Felchesmi Mramba: Bwawa la JNHPP ni mara 10 ya bwawa la Kidatu lililojengwa kwa miaka 5

Felchesmi Mramba: Bwawa la JNHPP ni mara 10 ya bwawa la Kidatu lililojengwa kwa miaka 5

Usibishane na mimi. Bishana na katibu mkuu wa wizara ya Nishati ndugu Mramba.
Tena Ni professional Engineer. Jamani haya ni mambo ya kitalaam. Mwenye hoja naye apinge kitaalam. Japo wengine tungependa kujua kwa faida yetu tu kwani tuko chuoni. Hivi teknolojia ya ujenzi wa mabwawa ya umeme ya1970-80 ndo inatumika mpaka sasa??
 
Jamaa alikuwa na ambitions za hatari ila kwenye kuzitekeleza ikawa ndio mtihani
Kuna msemo wa kibeberu unasema Go big or go home...
only doers understand the true meaning ya huo msemo, and JPM was one of them.
 
Usisahu Ethiopia Dam ni mara 3 ya JNHP...sis megawat 2145 wao ni elfu 6+.. huwezi ukalijenga at the same pace...km wao lilichukua 10yrs then ukigawa kwa 3 then 3 yrs ni muda sahihi kabisa...Hizi mbona hesabu za darasa la 7 aisee...[emoji1787][emoji1787]
Sasa mbona it is almost 5yrs na mradi wa JNHP haujaisha. Si kila kitu kinahitaji hesabu za magazijuto au kurahisisha.
Zingatia pia local context!
 
Msiwe kila kitu mnakubali tu hao nao ni wanasiasa. Bwawa la Nyerere ni mara mbili tu ya bwawa la Mtera na sio mara kumi.
Lakini technologia inayotumika pale si sawa na bwawa la Mtera...
 
Ange
Hakujua ana muda muchache ila alitamani kuona Tanzania yenye mafanikio , mutu yeyote mwenye familia anajua namna Gani au njia Gani amezitumia kuhakikisha ustawi wa familia yake kama Kuna rough ezicheza halafu upo hapa kumunanga hayati hongera kwako
Angejua ana muda mchache wa kuishi, angefanya Kama Mzee Mandela.
Angehakikisha tuna katiba nzuri ya kudhibiti alioamini ni mafisadi. Angehakikisha tuna mahakama huru yenye kukimbiliwa na raia wote.
Angehakikisha tuna bunge imara lenye wanaoamini hata bunge likivunjwa leo bado wako tayari kurudi kwenye uchaguzi, kwani Wana uhakika uchaguzi ukifanyika kutoka kwenye vyama vyao mpaka bungeni utakuwa huru.
Angeondoa kinga ya kutoshtakiwa kwa viongozi wote, kwani hakuna sababu ya kuhofu.
Angegawa maendeleo sawa bila kujali wapi hawakumpigia ama walimpigia kura wala asingehangaika na maujenzi ya viwanja vya ndege kama Chato.
Mwisho angejua ana muda mfupi asigombea 2020,angefanya kipindi kimoja tu kama Mandela.
Nina uhakika, angefanya hayo hapo juu, watanzania tungetembea kifua mbele hata mambo ya tozo,tungebembelezwa na asingetokea mtu wa kutuambia kama hatutaki tozo tuhamie Burundi.
 
unafikiri kwanini hakuna mzungu alie tayari kutoa madolari? think big here ndo utaelewa maana ya kumuita Chuma cha pua Magufuli.

