FIFA wanaua soka, Kila timu inayoshiriki kombe la dunia la vilabu kupewa takribani shilingi bilioni 130, Mpira wa Afrika unaenda kuwa farmers league

FIFA wanaua soka, Kila timu inayoshiriki kombe la dunia la vilabu kupewa takribani shilingi bilioni 130, Mpira wa Afrika unaenda kuwa farmers league

gearbox

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2024
Posts
563
Reaction score
1,768
Hasa hapa kwetu Afrika kwenye timu ambazo hazifiki hata asilimia kumi ya hicho kiasi

Unazipa timu bilioni 130 kwa kushiriki kombe la mwezi, inakuwa ngumu sana kwa timu zenye bajeti za bilioni 8 kushindana na hao wanaopewa mizigo mizito.

Vuta Picha leo hii hata Mtibwa kavuta hicho kiasi, Yanga na Simba wataweza kumsogolea ?
 
Msiokuwa na hela wekezeni sana kwenye scouting, vipaji afrika hii ni vya kumwaga, mchezaji wa bei ndogo anakuja kulingana na hao wa bei kubwa.

Inonga, che malone, pacome, azizi ni wachezaji wamekuja nchini hawana majina makubwa kulingana na UWEZO wao.
 
Hasa hapa kwetu Afrika kwenye timu ambazo hazifiki hata asilimia kumi ya hicho kiasi

Unazipa timu bilioni 130 kwa kushiriki kombe la mwezi, inakuwa ngumu sana kwa timu zenye bajeti za bilioni 8 kushindana na hao wanaopewa mizigo mizito.

Vuta Picha leo hii Yanga au Simba kavuta hicho kiasi, kuna shindani tena hapo ?
Ndiyo maana kila njia ilifanyika ili goli la Aziz Ki lisikubaliwe ili Mamemlodi waingine kwenye bwawa hilo la mihela ya FIFA.
 
Ndiyo maana kila njia ilifanyika ili goli la Aziz Ki lisikubaliwe ili Mamemlodi waingine kwenye bwawa hilo la mihela ya FIFA.
Kama refa alikuwa amepanga kuwabeba Mamelodi angewapa penalti kwa Mamelodi, Memelodi wenyewe wamefungwa na Esperance goli lenye utata wa offside, kama kuna njama za kuwabeba hilo goli lingekataliwa..Alijitahidi kuwa fair ila mistakes huwa zinatokea
 
Hasa hapa kwetu Afrika kwenye timu ambazo hazifiki hata asilimia kumi ya hicho kiasi

Unazipa timu bilioni 130 kwa kushiriki kombe la mwezi, inakuwa ngumu sana kwa timu zenye bajeti za bilioni 8 kushindana na hao wanaopewa mizigo mizito.

Vuta Picha leo hii Yanga au Simba kavuta hicho kiasi, kuna shindani tena hapo?
bajeti ya ahly ni dola milion 100+ kwa mwaka!

hizo dola mil 50 wala haziwafanyi wao kuwa bora zaidi kutuzidi,

afrika hii timu zijitahidi kufanya scouting, wachezaji wazuri ni wengi sana!

simba na yanga ingekua zinajiendesha kisasa zina uwezo wa kutengeneza mapato zaidi ya 20b kwa mwaka, kiasi ambacho kinatosha kuendesha timu na ikawa na ushindani........

1. kadi za wanachama
2. bidhaa za timu (jezi, skafu, kalenda, kanga, makoti, vyombo vya vyakula vyenye logo zao, etc...... hapa ndio pana pesa ndefu zaidi)
3. gate collection (hapa wanatakiwa kukodisha uwanja, ila wavune vizuri mapato through corporates, migahawa, viingilio, majukwaa unayauza kwa makampuni yajitangaze n.k)
4. media
5. ...
6....
7....

katika nchi kama hii ambayo wapenda mpira ni wengi, ni rahisi sana kuwageuza pesa!
 
So far
bajeti ya ahly ni dola milion 100+ kwa mwaka!

hizo dola mil 50 wala haziwafanyi wao kuwa bora zaidi kutuzidi,

afrika hii timu zijitahidi kufanya scouting, wachezaji wazuri ni wengi sana!

simba na yanga ingekua zinajiendesha kisasa zina uwezo wa kutengeneza mapato zaidi ya 20b kwa mwaka, kiasi ambacho kinatosha kuendesha timu na ikawa na ushindani........

