Fighting spirit ni jambo kubwa katika mpira ukiachana na ubora na mbinu

Fighting spirit ni jambo kubwa katika mpira ukiachana na ubora na mbinu

vibertz

JF-Expert Member
Joined
Mar 15, 2022
Posts
2,474
Reaction score
4,726
Kwenye mpira wa miguu hakuna kitu kizuri kama kupambania timu na hilo ndilo ambalo limeifanya Yanga wafikie hapa walipo ukiachana na mbinu na ufundi wa kocha Gamondi. Viongozi wa Yanga wanaonesha wanataka kitu, wachezaji wanaonesha wapo tayari kupambana kufikia lengo na kila mechi wanacheza kama fainali. Kwa mchezaji yeyote anapopewa nafasi lazima aivujishie jasho timu yake kwa asilimia zake zote. Kocha Gamondi nae yupo kuhakikisha wachezaji wanajituma na kupambana ili kuipa Yanga mafanikio na ndio maana alionekana kutaka kumzaba mshika kibendera ambaye alionekana wazi kutaka kuharibu jitihada za wanajeshi wake wanaopambana kwenye vita.

Timu ya Yanga ndio wapo hivyo kila mechi wanacheza kama fainali japo performance haiwezi kuwa sawasawa kwa kila mchezo ila wapo kupambania matokeo. Kwa upande wa wachezaji wa Simba fighting spirit yao huwa ni pale tu anapokuja mwalimu mpya, makocha wote wapya wanaopewa timu ya Simba hushinda mechi zao na wengine hushinda kwa kishindo kiasi kwamba uwezi kuamini kama ni Simba hii ndio iliyosua sua dhidi ya kocha aliyetangulia.

Benchikha wakati anaanza kuifundisha Simba mashabiki wa Simba waliona kuwa timu sasa ndio hii, na kocha ndio huyu. Watu wakasifia wachezaji wamebadilishwa mno na wakasema wanaona mwanga sasa juu ya Simba yao japo kuna baadhi ya watu wakatoa rai kuwa hii ni spirit kwavile ni kocha mpya tu ila muda ukatoa majibu hadi Benchikha akabakia benchini peke yake.

Hili ndio hilo hilo lililopo sasa kwa Simba ya Mgunda, wachezaji wameamua kujituma na kupambana kwavile ni kocha mwingine na wengine mikataba inaenda ukingoni hivyo lazima kuonesha wanastahili kubaki, ila sio mbaya mashabiki wakajaribu kupatiwa hitaji lao ili wathibitishe kwa uhalisia kuhusu uwezo wa kocha wao wanaomtumainia, wanaompigia chapuo kukabidhiwa timu moja kwa moja. Mgunda apewe timu msimu ujao wote aiongoze Simba
 
Kwa hiyo tunakubaliana shida ya Simba ilikuwa kocha na Sasa hakuna tena tatizo.
Ikumbukwe kwa misimu mitatu Sasa ukiwemo huu Simba Kila ifikapo mwisho wa msimu gari huwaka sana na kuleta matumaini (moto wa mabua)
Kisha msimu ukianza mgunda huyuhuyu atakataliwa peupe
 
Maelezo meeeengi, Utopolo hakuna kitu... Wanabahatisha tu na marefa wanaibeba. Ingekuwa marefa wapo faur halal bin halal Sasa hivi wasingekuwa tofauti na Namungo,Dodoma jiji na Kagera.

Ngja tuone Kimataifa kama wata maintain Kuvuka Makundi CL CAF kama inavyofanya SSC, Timu kubwa kuliko zote Afrika Mashariki na Kati na Kusini ya Afrika ukimtoa Mamelod.
 
Maelezo meeeengi, Utopolo hakuna kitu... Wanabahatisha tu na marefa wanaibeba. Ingekuwa marefa wapo faur halal bin halal Sasa hivi wasingekuwa tofauti na Namungo,Dodoma jiji na Kagera.

Ngja tuone Kimataifa kama wata maintain Kuvuka Makundi CL CAF kama inavyofanya SSC, Timu kubwa kuliko zote Afrika Mashariki na Kati na Kusini ya Afrika ukimtoa Mamelod.

