Felchesmi Mramba: Bwawa la JNHPP ni mara 10 ya bwawa la Kidatu lililojengwa kwa miaka 5

Felchesmi Mramba: Bwawa la JNHPP ni mara 10 ya bwawa la Kidatu lililojengwa kwa miaka 5

Mkuu umenena,Mabwawa yamejengwa mengi Kidatu,Nyumba ya Mungu,Mtera,Pangani, bila mbwembwe na porojo za kisiasa.
Transparency ilikosekana katika kuwatafuta wakandarasi wa mradi wa bwawa la Nyerere.
Tumeona hata Tanroad anafanya kazi iliomzidi kimo.
Arab contractors ndie main contractor,inamilikiwa na jeshi la Misri haijaonyesha makali ya kazi,sana sana ni doctorate degrees,bilateral relationship ndio hadithi zisizohuzika kwenye mradi wenyewe.
Lakini kwa ndani Waziri Mkuu Majaliwa alietembelea huo mradi mara kwa mara alionekana kutilia shaka utekelezaji wa mradi.
Anapokuja katibu mkuu akasema anajali Safety kwanza katika utekelezaji wa mradi sio maneno ya kupuuzia.
Kuna uwezekano wa kubadiri michoro mara kwa mara ili kwendana na usalama na ubora wa mradi.Kama yapo mambo yalipuuzwa ndio wakati wa kuyaunganisha.Hata lile bwawa maarufu la Ethiopia dam X aka Millennium Dam limefanyiwa mabadiliko mengi mno ili likidhi mahitaji.
Kwenye ujenzi wowote ule hata kibanda umiza marekebisho ni jambo la kawaida na pengine ndiyo sababu Katibu Mkuu akatoa tahadhari na kwamba hakuna makusudi ya kuchelewesha mradi. Hata hivyo taarifa kwamba ujenzi umefikia asilimia 60 inaongeza matumaini. Tuache kuihukumu serikali kwa kuwa makini, tujaribu kuwa na akiba ya maneno.
 
Bwawa la mtera linaingia mara kumi? Mzee unalifahamu bwawa la mtera lakini??
bwawa la mtera linazalisha megawati ngapi na hilo linalojengwa litazalisha megawati ngapi tuanzie hapo kwanza ndo tujue lipi kubwa na linaingia mara ngapi kwa mwenzie
 
Mabwawa ya umeme ya Kidatu, Nyumba ya Mungu, Mtera, Pangani yalimalizwa na waliomtangulia JPM bila mbwembwe na porojo za kisiasa.
Awam8 ya 5 (uwazi) Transparency ulikosekana katika kuwatafuta wakandarasi wa mradi wa bwawa la Nyerere JNHPP a.ka Rufiji Dam .
Tumeona hata Tanroad anafanya kazi iliomzidi kimo.

Viongozi waliopo na wanaokuja, wazingatie hili ulilolitoa kama angalizo.
 
Lakini ngoja nikuache na hili wazo: pamoja na 'ukichaa' mwingi aliokuwa nao Magufuli, upande ambao unabaki kuwa sifa kubwa kwake ni hiyo 'daring', hata kama ilikuwa ni ya pupa bila kutumia akili. Na nadhani, huku kuliliwa na wengi licha ya tabia zake mbaya inatokana na huo uthubutu wake.

unataka Mama akope matrillion? Nimeeleza hapo juu unaweza kopa unavyotaka tatizo miaka 10 ijayo utakua na madeni yaliyo zaidi ya Pato la taifa mtaanza tena kumlaumu ukopaji awamu ya 6? Je unadhani ni sustainable kukopa zaidi ya trillion 20+ ndani ya miaka 10 kwa ajili ya Miradi miwili tu? Hapo Bado tuna Mradi wa zaidi ya trillion 20 wa kuvuna gesi huko Lindi.

