwanini wasihujumu Bomba la gesi maana ndio umeme ni 60% unategemea gesi? Yaani wahujumu 40% itasaidia nini? Kwanini tunapenda conspiracy theories? CCM ni majizi najua ila eti hawataki kukamilisha ujenzi eti Ili watoe mikataba kwa makampuni ya kufua umeme mbona haiingii akilini? Kwanini usiseme haukamiliki sababu wanakula Hela za Mradi?? It makes more sense. Yaani wasile matrillion ya Nyerere Dam ila waje kugawana billion vichache vya PAP??

Issue ni uthubutu au matokeo? Kwahiyo Mama akikopa ajenge daraja kutokea Bagamoyo hadi Zanzibar mtamsifia sababu ya uthubutu pekee?? Dodoma hata airport haijajengwa Bado, ring roads hamna then unasema IMEKAMILIKA? Hivi kwanini nchi tunakosa vipaumbele wamehamia dodoma so what? Kuhamia dodoma Kuna umuhimu kuliko SGR au Nyerere Dam? Hayo Matrillion yaliyotumika kuhamia Dodoma si yangetumika kukamilisha kipande Cha Moro-Dom.

Let's be serious kama taifa
Halafu hata kuhamia kwenyewe Dodoma hakujakamilika. Ofisi ndiyo kwanza zinajengwa Mtumba.
 
Hawa watu magufuli aliwafukuza sasa samia kawarudisha wanajipanga kuhujumu kukamilika bwawa la nyerere ili waweze kuleta agenda zao za kuiba hela ya umma kwa kupendekeza dili zao za nishati mbadala.
Ratiba ya kumalizika ujenzi haikua imetayarishwa kwa kubahatisha. Tusisahau huyu mramba ni yule magufuli alimtimua kwa kuja na mpango kupandisha bei ya umeme na pia kushirikiana na wengine kuiongezea mkataba kampuni ya iptl kinyume na mpango wa kampuni hiyo kukabidhi mitambo yake tanesco baada ya mkataba wake kumalizika. Agizo la msgufuli lilikua kupunguzwa bei ya umeme kwa siku zijazo sio kuongeza.
Awamu hii ya mama samia imetekwa na wafanyabiashara ambao wanatanguliza maslahi yao binafsi. Bila shaka samia mwenyewe au familia yake ni wafanyabiashara wenye maslahi binafsi.
Kila siku muko kwenye suspicions tu, labda tupate malaika kutoka mbinguni maana kwa duniani hakuna mkamilifu.
 
1.Kikwete aliacha deni ni trillion 35 so whatever limeongezeka ni la JPM Kiufupi Ame double deni la taifa in less than 6 years!!!

2. Madeni ya private sector hayapo kwenye deni la taifa. Deni la ndani ni kama trillion 20, deni la nje ni zaidi ya trillion 40!! So serikali inadaiwa trillion zaidi ya 60.

3. Unadai madeni/mikopo ya watangulizi. Kama mlirithi Miradi kama Kuhamisha maji ya ziwa Victoria, Upanuzi wa airport, lami nchi nzima, Bomba la gesi na Kinyerezi 1 and 2, mwendokasi n.k basi muwe tayari kurithi na madeni sio mafanikio mnajifanya kuchukua credit afu madeni mnajifanya lawama ni kwa awamu zilizopita.

4.kumbe mnatambua mabadiliko ya thamani ya fedha na inflation? Mbona mlikua mnajisifia mara sijui bajeti imepanda kuliko awamu zote, mara Miradi inayojengwa imezidi uwekezaji wa awamu zote, makusanyo ya TRA yamezidi awamu zote n.k kwani mlikua hamjui kwamba thamani ya pesa enzi za JK au Mwinyi ni tofauti na sasa?? Acheni unafiki aisee.