Hivi mkuu unajua Bunge la Ujerumani lilikaa session kibao kuzungumza na kupinga mradi wa Nyerere Dam eti unaharibu mazingira hebu fikiria umbali uliopo kati ya Tanzania na Germany wao inawaharibia mazingira gani? Lini sisi bunge letu limekaa kujadili mambo ya miradi ya nchi ingine? Magufuli will always remain a hero.


yaani ni hivi miradi hii ni ya kibabe na ya kulazimisha ikibidi hata kwa pesa ya ndani maana inafanya nchi kupaa kiuchumi na kupunguza kutegemea mikopo ya wazungu wanayotumia kutukandamiza daima. mzungu akiukataa mradi wako ujue una maslahi kwako lazimisha kuukamilisha and thats why we will always like Magufuli, he was special president

Mama Samia ana elements za Magufuli kuna siku alipinga sana propaganda za wazungu akawaambia sisi sio masikini maana hata kijijini mlo wa mwanakijiji unazidi dola moja (mihogo asali na mayai na maziwa) na wao wanaandika majority tunaishi chini ya dola moja.
Vitu vingi ni vya maana kuboresha maisha yako. Lakini kabla hujafanya, lazima kwanza uweke mipango na vipaumbele kulingana na uwezo wako. Mipango ya nchi haiamuliwi kisiasa na mtu mmoja kadiri anavyojisikia. Tanzania haina uwezo wa kutekeleza miradi ya matrilioni kwa mpigo kwa ufanisi kama inavyofanya. Lazima kuna maeneo yataumia na kudhurika sana hasa ya huduma za kijamii. Kibaya sana ni kununua ndege kwa cash bila business plan.

Watch this space. Miradi hiyo itachukua kati ya miaka 10-15 kukamilika tena kukiwa na mizozo mingi. Pesa nyingi itafujwa. Uzuri watu hatudumu na wengi kumbukumbu ndogo. Lakini wapo watakaokuwepo kujadili busara ya ajabu iliyotumika kuamua kulitwisha taifa mizigo mizito bila mpangilio.
 
Hongera sana Bw. Felchesmi Mramba... Kumbe wenye akili kubwa bado wapo.

Kujenga a mega project kama JNHP kwa kasi waitakayo wananchi na wanasiasa ni kujitegea time bombs.

Sijui wengine akili wanaziweka wapi wanapojadili masuala nyeti, muhimu na hatari kwa maendeleo na uhai. Ndiyo tunahitaji umeme wa uhakika lakini tujue kuwa miradi ya mabwawa ya umeme ni hatarishi. Inahitaji muda na umakini!

Pamoja na mambo mengine... nchini Ethiopia Grand Ethiopian Renaissance Dam ujenzi ulianza 2011 na kukamilika 2020. GERD imeanza kazi 2022.

Tujiandae kisaikolojia. JNHP itachukua muda mrefu zaidi.
Usilinganishe mradi wa Ethiopia Renaissance Dam na huu wa Tanzania. Ethiopia walipitia kwenye upinzani wa Bwawa kutojengwa kwa muda mrefu. Misri walitishia kupiga bomu huo mradi. Kuna wakati ulisimama.

Vita ya wenyewe kwa wenyewe ilikuwa changa moto kubwa kumaliza mradi kwa wakati. Wakati wa vita ilochukua karibu mwaka na miezi saba.

Kujaza maji kwenye bwawa, Ethiopia inapata mvua mara moja tu kwa mwaka tofauti na Tanzania. Hivyo kujazwa kwa bwawa imechukua muda mrefu zaidi. Mvua Ethiopia unyesha kipindi cha mwezi wa July hadi sept. Kisha hakuna mvua tena mpaka mwaka utaofuata miezi kama hiyo. Hivyo mnakaa mwaka mzima ili kuona mvua tena.

Tusitafute visingizio vya kushindwa kumaliza mradi muda muafaka kwa kujaribu kubalance na miradi mingine. Hivi kweli mkandarasi wa kampuni husika na wataalamu wetu ni wajinga hawakujua kuwa mradi huu wa Nyerere utachukua muda mrefu walipoingia mkataba?

Ati leo ndo Katibu Mkuu aje na hizo sababu? kwa nini kumekuwa na visingizio vingi vikitafutwa, mara winchi ya kunyanyua sijui nini ni ngumu kuipata, mara mvua, ili mradi kutafuta utetezi.

Leo Katibu anafananisha ujenzi wa mabwawa ya Mtera na Nyumba ya Mungu ati yalichukua miaka mingi. Ni ujinga wa kutupwa. Hivi anataka kusema sisi watanzania hatujui kutafakari na niwajinga? Wakati wa ujenzi wa hayo mabwawa technolojia ya wakati huo na sasa ilikuwa tofauti.