Haya yote wanayofanya hawa waliopo sasa ni kinyume kabisa, na ni dhahiri sasa wanategeshea kuingiza upigaji kwenye miradi mingi. Kazi kubwa inayokuja ni kutafuta na kuwatumia wapigaji tu waje hapa kutunyonga, hiyo ndiyo mikakati yao wanayoiweka mbelke.
Upigaji unakujaje sasa? Kwanini wasihujumu Bomba la gesi maana ndio umeme ni 60% unategemea gesi? Yaani wahujumu 40% itasaidia nini? Kwanini tunapenda conspiracy theories? CCM ni majizi najua ila eti hawataki kukamilisha ujenzi eti Ili watoe mikataba kwa makampuni ya kufua umeme mbona haiingii akilini? Kwanini usiseme haukamiliki sababu wanakula Hela za Mradi?? It makes more sense. Yaani wasile matrillion ya Nyerere Dam ila waje kugawana billion vichache vya PAP??
Umezungumzia Dodoma mahali..., hiyo ni aina ya uthubutu ambayo imempambanua huyu kichaa aliyetokea kuwepo wakati huo, na hili kiukweli kalimaliza. Hutegemei tena serikali kurudi Dares Salaam hata wafanye nini hawa mashetani waliopo sasa hivi.
Issue ni uthubutu au matokeo? Kwahiyo Mama akikopa ajenge daraja kutokea Bagamoyo hadi Zanzibar mtamsifia sababu ya uthubutu pekee?? Dodoma hata airport haijajengwa Bado, ring roads hamna then unasema IMEKAMILIKA? Hivi kwanini nchi tunakosa vipaumbele wamehamia dodoma so what? Kuhamia dodoma Kuna umuhimu kuliko SGR au Nyerere Dam? Hayo Matrillion yaliyotumika kuhamia Dodoma si yangetumika kukamilisha kipande Cha Moro-Dom.

Let's be serious kama taifa
 
Yule alikuwa muongo Sana. Pale ubungo hakuna fyover, kile ni kidaraja cha juu. Flyover ni barabara ya juu yenye km 10 au zaidi.
Na alivowabomolea watu vitega uchumi vyao... Tukaoneshwa ramani tofauti kabisa na kilichojengwa!
Mungu alituamulia aisee!!
 
Pamoja na madhiafu ya jiwe, Ila ni lazima tukubali ni lini tulipaswa kuwa na miradi ya aina hiyo?
Tuna mradi wa kuzalisha umeme wa gesi, Ila tunanunua gesi kutoka kwa mwekezaji ili tuzalishe umeme. Mwekezaji siku akiamua kupandisha bei utafanyaje?

Tanesco tumewahi kupoteza mabilion ya pesa kupitia iptl, escrow, symbion, Richmond, Dowans n.k hizo pesa zote zilizopita huko zilitosha kuwa na mradi wetu wa kujitegemea.

Au Ilipaswa tuendelee tu na hao akina symbion na Dowans?
Matatizo tuliyonayo yanahitaji umakini wa wananchi katika kufanya overhaul ya system nzima!
Si mmeona kwa jiwe? Hamjifunzi tu? Ameenda na ukurupukaji wake nao umemfuata!
We need stronger policy systems not individuals!
 
Usilinganishe mradi wa Ethiopia Renaissance Dam na huu wa Tanzania. Ethiopia walipitia kwenye upinzani wa Bwawa kutojengwa kwa muda mrefu. Misri walitishia kupiga bomu huo mradi. Kuna wakati ulisimama.

Vita ya wenyewe kwa wenyewe ilikuwa changa moto kubwa kumaliza mradi kwa wakati. Wakati wa vita ilochukua karibu mwaka na miezi saba.

Kujaza maji kwenye bwawa, Ethiopia inapata mvua mara moja tu kwa mwaka tofauti na Tanzania. Hivyo kujazwa kwa bwawa imechukua muda mrefu zaidi. Mvua Ethiopia unyesha kipindi cha mwezi wa July hadi sept. Kisha hakuna mvua tena mpaka mwaka utaofuata miezi kama hiyo. Hivyo mnakaa mwaka mzima ili kuona mvua tena.

Tusitafute visingizio vya kushindwa kumaliza mradi muda muafaka kwa kujaribu kubalance na miradi mingine. Hivi kweli mkandarasi wa kampuni husika na wataalamu wetu ni wajinga hawakujua kuwa mradi huu wa Nyerere utachukua muda mrefu walipoingia mkataba?

Ati leo ndo Katibu Mkuu aje na hizo sababu? kwa nini kumekuwa na visingizio vingi vikitafutwa, mara winchi ya kunyanyua sijui nini ni ngumu kuipata, mara mvua, ili mradi kutafuta utetezi.

Leo Katibu anafananisha ujenzi wa mabwawa ya Mtera na Nyumba ya Mungu ati yalichukua miaka mingi. Ni ujinga wa kutupwa. Hivi anataka kusema sisi watanzania hatujui kutafakari na niwajinga? Wakati wa ujenzi wa hayo mabwawa technolojia ya wakati huo na sasa ilikuwa tofauti.

Hata kiwango cha uchumi wakati huo na sasa vilikuwa tofauti.

Na kwanini Tanzania tunapenda kutetea na kuhidhinisha matatizo kwa kutafuta sababu ili tu kuwadanganya wananchi. Kwanini tusiwe wakweli.

Katika Tanzania wanasiasa ndo wasemaji wakuu hata katika mambo ya kisayansi. Pia kwa kutafuta ulaji wanasayansi na wataalamu wetu wanaweka ujuzi na utaalamu wao pembeni ili tu kuwafurahisha wanasiasa.