5. Aliwaletea maji lakini haibadili ukweli kwamba alikopa sana hivyo inaua sustainability ya uchumi wetu maana makusanyo yanaishia kulipa mishahara na riba za madeni. So msijifiche kwenye maji kujustify mikopo ya trillion 30 ambayo mlidai ni pesa za ndani kumbe mnakopa!!!
Nakubaliana na ww kwenye vingi hapo ulivyonadika ila
Katika kitu ambacho nimeona wengi wanakikosea ni kuhusu deni la taifa na nani sijui alikopa sana.
Mwaka Jana niliona gazeti la jamhuri tena likiandikwa na mkongwe kabisa deodatus balile anasema Magufuli aliacha deni la taifa likiwa trillion 78.
Ilikua ni ajabu kwa mtu kama balile kuweka taarifa ile.
 
1.Kikwete aliacha deni ni trillion 35 so whatever limeongezeka ni la JPM Kiufupi Ame double deni la taifa in less than 6 years!!!

2. Madeni ya private sector hayapo kwenye deni la taifa. Deni la ndani ni kama trillion 20, deni la nje ni zaidi ya trillion 40!! So serikali inadaiwa trillion zaidi ya 60.

3. Unadai madeni/mikopo ya watangulizi. Kama mlirithi Miradi kama Kuhamisha maji ya ziwa Victoria, Upanuzi wa airport, lami nchi nzima, Bomba la gesi na Kinyerezi 1 and 2, mwendokasi n.k basi muwe tayari kurithi na madeni sio mafanikio mnajifanya kuchukua credit afu madeni mnajifanya lawama ni kwa awamu zilizopita.

4.kumbe mnatambua mabadiliko ya thamani ya fedha na inflation? Mbona mlikua mnajisifia mara sijui bajeti imepanda kuliko awamu zote, mara Miradi inayojengwa imezidi uwekezaji wa awamu zote, makusanyo ya TRA yamezidi awamu zote n.k kwani mlikua hamjui kwamba thamani ya pesa enzi za JK au Mwinyi ni tofauti na sasa?? Acheni unafiki aisee.

5. Aliwaletea maji lakini haibadili ukweli kwamba alikopa sana hivyo inaua sustainability ya uchumi wetu maana makusanyo yanaishia kulipa mishahara na riba za madeni. So msijifiche kwenye maji kujustify mikopo ya trillion 30 ambayo mlidai ni pesa za ndani kumbe mnakopa!!!
JK aliacha deni la $42 billion tafuta facts sahihi.

Magufuli alilipunguza mpaka $37 billion na kuli maintain hapo anachukua kwa mkono mmoja analipa kwa mkono mwingine; mpaka alipofariki. Ndio maana nchi ikatolewa kwenye ‘moderate risk, aliyoikuta Magufuli na kuwekwa kwenye ‘low risk’ borrowers.

Deni limeanza kupanda tena na Samia hadi kurudishwa tena kwenye ‘moderate risk’ of defaulting, majuzi tu.

Muwe mntafuta facts za third parties zinazotumiwa sokoni kuangalia debt sustainability za nchi sio porojo za Zitto Kabwe Twitter.
 
JK aliacha deni la $42 billion tafuta facts sahihi.
Acha uongo mkuu, unajua hii ni zaidi ya trillion 100!! Hivi upotoshaji huu ni kwa faida ya nani? Ni lini deni la taifa limewahi fika $42 Billion??
 
JK aliacha deni la $42 billion tafuta facts sahihi.

Magufuli alilipunguza mpaka $37 billion na kuli maintain hapo anachukua kwa mkono mmoja analipa kwa mkono mwingine; mpaka alipofariki. Ndio maana nchi ikatolewa kwenye ‘moderate risk, aliyoikuta Magufuli na kuwekwa kwenye ‘low risk’ borrowers.

Deni limeanza kupanda tena na Samia hadi kurudishwa tena kwenye ‘moderate risk’ of defaulting, majuzi tu.