Hata kiwango cha uchumi wakati huo na sasa vilikuwa tofauti.

Na kwanini Tanzania tunapenda kutetea na kuhidhinisha matatizo kwa kutafuta sababu ili tu kuwadanganya wananchi. Kwanini tusiwe wakweli.

Katika Tanzania wanasiasa ndo wasemaji wakuu hata katika mambo ya kisayansi. Pia kwa kutafuta ulaji wanasayansi na wataalamu wetu wanaweka ujuzi na utaalamu wao pembeni ili tu kuwafurahisha wanasiasa.

Hata wanahabari, sijaona alie jitokeza kuleta habari toka pande zote. Mfano kuhoji kampuni ya ujenzi wa bwawa. Kumhoji mtaalamu wa serikali msimamizi wa mradi. Na pia kuhoji wataalamu kadhaa wa mambo ya ujenzi wa umeme nchini na hata nje. Kuhoji viongozi wa serikali iliyopita na wasiasa kwa nini tuliaminishwa vingine na leo tunaaminishwa vingine. Walau tukawa na habari yenye ulalo wa ukweli.

Sijawahi kuona nchi yenye ushabiki wa ovyo usioangalia maslahi mapana ya nchi. Watanzania tunajisifia sana kuwa tumeendelea kielimu na mengineyo lakini tu kama makondoo. Tunapelekeshwa tu na kupokea kisha kushangilia kila litakalosemwa.

Maswali ya waandishi wa habari wa Tanzania mengi ni yakujipendekeza. Kujichekesha. Hatuna waandishi wenye maswali ya kufikirisha, maswali ya mitego au hata ya kukera tu. Waandishi wanauliza swali unaona huyu anajiuma uma, hawajiamini. Natamani ningekuwa mwandishi wa habari!
 
Huyu ni Katibu Mkuu wa Wizara husika.

Maana ya lugha hiyo ni kuwaandaa watu wakubali mipango ya kifisadi inayoandaliwa kwenye wizara hiyo.

Kesho utasikia habari za mipango ya dharura inayohitajika kufanywa ili nchi isiwe gizani.

Hawa watu ni wapuuzi sana, wanafikiri waTanzania ni wajinga.

Kabla ya ujenzi kuanza, mkandarasi na wataalam huko Tanesco hawakujua kuwa itahitaji muda mrefu kukamilisha ujenzi huo? Hii miradi inafanywa tu kwa kubahatisha bila ya kuwa na upambanuzi juu yake kuhusu muda utakaohitajika kuikamilisha?

Hayo mabwawa anayotolea mifano yake, yalijengwa kwa muda huo wakitumia teknologia gani? Leo hii hapajakuwepo na maendeleo/mabadiliko yoyote katika ujenzi wa mabawa haya?

Huku kuwadharau waTanzania kiasi hiki kunatokana hasa na nini?

Hawa watu inatakiwa kuwatafutia njia za kuwatia adabu, kwa sababu sasa wamevuka mipaka kabisa katika kuwaona waTanzania kuwa mabwege.
Utabaki na hasira isiyo na msaada. Tulia dikteta hayupo tena
 
Ye angeweza. Ni uthubutu tu. Kwani mangapi yameanzishwa na yamefanyika. Kuna lecturer mmoja aliniambia wakati serikali inaanza mchakato wa makao makuu dom kuwa hautafanikiwa kabisa. Baadae ye nae akawa mpiga tarumbeta. Nadhani hakuamini kilichotokea.
Matokeo si ndio haya tunaona? Uchumi umeyumba kuliko wakati wowote
 
Sasa mbona it is almost 5yrs na mradi wa JNHP haujaisha. Si kila kitu kinahitaji hesabu za magazijuto au kurahisisha.
Zingatia pia local context!
The Fact kua wakandarasi wali sign mkataba wa miaka mitatu, meana walijua kua it can be pulled of within that timeframe na walitengeneza project time frame ya 3rys.
its unfortunately kua kuna na mis management ya project.
Project ikienda nje ya muda hua ni hasara kwa pande zote na zaidi kwa mkandarasi km sababu za kuchelewa zimetokana na uzembe wake.
 
