Ficha IP Adress yako kwa kutumia VPN (Android users)

Ficha IP Adress yako kwa kutumia VPN (Android users)

habari wakuu,ninaomba maelekezo hatua kwa hatua namna ya kutumia hii VPN kwenye simu,nilidownload app moja ya kuangalia Mpira inaitwa live nettv sasa kuanzia juzi kuna channel hazifunguki,nikatuma Ujumbe kwenye page yao fb wakanielekeza nitumie VPN.
 
Kwa nini inaitwa VIRTUAL network wakati ni network ya ukweli?

Kwa mfano uliotumia wa COCA COLA Company, wafanyakazi au ofisi za kampuni popote duniani wanaweza kukutana ( kuwasiliana na ku access data za kampuni kwenye network moja), at the exclusion of all other unathorized guests, which means ni network ya ukweli.

Why VIRTUAL?
not physically existing as such but
made by software to appear to do
so. Sorry mkuu nlikuwa banned
 
Somo kuhusu VPN
Kirefu cha vpn ni virtual private network.Hii ni private network inayokuwezesha kutumia public network pasipo kutambulika.Private network ya kawaida huwa inakosa Usalama wa data.Unapokuwa kwenye public network watu wote mnaotumia hiyo network mnakuwa connected kiasi cha kwamba yoyote kwenye network haswa provider anaweza ku access data za mwengine.Kwa wale watumiaji wa tigo mfano utaona ukiwa una surf link yoyote kutokea facebook unakuja ujumbe wa kukumbusha unatoka facebook hiyo inaonesha Tigo wana access na data zako na wanaweza kufanya chochote
Jinsi VPN inavyofanya kazi
Kila kifaa kinachotumia network huwa na utambulisho wake unaoitwa IP address,VPN hufanya kazi ya kubadilisha IP address ya kifaa chako na kukupa nyengine ambayo sio ya kweli yani Virtual IP address ambayo inakuwezesha kutokutambulika ukiwa kweny network.
IP address hubeba utambulisho unaonesha nini unatafuta kwenye network,wapi ulipo na jinsi ya kufikia unachokitaka
Faida za VPN
VPN huweza kubadilisha IP address na kuwezesha kukufanya uonekane popote utakapo duniani,kukufanya uingie kwenye websites zinazozuiwa na kukufanya uepuke michujo yoyote kwenye internet
Usalama ni mkubwa na ni ngumu mtu kujua utambulisho wako halisi
Inapunguza gharama za ku surf
Jinsi ya kutumia VPN
Kuna njia nyingi za kutumia VPN lakini rahisi zaidi ni ile ya kutumia software inayobadilisha IP address yako kila unapoanzisha network
Kwa watumiaji wa simu hili ni rahisi zaidi kwani kuna apps zinazofanya kazi hii
App unayopaswa kuichagua inategemea unataka kuitumia VPN kwenye matumizi gani
Zifuatazo ni Apps bora za VPN kwa watumiaji wa Android
1.Hotspot Shield VPN&Proxy
Kitu cha pekee kuhusu app hii ni kusupport 4G na ina features nyingi kuliko vpn app nyenginezo
2.Unlimited free VPN-berrenet
3.Hideman VPN
4.SurEasy VPN
5.FinchVPN
6.Hola free VPN
7.Tunnel bear
Wenye professional zao
 
Maelezo mazuri yametolewa kuhusu VPN.
Lakini nina swali kuhusu VPN iliyokuwa kwenye simu
moja kwa moja ukiondoa APPS kibao zilizokuwepo Play Store na kwingineko
ambazo unadownload na kuinstall kwenye simu yako.

Je naweza kutumia VPN iliko kwenye simu? Na kama ndio najazaje?
Au VPN iliyoko ni tofauti na hizi APP za VPN?
Naomba ufafanuzi mzuri ili nielewe. Naambatanisha na Picha ya VPN ktk simu yangu.
WhatsApp Image 2018-05-03 at 11.53.36 AM.jpeg
 
Maelezo mazuri yametolewa kuhusu VPN.
Lakini nina swali kuhusu VPN iliyokuwa kwenye simu
moja kwa moja ukiondoa APPS kibao zilizokuwepo Play Store na kwingineko
ambazo unadownload na kuinstall kwenye simu yako.

