FIFA yaipa Yanga siku 45 kumlipa Okra Magic Tsh 66,612,000.00 na siku 30 kulipa fine ya Tsh 8,190,000.00

FIFA yaipa Yanga siku 45 kumlipa Okra Magic Tsh 66,612,000.00 na siku 30 kulipa fine ya Tsh 8,190,000.00

Utopolo kwenye post kama hii huwaoni.Kwenye majungu na uzushi ndio zao.
Msomali na "Mwanasheria" novice wanawala haswa.
 
Yanga SC ni club ya mambuzi na vibwengo mdundiko Kila mwaka wamejaa ushamba kwenye mikataba
 
  • Kicheko
Reactions: Tui
Timu la ovyo badala ya kulipa wachezaji linatumia fedha hizo kununua mechi!
 
  • Kicheko
Reactions: Tui
View attachment 3109287
Katika uamuzi wa hivi karibuni kutoka kwa Mahakama ya Usuluhishi wa Migogoro ya FIFA (FIFA Dispute Resolution Chamber), Yanga SC, moja ya klabu maarufu za mpira wa miguu nchini Tanzania, imetakiwa kumlipa mchezaji wa zamani wa Bechem United, Augustine Okrah, kiasi cha dola za Kimarekani 24,400 sawa na Tsh 66,612,000.00/= kama fidia ya mshahara ambao haukulipwa wakati wa kipindi chake na klabu hiyo.

Mzozo huu unahusiana na kuondoka kwa Okrah kutoka Yanga SC, maarufu kama Wana Jangwani, baada ya mkataba wake kuvunjika kwa njia isiyofaa, hali iliyopelekea Okrah na timu yake kuwasilisha malalamiko kwa FIFA. Baada ya uchunguzi wa kina, FIFA iliamua kuwa Yanga ilikiuka makubaliano ya mkataba na hivyo ikaamuru malipo hayo kufanyika.

Zaidi ya malipo hayo ya dola 24,400, Yanga pia imepigwa faini ya dola 3,000 sawa na Tsh 8,190,000.00/= kwa FIFA, na inatakiwa kulipa ndani ya siku 30 tangu tarehe ya kuarifiwa kwa uamuzi huo. FIFA imetoa onyo kali kwa Yanga, ikisema kuwa iwapo hawatalipa kiasi hicho kwa wakati, klabu hiyo itakabiliwa na adhabu zaidi, ikiwa ni pamoja na marufuku ya kusajili wachezaji wapya kitaifa na kimataifa hadi watakapomaliza malipo yao.

Hii si mara ya kwanza kwa Yanga SC kujikuta katikati ya mvutano wa kisheria na wachezaji wake. Msimu uliopita, Okrah aliitumikia Simba SC, mahasimu wakubwa wa Yanga, kabla ya kurejea ligi kuu ya Ghana akiwa na Bechem United, lakini alijiunga tena na Yanga mnamo Januari 2024 kabla ya mkataba wake kuvunjika ghafla.

Kwa mujibu wa uamuzi wa FIFA, endapo Yanga watashindwa kulipa kiasi kilichopangwa ndani ya siku 45, watafungiwa kusajili wachezaji kwa vipindi vitatu vya usajili mfululizo, hali itakayoathiri vibaya mipango yao ya kujipanga kwa mashindano yajayo ya kitaifa na kimataifa.​
View attachment 3109288
Hata watoe miezi miwili huu sio muda wetu wa kulipa.tutamlipa WAKATI wa dirisha la usajili.
 
Hili timu Kila mwaka lazima lipekwe FIFA Kwa madeni na ni tangu zamani hata kabla ya Hersi ni hivi hivi.Linaaibisha Sana ligi yeti.
 
  • Kicheko
Reactions: Tui
Back
Top Bottom