Filamu ya Royal Tour Ingezinduliwa Tanzania Badala ya Marekani kuepuka gharama

Nimekuelewa wanachokifanya ni kujibrand wenyewe maana huwezi kuonesha faida ya moja kwa moja ya jambo kama hili isipokua hiyo.
 
Yani kitu kimetengenezwa kwa 7-9B halafu kizunduliwe Tanzania ambapo 3/4 ya Wananchi wake hawawezi kula milo 2 -zitakiwa akili au matope??
Filamu ilitengenezwa na kampuni gani? Nilitegemea kabla ya premiering, kampuni iliyotengeza movie yenyewe pamoja key players kufanya promotions mbalimbali ikiwa ni pamoja kufanya interviews nyingi kwenye vyombo mbalimbali vya dunia. Sasa kwenda kufanya premiering Marekani tena katika ukumbi usiojulikana ni kupoteza muda tu. Watalii wa Tanzania hawatoki Marekani tu; kwa style hii itabidi mama atembee dunia nzima kwenda kufanya shoo hizo iwapo yuko serious na kutangaza utalii kweli. Wakati wa Kikwete kulitoka filamu ya kuitangza utalii na kuna wakati Mama Salma alichukua Gulfstream ya Rais kwenda Brazili peka yake eti kutangza utalii. Leo hii hapo Youtube kuna video nyingi sana zinazopromote utalii Tanzania


Je hii filamu inayozinduliwa itakuwa na tofauti ipi kulinganisha na hizo zilizotangulia?
 
Yani kitu kimetengenezwa kwa 7-9B halafu kizunduliwe Tanzania ambapo 3/4 ya Wananchi wake hawawezi kula milo 2 -zitakiwa akili au matope??
Nikuulize pia the same question.

Nini kipaumbele cha mtu ambaye hana uwezo wa kupata milo miwili??

Bila shaka utachagua Filamu.
 
Tangu mwanzo nilisema hakukuwa na haja ya kutengeneza filamu ya ku promote utalii kwa sababu zipo nyingi tu Rais mwenyewe hawezi ku promote utalii mimi ninaelewa hivyo na ninaamini hivyo kwa sababu ni mtaalamu wa mambo hayo kwa miaka zaidi ya 45 na nimesomea
 
Ngoja uambiwe posho zao sasa

Raisi atembei cheap kuna team hapo ya walinzi wake ilishatangulia kama week kabla, kuhakiki usalama wa sehemu anayofikia na kuafiki security details zake.

Hao jamaa kwa week mbili kipindi wameenda Glasgow kila mtu posho yake si chini ya £6000.

Halafu sasa yeye mwenyewe anaenda na kundi lake rasmi sikia tu hizo posho zao na idadi ya watu.

Now piga picha lile kundi la Dubai kila taasisi, wizara na kundi la raisi lilioenda kwa posho ya wastani wa dola $4500 kila mtu kwa week plus ticket fair.

Walinzi wa mama wasipojenga nyumba za kueleweka ndani ya huu mwaka mmoja awajengi tena.

Ukumbi wenyewe huko anapoenda zindua hiyo filamu unaenda jaza wabongo kushinda wazungu.

Maza anaupiga mwingi
 
Makushabu Ni hatari Sana kwa mustakabari wa Taifa.
 
Sasa kama majority ni wabongo tija yake ni ipi

Si bora angezindua hapa hapa tu.
 
Huyu mama tumepigwa...shamba la bibi tena
Awamu zote hua tunapigwa tu,aina ya Kichapo ndio hua inatofautiana.Awamu iliyopita kulikua na mtaalam wa kuwamaliza watu na kuwaweka kwny viroba,awamu hii tuna mla bata.
 
Nchi imerudi mikononi mwa wachache so Rudi nyumbani kwako ulee watoto wako , achana na hizi. Siasa za. Maji taka
 
Lengo ni kuwavutia watalii ambao ndio wako huko. Kwa hili ninamuunga mkono raisi.
Timing ni mbaya.

Kwasasa Vita vya ukaraine ndio ina make headlines.

Hiyo filamu haitapata attention inayokusudiwa.

Angesubiri basi hata vita iishe. Uchumi uimarike aiachie haraka ya nini??
 
Marekani anapigana vita Ukraine?
Au huna habari kuna mamia ya watalii toka Ukraine walikwama hapa.

Hapa nazungumzia attention ya dunia iko wapi kwa sasa.

Watu wanapambana na vita na madhara yake na korona pia.

Wrong timing again.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…