Je naweza kutumia VPN iliko kwenye simu? Na kama ndio najazaje?
Au VPN iliyoko ni tofauti na hizi APP za VPN?
Naomba ufafanuzi mzuri ili nielewe. Naambatanisha na Picha ya VPN ktk simu yangu.
View attachment 764431
Watalamu jibuni swali hili mtakuwa mumetusaidiwa wengi sanaaa
 
Virtual private network ni mfumo ulioanzishwa mwanzo kwajili ya biashara kubwa baadae hata watumiaji binafsi walilazimika kutumia ,

Mfano: coca cola company iko karibu dunia nzima bila kutumia vpn wangelazimika kutumia cables kuunganisha office zao mfano Canada, Georgia, Tanzania ila haiwezekani kwaiyo watatumia internet na vpn itahusika hapo ili kulinda taarifa zao kutoka kwa hackers.

Mfumo huu unaosaidia ukiwa kwenye mtandao usionekane uko wapi(hide your location), pia unakusaidia kuficha taarifa zako (data encryption), pia unakusaidia kuingia website zilizofungiwa(unblock site) sehemu uliopo mfano ukiwa china sites kama YouTube, google, facebook, zimefungiwa ukitaka kiziacces lazma utumie vpn,

Vpn pia inauwezo wakuficha I.p address yako isijulikane iko wapi?

Vpn zipo nyingi na kila moja ina idadi ya servers , zipo za free na zipo zakulipiwa kwa jinsi yakutumia vpn ingia YouTube kila moja ina jinsi yaku install + configuration. .
Poa
 
Vpn Wanasema Kuwa Inalinda Taarifa Za Mtumiaji Ili Asiweze Kudukuliwa Na Wana Usalama Na Wahalifu,,sasa Nachohitaji Kujua,,ni Hiki, Mwanzoni nilikua natumia pc yangu bila vpn,,naperuzi mitandaon na kufanya mamb yote bila vpn inamaana hapa kama taarifa zangu wadukuzi walikuwa wanazipata vzuri tu,,Na sasa nimedownload cyberghost vpn swal lang ni je,,inauwezo wa kudaka taarifa zangu za nyuma zote ambazo zilikuwa ziko wazi na kuzificha ,,,au inaanzia kufanyia kazi taarifa zinazoingia mara baada ya kuinstall na kuanza kuitumia yan taarifa mpya,,?
 
Vpn Wanasema Kuwa Inalinda Taarifa Za Mtumiaji Ili Asiweze Kudukuliwa Na Wana Usalama Na Wahalifu,,sasa Nachohitaji Kujua,,ni Hiki, Mwanzoni nilikua natumia pc yangu bila vpn,,naperuzi mitandaon na kufanya mamb yote bila vpn inamaana hapa kama taarifa zangu wadukuzi walikuwa wanazipata vzuri tu,,Na sasa nimedownload cyberghost vpn swal lang ni je,,inauwezo wa kudaka taarifa zangu za nyuma zote ambazo zilikuwa ziko wazi na kuzificha ,,,au inaanzia kufanyia kazi taarifa zinazoingia mara baada ya kuinstall na kuanza kuitumia yan taarifa mpya,,?
Wanakuja
 
Vpn Wanasema Kuwa Inalinda Taarifa Za Mtumiaji Ili Asiweze Kudukuliwa Na Wana Usalama Na Wahalifu,,sasa Nachohitaji Kujua,,ni Hiki, Mwanzoni nilikua natumia pc yangu bila vpn,,naperuzi mitandaon na kufanya mamb yote bila vpn inamaana hapa kama taarifa zangu wadukuzi walikuwa wanazipata vzuri tu,,Na sasa nimedownload cyberghost vpn swal lang ni je,,inauwezo wa kudaka taarifa zangu za nyuma zote ambazo zilikuwa ziko wazi na kuzificha ,,,au inaanzia kufanyia kazi taarifa zinazoingia mara baada ya kuinstall na kuanza kuitumia yan taarifa mpya,,?
Jibu nimeshapigia mstari
 
