a4afrika
JF-Expert Member
- Apr 13, 2012
- 1,456
- 1,459
Binafsi Rumba ndio favorite Muziki kwangu, kila siku lazima nisikilize rumba.Huyu jamaa ni Mfalma we Rhumba za kweli. Ni mwanamuziki ambaye ukiwa mpenzi wa Rhumba lazima utenge siku maalum ya kusikiliza mziki wake.
Bahati mbaya Dunia ya Sasa inataka vitu feki kuliko original.
Kama Dunia ingetenda haki, basi FERRE GOLA angekua juuu sana.
Mfalme huyu hajapata heshima anayo stahili na wala nyote yake haiwaki inavyopaswa .
Gola anazo nyimbo nzuri zenye ushauri na kukupa maadili ya maisha. Mungu amtunze huyu Franco wa kizazi hiki.
Leo nimeamka na Rhuma ya Gola, nilipofika kwenye ngoma inaitwa "Qui vivra verra" imebidi niweke repeat mode. Jamaa amelalamika sana juu ya haya maisha ya kubangaiza huku akiamua kumuachia Mungu aamue hatma yake.
Imejikimbusha ngoma zake zingine kama Maboko Pamba, hii nayo ni balaa lingine.
Jaribu kusikiliza Qui vivra verra, sikiliza mwanaume analia sababu ya maisha magumu, sikiliza guitar rhythm na Bass tulivu. Sikiliza solo yenye heskima na heshima.
Wimbo wa mwaka 2013 lakini utadhani umetoka Jana.
Team Golla kula Tano mwanangu.
Kwa bahati mbaya sijawahi vutiwa na content kutokana na barrier ya Lugha.
Vyombo na Tone ya muimbaji/waimbaji inatosha kabisa kwangu. Kwa kuzingatia vigezo hivyo huwa sijali kabisa wimbo umeimbwa na nani wala unahusu nini.
Hakika Rumba ni habari nyingine. Tafuta mixing ya
Kupanda, Frere ardour by Madilu.
Callins na Icon of Afrika by Wazekwa
Bana ba Cameron by Samangwana
Cadenas, 1000Mawa, attente, by ipupa
Mercure, 100 Kilos by Gola
Reine de saba by Heritier Wata
Mamiwata by Mayaula
Mario, Ngugi, layile by Franco
Ndaya by Mpongo Love
Double Mbonda by Koffi
Na wengine weeeeeengi....
Washa redio yako, kwa sauti reasonable kidogo sio ya kujibanabana kivile. Kula rumba hilo ukiendelea kufanya yako.
Aisee, wakati nasoma msuli hauwezi kwenda bila kusindikizwa na rumba.
Afrika is Great!