Hata wanahabari, sijaona alie jitokeza kuleta habari toka pande zote. Mfano kuhoji kampuni ya ujenzi wa bwawa. Kumhoji mtaalamu wa serikali msimamizi wa mradi. Na pia kuhoji wataalamu kadhaa wa mambo ya ujenzi wa umeme nchini na hata nje. Kuhoji viongozi wa serikali iliyopita na wasiasa kwa nini tuliaminishwa vingine na leo tunaaminishwa vingine. Walau tukawa na habari yenye ulalo wa ukweli.

Sijawahi kuona nchi yenye ushabiki wa ovyo usioangalia maslahi mapana ya nchi. Watanzania tunajisifia sana kuwa tumeendelea kielimu na mengineyo lakini tu kama makondoo. Tunapelekeshwa tu na kupokea kisha kushangilia kila litakalosemwa.

Maswali ya waandishi wa habari wa Tanzania mengi ni yakujipendekeza. Kujichekesha. Hatuna waandishi wenye maswali ya kufikirisha, maswali ya mitego au hata ya kukera tu. Waandishi wanauliza swali unaona huyu anajiuma uma, hawajiamini. Natamani ningekuwa mwandishi wa habari!
All in all... JNHP is a mega project. It will take a while and cycles or do undo to finalize and commission!
 
Katibu mkuu wizara ya Nishati ndg. Felchesmi Mramba amesema bwawa la Julius Nyerere halitakamilika hivi karibuni kama ilivyoaminishwa na baadhi ya wanasiasa.

Amesema bwawa hilo ni kubwa sana hivyo usalama wake unapaswa kuzingatiwa ktk hatua zote za ujenzi wake.

Ametolea mfano kuwa mabwawa ya Mtera, Kidatu na Kihansi ambayo ukubwa wake kila moja ni madogo mara kumi ya lile la Nyerere yalijegwa kwa miaka 5 kila moja.

Ameongeza kuwa bwawa la Nyumba ya Mungu lilijengwa kwa zaidi ya miaka 5.

Source: ITV (Kipindi Maalum).

View attachment 2244046
Hawa watu magufuli aliwafukuza sasa samia kawarudisha wanajipanga kuhujumu kukamilika bwawa la nyerere ili waweze kuleta agenda zao za kuiba hela ya umma kwa kupendekeza dili zao za nishati mbadala.
Ratiba ya kumalizika ujenzi haikua imetayarishwa kwa kubahatisha. Tusisahau huyu mramba ni yule magufuli alimtimua kwa kuja na mpango kupandisha bei ya umeme na pia kushirikiana na wengine kuiongezea mkataba kampuni ya iptl kinyume na mpango wa kampuni hiyo kukabidhi mitambo yake tanesco baada ya mkataba wake kumalizika. Agizo la msgufuli lilikua kupunguzwa bei ya umeme kwa siku zijazo sio kuongeza.
Awamu hii ya mama samia imetekwa na wafanyabiashara ambao wanatanguliza maslahi yao binafsi. Bila shaka samia mwenyewe au familia yake ni wafanyabiashara wenye maslahi binafsi.
 
La ethipia sidhani kama project nzima imeisha .. nafikiri ndo kwanza wamejaza maji awamu ya kwanza na inaweza chukua zaidi ya 3 yrs . Hizi project si mchezo. Kujaza maji tu ni miaka achana na kujanga
Bora wewe umejielekeza vyema. Pro JPM wana macho lakini ni vipofu...hawaoni! Wana akili lakini hawazitumii ipasavyo!
Wanapaswa wajue kuwa miradi mikubwa ya umeme wa maji ni hatari zaidi kuliko comfort ya kubofya switch ya umeme.
Mradi ukikamilika sijui maji watayapata wapi kutosha kujaza bwawa ukizingatia kuwa upstream kwenye mito na vijito tayari kina ni changamoto. Na je wakiyaelekeza maji bwawani... national food basket - the Rufiji basin maisha yatakuwaje? Tayari ni magumu within Great Ruaha River ecosystem bila bwawa. Je, bwawa likiwepo maji yatatosheleza mahitaji?
Na kutokana na haya mabadiliko ya tabianchi... ipo siku kutatokea mafuriko ya hatari... watalazimika kufungulia JNHP kuruhusu free flow ya maji... Sasa sijuhi watu wa down stream kama watabaki salama!

Nilimuelewa sana Dr. Slaa... kwamba JPM alijua hana muda mrefu kwa hiyo alijicommit kufanya vitu vingi kwa haraka kusaka legacy. Lakini vingi alivyofanya ni mzigo kwa taifa!
 
