Fidia ya Tsh. Bilioni 75 iliyolipwa na Serikali kwa Winshear Gold Corp ingeweza kununua Mashine 83 za CT-Scan

Uamuzi wa Serikali kuifanyia marekebisho Sheria ya Madini ya mwaka 2010 yaliyofanyika mwaka 2017 na kanuni zake ni chanzo cha Serikali kulipa Sh75 bilioni kwa mwekezaji Winshear Gold iliyemfutia leseni.

Fedha hizo zingeweza kutumika kuboresha sekta kadhaa za maendeleo, lakini zimeishia mikononi mwa mwekezaji kutokana na uamuzi uliofanywa na Serikali miaka michache iliyopita.

Fedha zilizolipwa kwa kampuni hiyo zingeweza kujenga zahanati 267 na vituo vya afya 68.

Kwa upande wa magari ya kubebea wagonjwa, yangeweza kununuliwa 250, moja likigharimu Sh300 milioni na kila mkoa ungeweza kupatiwa magari tisa.
 
Mkuu mbona unawaza miundombinu tu Kila wakati?

Badala ya kusema ingeweza kuajiri walimu kadhaa au kuongeza mishahara ya walimu kiasi kadhaa au tungewapa posho walimu wanaolea taifa hili kiasi kadhaa au tungeboresha miundo ya utumishi wa walimu walau kima cha chini kianzie Milioni Moja n.k

Mawazo ya namna hii ndio tunahitaji baada ya miaka kadhaa utakuwa na taifa bora kabisa lililoelimika.

Pia, utakuwa umeongeza tija kubwa na value ya human labour sio Kila mara majengo tu na magari hizo ni teknolojia zinachakaa lakini ukiwekeza kwa watu Mzee unajenga taifa
 
Tumepata mgodi lakini au?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…