Faur maanake nini?
Ulivyofungwa nje ndani na Yanga ni kipi ulidhurumiwa na waamuzi?
Belouizdad, Mamelodi na Medeama walishindwa kuifunga Yanga ndani ya dakika 90 je kwa msaada wa mwamuzi yupi? Hao waamuzi wanafanya makosa yanayoweza kuinufaisha timu yeyote ile hata Simba wamenufaika na hayo maamuzi ya waamuzi na pia waamuzi wanaweza kudhurumu haki ya timu yeyote ile hata Yanga imehusika kudhurumiwa haki kwenye baadhi ya mechi na sio Yanga peke yake hata Simba wamedhurumika na timu zinginezo. Ndio mpira ulivyo na ndio maana ulaya wakaona madhaifu ya waamuzi kuona matukio kwa ufasaha ikabidi waboreshe kwa teknolojia mbalimbali ikiwemo VAR na goal line technology ili kusaidia waamuzi katika matukio.

Umezungumzia muendelezo wa Yanga kimataifa ni ajabu umeshindwa ku notice kuwa Yanga wameweza kuwa na muendelezo ndani ya misimu miwili hii mfululizo wamefanya vyema kwa kucheza fainali na robo fainali ya CAF inter club championship na ndio maana unaona kwenye rank kasogea kutoka kuwa na point 0.5 hadi kuwa na point 31.
Hivyo Yanga inaenda kuwa timu tishio zaidi sio kwa mdomo bali kwa vitendo, na itakuwa ni kawaida kwao kucheza hatua ya nusu fainali klabu bingwa. Waliweza kuwakabili Mamelodi mliyeshinda humu kuwaimba na nyimbo za UBUTHU BOTHO lakini Yanga walicheza kikubwa bila uwepo wa wacheza watatu muhimu na bado likapatikana goli lililoleta taharuki kubwa kwa kukataliwa. Wakati nyie mkijiona wakubwa kwa kuwa pale pale, Yanga anataka kuwa mkubwa kwa kuvuka zaidi ya hapo mnapoishia miaka nenda rudi.
 
Maelezo meeeengi, Utopolo hakuna kitu... Wanabahatisha tu na marefa wanaibeba. Ingekuwa marefa wapo faur halal bin halal Sasa hivi wasingekuwa tofauti na Namungo,Dodoma jiji na Kagera.

Ngja tuone Kimataifa kama wata maintain Kuvuka Makundi CL CAF kama inavyofanya SSC, Timu kubwa kuliko zote Afrika Mashariki na Kati na Kusini ya Afrika ukimtoa Mamelod.
Daah walimwengu mna vituko sana. Hao marefa wanaipendelea Yanga tu? Mbona Yanga kakufunga nje ndani au bado alipendelewa? Ilikua atinge nusu fainali ambayo wewe unaiota ila kwa hila za marefa ikashindikana bado marefa waliibeba?

Kuna wenzako wengi tuliwaambia hiki kichaka cha robo kinafyekwa na kilifyekwa sasa ivi mnabaki kusema marefa wanaipendelea Yanga
 
Faur maanake nini?
Ulivyofungwa nje ndani na Yanga ni kipi ulidhurumiwa na waamuzi?
Belouizdad, Mamelodi na Medeama walishindwa kuifunga Yanga ndani ya dakika 90 je kwa msaada wa mwamuzi yupi? Hao waamuzi wanafanya makosa yanayoweza kuinufaisha timu yeyote ile hata Simba wamenufaika na hayo maamuzi ya waamuzi na pia waamuzi wanaweza kudhurumu haki ya timu yeyote ile hata Yanga imehusika kudhurumiwa haki kwenye baadhi ya mechi na sio Yanga peke yake hata Simba wamedhurumika na timu zinginezo. Ndio mpira ulivyo na ndio maana ulaya wakaona madhaifu ya waamuzi kuona matukio kwa ufasaha ikabidi waboreshe kwa teknolojia mbalimbali ikiwemo VAR na goal line technology ili kusaidia waamuzi katika matukio.