Kwani hizo trilioni 78 kakopa zote yeye?kwanza hili sio deni sahili, deni sahini ni 64Tirioni hizo 78 sijui umezitoa wapi.
Weka deni lake yy km yy without
1. Including la private sector(maana unapozungumzia deni la taifa lina include both private and public),
2. Madeni ya watangulizi wake,
3. then toa madeni yaliyoiva kipindi chake(accumulative interest)
3. Toa inflation
4. Ondoa kushuka thamani kwa Shillingi yetu against dola.

Km ww hakufanikiwa kubadili maisha yako ni ww sisi wa gomz aliyabadili, kipindi chake tulipata barabara za mtaani na maji ya dawaso(kutoka kununua maji ya visima kwa tank kwa 300k mpaka buku 4 mia nae) and kupata hati within a month After 30yrs of waiting na kuzungushwa tangu tuhamie huko.
so we greatefull ht kwa hicho kidogo alichotufanzia wana gomz.
Kwani hizo trilioni 78 kakopa zote yeye?kwanza hili sio deni sahili, deni sahini ni 64Tirioni hizo 78 sijui umezitoa wapi.
Weka deni lake yy km yy without
1. Including la private sector(maana unapozungumzia deni la taifa lina include both private and public),
2. Madeni ya watangulizi wake,
3. then toa madeni yaliyoiva kipindi chake(accumulative interest)
3. Toa inflation
4. Ondoa kushuka thamani kwa Shillingi yetu against dola.

Km ww hakufanikiwa kubadili maisha yako ni ww sisi wa gomz aliyabadili, kipindi chake tulipata barabara za mtaani na maji ya dawaso(kutoka kununua maji ya visima kwa tank kwa 300k mpaka buku 4 mia nae) and kupata hati within a month After 30yrs of waiting na kuzungushwa tangu tuhamie huko.
so we greatefull ht kwa hicho kidogo alichotufanzia wana gomz.
1.Kikwete aliacha deni ni trillion 35 so whatever limeongezeka ni la JPM Kiufupi Ame double deni la taifa in less than 6 years!!!

2. Madeni ya private sector hayapo kwenye deni la taifa. Deni la ndani ni kama trillion 20, deni la nje ni zaidi ya trillion 40!! So serikali inadaiwa trillion zaidi ya 60.

3. Unadai madeni/mikopo ya watangulizi. Kama mlirithi Miradi kama Kuhamisha maji ya ziwa Victoria, Upanuzi wa airport, lami nchi nzima, Bomba la gesi na Kinyerezi 1 and 2, mwendokasi n.k basi muwe tayari kurithi na madeni sio mafanikio mnajifanya kuchukua credit afu madeni mnajifanya lawama ni kwa awamu zilizopita.

4.kumbe mnatambua mabadiliko ya thamani ya fedha na inflation? Mbona mlikua mnajisifia mara sijui bajeti imepanda kuliko awamu zote, mara Miradi inayojengwa imezidi uwekezaji wa awamu zote, makusanyo ya TRA yamezidi awamu zote n.k kwani mlikua hamjui kwamba thamani ya pesa enzi za JK au Mwinyi ni tofauti na sasa?? Acheni unafiki aisee.

5. Aliwaletea maji lakini haibadili ukweli kwamba alikopa sana hivyo inaua sustainability ya uchumi wetu maana makusanyo yanaishia kulipa mishahara na riba za madeni. So msijifiche kwenye maji kujustify mikopo ya trillion 30 ambayo mlidai ni pesa za ndani kumbe mnakopa!!!
 
Hapa mchezo huko hivi; pesa tuongeze kwenye mishahara na marupurupu mengine, pia tukamirishe miundo mingine ili tuoneka tunapiga kazi!
Lakini kiukweli watu kufanya kazi kwa ajiri ya vizazi vijavyo hatuna mtizamo huo!
Huyu anayesema bwawa dogo lilitengenezwa ndani ya miaka mitano, hili kubwa haiwezekani likatengenezwa kwa muda mfupi! Ni mwongo sana huyu
 
Wafuasi mna imani sana. Hapa sio mambo ya emotional mkuu ni swala la mpunga na kutumia akili.

Mtaani watu kama jpm wapo wengi sana. Akipata kidogo tu anaamini anaweza kufanya kila kitu kwa hicho hicho kidogo mwisho wa siku anapitia wakati mgumu sana mambo yoote yanakwama.

Mfano kama angeanzisha Bwawa pekee sasa hivi tungekuwa tunasubiri Ufunguzi tu. One at a time.
Hakuna cha ufuasi, hapa ni usimamizi na kukitumia vizuri kinachopatikana, akili zetu ni mgando na kuaminishwa kuwa vitu fulanifulani mpaka wajomba watusaidie
 
Back
Top Bottom