Vpn Wanasema Kuwa Inalinda Taarifa Za Mtumiaji Ili Asiweze Kudukuliwa Na Wana Usalama Na Wahalifu,,sasa Nachohitaji Kujua,,ni Hiki, Mwanzoni nilikua natumia pc yangu bila vpn,,naperuzi mitandaon na kufanya mamb yote bila vpn inamaana hapa kama taarifa zangu wadukuzi walikuwa wanazipata vzuri tu,,Na sasa nimedownload cyberghost vpn swal lang ni je,,inauwezo wa kudaka taarifa zangu za nyuma zote ambazo zilikuwa ziko wazi na kuzificha ,,,au inaanzia kufanyia kazi taarifa zinazoingia mara baada ya kuinstall na kuanza kuitumia yan taarifa mpya,,?
Kama hautumii VPN haina maana kuwa taarifa zako zinaweza kudukuliwa. Unapotumia web au application yoyote inayotumia SSL/https taarifa zako ziko salama kwa vile zipo encrypted kwa hiyo VPN haiongezi chochote kwa upande huo.

VPN inasaidia kuficha ni site gani unazotumia kutoka kwa ISP wako i.e ISP wako anaona tu kuwa kuna connection kwenda VPN servers haoni kama unafungua JF au FB.

Pia kwa kiasi fulani inaficha upo wapi kwa upande wa site unayofungua kwa hiyo kama VPN server ipo marekani ukifungua Netflix wao wanaona kuwa IP yako ni ya Marekani.Hapa kuna tatizo la kuwa ukikosea tu hata mara moja kuacess hiyo site bila VPN wanajua ukweli uko wapi, na sio rahisi kutokosea kwa matumizi ya kawaida hata warusi waliokua wanasambaza habari feki FB walitereza mara kadhaa na kufichua walipokuwepo kweli.

Ni muhimu kuelewa kuwa unapotumia VPN maana yake unamwamini anayeendesha hiyo VPN na taarifa zako zote maana ni middleman kwenye mawasiliano yako, ni impossible kujua ni nani anaendesha hiyo VPN na lengo lake ni nini. Kwa mfano Facebook walinunua kampuni ya VPN na kuiendesha kisiri ili kujua watu wanatumia Apps na mitandao gani.

Pia VPN app nyingi ni feki au zinakusanya taarifa zako na kuziuza kwa third parties kwa ajili ya kukulenga na matangazo, fikiria VPN itakuwaje bure wakati inahitaji resources na servers nyingi kuiendesha? "If you are not the customer, you are the product".
 
Unaposeti VPN kwa kutumia setting kuna sehemu ya Name na Server address naomba msaada hapo. Au unajaza tu jina lolote
 
Maelezo mazuri yametolewa kuhusu VPN.
Lakini nina swali kuhusu VPN iliyokuwa kwenye simu
moja kwa moja ukiondoa APPS kibao zilizokuwepo Play Store na kwingineko
ambazo unadownload na kuinstall kwenye simu yako.

Je naweza kutumia VPN iliko kwenye simu? Na kama ndio najazaje?
Au VPN iliyoko ni tofauti na hizi APP za VPN?
Naomba ufafanuzi mzuri ili nielewe. Naambatanisha na Picha ya VPN ktk simu yangu.
View attachment 764431
Nahitaji pia kujua hapa
 
Unaposeti VPN kwa kutumia setting kuna sehemu ya Name na Server address naomba msaada hapo. Au unajaza tu jina lolote
Unajaza settings za VPN server yako, so kama umenunua VPN service sehemu watakupa hizo settings kama wanasupport VPN bila App.
 
Back
Top Bottom