Umezungumzia muendelezo wa Yanga kimataifa ni ajabu umeshindwa ku notice kuwa Yanga wameweza kuwa na muendelezo ndani ya misimu miwili hii mfululizo wamefanya vyema kwa kucheza fainali na robo fainali ya CAF inter club championship na ndio maana unaona kwenye rank kasogea kutoka kuwa na point 0.5 hadi kuwa na point 31.
Hivyo Yanga inaenda kuwa timu tishio zaidi sio kwa mdomo bali kwa vitendo, na itakuwa ni kawaida kwao kucheza hatua ya nusu fainali klabu bingwa. Waliweza kuwakabili Mamelodi mliyeshinda humu kuwaimba na nyimbo za UBUTHU BOTHO lakini Yanga walicheza kikubwa bila uwepo wa wacheza watatu muhimu na bado likapatikana goli lililoleta taharuki kubwa kwa kukataliwa. Wakati nyie mkijiona wakubwa kwa kuwa pale pale, Yanga anataka kuwa mkubwa kwa kuvuka zaidi ya hapo mnapoishia miaka nenda rudi.
Ukiacha ushabiki wako wa Yanga ila huu ndio uchambuzi wa Mpira. Mwenye kuelewa na aelewe.
 
Maelezo meeeengi, Utopolo hakuna kitu... Wanabahatisha tu na marefa wanaibeba. Ingekuwa marefa wapo faur halal bin halal Sasa hivi wasingekuwa tofauti na Namungo,Dodoma jiji na Kagera.

Ngja tuone Kimataifa kama wata maintain Kuvuka Makundi CL CAF kama inavyofanya SSC, Timu kubwa kuliko zote Afrika Mashariki na Kati na Kusini ya Afrika ukimtoa Mamelod.
Una bachelor ya u mbumbumbu
 
Msa
Faur maanake nini?
Ulivyofungwa nje ndani na Yanga ni kipi ulidhurumiwa na waamuzi?
Belouizdad, Mamelodi na Medeama walishindwa kuifunga Yanga ndani ya dakika 90 je kwa msaada wa mwamuzi yupi? Hao waamuzi wanafanya makosa yanayoweza kuinufaisha timu yeyote ile hata Simba wamenufaika na hayo maamuzi ya waamuzi na pia waamuzi wanaweza kudhurumu haki ya timu yeyote ile hata Yanga imehusika kudhurumiwa haki kwenye baadhi ya mechi na sio Yanga peke yake hata Simba wamedhurumika na timu zinginezo. Ndio mpira ulivyo na ndio maana ulaya wakaona madhaifu ya waamuzi kuona matukio kwa ufasaha ikabidi waboreshe kwa teknolojia mbalimbali ikiwemo VAR na goal line technology ili kusaidia waamuzi katika matukio.

Umezungumzia muendelezo wa Yanga kimataifa ni ajabu umeshindwa ku notice kuwa Yanga wameweza kuwa na muendelezo ndani ya misimu miwili hii mfululizo wamefanya vyema kwa kucheza fainali na robo fainali ya CAF inter club championship na ndio maana unaona kwenye rank kasogea kutoka kuwa na point 0.5 hadi kuwa na point 31.
Hivyo Yanga inaenda kuwa timu tishio zaidi sio kwa mdomo bali kwa vitendo, na itakuwa ni kawaida kwao kucheza hatua ya nusu fainali klabu bingwa. Waliweza kuwakabili Mamelodi mliyeshinda humu kuwaimba na nyimbo za UBUTHU BOTHO lakini Yanga walicheza kikubwa bila uwepo wa wacheza watatu muhimu na bado likapatikana goli lililoleta taharuki kubwa kwa kukataliwa. Wakati nyie mkijiona wakubwa kwa kuwa pale pale, Yanga anataka kuwa mkubwa kwa kuvuka zaidi ya hapo mnapoishia miaka nenda rudi.
Msamehe mbumbumbu wa Rage
 
Mahabiki wa Yanga na 5imba ni wachache sana waloelimika lkn wengine ukisifia upande Mmoja hata kama ni kweli lazima wang'ake tu 🤣 Sasa tegemea
Moja kuungwa Mkono na shabiki wa Yanga.
Mbili kuzodolewa na mashabiki wa 5imba.
Tatu kuungwa Mkono na mashabiki wa chache wa mpira
 
Back
Top Bottom