Muwe mntafuta facts za third parties zinazotumiwa sokoni kuangalia debt sustainability za nchi sio porojo za Zitto Kabwe Twitter.
Debt sustainability inapimwa kwa Debt as percentage of GDP. So hata udaiwe kama ni taifa maskini ila deni lipo chini ya 50% utakopesheka among other factors of course. So maybe useme JPM alipandisha GDP ila kusema alishusha deni unapotosha mnoo.

Screenshot_20220531_132829.jpg
Screenshot_20220531_135551.jpg
 
Let's be serious kama taifa
Mkuu 'Zitto Jr.' hakuna wakati ambao sijawahi kuwa 'serious' ninapojadili mambo yanayohusu waTanzania na nchi yao. Nimeona hili nilitoe mwanzo kabisa; na wakati mara nyingi nikwa nathamini michango yako humu JF, kuwa mmoja wa watu ninaowasoma kwa makini hata kama sikubaliani na baadhi ya unayoandika. be certain that I am very serious when it comes to the welfare of Tanzania and its people. Never doubt that again.
Sina msukumo wa kufaidika kwa njia yoyote juu ya msimamo huu.
Issue ni uthubutu au matokeo?
Kwani bado unamashaka na matokeo ya kuhamia Dodoma? That's fait accompli!
Kuna mambo mengi sana niliyochukizwa na tabia za Magufuli, lakini yapo pia mengine ambayo natamani angeishia kuyafanya bila ya hayo mabovu yaliyoharibu uongozi wake.

"Uthubutu" ni moja ya sifa muhimu sana kwa kiongozi yeyote, hasa kama akiwa 'decisive' katika kufanya maamuzi yake. Mabadiliko ya nchi yoyote hutokana na viongozi wenye uthubutu.

Kwa bahati mbaya sana uthubutu wa Magufuli ulichanganyika na ukichaa wakati mwingine; mfano, ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa kijijini kwake!
Dodoma hata airport haijajengwa Bado, ring roads hamna then unasema IMEKAMILIKA? Hivi kwanini nchi tunakosa vipaumbele wamehamia dodoma so what? Kuhamia dodoma Kuna umuhimu kuliko SGR au Nyerere Dam? Hayo Matrillion yaliyotumika kuhamia Dodoma si yangetumika kukamilisha kipande Cha Moro-Dom.
Haya mengine uliyoongeza huku sioni mantiki yake na sina haja ya kuyajibu..., utasubiri umalize kila kitu kwenye jambo moja ndio ufanye lingine? Kama nchi utawezaje kuiendesha namna hiyo!
Upigaji unakujaje sasa? Kwanini wasihujumu Bomba la gesi maana ndio umeme ni 60% unategemea gesi? Yaani wahujumu 40% itasaidia nini? Kwanini tunapenda conspiracy theories? CCM ni majizi najua ila eti hawataki kukamilisha ujenzi eti Ili watoe mikataba kwa makampuni ya kufua umeme mbona haiingii akilini? Kwanini usiseme haukamiliki sababu wanakula Hela za Mradi?? It makes more sense. Yaani wasile matrillion ya Nyerere Dam ila waje kugawana billion vichache vya PAP??
Leo umeamka vibaya, au umekwishaingizwa kichwa kichwa. Watu hawachelewi kugeuka magunia ya chumvi nchi hii.

Kukopa (madeni) siyo dhambi, mradi hela inayokopwa inafanya kazi iliyolengwa. Ni nchi gani isiyokopa kwa shughuli zake mbalimbali?

All in all, sijaona hoja ya kujadili katika majibu yako yote katika mjadala huu. Sitahangaika na hayo mengine.
 
Debt sustainability inapimwa kwa Debt as percentage of GDP. So hata udaiwe kama ni taifa maskini ila deni lipo chini ya 50% utakopesheka among other factors of course. So maybe useme JPM alipandisha GDP ila kusema alishusha deni unapotosha mnoo.