1. kadi za wanachama
2. bidhaa za timu (jezi, skafu, kalenda, kanga, makoti, vyombo vya vyakula vyenye logo zao, etc...... hapa ndio pana pesa ndefu zaidi)
3. gate collection (hapa wanatakiwa kukodisha uwanja, ila wavune vizuri mapato through corporates, migahawa, viingilio, majukwaa unayauza kwa makampuni yajitangaze n.k)
4. media
5. ...
6....
7....

katika nchi kama hii ambayo wapenda mpira ni wengi, ni rahisi sana kuwageuza pesa!
Naona Azam na Yanga wanapambana kutumia hiyo mianya walau ila bado saaanaa
Sijui Kwa Simba nao
 
Kama refa alikuwa amepanga kuwabeba Mamelodi angewapa penalti kwa Mamelodi, Memelodi wenyewe wamefungwa na Esperance goli lenye utata wa offside, kama kuna njama za kuwabeba hilo goli lingekataliwa..Alijitahidi kuwa fair ila mistakes huwa zinatokea

Weka evidence kama mamelodi amefungwa goli la offside na Esperence

Weka ushahidi. Kuprove hoja yako
 
Kama refa alikuwa amepanga kuwabeba Mamelodi angewapa penalti kwa Mamelodi, Memelodi wenyewe wamefungwa na Esperance goli lenye utata wa offside, kama kuna njama za kuwabeba hilo goli lingekataliwa..Alijitahidi kuwa fair ila mistakes huwa zinatokea
Aziz Ki hakufunga goli likakataliwa? Jitihada zilifanyika swali Lomalisa spate red card aibu ukala kubwa
 
Hasa hapa kwetu Afrika kwenye timu ambazo hazifiki hata asilimia kumi ya hicho kiasi

Unazipa timu bilioni 130 kwa kushiriki kombe la mwezi, inakuwa ngumu sana kwa timu zenye bajeti za bilioni 8 kushindana na hao wanaopewa mizigo mizito.

Vuta Picha leo hii Yanga au Simba kavuta hicho kiasi, kuna ushindani tena hapo?
Yeah!...mpira wa Sasa umevamiwa na mabwanyenye..

Usisahau FIFA ni shirika la Kibepari linalotafuta faida.
 
Kwa Africa Ni timu 4 tu zinaenda zilizofanya vizuri ndani ya miaka mitano,

Simba hayumo lakini anashika namba 7 kashaingia robo fainali mara nyingi miaka mitano iliyopita,

Yanga yupo nje ya top 10 kaanza kupata mafanikio mwaka jana
Bingwa wa CAF champions league ana tiketi ya moja kwa moja bila kujali ranks.. yule refa alitufanyia umafia sana kule south afrika, timu zilizobaki semis zote tunazimudu, tulikua tunaenda kukipiga na wakina man city.
 
Mamelodi analazimishwa afike mbali sababu yeye peke yake ndie anategemea ranking.

1.AL AHLY ameshafuzu sababu ndani ya misimu mitano iliyopita amebeba ligi ya mabingwa mara 2.

2.Waydad ameshafuzu sababu ndani ya misimu mitano iliyopita amebeba kombe la klabu bingwa mara moja

3. Esperence ameshafuzu sababu ndani ya misimu mitano iliyopita amebeba kombe la klabu bingwa mara mbili.

4. Nafasi ya nne ndio bado tupu. Maana ni only 3 teams ndizo zilizobeba ubingwa wa africa last 5 years.

Na hiyo nafasi ndio itapewa klabu ambayo itakuwa na ranking ya juu. Kama hatatokea bingwa mpya. Mfano yanga tungeenda fainali na kutwaa ubingwa hiyo nafasi tungepewa sisi.

Tp mazembe akienda fainali na kutwaa ubingwa hiyo nafasi anapewa yeye

Na hata mamelodi kama akitwaa ubingwa anapewa yeye.

Kama mamelodi ataukosa ubingwa na tp mazembe nae ataukosa ubingwa basi mamelodi atapewa hiyo nafasi ya nne ya kushirikiki kwa kigezo cha ranking ya juu.
 
bajeti ya ahly ni dola milion 100+ kwa mwaka!

hizo dola mil 50 wala haziwafanyi wao kuwa bora zaidi kutuzidi,

afrika hii timu zijitahidi kufanya scouting, wachezaji wazuri ni wengi sana!

simba na yanga ingekua zinajiendesha kisasa zina uwezo wa kutengeneza mapato zaidi ya 20b kwa mwaka, kiasi ambacho kinatosha kuendesha timu na ikawa na ushindani........