Tatizo la kwanza kwenye huo mradi tangu unaanza ni kutanguliwa na siasa nyingi badala ya utaalamu, tatizo la pili ni kukosekana uwazi katika mchakato wake mzima hadi kampuni ya wamisiri ilipoanza kujenga.
Pia Kuna uongo mwingi sana raia wameaminishwa kuhuusu huo mradi.
Maisha ya meko ilikuwa uongo uongo mwingi. Hakuna ajabu
 
Tuacheni siasa kwenye uchumi, kama mmeamua SGR then iwe SGR mnafunga mikanda mnafuta maposho, mnafuta mbio za mwenge, mnafuta sensa hadi uchumi utengemea sio mnafanya Kila kitu kwa mkupuo lazima mfeli.
Hilo la mwenge wangelifanya ningefurahi sana. Sijawahi kuona faida za mwenge kitaifa.
 
Hapana. Nchi yetu ina matatizo makubwa sana na ni kichaa tu atakayeshangilia au kusifu haya yanayotokea. Ilikuwaje mtu mmoja awe na nguvu ya kuanzisha miradi complex namna hiyo bila kupata ushauri? Kwa nini hawa wanaopiga kelele sasa hivi hawakutoa hiyo tahadhari kipindi hicho, including aliyekuwa makamu wa rais? Kwanini baada ya haya yote kutokea tunaona ni kama hakuna makosa yaliyofanyika na tukabadilisha mfumo kwa haraka sana ili yasitokee tena na badala yake tunajivuta? Hatuoni kwamba hata sasa hivi kuna makosa makubwa kabisa yanaweza kuwa yanafanyika na tusijue sasa hivi kwa sababu mfumo wetu ni mbovu?
Katiba ndio shida. "Rais si lazima akubali ushauri wowote"
 
Kuna msemo wa kibeberu unasema Go big or go home...
only doers understand the true meaning ya huo msemo, and JPM was one of them.
Ali go big kwenye nini sasa...miaka yake 5 alikamilisha nini ambacho tutasema kweli hiki kimebadili maisha ya watz kwa deni la trilioni 78 aliloacha?
 
Punguza hasira mkuu, umeme wa nchi 60% unazalishwa kwa gesi so unaposema JNHPP Inacheleweshwa kisa ufisadi haingii akilini, kwanini ufisadi usifanyike kwenye Bomba la gesi ambako ndio expensive kufanya maintenance na kufua umeme??

Issue kubwa ni kwamba Miradi mingi Ina overlaps, SGR hapo hapo Bwawa hili, Bado sensa inakuja, hapo Bado Mabilion tunalipa riba Kila mwezi ya madeni ya taifa ya nje. Ukitaka kufanikiwa fanya jambo moja kwa ufanisi ila kuanza mambo mengi kwa mkupuo kisa kuonekana Unaleta mabadiliko lazima yachelewe.

Unadhani trillion 1 na kitu tunayoingiza kwa mwezi inaweza facilitate Miradi yote mikubwa, wagebill, na interest rates Kila mwezi??
Katibu mkuu hajaeleza hayo unayoeleza wewe, na ningetegemea kuwa anao uwezo mzuri kabisa wa kuelezea hayo kwa ufasaha mkubwa na akaeleweka.

Kuna shida gani kwa serikali hii iliyopo sasa kukaa chini na kuchambua miradi yote hiyo na kuona uwezo uliopo na kinachowezekana kufanyika halafu wakaelezea hali halisi ilivyo kwa wananchi!

Lakini ngoja nikuache na hili wazo: pamoja na 'ukichaa' mwingi aliokuwa nao Magufuli, upande ambao unabaki kuwa sifa kubwa kwake ni hiyo 'daring', hata kama ilikuwa ni ya pupa bila kutumia akili. Na nadhani, huku kuliliwa na wengi licha ya tabia zake mbaya inatokana na huo uthubutu wake.