View attachment 2245670View attachment 2245671

Nenda sasa kasome full original report source ya huyo mwandishi ata kwenywe website ya World Bank. Mimi nakuwekea tu sehemu ya extracts.

94A4AD4D-388B-4CEB-940D-9BFEC4B32416.jpeg


Ni hivi Magufuli alikuta deni kubwa la JK alikuwa anaalishusha miaka yote toka aingie madarakani kila mwaka.

Ndio sababu ya nchi kutolewa kuwa moderate risk defaulters hadi kuwa ‘low risk’ defaulters na kuachiwa kukopa private banks.

Mwambie Samia akakope bank nje ya nchi kama atapewa mkopo sasa hivi wakati nchi imeondolewa hadhi ya low risk.

Halafu debt sustainability aingalii GDP tu kuna vitu vingi vya mapato ya serikali pia yanazingatiwa kama amount ya malipo, inflation, rates (nominal and interests), na mambo mengine ya risks assessment za finance.

Magufuli aliikuta nchi ipo kwenye moderate risks kwa zaidi ya miaka 10 kwa lugha nyingine kipindi chote cha uraisi wa J.K akaishusha mpaka low risk.

Hakuna mtu aliekopa Tanzania kwa haraka na huku akishindwa kulipa madeni yake na kuicha nchi pabaya kama Jakaya Kikwete soma hiyo report yote vizuri.

Hawa watu waliopo sasa hivi serikalini ni genge la wahuni tu wazushi na waongo.
 
Serikali kuhamia Dodoma kumekuwa na faida gani kwa nchi? Zingatia kwamba magogoni shughuli nyingi zimekuwa zikiendelea huko na mawaziri wanafanyia mikutano yao mikoa mbalimbali ya nchi.
Katibu mkuu hajaeleza hayo unayoeleza wewe, na ningetegemea kuwa anao uwezo mzuri kabisa wa kuelezea hayo kwa ufasaha mkubwa na akaeleweka.

Kuna shida gani kwa serikali hii iliyopo sasa kukaa chini na kuchambua miradi yote hiyo na kuona uwezo uliopo na kinachowezekana kufanyika halafu wakaelezea hali halisi ilivyo kwa wananchi!

Lakini ngoja nikuache na hili wazo: pamoja na 'ukichaa' mwingi aliokuwa nao Magufuli, upande ambao unabaki kuwa sifa kubwa kwake ni hiyo 'daring', hata kama ilikuwa ni ya pupa bila kutumia akili. Na nadhani, huku kuliliwa na wengi licha ya tabia zake mbaya inatokana na huo uthubutu wake.

Kuna kosa gani hata kama ni kukopa kukamilisha mradi muhimu kabisa kama Bwawa la Mwalimu Nyerere!

Haya yote wanayofanya hawa waliopo sasa ni kinyume kabisa, na ni dhahiri sasa wanategeshea kuingiza upigaji kwenye miradi mingi. Kazi kubwa inayokuja ni kutafuta na kuwatumia wapigaji tu waje hapa kutunyonga, hiyo ndiyo mikakati yao wanayoiweka mbelke.

Umezungumzia Dodoma mahali..., hiyo ni aina ya uthubutu ambayo imempambanua huyu kichaa aliyetokea kuwepo wakati huo, na hili kiukweli kalimaliza. Hutegemei tena serikali kurudi Dares Salaam hata wafanye nini hawa mashetani waliopo sasa hivi.
 
Kama kulikuwa na ulazima mkubwa hivyo wa kujenga hilo bwawa na kuachana na gesi basi angemaliza kwanza bwawa kabla ya kuanza SGR na serikali kuhamia Dodoma.
Pamoja na madhiafu ya jiwe, Ila ni lazima tukubali ni lini tulipaswa kuwa na miradi ya aina hiyo?
Tuna mradi wa kuzalisha umeme wa gesi, Ila tunanunua gesi kutoka kwa mwekezaji ili tuzalishe umeme. Mwekezaji siku akiamua kupandisha bei utafanyaje?