1. kadi za wanachama
2. bidhaa za timu (jezi, skafu, kalenda, kanga, makoti, vyombo vya vyakula vyenye logo zao, etc...... hapa ndio pana pesa ndefu zaidi)
3. gate collection (hapa wanatakiwa kukodisha uwanja, ila wavune vizuri mapato through corporates, migahawa, viingilio, majukwaa unayauza kwa makampuni yajitangaze n.k)
4. media
5. ...
6....
7....

katika nchi kama hii ambayo wapenda mpira ni wengi, ni rahisi sana kuwageuza pesa!
Mkuu umezungumza kama vile ulikuwa kwenye mawazo yangu ila nafikiri Simba wanaweza kuwa matajiri kama wakifanya yafuatayo:-
1: Siku ya simba day wanaweza kuleta timu kubwa mbili au 3 kwa siku tofauti tofauti ambapo kuwepo na tofauti ya siku mbili mbili, wanaweza vuta hela Sana.
2: wanaweza kuanzisha card zao ambazo zinaweza kuwa ni special kwenye kuingia uwanjani,bank, kulipia ada yao ya uanachama, Malipo ya kununua jezi,vikombe nk.
3: kutangaza kila mwaka kwenye Media kuhusu ishu ya kampuni inayotaka kuingia kwenye udhamini na hivyo kufungua milango ya wafanyabiashara kuingia makubaliano. Hapo inahitajika mtu wa marketing afanye Kazi yake.
4: Kuwepo na kadi special za wanachama kuanzia wale wa VIP, VVIP NK ambapo kadi zinaweza anza hata kuanzia million 10, million 5, million 3, million 2, million, laki tano nk. Hapa hela inayopatikana inaweza tumika katika usajili na Mambo mengine madogo madogo.

Hawa waliochangia wanaweza pata faida km ifuatavyo:-
1: kupata tickets bure wao na familia yao Katika kila mechi nje na ndani ya nchi.
2: kupata jezi free
3: kupata hata vinywaji na ikiwezekana vitafunwa, kupata viatu,na mengineyo. Hapa ni kwa wale wa kuanzia million na na kuendelea.
4. Kama timu inaweza fanya Hivi katikati ya msimu,hela inaweza tumika katika uwekezaji.

Pia yapo mengi tu kwa timu kuweka mikakati ikiwemo kujua idadi ya fans wa simba kupitia katika card na kusajili watu wa ndani na nje ya nchi na wao kupata hadhi yao na hata taarifa za Simba, mazoezi ya simba, wachezaji wanaoona wanafaa,nani aingie na nani atoke,waweke mitandao ambayo wanaweza toa maoni yao na viongozi wakasoma,kuwajibu n huko pia hata youtube na other social media ambapo mpunga unaweza kuingia vizuri tu kila mwezi.

Kama kuna watu wanataka hata kumleta mchezaji ghali na atamlipia,au kuna wanaotaka kujitolea mbona very simple?wapo wanaotaka kumpa zawadi mchezaji anaweza fanya hivyo akatoa hela yakr na ikafika kupitia katika mitandao hyo hyo ya kijamii.

Kwa Sasa kuna mambo ya hovyo yanayofanyika kama ifuatavyo:-
1: malumbano ya uongozi na uongozi
2: kocha na wachezaji.
3:hakuna platform ya hawa fans kutoa maoni yao na kubaki kutoa kwenye mitandao ambayo inachochea katika mifarakano kati ya wachezaji, kocha na viongozi.
4: kuvujisha taarifa za wachezaji wanaotakiwa simba kabla ya kumalizana nao na hivyo kufanya timu pinzani au kumuongezea mchezaji gharama za usajili au hata kuingia Katika radar za timu zingine ambazo hazijafanya scouting bali kuisubiri Simba ifanye scouting,itoe wachezaji kwenye mitandao na wao waongeze dau na kwa kuwa simba kwenye hela ni mkono mfupi, inashindwa katika mihimili gharama za mchezaji baada ya kuwa aghali,wanaishia kula kwa macho, AZIZI K walianza nae hadi kwenye mitandao, baadae MANGUNGU akasema deal done na kuonyesha gharama za kumsajili mchezaji, yanga wakaongeza hela, leo amekuwa msaada Sana kwa yanga. Kuna Manzoki nae yuko wapi,ni magazeti, viongozi, na mitandao kila Siku kuipamba simba ila mwisho wa siku wanakuja Kuchukua wachezaji wanaokaa benchi tu na wa gharama nafuu Sana.
Kama wataendelea Hivi basi simba inaweza shuka daraja na kubaki na sifa tu ya kile miaka ya nyuma ilipofikia robo fainali tu.

Pia huyu mwekezaji nae auze hisa zake maana tunasikia kuwa kuna watu wanataka kuweka mpunga wa maana.

Mwisho
Simba sio ya MO bali ni ya mwekezaji pamoja na wanasimba hivyo kunahitajika kuifikisha simba katika mafanikio na sio mtu mmoja tu aendeshe timu bila kuweka ushirikiano na watu wengine maana kidole kimoja hakivunji chawa.
 
Back
Top Bottom