Kuna kosa gani hata kama ni kukopa kukamilisha mradi muhimu kabisa kama Bwawa la Mwalimu Nyerere!

Haya yote wanayofanya hawa waliopo sasa ni kinyume kabisa, na ni dhahiri sasa wanategeshea kuingiza upigaji kwenye miradi mingi. Kazi kubwa inayokuja ni kutafuta na kuwatumia wapigaji tu waje hapa kutunyonga, hiyo ndiyo mikakati yao wanayoiweka mbelke.

Umezungumzia Dodoma mahali..., hiyo ni aina ya uthubutu ambayo imempambanua huyu kichaa aliyetokea kuwepo wakati huo, na hili kiukweli kalimaliza. Hutegemei tena serikali kurudi Dares Salaam hata wafanye nini hawa mashetani waliopo sasa hivi.
 
Ali go big kwenye nini sasa...miaka yake 5 alikamilisha nini ambacho tutasema kweli hiki kimebadili maisha ya watz kwa deni la trilioni 78 aliloacha?
Kwani hizo trilioni 78 kakopa zote yeye?kwanza hili sio deni sahili, deni sahini ni 64Tirioni hizo 78 sijui umezitoa wapi.
Weka deni lake yy km yy without
1. Including la private sector(maana unapozungumzia deni la taifa lina include both private and public),
2. Madeni ya watangulizi wake,
3. then toa madeni yaliyoiva kipindi chake(accumulative interest)
3. Toa inflation
4. Ondoa kushuka thamani kwa Shillingi yetu against dola.

Km ww hakufanikiwa kubadili maisha yako ni ww sisi wa gomz aliyabadili, kipindi chake tulipata barabara za mtaani na maji ya dawaso(kutoka kununua maji ya visima kwa tank kwa 300k mpaka buku 4 mia nae) and kupata hati within a month After 30yrs of waiting na kuzungushwa tangu tuhamie huko.
so we greatefull ht kwa hicho kidogo alichotufanzia wana gomz.
 
Utabaki na hasira isiyo na msaada. Tulia dikteta hayupo tena
Wewe utakuwa ni kilaza kama unafikiri nipo hapa kumshangilia dikteta.
Lakini ni muhimu ujue, hawa waliopo sasa ni wabovu zaidi ya dikteta kwa maslahi ya Tanzania.
 
Tatizo la kwanza kwenye huo mradi tangu unaanza ni kutanguliwa na siasa nyingi badala ya utaalamu, tatizo la pili ni kukosekana uwazi katika mchakato wake mzima hadi kampuni ya wamisiri ilipoanza kujenga.
Pia Kuna uongo mwingi sana raia wameaminishwa kuhuusu huo mradi.
Mkuu umenena,Mabwawa yamejengwa mengi Kidatu,Nyumba ya Mungu,Mtera,Pangani, bila mbwembwe na porojo za kisiasa.
Transparency ilikosekana katika kuwatafuta wakandarasi wa mradi wa bwawa la Nyerere.
Tumeona hata Tanroad anafanya kazi iliomzidi kimo.
Arab contractors ndie main contractor,inamilikiwa na jeshi la Misri haijaonyesha makali ya kazi,sana sana ni doctorate degrees,bilateral relationship ndio hadithi zisizohuzika kwenye mradi wenyewe.
Lakini kwa ndani Waziri Mkuu Majaliwa alietembelea huo mradi mara kwa mara alionekana kutilia shaka utekelezaji wa mradi.
Anapokuja katibu mkuu akasema anajali Safety kwanza katika utekelezaji wa mradi sio maneno ya kupuuzia.
Kuna uwezekano wa kubadiri michoro mara kwa mara ili kwendana na usalama na ubora wa mradi.Kama yapo mambo yalipuuzwa ndio wakati wa kuyaunganisha.Hata lile bwawa maarufu la Ethiopia dam X aka Millennium Dam limefanyiwa mabadiliko mengi mno ili likidhi mahitaji.
 
Back
Top Bottom