Tanesco tumewahi kupoteza mabilion ya pesa kupitia iptl, escrow, symbion, Richmond, Dowans n.k hizo pesa zote zilizopita huko zilitosha kuwa na mradi wetu wa kujitegemea.

Au Ilipaswa tuendelee tu na hao akina symbion na Dowans?
 
Huelewei uchumi wa kati tulifikaje, wewe ndio akili kisoda.
Sema walioachiwa ndo hawana akili. Boss aliipeleka nchi uchumi wa kati ndani ya muda mfupi, niamini mimi angeliendelea kuwepo ingekamilika ndani ya muda wake. Waliobakia ndo AKILI KISODA KUMUDU HEKAHEKA HIZO.
 
Hakuna tatizo lolote kununua gesi yetu kutoka kwa mwekezaji ikiwa ni rahisi kuliko gesi kutoka nje na mwekezaji analipa kodi, anatoa ajira na angesababisha ukanda wa kusini kushamiri ajira.
Ni lazima tutoke hapa. Tuna gesi mtwara, Ila tunaambiwa hatuna uwezo wa kuchimba(ni kweli) hivyo wawekekezaji watakaofanya exploration na kuchimba ndio tutanunua kwao.
Japo mm siamini kama pesa hatuna, Bali tuna vipaumbele vya ajabu tu. Trillion 70 tukiamua kuitafuta ndani ya miaka mitano tunaipata au tungeshaipata na tungekuwa na mradi wetu wenyewe wa kuchimba gesi.
Kwani waarabu wao waliwezaje kwenye mafuta na gesi hadi wakafaidika? Leo tunakubali kukabidhi mradi mkubwa Kama huo kwa wawekezaji ambapo tutachukua miaka mingi sana kuwategemea. Huku bado tuna mentality kwamba hatuwezi
Tumelaaniwa
 
Serikali kuhamia Dodoma kumekuwa na faida gani kwa nchi? Zingatia kwamba magogoni shughuli nyingi zimekuwa zikiendelea huko na mawaziri wanafanyia mikutano yao mikoa mbalimbali ya nchi.
Kuwe au kusiwe na faida hilo ni jambo tofauti wakati huu, lakini ukweli ni kwamba serikali imeshahamia Dodoma.

Kama Samia au kiongozi mwingine yeyote akitaka kuirudisha Dar es Salaam, hapo itabidi afikiri mara mbili mbili juu ya 'implication' ya tendo hilo.

Lakini hili la "faida", kwani uamzi wa kuhamia huko umeanza jana au juzi? Hili lilishakuwa limeamriwa toka siku nyingi, lilisubiri tu utekelezaji, hadi alipotokea kichaa mmoja akafanya kweli!

Kwa hiyo mjadala wa faida hilo ni swala tofauti kabisa.
 
Siasa za maskini kujitegemea wenyewe kuleta maendeleo ni porojo tu. Yeye mwenyewe alikuwa anakopa na kuchukua misaada kutoka kwa aliowaita mabeberu.
JPM namkubali kwenye mambo mawili tu.
Mosi,alikuwa na nia njema ya kuhakikisha hii nchi inapiga hatua kubwa kimaendeleo.
Pili,ni ile kutaka kutujenga Watanzania tujitegemee wenyewe kuleta maendeleo yetu, kwani hakuna shangazi wala mjomba wa kutupa maendekeo.
Tatizo lake ni kujiona kuwa yeye ni mwenye akili kuliko Watanzania wote hivyo kutotaka kusikia na kufuata ushauri wa wengine hasa wataalamu na washauri/wasaidizi wake, kisa tu kawa rais, wakati kumbe ni "below average".
 
Back
Top Bottom